Tuesday 11 August 2015

TATIZO LA KUFIKA KILELENI HARAKA..2

Kawaida baada ya mwanaume kuwa na tabia ya kumaliza haraka kinachofuata ni kuanza kukwepa sex kitu ambacho inakuwa ngumu zaidi kudhibiti tatizo, mwanaume akiwa anauwezo wa kuthibiti kumaliza mapema pia huweza kuwa na hamu zaidi ya kufanya mapenzi.

Wengine hutumia njia ya kuondoa mawazo kujihusisha na tendo lenyewe kwa kuwaza vitu vingine hata hivyo hapo ni kujinyima raha na huweza kupelekea vitu kuwa ovyo zaidi.
Si vema kuhamisha mawazo yako kutoka kwenye akili zako wakati wa tendo la ndoa kwani ni sex muunganiko wa roho, mwili na nafsi.
Jambo la msingi ni kuwa na ufahamu wa viwango tofauti vya msisimko wa kimapenzi kuhusiana na kiungo chako (uume).
Unatakiwa kujua ni namna gani unajisikia unapokaribia kufikia hatua ambayo hakuna kurudi nyuma (ejaculatory inevitablility kifupi EI).

Ukishakuwa umefahamu unavyojisikia kuelekea point of No return hapo haitakuwa vigumu kufanya marekebisho ambayo yatakuruhusu kubaki umesisimka lakini bila kumaliza (kukojoa).

Kusisimka kimapenzi huwa ni mzunguko wa hatua 4 muhimu ambazo kwanza ni kupanda kwa mdadi, huu ni wakati ambao kupumua huongezeka, uume husimama (hudinda), hatua ya pili ni kilimani, hii ni hatua ambayo uume huwa umebaki umesisimka kwa kiwango cha juu, hatua inayofuata ni hatua ya tatu ambayo ni kumaliza au kukojoa, na hatua ya mwisho ambayo kupumua hurudi kama kawaida na uume hurudi na kuwa kawaida.
Ufunguo muhimu katika kuthibiti kumaliza mapema ni ku-maintain hatua ya pili yaani kubaki hapo kilimani bila kupiga risasi hata kama umelenga vizuri na unajisikia kuachia, hapa ndipo panahitaji imani na kujikana maana huwa ni kuelekea kwenye raha kamili ya sex kwa mwanaume, ila kumbuka uliye naye anahitaji uendelee zaidi.

Nini kifanyike kuthibiti hii hali?
Usitumie drugs au kilevi eti ndo unaweza kuthibiti hii hali, vitu kama hivi huweza kukupa interference na kupunguza uwezo wa kuelewa wakati muhimu wa wewe kuthibiti kumaliza mapema.
Kwanza jikubali, wanaume wengi huamini kwamba sex ni kwenye uume tu na pia kufanya mapenzi ni pale uume ukiingia kwenye uke tu.
Kufikiria hivyo ni tiketi ya moja kwa moja ya mwanaume kuwahi kukojoa au kumaliza.

Kufanya mapenzi kunakoridhisha (best sex) ni pamoja na kupeana mahaba, romance kuanzia juu kichwani kwenye nywele hadi kwenye kucha za vidole miguuni.
Mwanaume anayejifunza kujipa raha kimapenzi kupitia sehemu zote zinazompa raha (chuchu, lips, shingo, midomo, ulimi, nk) huweza kurelease tension kupitia hizo sehemu na kutosubiri sehemu moja tu yaani uume ndo iwe sehemu ya kupata raha ndo maana huweza kukojoa mapema.
Ni kwamba mwanaume anakuwa amefunga outlet zingine na kubaki na uume tu hivyo ni rahisi kufikia point ya no return tena kwa haraka mno.
Ukishajifunza kupata raha ya mapenzi (sexual pleassure) kuanzia nywele kichwani hadi kucha miguuni maana yake mwili mzima unachukua raha ya mapenzi badala ya uume peke yake na matokeo yake utabaki ndani ya mke wako kwa muda mrefu.

Kujipa raha ya mapenzi ya mwili mzima ni njia ya ku-relax na kurelax ni moja ya njia muhimu za kujipa good sex.
Kwa mfano kuoga pamoja kwanza au kufanyiana massage kwanza kabla ya kuanza kwa tendo la ndoa husaidia mwanaume kurelax na zaidi kuupa mwili mzima sexual pleassure matokeo yake ni kufanya mapenzi kwa muda unaotosha na bibie kuridhika.

