Thursday 24 November 2016

USAFI NI MUHIMU.


Jambo moja ambalo kila siku hulalamikiwa na wanawake kuhusu waume zao ni suala la mwanaume kuwa mchafu, kuingia kitandani huku ananuka kama soksi chafu na wakati huohuo unataka kuwa karibu na mke wako kimapenzi kila sehemu ya mwili wako.
Sidhani kama hilo ni jambo la kistaarabu!

Kuna siku kilirushwa kipindi redioni kinachowaomba wanawake kuuliza maswali au kutoa malalamiko kuhusu usafi na tendo la ndoa kuhusu waume zao, tofauti na nchi zinazoendelea ambazo wanawake huogopa kuongea kwa uhuru (in public) kuhusu waume zao, kwa kuwa ilikuwa katika nchi zilizoendelea wanawake waliongea kwa mfululizo na kutoa malalamiko yafuatayo:
Kwanza kuna wanaume hata huwa Hawajali usafi, wapo ambao hata kuoga ni kazi, kupiga mswaki kazi, au kujiandaa kiusafi wakati wa kwenda kitandani na matokeo yake mke hujikuta badala ya kusisimka anakasirishwa.
Saa nne usiku, unaingia kitandani na unataka sex, midevu yako haijanyolewa vizuri na matokeo yake inamchoma mke utadhani kidevu kina sandpaper, hujaoga na jasho la ofisini kupitia kwapa zako linanuka kama compost pile.
Kucha ndefu na chafu kwa ndani utadhani ni kucha za monkey.
Katika utafiti uliofanywa baada ya kuwauliza wanafunzi (chuo) 332 kile ambacho huwavutia zaidi kwa wanaume, iligundulika kwamba namna mwanaume ananukia huvutia zaidi kuliko namna anavyoonekana kwa mwanamke.
“Hii ina maana kwamba ni mwanaume hata kama umepiga pamba za uhakika huku unanukia kama panya aliyeoza huna maana”.
Hivyo ni muhimu sana kwa mwanaume kujifunza kutumia kipande cha sabuni, ni vizuri kuoga kabla ya kujirusha kitandani hata kama ulikuwa na busy day.
Pia Kumbuka kujinusa mwenyewe na kuamini kila kitu kipo shwari si gauge nzuri.
Pia Kumbuka mwanamke ana uwezo mkubwa kunusa kuliko mwanaume.
Usafi na sex ni vitu vinavyoendana huwezi kuvitenganisha.

Monday 21 November 2016

UKAGUZI WA NAMNA.HII KTK NDOA.

Uwezo wa kumwamini na kujisikia salama na kutulia kati ya wanandoa ni moja ya misingi ya kila mmoja kutoa upendo kwa mwenzake. Bila msingi imara katika kuaminiana au bila kuweza kuimarisha kuaminiana huweza kuleta mzozo mkubwa kwenye ndoa.

Mume na mke hujisikia raha na furaha ya ajabu wakati kila mmoja akifahamu kwamba mwenzake anamwamini (trust) na hii furaha hudumu kwa muda wote ingawa kwa wale wasioaminiana hujikuta wanajiingiza kwenye migogoro na kukwaruzana au mmoja kumkalia mwenzake na kumnyima uhuru na kuwa mtumwa.

Inawezekana wewe ni mwanamke umeolewa na mwanaume ambaye hakuamini kwa lolote, hata ukiondoka na gari ukirudi nyumbani anaanza kukuuliza sehemu zote ulizoenda, umekutana nani, na mmeongea kitu gani ikiwezekana je kwenye gari ulimpakia nani nk.
Haishii hapo bali hujumlisha umbali ambao umemwambia na anaenda kulinganisha na ule umbali ambao gani limesafiri ili ajue ni kweli vinalingana, kama hiyo haitoshi kwa kuwa kuna tofauti na Km 5 anarudi tena kukuuliza imekuwaje ulikoenda na umbali vinatofautiana?

Au umemuomba fedha kwa ajili ya kununua vitu vya kutumia katika familia naye amekwambia kwanza uandike list ya mahitaji yote na bei zake, anakupa pesa kiasi kilekile sawa na vile umeonesha kwenye orodha yako.
Unaporudi anakuomba umuoneshe vitu vyote umenunua na anaomba umpe risiti zote alinganisha kama bei inalingana na vitu umenunua kama haitoshi kila tofauti iliyopo kwenye risiti na orodha ya kwanza inabidi ujieleze.
Anakagua kuhakikisha je vitu umenunua vinalingana thamani na pesa kama kuna kitu umekosea au kina hitilafu anakwambia ukarudhisha au umlipe fedha zake kwani yeye si mtu kwamba anatikisa pesa zinadondoka tu, Kama vile haridhiki anasahihisha hadi spelling za kwenye risiti ilimradi tu aonekane yeye yupo sahihi na si vinginevyo.
Je, hapo kuna kuaminiana?

Inawezekana wa kwako hafanyi hayo hapo juu ila naomba hebu jaribu kujiuliza maswali yafuatayo:
Tafadhari tulia na uwe mkweli na Shahidi ni wewe mwenyewe na moyo wako.
Je, Kila wakati anataka kila kitu kifanyike katika namna anayotaka yeye na si vinginevyo?

Je, Kila wakati yeye ndiye yupo sahihi na si vinginevyo?

Je, Hutafutiza vimakosa hadi vipatikane na hakuna siku anaweza kusifia (compliments)?

Je, Hakupi nafasi kujieleza au kutoa maelezo pale kosa likifanyika?

Je, Hujisikia wivu na kutojiamini hata kama hakuna sababu?

Je, Anakakikisha unajisikia hatia (guilt) kwa kila kitu unafanya?

Kukaliwa na mwenzi kwa namna hii huweza kusababisha mmoja hujiona yupo jela, hana uhuru na mtumwa na hana nafasi kujiachia (express) na matokeo yake ni Kujiona anaishi in hell na hujiona kama anaishi na adui badala ya mume au mke na hujiona kila siku hafai.

Sunday 20 November 2016

JINSI YA KUFANYA ILI KUMVUTIA MWANAUME MNAPOKUTANA KWA MARA YA KWANZA.

Ukweli kila mwanamke hutuma signal kwa mwanaume na wanaume wengi huweza kufanya detection ya hizo signal kwa sekunde tu na signal za kwanza ambazo mwanamke huzituma na kupokelewa na mwanaume ni mwonekano na lugha ya mwili.

Ni rahisi mno kwa mwanamke kumvutia mwanaume kwani wanaume huvutiwa sana kwa kile wanaona, hata hivyo jambo la msingi kwa mwanamke ni kufahamu kwamba ni aina gani ya attention anahitaji kutoka kwa mwanaume kwani wavuvi huamini kinachodhihirisha aina ya samaki utakayemkamata ni aina ya chambo unayotumia.

Je, unahitaji mwanaume kuvutiwa na wewe kama mwanamke (person) au kama chombo cha starehe (an object) hivyo basi ni muhimu kuzingatia mambo ya msingi ili kupata kile unahitaji.

Mwanamke kujiamini ni jambo la kwanza na msingi kabisa kwa kumvutia mwanaume, kujiamini wewe mwenyewe na mazingira yanayokuzunguka huweza kumvutia mtu anayefanana na wewe, pia utajisikia na kuona watu wanavutiwa na wewe pia.

Mwonekano wako (appearance) ni jambo la msingi sana, mwonekano wako na jinsi unavyotumia mwili wako kuongea huvutia sana hata hivyo ili uliyemvutia abaki na wewe unahitaji personality na uchangamfu.

Pia Kumbuka kwamba jinsi unavyoonekana na kufanya pale mnakutana kwa mara ya kwanza ni muhimu sana kwani akikutana na wewe wakati upo ovyo kuliko wakati wote hawezi nkupoteza muda kuwa na wewe tena (first impression)

Pia hakikisha unampa mwanaume sababu ya msingi ya yeye kukufikiria wewe, hapo inabidi uwe mbunifu kuhakikisha milango yake ya fahamu itafanya akukumbuke, mwanamke hupendeza akivaa nguo soft, pia kuvaa smile usoni kiasi kwamba inakuwa ngumu kwa yeye kukuondoa kwenye mind yake.

Jitahidi kuhakikisha anajisikia yeye ni very important, elekeza akili yako kumsikiliza na pia respond kwa kile anaongea na ku-respect mawazo yake. Cheka wakati anatoa jokes zake hata kama jokes zake hazina kichwa wala miguu hapa ni kuwa na interest kwenye interest zake.

Na mwisho usithubutu kuvaa kitu kingine na ukasababisha yeye ku-fall in love na sanamu kwani siku akikugundua wewe halisi hapatatosha. Onyesha originarity yako na kwamba ni wewe kamili na si mwingine katika haiba, akili na tabia.

Thursday 10 November 2016

TALAKA UHUMIZA


Talaka huumiza kuliko kifo, hata hivyo kwa baadhi ya wanawake walioolewa sasa wanaona talaka ni uhuru na maisha.
Hujiona wao young and beautiful, hakuna mtu wa kumwambia fanya hili au kile, no demands, hakuna kulaumiwa, kuonywa, kusemwa, kuamrishwa, hakuna kumpikia dinner wala lunch, hakuna utumwa, na akiangalia nje ya ndoa anaona mwanga ni mzuri unaopendeza, anajiuliza kwa nini kuteseka wakati huko nje kuna wanaume wengi tu wananihitaji.
Anafikiria namna anaweza kurudi kwenye maisha ya ujana upya, ulimwengu mpya kwani hakuna kuzozana tena, hakuna kulalamikiana tena, hakuna kuulizana umetumiaje fedha.
Mwanamke anafanya kweli, anaachana na mume wake na kila mtu kuanza kivyake.
Kwa mara ya kwanza anaona mambo ni mazuri, baada ya kusuguana na mume kwa muda mrefu sasa anajiona amepata ahueni, uhuru kwa kwenda mbele.