Kuwa na uwezo wa kupumua vizuri (deep breath) hii haina maana kwamba wakati unafanya mapenzi huwa hupumui, la hasha bali upumuaji wako inawezekana si ule usiotakiwa kwani wanaume wengi huzuia kupumua wakiwa kwenye sex.
Wengine huogopa kusikika wanapumua tofauti, sex ni kazi kama kazi zingine sasa usipopumua unadhani kitatokea nini, ikiwezekana pumua huku unatoa visauti, achia kupumua usijivunge kwani unapoficha kupumua maana yake unakaribisha uume ukusaidie kupumua na njia sahihi kwa uume kupumua ni kukojoa mapema.
Wengi baada ya kujifunza kupumua kwa kujiachia wamefanya mabadiliko makubwa sana katika muda wa kuwa ndani bila kumimina risasi.
· .
Ukishajua kuutumia mwili mzima kuhusika na raha ya mapenzi pamoja na kupumua sasa inakuja technic nyingine ya kujipiga stop.
Unaweza kuwasiliana na partner wako jinsi ya kupeana signal kwamba nakaribia kile kituo ambacho nikifika sitarudi tena, hakuna break.
Unaweza kutoa uume nje huku ukiendelea kupumua na ukiona unapata zile feelings kwamba huwezi kukojoa basi unaweza kurudi na kuendelea tena, kiasi cha kujipiga stop na kuendelea ni uamuzi wa ninyi wawili mnaohusika hasa baada ya mke kuridhika.

Kwa wale ambao kufanya mapenzi kupo katika level nyingine (oral sex) wanaweza kutumia oral sex kuthibiti mwanaume kumaliza mapema kwa mwanaume kujipa stop akiona anakaribia kumaliza kwa oral sex hii ni baada ya kupata mafanikio hasa baada ya kuona sasa mwanaume anaweza kwenda mbali zaidi ya kawaida yake.

Pia aina ya milalo wakati wa mapenzi huchangia mwanaume kumaliza mapema, kwa mfano missionary position (mwanaume juu mwanamke chini) huu huwezesha mwanaume kumaliza haraka kuliko mwanamke kuwa juu na mwanaume chini, otherwise mwanaume ni vizuri ukafanya utafiti wako kujua ni mlalo gani huwa unajisikia kuchelewa kumaliza na mke wako kuwahi kufika kileleni.

Pia ni vizuri kufanya mapenzi bila kuwa mabubu,kufanya mapenzi huku mnaongea husaidia mwanaume kurelax (na mwanamke pia) na husaidia mwanaume kuchukua muda mrefu kumaliza
Kujifunza kuthibiti kumaliza mapema kunaweza kuchukua muda mrefu na mazoezi ya kutosha, unaweza kujisikia ksumbuka tu wakati unajitahidi kuthibiti hata hivyo kwenye nia njia ipo na wewe utaweza tu nakuamini.

Mwisho, kujifunza mwanaume kumaliza mapema kutampa mpenzi wako raha kubwa sana kimapenzi. Wanawake hupenda good sex ambayo ni leisure, playful, whole body, massage kwa wingi.
Na wanawake wengi hulalamika kwamba wanaume huwa na haraka tukiwa kwenye miili yao, tupo too much mechanical, tunakimbilia kule chini tuingize tumalize na tuishie zetu kwa usingizi, tuna focus matiti na maeneo ya uke tu.
Wanawake hujisikia mwili mzima ni uwanja wa kucheza kimapenzi na hushangazwa na wanaume kugundua visehemu kidogo tu katika uwanja mzima na kuvipenda.
Hata uume pia umeumbwa kwa ajili ya leisure, kuchezewa, mapenzi ya mwili mzima, massage ya mwili mazima ndipo sex, kuwa focused kwenye uume peke yake huweza kuupa uume mgandamizo ambao hupelekea kutoa risasi mapema.

Kimsingi kama wanaume wangekuwa wanafanya mapenzi kwa namna ambayo wanawake wanapenda basi kusingekuwa na malalamiko na wanaume wangekuwa na matatizo kidogo yanayohusiana na tendo la ndoa.

USIKOSE SEHEMU YA MWISHO..

No comments:

Post a Comment