Sasa nikueleze ukweli wenyewe!

Kawaida wanawake wengi (siyo wote) wanaoachana na waume zao umri wao mara nyingi ni kuanzia miaka 28 – 40.
Maana yake huko nje wanakoamini kuna wanaume wa kuwaoa wapo wanaume wa aina mbili tu, kwanza ni wale ambao nao wameachana na wake zao na pili ni wale ambao ni single (hawajawahi kuoa).
Mara nyingi hawa wanawake huwaogopa sana wanaume wa kwanza hapo juu kwa kuwa ndo walewale ambao wameachana nao, hivyo Hujiuliza swali “kwa nini ameachana na mke wake?”
Hii ni dalili kwamba anaweza kuwa ni big trouble!
Hii ina maana sasa amepunguza idadi ya wanaume ambao anaweza kuoana nao tena kwani tumebakiwa na wanaume ambao hawajawahi kuoa yaani wapo single.
Hapa anamtafuta mwanaume ambaye ana sauti nzuri, mtaalamu wa kuongea, romantic, tender, passionate, mwelewa, mwenye fedha za kutosha, mwenye taaluma nzuri kama vile lecturer, Diplomat au millionaire, mwanaume ambaye hata
Watoto wake watajiona wana baba wa uhakika, ambaye si mlalamikaji, anayeweza kuwafanya kusafiri kila Mahali wanapotaka duniani na mwanaume ambaye atavutiwa na yeye tu na si vinginevyo.
Tuseme wewe mwanamke uliyeamua kutimka kwa mume wako sasa una miaka 38, je unadhani ni rahisi kumpata mwanaume wa aina hii ambaye amekuzidi umri au mnakaribia au sawa.
Ni mwanaume gani mwenye sifa kama hizo anaweza kukubali kuoana na mwanamke aliyeachana na mume wake?
Kama amekuzidi umri na wewe una miaka 38 inakuwaje hadi sasa awe hajaoa, utasema alikuwa anasoma PhD, yaani na PhD yake aje akuoe wewe uliyeachika na mume wako?
Si rahisi kama unavyofikiria!
Ukweli ni kwamba mwanaume wa aina hii anapatikana kwenye TV na Movies!
Anapatikana kwenye mawazo, anapatikana fantasy land na si kwenye maisha halisi!
Nafasi ya kumpa mwanaume wa aina hii ni moja kati ya milioni moja.
“Don’t permit the possibility of divorce to enter your thinking, even in a moment of great conflict and discouragement, divorce is not a solution”
Unaweza kujikuta wewe mwanamke ndiye unawawinda wanaume, kwa taarifa yako mwanaume hayupo wired kuwa kuwindwa badala yake yeye hufurahia kuwinda.
Utajikuta ni lonely na unazeeka haraka kuliko ulivyotegemea.
Wanawake walioolewa ambao walikuwa rafiki zako wataanza kujisikia uncomfortable na wewe, wanakuona ni mwanamke loose na dangerous kwa waume zao na wanaanza kukukwepa na kuweka ulinzi mkali kwa waume zao, na wanaume ovyo nao wanaanza kukushangaa mboni hutaki kulala nao, wanakuona wewe ni cheap target!
Kutafuta talaka ni kupoteza uraia wako, hadhi yako na uhuru wako.
Utajikuta unakaa nyumbani mwenyewe peke yako usiku hadi usiku, hofu itaanza kukuingia, kujiamini kunaanza kupotea, unaanza kujiona huvutii tena na watu wanakudharau.
Talaka ni kubadilisha matatizo ya zamani na kujipa matatizo mapya.
“Guard your relationship against erosion as if you were defending your very lives”
Kumbuka ukishirikiana na mume wako mnaweza kurudi tena kwenye raha ya maisha kama vile mwanzo mlipoanza ndoa yenu.

Sunday 6 November 2016

NI MAKOSA KUMPA MCHUMBA HUDUMA ZA MKE/MUME


Kawaida huwezi kumpa kila mwanaume huduma za mume wakati bado ni mchumba tu.
Vijana wengi leo wanapochumbiana au kutafuta urafiki wa kawaida kati ya kaka na dada (dating) wengi hawajajua kwamba hiyo ni hatua ya mwanzo kabisa na ni kama usaili tu wa kumpata mtu wa kuoana naye.

Ndoa na uchumba (girlfriend/boyfriend) ni vitu viwili tofauti kabisa uchumba huhusisha kumfahamu mwenzako kama anafaa kuwa mke au mume na ndoa ni agano na kumkubali mtu kuishi naye “ hadi kifo.

Hata siku moja uchumba si ndoa na ndoa si uchumba.

Ukimpa mchumba haki za mume au mke siku mkiachana na huo uchumba (kitu ambacho ni kawaida kama ukiona candidate uliyenae katika uchumba hawezi kwa excellent material ya ndoa) utaumizwa zaidi hasa mwanamke kwani mwanaume anaweza kumpata binti mwingine jioni yake au usiku huohuo na akaendelea na maisha.

Kinachoshangaza pia ni kwamba hata relationship inapovunjika mara nyingi mwanaume huumia kidogo kwa kuwa mwanaume siku zote anapoingia kwenye mapenzi huingia na “open mind”, wakati mwanamke akimpata mwanaume (uchumba) anajiona amampata “the Special one”.

Utasikia akina dada wengi wanasema “Nipo kwenye committed relationship” wakati ni ugirlfriend na uboyfriend tu, ni kweli uposahihi hata hivyo unatakiwa kuacha nafasi kwa ajli ya kuchunguza na si kumfanya huyo mwanaume ni mume wako na kumpa haki zote au services zote kiasi kwamba mahusiano yakivunjika unaanza kusaga meno.

Si busara kumpa mwanaume kila kitu katika mahusiano ya uchumba wakati hujaoana naye. Unamfulia nguo, unalala kwake, unampikia chakula wakati yeye ni boyfriend tu!

Swali ambalo mwanaume anajiuliza ni kwa nini aingie gharama za kukuoa kama umeshakuwa mke hata bila ring kwenye kidole?

Kwa nini akuoe wakati tayari ameshajua kila kitu kuhusu wewe?

Kwa nini anunue ng’ombe kama maziwa na nyama vyote anapata bure?

Kumbuka wazazi wetu walikuwa makini sana na hayo na mwanamke yeyeyote hakujifanya mke wakati ni mchumba tu. Uchumba ni daraja tu la kupita kufikia ndoa. Huwezi kugawa zawadi zote ambazo zipo kwenye begi kabla ya kufika kwa mwenyeji wako katika safari ya kuelekea kwenye ndoa.

Wanaume ni binadamu si Mungu na kila binadamu ana sifa ya kugeuka nyuma pale anapoona njia anayoenda si yenyewe.

Uwe na lengo lakuhakikisha unaweza kuweka mipaka na usimfanye huyo mwanaume ndo kila kitu hapa duniani kwani kuna siku anaweza kubadili uamuzi ndipo kujuta kutakuja.

Ni busara kwa wewe mwanamke hata kama una mchumba uendelee kujihusisha na kazi yako, taaluma yako kiasi kwamba hata ikitokea amekuacha huwezi kuchanganyikiwa.

Kama umewekeza kwa mchumba upendo na mapenzi ya asilimia 100 Je, baada ya kuoana utawekeza kiaasi gain?

Saturday 5 November 2016

MAMBO HUBADILIKA MKISHAOANA NA KUANZA KUISHI PAMOJA.


Watu wawili wanaopendana na kuishi kila mmoja kivyake ni tofauti sana na watu wanaopendana na kuishi nyumba moja.
Wapo ambao hujiuliza inakuwaje wapenzi wawili waliokuwa wanapendana na kuwa na moto wa mapenzi wa kiwango cha juu sana wakianza kuishi pamoja mambo huanza kubadilika? Pia wapo ambao hukubaliana kwamba baada ya kuoana na kuishi pamoja watajitahidi sana kuhakikisha wanapendana kama mwanzo hata hivyo baada ya kuanza kuishi pamoja hujikuta wamekuwa dada na kaka na hakuna moto wa mapenzi tena.

Jambo la msingi unatakiwa uwe makini kwani kuishi kila mpenzi kwake ni tofauti na kuishi na mpenzi nyumba moja na kitanda kimoja.
Pia wapo wanaume au wanawake baada ya kuoa au kuolewa hufikiria na kuamini kwamba wale wameoana nao si wazuri kama wale walioko nje hata hivyo ukweli ni kwamba kwa kuwa huishi naye masaa 24 kwa siku Ndiyo maana unaona ni mzuri, ukiishi naye kwa saa 24 siku 365 kwa mwaka ndo utajua ni tofauti kabisa.

Inawezekana wakati mnaishi tofauti na mpenzi wako ilikuwa ni kulala saa sita au nane usiku kwani mlikuwa mnapigiana simu na kutumiana sms kiasi ambacho hamkulala hata hivyo baada ya kuoana sasa kila mmoja anakuwa sehemu ya maisha ya mwenzake kila siku inayopita duniani.

Sasa unalala naye, unaamka naye na kula chakula naye. Mnamiliki sebule moja, chumba cha kulala kimoja na kitanda kimoja, frji moja nk. Unajifunza tabia zake kwa undani, unajifunza nini anapenda na nini anachukia, unajifunza udhaifu wake na uimara wake unajua nini anapenda kwenye TV na zaidi rafiki zake watakuja kwenu upende usipende na kufanya au kuongea mambo yao.
Simu za rafiki zake zitapigwa kwenu, utakuwa domesticated man au domesticated woman.

Unapoishi na mtu mwingine taratibu hubadilika, masuala ya sex yatabadilika kwani utalazimika kufahamu hisia zake kimapenzi mahitaji na kile anapenda siku zote na wewe kuwa mbunifu maana unaye kila siku.

Pia unatakiwa kuripoti kila siku kama utachelewa kurudi nyumbani utalazimika kumwambia mapema. Lazima utambue kwamba sasa utakuwa na mtu ambaye ana hofu na wewe kuchelewa au kutokupata habari zako ndani ya saa 6 mchana na huruhusiwi kwenda kimya hadi sita usiku bila yeye kujua upo wapi na kama ni salama.

Pia kuishi pamoja ni kujifunza kuwa kitu kimoja na usipokuwa makini unaweza kujikuta excitement zote za nyuma zinaisha na maisha yanakuwa tofauti na yale kabla ya kuishi pamoja.
Unahitaji kuwa mbunifu wa namna ya kufanya kila siku inayokuja duniani ili mambo mazuri yanayofanya kila mmoja kuwa excited na mwenzake la sivyo badala ya kuishi kama wapenzi mtaishi kama dada na kaka wanaolala pamoja na ambao moto wa mapenzi umezima.

Friday 4 November 2016

KUACHANA SI SULUHISHO.


Wewe ambaye umeoa au kuolewa na upo unafikiria kuachana na mwenzi wako.

Fikiria upya uamuzi wako.
Fikiria hao watoto mlionao, Fikiria nyakati zote nzuri mlizokuwa nazo pamoja kama mke na mume, Fikiria sehemu tofauti ambazo mlitembelea pamoja, marafiki wazuri mliokuwa nao wote wawili kama mke na mume.
Iepuke talaka kwa gharama zote, sababu zinazokufanya uamue kuachana na huyo mume wako au mke wako zinaweza kuwa ndizo zitakazokuwa sababu mara nyingine tena mbele ya safari kama utaamua kuoa au kuolewa tena.
Sasa unaachana na Jimmy kwa kuwa umechoka na tabia zake za kulewa sana pombe, au kukutaka sex mara nne kwa siku na next time unaweza kujikuta unaachana na John kwa kuwa anakupiga mingumi usiku kucha na yeye sex kwa mwaka mara moja.
Inawezekana unataka kuachana na mary kwa sababu ni msumbufu na anakusema hata kwa vitu vidogo, hata hivyo unaweza kujikuta unaacha na Joyce baadae kwa sababu si mwaminifu katika fedha.
Sasa utaishia wapi na hiyo project ya kuachana na kila unayeoana naye?
Ukiangalia kwa makini kinachobadilika ni tabia na mhusika tu ila wote ni binadamu na binadamu asiye na kasoro bado hajazaliwa hadi leo.


Maisha ni matamu sana kiasi cha kuyapoteza kwa kupeana talaka.
Wanaume wote duniani wanafanana pia wanawake wote duniani wanafanana , na sote ni binadamu.

Wapo wanandoa ni wazembe kiasi ambacho huacha kutumia kila alichonacho kuhakikisha ndoa inarudi kwenye mstari, kukimbilia talaka si jibu bali ni kusukuma tatizo mbele na matokeo yake utakuja kukutana nalo tena mbele ya safari.
Hata kama kuna mtu amekuahidi kwamba ukiachana na huyo uliyenaye basi yeye atakufanya uwe mtu mwenye furaha, hatakuumiza wala kukuacha, ni mwongo na anakudanganya kwani katoka sayari gani na binadamu gani.
Anaonekana anakufaa kwa kuwa huishi naye ukianza kuishi naye utajikuta umeruka mikojo.


Jiulize mwenyewe upya.
Hivi kweli nimetumia uwezo kiasi gani kuhakikisha mwenzi wangu anajua namna tunahitaji kuirudisha ndoa yetu kwenye mapenzi upya kama tulivyoahidiana siku tunaoana?

Je, ni kweli nimefanya kila linalowezekana kusamehe na kusahau?

Je, ni kweli tunataka kuachana na kupeana talaka kwa sababu za msingi?

Kabla ya kuwasiliana na ndugu zako, rafiki zako, washauri wako, wanasheria au wachungaji wako Jaribu kukaa mwenyewe, na mwenzako kujadili upya na kwa upendo namna ya kutatua tatizo lenu na hakuna anayejua shida ya ndoa yako isipokuwa wewe na mwenzi wako.
Usifanye uamuzi wa kuachana kwa haraka ukiamini unaingia kwenye uhuru.
Dawa ya kuachana au talaka ni kusamehe bila masharti.

Thursday 4 August 2016

KWA WANAWAKE MLIO KWENYE NDOA.


Mama mmoja alikuwa anamuogesha mtoto wake wa kiume wa miaka 4 alishangazwa na maelezo ya huyo mtoto pale alipomwambia mama yake
“Mama Unajua nampenda sana mdudu wangu (ka uume kake)”
Huku ameshika na kumuonesha mama yake bila wasiwasi.
Kwa aibu mama yake akaanza kutoa maelezo ya ziada zaidi kuhusiana na anatomy ya mwili wa binadamu kwa kumwambia mtoto
“Ni kweli Mungu ametuumba na ametupa mikono, vidole, magoti, masikio, pua na miguu na kila kiungo kina umuhimu na maana katika mwili”.
Yule mtoto hakujibu chochote wakati mama yake anaongea na baada ya mama kumaliza maelezo yake mtoto akaendelea kusisitiza kwamba
“Lakini mama, bado mimi napenda sana mdudu wangu”

Kuna vitabu vinaeleza kwamba “the man’s best friend is a dog, si kweli, ukweli ni kwamba rafiki wa kweli wa mwanaume ni Uume wake ambaye urafiki (bonding) huanza mapema tangu mtoto.
Na kila siku inayopita duniani ni lazima amshike kwa mikono yake si mara moja tu bali zaidi ya mara moja na si kushika tu bali kumuona kwa macho yake.
Sidhani kama kuna mwanaume ambaye kila akienda “for peeing” huwa hashiki au kuuona Uumr wake.
Uume hufurahia kila siku na kutabasamu kila wakati bila kujali jana au juzi alihudumiwa vipi, kama ni mke au mke mtarajiwa lazima ufahamu kwamba unahitaji kuwa comfortable kuwa naye na si kuwa naye tu bali kumfahamu namna unatakiwa kuhudumiwa ili kumridhisha mume wako.

Hata kama kuna wanawake Wachache ambao siku ya kwanza ya kuona genitals za waume zao hukiri kwamba ni kweli hawajawahi kuona kitu ugliest katika maisha yao kama hapo kwenye residency ya Uume
Hata kama ni kweli ni vizuri kuwa siri yako wewe mwenyewe mwanamke.

Kama mume wako ni kijana wa miaka ya 20+ au 30+ inawezekana Uume wake kila ukikuona half naked au hata kupanda tu kitandani yeye hukuinulia salute kirahisi, ukweli ni kwamba namna mume wako anavyozidi kuongeza umri maana yake utahitaji kazi zaidi ili akupe the same salute haraka haraka.
Pia tukumbuke kwamba wanawake wengi wanapoolewa huwa hawapewi Manual au sexual instructions ya namna ya kuhudumia Uume ni vizuri sana kukumbushana.
Kwa wale wa darasa la kwanza ni vizuri kufahamu kwamba Uume una maeneo tofauti ambayo huwa sensitive kuliko eneo lingine.
Maeneo ambayo upo sensitive ni upande wa chini ya shaft na kichwa, ni vizuri sana kumpa attention ya ziada kwenye michirizi (ridge) ya chini ya kichwa kwani kuna eneo ni sensitive kuliko kawaida kama likihudumiwa vizuri (both manual and orally) kwani ukimpatia unaweza kuona mume wako anaruka na kugonga dali (ceiling).

Uume umezungukwa na sensors za kila aina, stroke tofauti kwenye shaft huweza kumpa mume feelings za ajabu kiasi cha kumfikisha kwenye msisimko wa uhakika. Unapojikita kwenye maeneo ambayo ni more sensitive maana yake anaweza kufika kileleni haraka zaidi. Mwanamke anayefahamu kuhudumia Uume anafahamu namna ya kuufanya Uume kusimama (aroused) bila kumfikisha kileleni.
Jambo la msingi ni kufahamu namna ya kumpandisha hadi karibu na kilele cha mlima na kumrudisha tena ground zero over and over kwa strokes tofauti, touch tofauti, caresses tofauti iwe polepole, haraka haraka, nyepesi au nzito vyote humpa uhondo mume wako.
Kuna wakati mume wako atahitaji direct stimulation na kuna wakati atahitaji indirect stimulation kwani ikienda kinyume chake anaweza kumaliza mapema na wakati mwingine Uume hufanya yale ambayo hakutumwa kama vile kuamua kwenda kulala mapema kabla ya muda.

jambo la msingi ni wewe mke wake kufanya ugunduzi ili kufahamu namna mwili wa mume wako unavyofanya kazi, si mke tu ambaye hufurahia kukunwa mgongo au mguu au kichwani hata mume pia.

Tuesday 2 August 2016

HUWA WAPO TOFAUTI.


Wanaume hufurahia sana kufika kileleni.
Hata kama ni sekunde chache hata hivyo zinalipa zaidi kuliko raha ya hekaheka zote hadi kufika hapo.
Ni kweli kwamba mwanaume na mwanamke ni tofauti sana linapokuja suala la kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa.
Mwanamke anaonekana ndiye mwenye uwezo zaidi wa kuwa na wakati mrefu wa kukaa kileleni na pia ana uwezo wa kujirudia kufika kileleni zaidi ya mara moja.
Pia inaeleweka wazi kwamba ni rahisi sana kwa mwanaume kufika kileleni kuliko mwanamke kwani ni wanawake wengi ambao pamoja na kushiriki tendo la ndoa bado hawajawahi kufika kileleni wakati itakuwa gumzo ikitokea kwamba kuna mwanaume ameshashiriki tendo la ndoa na hajawahi kufika kileleni, hayupo!
Pia mwanamke anao uwezo wa kudhibiti kufika kileleni, hata kama mwanaume ataweza kudhibiti kumaliza mapema (ejaculate) kabla hajafikia point ya no return, hata hivyo akishafika hiyo point hawezi kusimama au kugoma asifike kileleni.
Wakati huohuo mwanamke anaweza kuwa alikuwa kileleni na akasikia mtoto analia, anaweza kuacha na kumhudumia mtoto na kuanza kila kitu upya.
Tofauti nyingine katika kufika kileleni kwa mwanaume na mwanamke ni wakati kwa maana kwamba kwa mfano mume amesafiri kwa wiki mbili kwa ajili ya business, mwili wa mwanamke huweza kujizima kiaina kwa sababu hayupo sexual active na atahitaji muda zaidi kuupasha mwili kuwa tayari kwa sex na hatimaye kufika kileleni.
Mwanaume kwa upande mwingine ni kinyume na mwanamke, kama hakuwa na sex kwa wiki mbili basi mwili wake utajaza risasi za uhakika na siku akikutana na mke wake hatachukua muda kufika kileleni, kwanza ile kumuwaza mke wake tu tayari Uume unaanza kufanya vitu vyake (erections).
Jambo la msingi ni mume na mke kufahamu tofauti zilizopo na kuzifanyia kazi ili kusherehekea kitendo cha kuishi pamoja.

Saturday 30 July 2016

TUWE MAKINI NA KAULI ZETU.


Katika maisha haya tunayoishi, wapo watu wenye tabia ya kutishia wenzao baada ya mizozo mbalimbali.
Yupo anayemtishia mwenzake eti asipoangalia atamuua, mwingine anamtishia kumnyima kitu fulani iwe fedha, chakula na kadhalika.
Kwa wengine matishio wanayotoa ni hasira tu wala hayamaanishi maamuzi ya kweli.
Kwa maneno ya mitaani huwa wanasema ``anamtishia nyau.
Huku wengine wakichukulia matishio mengine ni utani, hebu sikia kisanga hiki ambapo familia imejikuta ikisambaratika kisa mume kamtishia nyau mkewe kwamba atamuacha kama hakuwa makini.
Kisa hiki kanisimulia mama mwenyewe yaliyomkuta ambapo sasa anaishi na mume mwingine na tayari wamezaa mtoto mmoja.
Baba huyu (mume wa pili wa mama huyu), ni mume wa mtu mwenye familia yake inayoishi hapa hapa jijini.
Naam, ilikuwaje? Kwa mujibu wa simulizi ya mama huyu, aliwahi kuolewa na mwanaume mmoja wakazaa watoto wawili, msichana na mvulana. Mama akiwa anakaa nyumbani, huku mume akihangaika na biashara.
Mara kwa mara mume huyu akiwa anamwambia mkewe kuwa iko siku atamwacha.
Tishio hili, kwa mujibu wa mkewe lilikuwa linamkera sana. (hata hivyo binafsi siamini bwana yule alikuwa anasema vile bila sababu.
Lipo jambo ambalo mke huyu alinificha).
Naam. Baada ya mke kutafakari kwa muda, eti akaamua kutafuta chumba sehemu nyingine kwa siri bila mumewe kujua.
Baada ya kukipata, akatafuta mzozo ili apate mwanya wa kuondokea. Huku na huko akamvizia mume akiwa anakula na kumuuliza; hivi hilo tishio kwamba iko siku utaniacha lina maana gani? Mume akahamaki na kusema; unadhani utani? Nitakuacha kweli, wanawake mbona tele, hujui mke mmoja anakinaisha? Maneno hayo kwa mujibu wa mama huyu yalimchefua kweli kweli. Lilizuka zogo la kishoka ambapo (mama aliamua kwenda kulala. Asubuhi mume akaenda kazini kwake hadi jioni.
Huku nyuma mama akafungasha vitu vyake akavipeleka kwenye makao yake mapya, kisha kurejea ili amsubiri mume amuage. Ilikuwa ni kichekesho kitupu.
Bwana kurejea nyumbani alimkuta mke akiwa sebuleni huku kashika tama (mkono shavuni). Mume kuuliza kulikoni ``nilimjibu nimesubiri nikuage, si umekuwa ukiniambia iko siku utaniacha? Sasa hivi naondoka, siwezi kuvumilia kuachwa heri nikuache wewe mapema, watoto wako nakuachia pia japo huyu wa pili ni mdogo, kwa heri ya kuonana? Mpenzi msomaji, hivi ndivyo mama huyu alivyoondoka kwa mumewe kama alivyonisimulia mwenyewe.
Bwana yule hakuamini macho wala masikio yake akabakia ameduwaa asijue la kusema.
Pengine alikuwa akijutia kauli yake ya kumwacha mkewe siku moja. Kwa mujibu wa mama huyu kule makao mapya akatafuta sehemu ya kupikia vyakula (mamantilie) akafanikiwa na ndipo akampata mzee mmoja aliyekuwa mteja wake na katika mazungumzo ya mara kwa mara wakawa wapenzi na sasa mzee huyu amempangishia chumba eneo jirani na anakofanya kazi. Na siku mama huyu ananisimulia kisa hiki walikuwa wote na mzee pamoja na mtoto wao.nilipotaka kujua mume wa awali wa mama huyu yuko wapi niliambiwa tayari alishafariki. Pia mmoja wa watoto (yule mdogo) naye aliugua akafariki ambapo yule mkubwa ameolewa na ameshazaa.
Mwanamama huyu anasema amejaribu kumsaka bintiye huyo bila mafanikio. Yasemekana baba yake kabla ya kuaga dunia aliagiza kuwa mtoto huyo asipewe mamake kutokana na ukatili aliomfanyia wa kumuacha huku bado alikuwa anampenda kwa dhati. Hakika, Maisha Ndivyo yalivyo.
Jamaa alifikiri anatishia nyau kumbe yakawa ni kweli. Kisa hiki kinatukumbusha kuwa makini na kauli tunazotoa midomoni mwetu kwani zingine ni mauti kwetu.
Hata hivyo yawezekana mama na baba wa familia niliyogusia hapo juu, wote walikuwa na matatizo Fulani ambayo hayakuwa dhahiri.
Mume kumtishia kumwacha lazima lipo jambo alilokuwa akifanya mkewe lisilompendeza.
Na mke huyu pengine naye alishamchoka mumewe hivyo kutafuta sababu za kutengana au kuachana.
Huwezi kujua. Nyumba za watu zimeficha mengi.
Utaona baba na mama wakicheka pale wanapokuwa na wageni sebuleni, lakini wakiondoka huo moto unaowaka humo ndani ni balaa tupu. Wengine hawalali chumba kimoja au kitanda kimoja. Wengine tokea wanaingia garini kwenda kazini hadi wanafika hawaongei, hawacheki.
Maisha gani hayo?
Tumrudie Mungu abariki nyumba zetu.
Kwani amri kuu aliyotuachia `upendo tupendane`, tumeiweka kando. Turejeshe upendo ili amani na utulivu vitawale maisha yetu.

Niwatakie Jumapili njema.

JINSI YA KUIJENGA NDOA YAKO.


Kujenga ndoa kuna fanana sana na kujenga jengo lolote kama nyumba tunazoishi.
Kwanza unaanza kwa kuwa na michoro mizuri (plan) na hatimaye unajenga jengo lenyewe.
Ndoa ni mahusiano ya juu sana kwa binadamu ni maamuzi ya ku-share moyo, akili, mwili; vyote kwa pamoja.

Katika kujenga jengo lolote suala la vifaa haliwezi kukwepeka kwani ndivyo husaidia jengo kusimama na ndoa ni hivyo hivyo kuna tools ambazo lazima utumie katika kujenga ndoa imara.

Kabla ya kununua hizo tools za kutumia kujenga ndoa kumbuka kwamba wewe na mwenzi wako wote mpo timu moja na lengo si kushindana kwani hatuhitaji mshindi bali tunahitaji kufanya kazi kama timu.
Ndoa si nani anashinda bali ni wanandoa wote kuelekeza nguvu kusukuma au kuvuta kama kuelekea upande mmoja.
Katika ndoa si lazima ushinde kila mgogoro unapojitokeza na wewe kuwa sahihi kuliko mwenzio bali ni kusaidiana na kumtanguliza mwenzako.

Kifaa cha kwanza ni:-

1. KUWASILIANA.
Ni muhimu kuwa na mwasiliana ya pamoja kila siku. Tunapozungumzia mawasiliano tunaenda katika nyanja zote zinazomuhusu mtu pamoja na kuhusisha milango yote mitano ya fahamu yaanu kuguswa, kunuswa, kusikia, kuonana na kuonja hahaha!
Hapa ni mawasiliano ya kihisia, kiakili, kimwili na kiroho

Kihisia- jitahidi kutiana moyo kati yenu na pia fahamu kwamba katika kuwasiliana ni asilimia 7 tu ni maneno asilimia 93 ni jinsi ya tone ya sauti yako na body language. Jinsi unavyoonekana wakati mwenzako anaongea na sauti yako unavyojibu huwasilisha hisia zako kwa mwenzi wako hivyo uwe makini kuhakikisha humuumizi. Watu wanapanda gari wote kwenda kazini na hawaongei hadi wanafika na hata wakiongea majibu ni mkato tu, kihisia hapo kuna jambo.

Kiakili: -je, kuna gazeti umesoma na kuna kitu kimekufurahisha nawe wataka mwenzi wako ajue?
Mweleze basi. Je, una story yoyote unataka kumsimulia mkeo au mumeo msimulie basi.

Kimwili: -mpe miguso mingi tu ambayo si ile ya chumbani wakati unataka ile kitu. Mkumbatie, mbusu, mshike mkono, unampompa mguso (touch) maana yake unamjali na touch ni hitaji la msingi la binadamu. Kama mnaweza oga pamoja it is so fun and so nice.

Kiroho:- kuna wanandoa wengi husahau kushirikiana katika mambo ya kiroho hata kama wapo imani moja. Unahitaji kumuombea mwenzi wako, na pia unahitaji kuomba pamoja kama wanandoa hii husaidia kuinua mahusiano yenu. Imba pamoja nyimbo za kumsifu Mungu. Soma Neno kwa pamoja na kila mmmoja kushiriki kutafakari.

2. KUBARIKI
Mbariki mwenzi wako kila iitwapo leo.
Anza leo kutoa maneno ya baraka kwa mume wako au mke wako hata kama hukuzaliwa familia ambayo imekuridhisha kumbariki mwenzako.
Mpe sifa anazostahili kwa mambo mazuri anafanya, inawezekana anafanya kazi kwa juhudi, anapika vizuri, anakutunza vizuri, anakupenda, anakuridhisha kitandani, mwambie “asante, nakupenda, pole sana, ubarikiwe, unapendeza nk.
Hata kama wewe ni mgumu mno kutoa neno la baraka basi anza leo kwa neno lolote dogo unaloona mwenzi wako amekufanyia.

3. KUSHIRIKIANA.
Shirikiana mambo mengi katika maisha kwa kadri mnavyoweza.
Kuwa pamoja katika muda, mawazo, kucheza, kutazama TV program pamoja, kikombe cha kahawa au chai pamoja, kusafisha nyumba pamoja, kuendesha baiskeli pamoja., kula chakula sehemu pamoja, kufanya vitu mmoja anapenda pamoja nk.
Mnapotumia muda pamoja husaidia kuwaunganisha zaidi na kuwa kitu kimoja.

Kifaa cha nne ni:-

4.KUITIKIA BILA KULAUMU KWANZA.
Usibishe, itikia kwa kukubali kwanza. Jinsi unavyoitikia kuna elezea zaidi kuliko vitendo wakati mwingine.
Je, kama mume wako au mke wako amechelewa kurudi nyumbani, na hajapiga simu, huwa una respond vipi. Kitu cha msingi si kurukia na kuanza kulaumu bali kwanza kumsikiliza na kujua sababu ni ipi kuliko kulalamika na kuanzisha moto au zogo la nguvu.

"Ndoa haijengwi wa vitu tunavyonunua dukani tu, bali hujengwa kwa upendo kwanza"

Friday 29 July 2016

UWEZO WA UUME UBADILIKA.


Hakuna ubishi kwamba utendaji kimapenzi kwa mwanaume hupungua kufuatana umri unavyoongezeka.

Umri unavyoongezeaka hata kiwango cha homoni za testosterone hupungua na jinsi kiwango cha homoni kinavyopungua mwanaume huchukua muda mrefu kuweza kusisimka na baada ya kusisimka hutumia muda mrefu kusimamisha au kudindisha na si hivyo tu bali hutumia muda mrefu kufika kileleni na kubwa kuliko yote ni kwamba akisha fika kileleni huchukua muda mrefu zaidi kusimamisha tena ili kufika kileleni kwa mara nyingine.
Pia umri huweza kupunguza kiwango cha mbegu anazotoa pamoja na ubora wake.

Pia mwanaume anapozeeka huweza kupunguza uwezo wa utendaji wa kibofu chake cha mkojo, tafiti zinaonesha kwamba mrija wa mkojo huwa dhaifu kadri mwanaume anavyoongezeka umri pia misuli ya kibofu hupunguza uwezo.

Kubwa kuliko zote ni suala la mabadiliko ya uume kadri miaka inavyongezeka na kawaida huwa na mabadiiko makubwa mawili.

Mwonekano (Appearance)

Kichwa cha Uume hubadilika rangi yake kutokana na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenda huko chini.

Pia nywele (pubic hair) huweza kuanza kupotea hii ni kutokana na homoni ya testosterone kupungua.
Kwa hiyo ukifika umri huo usishangae kuwa na massive deforestation au kuota kipara ukaanza kutafuta mchawi nani.

Kimo (size)
Kuongezeka uzito au kujazia eneo la kiuno au chini ya tumbo ni jambo la kawaida kwa mwanaume anapoongezeka umri kwa sababu mafuta hujaa maeneo ya chini ya tumbo (abdomen).
Kadri fat inavyojaa maeneo ya tumbo kwenda chini husabaisha shaft ya uume kujaza fat ambako husababisha urefu wa Uume kupungua.

Pia mwanaume mwenye kitambi (obesity) huweza kuuzika uume wake kwa fat inayokuwa deposited kwenye tumbo lake na anaweza kuongeza urefu wa uume hadi inch moja kama ataamua kupunguza uzito.

Kwa ufupi ni kwamba kama mwanaume mwenye miaka 30 huweza kusimamisha uume wake na kuwa na urefu wa inches 6 basi akifikisha miaka 60 au 70 uume wake unaweza kupungua na kuwa na urefu wa inches 5 ikisimama.

Thursday 28 July 2016

MPE MKEO KILE ANAKIHITAJI.


Kila mwanamke ana sehemu ambazo husisimka zaidi na kupelekea kunyegeka na kuwa na hamu na kutana tendo la ndoa, mwanaume Unahitaji kujua ni sehemu ipi mke wako husisimka zaidi ukizingatia kwamba kila mwanamke ana sehemu yake. Mwanamke mwingine akiguswa viganja vya mikono tu chini analowa kabisa, na mwingine ukigusa matiti mtakosana maana unamuumiza. Mwanaume mtundu katika mapenzi hujua mke wake anasisimka na kuwa hoi akichezewa wapi.
Ukishafahamu ni sehemu ipi na inafanywa vipi ili asisimke basi huna budi kutumia muda wako wa foreplay kumpa bibie tamutamu yake hadi aridhike kwamba ana mwanaume anayemjali na si kurukia tu kule chini na kuanza kuchimba dhahabu bila hata kujua mgodi wenyewe upoje.

UBUNIFU
Wanawake wengi katika ndoa na mahusiano hulalamika sana hasa kutokana na kukosa msisimko wa mapenzi wakati wa faragha. Wanalalamika kwa kuwa wanaume kila siku hutoa kitu kilekile, anakubusu, anakugusa kidogo na akiona chini kumelowa tayari anachomeka kama anapigilia misumari na ikiingia tu anapigilia akiona tayari huyo amemaliza na kuondoka zake.
Wanawake wanapenda surprise na kusisimuliwa katika njia mpya, mwanamke anahitaji kitu kipya baada ya muda, anahitaji sex position mpya, anahitaji busu jipya, anahitaji kunyonywa kupya na anahitaji kusikia neno jipya kwenye masikio yake.
Ni juu yako wewe mwanaume kujifunza mbinu mpya na kuwa mbunifu kitandani, wanaume ndivyo tulivyo tunahitaji kuwa wabunifu, fanya kitu kipya ambacho kitamfanya mwanamke ajisikie ana mwanaume ambaye anazijali na kuzijua hisia zake na hatimaye ndoa itakuwa ni yenye amani sana.

NI MUHIMU KWENU MLIOOLEWA.


Ni vizuri kama mwanamke kufahamu kuwa "Uume"

Mara zote upo tayari, Uume huwa haufuati ratiba (schedule), ukweli Uume haujui hata ratiba ni kitu gani na hufanywa vipi pia Uumr una kumbukumbu ndogo sana.

MFANO:
Wewe na mume wako mlikuwa na wakati mzuri sana usiku wa jana (love making) na kila mmoja aliridhika na kujiona ametosheka. Asubuhi wewe mwanamke unaamka mapema na kuamua kufanya usafi chumbani huku mumeo bado amelala. Unaamua kuvaa tu T-shirt bila bra ndani na katika inama matiti yanaonekana kuchezacheza ndani ya T-shirt uliyovaa kiasi cha kumvutia mumeo ambaye anaamua kuamka na kuja kukupa hug kwa nyuma na unagundua bila shaka kwamba Uume wake umeshaanza kutroti na hauoneshi dalili kwamba umelala.
Unajiuliza
“Tulifanya sex jana usiku tu, sijaoga bado, nimevaa ovyo, hivi mume wangu ana tatizo gani kunitaka tena asubuhi hii yote wakati anafahamu ninafanya kazi?”
Ukiongea na wanandoa ambao huridhishana watakwambia kuna kitu kinaitwa ‘spontaneity or quickies, chapuchapu, kimoja cha haraka nk”
Kwa kuwa mwanaume huvutiwa na kile anaona, ile kumuona mke wake na headlights, au katika chupi yake au akitoka kuoga na khanga yake kwa tukio kama hilo mume anaweza asijali atachelewa kanisani au kazini au mkutanoni kwani anakuwa ameshaigusa trigger na kwake kinachofuata ni kutoa risasi.
Wapo wanawake ambao wameamua kuwapa waume zao sex wiki mfululizo wakiamini kwamba itasaidia kuwafanya waume zao kupunguza uhitaji wa sex hata hivyo wiki inayofuata mume anakuwa na nyege ya juu kuliko wiki iliyopita.
Hawajajua "Mr.Uume" yeye hana tatizo kwani huwa hatunzi kumbukumbu za nini kilitokea jana au wiki iliyopita anachojua yeye ni sasa na anatunza smile lake kila iitwapo leo.
Mwanaume ni mwanaume na atabaki mwanaume na moja ya sifa ya mume ndani ya ndoa ni ule uhitaji wa sex kwa namna ya tofauti.
Kama ulihitaji mtu ambaye atafanya mambo kama unavyohitaji wewe kimapenzi basi ulitakiwa kubaki single, lakini umeoana na mwanaume ambaye ana mahitaji tofauti na wewe na moja ya mahitaji muhimu kwake ni sex.
Pia ieleweke kwamba kuna siku mume anaweza kuamka akiwa na full erections, anaweza kuku-approach na wewe ukakataa, hata hivyo kukataa kwako hakuwezi kupunguza hamu yake ya kukuhitaji wewe kimwili.
Kuna wakati hitaji la sex kwa mwanaume huwa mfano wa kitu cha urgent, anahitaji sexual release, kama ni bunduki yake basi huwa inakuwa ipo loaded na risasi ya mwisho imeshawekwa kwenye chamber, na jicho limeshawekwa kwenye target huku trigger imeshavutwa nyuma ili iweze kuruhusiwa hivyo kukataliwa kwake huwa ni kitu frustrating na hujiona ni loser.

Nikupe Tips za kukuhakikishia wewe mwanamke unakuwa na moto wa mapenzi chumbani.


1.Panga kabajeti kadogo baada ya muda fulani kwa ajili ya kununua kivazi ambacho unaamini ukivaa kinaweza kumvutia mumeo chumbani


2.Angalau kwa mwaka mara moja nenda kwenye social event yoyote na mumeo huku hujavaa chupi, usimwambie mumeo hadi muwe mmeshaondoka nyumbani na mnong’oneze sikioni na mwambie “honey unajua leo sijavaa chupi” utamfanya akuwaze siku nzima huku wewe mwenyewe ukisisimka mara kwa mara ukikumbuka chini ni empty!


3.Baada ya siku kadhaa “have fun” na mumeo chumbani unaweza kuwa naked kwa muda unaotaka wewe kwa ajili ya kufurahia reaction yake inakuwaje.

4.Tafuta aina mpya ya perfume ambayo siku ukijiweka basi ni siku ambayo unakuwa na mahaba ya uhakika na mumeo hivyo basi kila mara ukitaka maana yake unahitaji mahaba pia.

5.Jaribu kitu kipya kimoja baada ya muda fulani kwa ajili ya kumsisimua mume wako.

Wednesday 27 July 2016

KUWA NA UMRI MKUBWA.


Huwezi kugoma kutozeeka, ni muhimu sana kutarajia mabadiliko jifunze kukabiliana na hiyo hali au tarajia mabadiliko kwani mwanamke mwenye umri wa miaka 29 hawezi kuwa sana na mwanamke mwenye miaka 40 na mwanaume mwenye miaka 28 si sawa na mwanaume mwenye miaka 45.
Inawezekana wewe ni mwanaume na umeanza kupoteza nywele kichwani na inawezekana umeanza kujazia uzito wa ziada kwenye tumbo na una kakitambi ka kiana.
Ulizoea kuruka kirahisi sasa ni mzito huwezi kuruka tena, hapo sijakuuliza masuala chumbani na huo uume wako una behave vipi.
Inawezekana wewe ni mwanamke na umri ni kweli unaenda na huamini namna gravitational force inavyokuvuta kila kitu kushuka chini ya sakafu.
Unashangaa matiti yanashuka chini na kulala tofauti na zamani, uso nao unainama na kuweka wrinkles, unashangaa nywele zinakuwa ngumu na kuanza kupotea zenyewe bila taarifa, chini kunagoma kuwa wet hata baada ya kusisimuliwa kama ilivyokuwa kawaida yako kwani kwa maongezi tu kila kitu chini kulijibu.


MABADILIKO YA KIMAPENZI HUWA NI KAWAIDA KWA MWANAUME ANAPOONGEZEKA UMRI.

Kumbuka ulipokuwa teenager (siyo wote) ile kusoma gazeti ambalo ni romantic ulikuwa unasisimka, ile kumpita mwanamke mrembo mwili ulikuwa unasisimka.
Mwanzo wa ndoa yako, ukiona mke wako kapanda kitandani tu ulikuwa unasisimka na kuwa tayari kwa uume wako ulikuwa tayari ushajinyosha na unakugusa ceilings.
Inawezekana kutokana na mwili wako kusisimka kimapenzi haraka kumejenga tabia fulani kwako na kwa mke wako na siku mambo yakiwa tofauti mnaanza kuhaha kudhani kuna tatizo limejitokeza kumbe ni kawaida kwani ni kuongezeka kwa umri.
Inawezekana hata namna ya kuandaana ilikuwa ni one sided kwa maana kwamba mwanaume ndiye alikuwa anasisimuliwa kwa muda mrefu zaidi na mwanamke kwa muda mfupi.
Sasa umri umeongezeka na usipoandaliwa vizuri unaweza kujikuta uume unabaki soft muda wote bila kuleta mabadiliko yoyote kama kawaida yake.
Maana yake mwanaume anapoongezeka umri anahitaji direct penile stimulation kuliko zamani.
Ukweli ni kwamba mwanaume anapokuwa kijana hadi kuwa mzee ni mfano wa godoro jipya, ukilinunua huwa gumu na baada ya miaka kadhaa utaona kasheshe yake.
Pia mwanaume anapoongezeka umri anaweza kushangaa anamaliza sex bila kukojoa (ejaculate) kitu ambacho haikuwa kawaida yake, kwani older men kawaida hawahitaji kufika kileleni kama young men.
Hata hivyo hiyo ina faida kwa mwanamke kwani sasa mwanaume anaweza kufika mbali katika kumridhisha mke wake ndiyo maana umri unavyoongezeka mwanaume huwa mzuri zaidi kimapenzi.
Kama ni mwanamke Kumbuka kwamba si kushindwa kwako kama ukiona mume wako wa 40+ amemaliza nusu saa bila kufika kileleni, wala haina maana kwamba humvutii au hupendeza bali ni kuonesha kwamba mwili wake unazeeka.
Inawezekana ilikuwa kawaida yake akimaliza mara ya kwanza baada ya dakika 2 au 3 anaweza kurudi na kuanza upya kukupa mahaba wewe mke wake na sasa hawezi tena.

Monday 11 July 2016

WANATOFAUTIANA KTK SUALA LA KUFIKA KILELENI.


*Je, kufika kileleni kwa mwanamke anapofanya mapenzi ni tofauti na mwanaume?

Tafiti nyingi zimefanyika na mojawapo ni ile iliyoruhusu Wanawake na wanaume wote kuandika vile wanajisikia wanapofika kileleni na baadae wakaruhusu watu wengine wasome na wapendekeze nani ameandika kati ya mwanamke au mwanaume hata hivyo ilikuwa vigumu kwa wasomaji kufahamu maelezo yaliyoandikwa yameandikwa na mwanaume au mwanamke.
Hii ina maana kufika kileleni kwa mwanaume na mwanamke huhusisha uzoefu unaofanana.
Hata hivyo kuna tofauti ya uzoefu wa kufika kileleni kwa Wanawake na hata mwanamke mmoja na hii tofauti hutokana na aina ya kusisimuliwa ili kufika kileleni kuanzia kisimi, uke, G-spot, matiti n.k

*Je, ni kweli kwamba kinachomfikisha kileleni mwanamke huyu ni tofauti na mwanamke yule?


Ni kweli, na pia hata mwanamke huyo mmoja kinachomfanya asisimuliwe kufika kileleni leo ni tofauti na wiki ijayo na mwezi ujao na hata miaka matano au kumi ijayo.
Wapo wanaopenda kusisimuliwa G-spot na wengine hawataki, wapo wanaopenda kusisimuliwa kisimi wengine hakuna lolote, wapo wanaopenda kusisimuliwa uke na wengine hawataki. Wengine matiti au masikio au shingo nk kila mmoja au hata huyo mmoja uliyenaye anatofautiana kutokana na mzunguko wake wa siku kwa mwezi.
Kama tunavyopenda vyakula tofauti na nguo tofauti na usisimuliwe wapi kwa mwanamke kufika kileleni ni tofauti.
Kuamini kwamba kumsisimua mwanamke Mahali fulani ndipo huweza kumfikisha kileleni bila kuwasiliana naye wakati mwingine huweza kuwa kero.

*Je, mazoezi ya kukaza misuli ya uke huweza kuongeza uwezekano wa mwanamke kufika kileleni kirahisi?

Mazoezi hayo ni muhimu mno. Uwezo na uimara wa misuli ya PC (puboccoccygeus) unahusiana mno na mwanamke kufika au kufurahia tendo la ndoa.
Wanawake ambao hawawezi kufika kileleni kirahisi wana misuli ya PC iliyodhaifu (loose).
Mwanamke anayeweza kufika kileleni kwa kusisimuliwa kisimi ana misuli imara hata hivyo mwenye misuli imara zaidi ni yule anayeweza kufika kileleni kirahisi kwa uke wake.


Wanawake huwa na tofauti za kufika kileleni kutokana na aina ya kusisimuliwa pamoja na sababu zingine kama vile anavyojisikia huo wakati, na kiwango cha homoni.
Si suala la kubonyeza button na mwanamke akafika kileleni. Kufika kileleni si conditioned reflex.
Mara nyingi lengo la mume katika sex ni kuhakikisha mke anafika kileleni je kuna tatizo kuwa na mtazamo kama huo?
Kawaida tunapozungumzia maisha huwezi kukwepa kuweka malengo.
Linapokuja suala la sex ni kweli kwamba wanaume huwa goal-directed na Wanawake huwa pleasure-directed.
Tatizo huja pale watu wameshindwa kufahamu hiyo siri na hasa wanaposhindwa kuwasiliana na wapenzi wao.
Mwanamke anaweza kufika kileleni kwa kusisimuliwa sehemu zingine za mwili kama vile masikio nk hivyo bila kuwasiliana inaweza kuleta shida kwani we are all unique.

FANYA JITIHADA KUIFANYA NDOA YAKO KUWA MPYA.


Baada ya muda katika ndoa kila kitu kinaweza kuwa katika ratiba isiyobadirika, huwa vilevile, routine, predictable, uniform, sare jana juzi, leo na kesho maongezi ni yaleyale, ratiba ya kuwa mwili mmoja ni vilevile hakuna kipya na hakuna raha.

Inawezekana hawa wewe msomaji kile kinachotokea kwenye ndoa yako kinakupa wakati mgumu na unajiuliza hivi nitaishi bila kuridhika kiasi hiki hadi lini.

Hata hivyo kabla hujaanza kumlaumu partner wako ni vizuri ukajiuliza maswali yafuatayo huku ukitafakari kwa undani wewe mwenyewe bila kumnyoshea mwingine kidole

Hivi wakati mnachumbiana (let say dating) ni vitu gani ulikuwa unavifanya ili huyu partner wao aonekane yeye ni special kwako?

Je, hapa karibuni au wiki hii umefanya kitu gani kwa partner wako aonekane yeye ni special?

Je, unakumbuka ni kitu gani na lini mmekuwa pamoja na mmefanya kitu special na mkawa na wakati mzuri nje ya hapo nyumbani mnapoishi?

Je, ni mara ngapi mnakuwa wote kufanya kile kila mmoja anakifurahia kufanya?

Ukiulizwa utaje vitu vitano ambavyo partner wako anavipenda au anaviona vya maana sana katika maisha yake na kujisikia vizuri katika maisha unaweza kutaja? Na je umehusika vipi kuhakikisha anavipata?

Je, mume wako au mke wako yupo namba ngapi kwenye list yako ya vitu vya thamani duniani?
Haya maswali yakipata majibu yake inaweza kuwa njia sahihi kwako kuanza kutengeneza mahusiano yenye direction mpya kuelekea furaha na amani.
Najua mtu yeyote akikuuliza je, unampenda huyo partner wako jibu utakalo toa ni “ndiyo nampenda” hata hivyo ulivyo busy na kazi na watoto na kazi zingine ni dhahiri kwamba humpendi na kama unampenda basi hujaweka efforts zinazotakiwa.
Ni kweli hivyo vitu ni muhimu sana hata hivyo ndoa ni zaidi ya vyote, hata kama umekuwa unasema nitafanya hivyo karibuni hata hivyo karibuni yako sasa ni mwaka hakuna kitu.

Wakati uliokubalika ni sasa, sasa ni wakati wa kuwekeza kiasi cha kutosha kwa partner wako, na utatakiwa kurekebisha ratiba yako ili partner wako aingizwe kiuhakika katika ratiba yako ngumu.

Ukweli ni kwamba hata watoto hufurahia kuwa na wazazi wanaopendana kuliko wao kufurahia kuchezea gitaa linalotoa sauti nzuri au kufunga goli anapopelekwa na mzazi kucheza soka kuliko wazazi ambao hawapendani ndani ya nyumba.

Ndoa yako ni muhimu sana, na mke wako au mume wako ni muhimu sana kumbuka Mungu aliumba ndoa, kabla ya kazi na kabla ya watoto.

Saturday 9 July 2016

NI MWENZI WAKO,KUWA HURU NAE.


Kuongea suala la tendo la ndoa katika ndoa au kwa mume wako au kwa mke wako ni moja ya topic ngumu sana chini ya jua au katika uso wa dunia.
Kama utakuwa na maongezi au mawasiliano kuhusiana na suala la sex katika ndoa yako maana yake mtakuwa wazuri katika hiyo department.
Wanandoa wengi ambao wamekuwa na tabia ya kuongea kuhusu maisha yao ya sex kwa uhuru na ukweli wamekuwa na maisha mazuri chumbani kwao kwani si rahisi kufahamu mwenzako anahitaji kitu gani hadi umwambie.
Kuwa wakimya kuhusiana na kuongea kuhusu sex na mke wako au mume wako husaidia kuwa wajinga zaidi na wakati mwingine kutoridhishana sawa na uhitaji wa mwili wako au feelings zako.
Hatari kubwa zaidi ni pale wanandoa wanaposhindwa kuongea wenyewe na matokeo yake kutoridhika na kutoridhika ndiko husaidia kukwetua njia ya mmoja au wote kuanza kuangalia nje (kuchepuka)
Firikia wewe ni mwanamke una vitu mume wako akifanya basi huwa unajisikia kusisimka na mwili kuanza kutoa kuwa juicy na kutamani sana sex na mume wako.
Kwa nini usiwe huru ukamwambia kwamba unapenda iwe hivi:

Mueleze:-

WAKATI NIMESISIMKA
Natamani mume wangu uwe na wewe unatoa sauti au na wewe uwe unaongea,

Napenda uwe unaongea maneno matamu ya kimapenzi,

Napenda mume wangu uniambie nini unakipenda kwenye mwili wangu,

Napenda unigunise na kunichezea namna hii (onesha),

Napenda ufanye hivi kwenye chuchu na matiti yangu,

Napenda unitazame usoni,

Napenda unichezee kisimi namna hii (mwambie unapenda afanye kwa kutumia nini na namna gani)

Napenda ufanye hivi kwenye G- spot,

Napenda kuchezea uume wako hivi nk

WAKATI WA SEX
Napenda na wewe uwe unaguna na kutoa sauti za kimahaba au uongee maneno matamu na elezea namna unafurahia au unajisikia kuwa ndani yangu,

Napenda uendelee kunibusu namna hii,

Endelea kusisimua kisimi changu namna hii (eleza kwa kutumia nini)

Natamani tunapoanza tuanze kwa mlalo huu na baadae tumalize kwa mlalo (love making position) hii,

Natamani uanze kwa kasi au msuguano wa polepole na baadae haraka zaidi namna hii,

Nioneshe kama na wewe unafurahia,
Nk

UNAPOFIKA KILELENI
Napenda upunguze kasi na kuniacha au napenda uongeze kasi unapoona nakaribia kufika kileleni,

Napenda unikumbatie na kunibusu nk

BAADA YA KUMALIZA SEX
Napenda sana uendelee kubaki ndani yangu hadi tulale usingizi nk,

Napenda unikumbatie huku tunalala,

Napenda angalau mkono wako au mikono yako ibaki mwili mwangu huku tunalala,

Natamani tuendelee kupiga story,

Natamani uendelee kunibusu.
Kumbuka huu ni mwongozo tu kwani kila mwanamke ana mahitaji yake kutoka kwa mume wake jambo la msingi ni kwamba jisikie huru kuongea na mume wako nini unahitaji kabla, wakati na baada ya sex.

Friday 8 July 2016

FANYA HAYA KUMVUTIA MWENZI WAKO.


Wengi huwa wanajiuliza “nifanyeje ili mwenzangu awe na hamu au nimvutie?” ingawa unapenda sana mume wako awe na hamu na wewe jambo la msingi ni wewe kukaa chini kwanza na kujichunguza vile unajiona na kujisikia wewe mwenyewe.
Wewe mwenyewe unajionaje, unajiamini vipi na unavyovutia, unavyopendeza? kwani kama wewe mwenyewe hujioni unavutia basi inakuwa ngumu sana mume wako kuona unavutia.
Mahusiano mazuri kimapenzi na mume wako hayaji tu kwa kuwa mnakaa pamoja bali kwanza wewe mwenyewe unajisikiaje au unajiamini vipi kuhusiana na mwonekano wako.
Hatua inayofuata ni wewe na yeye kuanza kuongea pamoja kuhusiana na suala la mahusiano ya kimapenzi katika ndoa yenu.
Ni kawaida kwa wanandoa kuwa na up na downs zinazohusiana na tendo la ndoa hata hivyo kunapokuwa na ukame wa kimapenzi au ukaribu wa kimapenzi ni muhimu kwa wanandoa wenyewe kukaa chini na kuanza kujadili wapi pamepungua au kitu gani kinakosekana na si kuanza kulaumiana bali kila mmoja kuwa wazi kuelezea na kusema kile anahitaji katika mahusiano ili moto wa mapenzi urudi tena.

Je, kama mwanamke, unahitaji mume kuwa karibu na wewe kwa kukubusu mara kwa mara ua kukukumbatia mara kwa mara?

Je, unahitaji kushikwa mikono au mwili wako na mume wako mara kwa mara?

Je, kuna migogoro nje ya chumbani au kutokuelewana au una hasira kutokana mambo fulani fulani kitu kinachofanya mume wako kuwa mbali na wewe kihisia?
Nk
Ukijiuliza hayo maswali na mengine na kukaa na mume wako kujadili mnaweza kufika Mahali kila mmoja akafahamu nini wajibu wake ili kurudisha moto wa mapenzi chumbani kwenu.
Mawasiliano yaliyo wazi na yanayomruhusu kila mmoja kusema kile anahitaji ndiyo njia sahihi ya kurudisha ukaribu wa kimapenzi upya katika ndoa.
Baada ya kufahamu hatua tatizo lipo wapi weka plan na kuanza kufanyia kazi na hakikisha kila mmoja anakuwa positive kwa mwenzake bila kulaumiana.
SWALI

Ndoa yetu ina miaka 4 na tunafanya tendo la ndoa mara moja kwa miezi mwili. Kila siku usiku mume wangu husema kwamba amechoka na hawezi tendo la ndoa kwa kuwa alikuwa na siku ngumu hata hivyo nafahamu aina ya kazi alikuwa nazo mchana kwa kuwa tunafanya kazi pamoja.
Kinachonishangaza ni kwamba anasisimka sana akimuona mwanamke mtaani hasa kama anavutia.
Ninachojiuliza kwa nini mara zote anasema amechoka kwangu na je nifanyeje ili awe na hamu na avutiwe na mimi?
Mama B

Thursday 23 June 2016

MAHUSIANO BAADA YA USALITI.


Baada ya affair kutokea au kugundulika huwa ni wakati mgumu kwa wanandoa; jambo la msingi ni kwamba kuaminiana kulikoyeyuka huweza kurudi hasa baada ya hasira kwisha na wanandoa kuanza kuwa karibu kihisia tena.
Hii hutokea tu na pale tu kama wahusika wameelezana na kufahamu sababu za kwa nini affair ilitokea.
Ukweli ni kwamba kuelezea sababu za kwa nini affair ilitokea ni moja ya jambo gumu sana na pia ni moja ya jambo muhimu sana katika kuiponya ndoa.
Ni muhimu kujua sababu za affair kwa kuwa kama wewe ni uliyesalitiwa na mwenzako utatakiwa kujifunza kwa mapana yote kwa nini mwenzako alichepuka (affair) ili kuweza kurudisha ukaribu wa kimapenzi na kuaminiana upya.
Kama wewe ndiye umesaliti ni vizuri kuelezea sababu za kuchepuka kwako kwa sababu ndicho mwenzako anapenda kufahamu.
Kujua sababu za affair ni kuchambua au kuweka wazi sababu zilizofanya mwingine achepuke.
Ili kufahamu vizuri maana ya kwa nini affair ilitokea hebu tujaribu kuweka suala la affair katika ndoa kama vile nyumba inavyoingiliwa na majambazi usiku.

Baada ya nyumba kuvunjwa ni muhimu kuchunguza nini kilifanya majambazi kuvunja na kuingia kuiba kirahisi, ni mianya ipi ilisababisha hao wezi kuvunja na kuingia kirahisi?
Je, tatizo ni majirani hatari?
Na je, ulichukua hatua gani kujilinda na hao majirani ambao wamesaidia kuwapa majambazi data au siri na namna ya kuvunja na kuingia katika nyumba yako?
Je, uliwaona watu wageni ambao walikuwa wanapita karibu na nyumba na hukutilia maanani na ukaona ni jambo la kawaida?
Je, nyumba yako haikuwa na milango ya uhakika?

Kuingiliwa na majambazi na kuibiwa haina maana kwamba unawajibika na tabia mbaya za wale majambazi.
Hata hivyo ukihamia nyumba nyingine utajisikia secured kama utafahamu sababu zilizofanya majambazi kupata mwanya wa kuvunja na kuingia kukuibia nyumba yako ya kwanza.
Hutakuwa na uhakika wa usalama wako kuibiwa na majambazi kama hutafahamu sababu zilizofanya uibiwe mara ya kwanza.
Trust na usalama wa kuwa karibu kimapenzi katika ndoa umeharibiwa na mwenzako ambaye amekusaliti, kama majambazi walivyoingia na kuvunja nyumba na kuiba, hutakuwa salama hadi ujue sababu zilizochangia.
Au inawezekana mmoja wenu alikuwa na urafiki na mtu wa nje ambaye alikuwa hana heshima na ndoa yenu.
Pia inawezekana kulikuwa na dalili za mwenzako kutoka nje na wewe ukapuuzia. Inawezekana hakukuwa na ukaribu wa kimapenzi kati yenu na hiyo ikatoa mwanya kwa yeye kuvutiwa kihisia na mtu wa nje.
Inawezekana kuzozana kwenu kila siku kumefanya muwe mbali kimapenzi na kihisia hivyo kutoa mwanya kwa mwingine kutoka nje.
Inawezekana mmoja alikuwa hamheshimu mwenzake na alipopata anayemheshimu nje akaishia kuchepuka.
Inawezekana kulikuwa na ukame wa tendo la ndoa ndani ya ndoa yenu na mwingine akajikuta anapenda kutuliza kiu nje.
Au inawezekana ni shetani tu.............................
Ukishajua sababu basi inakuwa rahisi kubadilisha mambo na si wanandoa wote huwa tayari kukubaliana na hizi changamoto.

Wednesday 22 June 2016

NI VIZURI KUZINGATIA KWANZA..


Inakuwaje watu wawili waliopendana deep idara zote inafika siku wanakuwa baridi na wanajiona ni watu wawili tofauti kabisa kwenye ndoa yao?

Kuna mambo mengi sana husababisha kuanzia na yale yaliyo ndani ya ndoa yao na yale yaliyo nje ya ndoa yao hata hivyo ukweli love is so terrible and is so important, kuna wakati mwingine mpenzi (mke au mume) anaweza kukupa au kukunulia gari au kukujengea nyumba ya uhakika lakini bado ikawa haina maana kama hatatimiza mambo ya msingi kuhusiana na upendo wake kwako.

Ndiyo unakuja ule usemi
“Buying very expensive gifts doesn’t make woman happy but real love and affections”

Kuna aina tofauti za migogoro na jinsi ya kukabiliana nayo, wengine mgogoro ukizuka hata majirani wanajua leo kuna vita kati ya Mr na Mrs wake na baada ya muda wanarudi kwenye mstari. Wengine vita vyao huwa slow, kimya kimya, hakuna kelele ni cold war na kila mmoja huanza mbali na mwenzake kihisia, kiroho na kimwili polepole ila matokeo yake ni hatari tupu.

Kama ni mwanandoa mpya ni vizuri kuwa makini katika maamuzi mbalimbali mnayofanya na kufikiria kwa makini huku ukiangalia zaidi ya miaka 5 ijayo, kwa mfano;

Jerry na Judy wameamua baada ya kuoana tu wanazaa mtoto haraka iwezekanavyo kwa kuwa kila mmoja ana kazi hivyo shida ipo wapi kama pesa zipo. (Ingawa ukweli pesa huwa hazitatui matatizo yote)

Hata hivyo uamuzi wa kuwa na mtoto haraka kabla hawajajuana vizuri na kufikia mahali wakawa wanafahamiana tofauti na uchumba ni jambo la msingi. (siyo lazima ukubali huu ushauri kwani inatokana mmejuana kiasi gani na mchumba wako)

Kuna watoto wakizaliwa huja na package ambayo mzazi hulali kama vile kulia (cry) muda wote na mke kumtumikia huyo mtoto all the time (acha ile ya kumaliza madaktari wote kujua kwa nini mtoto analia usiku mzima na wanakwambia hakuna tatizo) na kufikia mahali mume akawekwa pembeni kwani mtoto kwanza na wakati huohuo ndoa bado changa.

Mke hujikuta mtoto anamuhitaji na mume anamuhitaji na hawawezi kubalance kwani bado ni mgeni na hii institution.


Watoto wengine huwa na matatizo ya kula, kiasi kwamba mama hujikuta hawezi hata kumwachia mtu yeyote amtunzie mtoto na matokeo yake mama hujikuta muda wote anatumikia mtoto na wakati mwingine kuacha kazi (ajira) na pia mume kuwekwa pembeni.

Matokeo yake wanandoa hujikuta wanakuwa mbali na feelings kufa na kila mmoja anaanza kuona ndoa hairidhishi wakati hata miaka 2 haijamaliza.

Jambo la msingi ni mwanamke kufahamu vizuri aina ya mume uliyenaye kwani kuna wanaume ambao wanaweza kuwa baba na kuna wengine ni kazi, wanaendana na usemi kwamba:

“Men don’t become fathers overnight, where as women have strong maternal instinct in them”

Suala la kule mtoto linahitaji mke na mume wote kushirikiana kuhakikisha si mmoja ndiye anakuwa na mzigo zaidi.

Tuesday 21 June 2016

KUPENDELEA MTOTO MMOJA ZAIDI YA WENGINE.


Tabia ya kumpendelea mtoto mmoja au kila mzazi kuwa na mtoto wake ambaye anagusa zaidi moyo wake ipo sana katika familia zetu.Wengi huwa hawataki kulitaja au kuliongelea kwa undani ingawa ni kweli familia nyingi zitakiri kwamba hili ni tatizo sugu na pia inawezekana wewe ni mmoja ya watoto waliopendwa au ambao hawakupendwa na moja ya wazazi wenu.

1.Kwa nini upendeleo hutokea kwa mtoto mmoja?

Inawezekana tabia ya huyo mtoto ni njema zaidi kuliko wengine, wakipewa kazi mmoja anafanya na mwingine hafanyi mara zote, anayetii hujikuta anapendwa zaidi.
Inawezekana tabia ya huyo mtoto ni rahisi na mwenzake au wenzake ni ngumu.
Inawezekana mtoto anafanana na mzazi zaidi kuliko wengine (tabia na mwonekano).
Inawezekana huyo mtoto anafanikisha matarajio ya wazazi wake au mzazi mmoja.

Inawezekana kwa sababu ni mvulana peke yake au msichana peke yake mzazi hujikuta anampenda zaidi.
Pia inawezekana talents zake au vipaji vyake vinafanana na vile mzazi anataka mtoto awe au inawezekana ndiyo values za familia.
Pia inawezekana mtoto asiyependwa ni mtoto ambaye ni mbishi au ni mtoa hamasa (challenge authority) kuliko mwenzake au wenzake. Mtoto ana njia zake au mitazamo yake kuhusu maisha na vitu hivyo wazazi au mzazi hujikutana wanabishana kila kitu.

Pia kuna mazingira ya kuzaliwa ambayo hufanya mtoto kupendelewa zaidi ya wenzake kama vile mtoto kuzaliwa siku au wakati (huohuo) ambao mzazi wa baba au mama (babu au bibi) yake anafariki, ingawa haina ushahidi wa kisayansi ila matukio mengi huonesha kwamba mtoto wa aina hii huonekana wa thamani kuliko wengine na ni kama vile roho ya babu au bibi huenda kwa mtoto anayezaliwa na wazazi kujikuta wanampenda kuliko kawaida.
Au inaweza kuwa ngumu sana mzazi kuweka bond na huyo mtoto kutokana na huzuni, stress na depression mzazi alipata wakati anazaa na wakati huohuo mzazi wake mwenyewe (baba au mama) naye anafariki.

Mtoto kuzaliwa bila kutegemea hasa baada ya wazazi kudhani wamemaliza kuzaa.
Mtoto kuwa na matatizo ya afya hivyo wazazi kutumia muda mwingi kwake na wengine kujiona mwenzao anapendelewa.
Wakati mwingine inatokea tu mzazi hujikuta anampenda mtoto fulani katika familia kuliko wengine.

2. Nini mojawapo ya Dalili za mtoto kupendelewa?

Kununuliwa zawadi zaidi ya wenzake.
Kutoa adhabu rahisi kuliko wenzake kwa kosa moja, wenzake wanakula fimbo yeye anaonywa tu.
Sherehe au sikukuu zake kuwa tofauti na wenzake kwa jinsi zinavyoandaliwa nk.
Wenzake wakiomba kitu hichohicho wanakataliwa lakini yeye anapewa au kuruhusiwa.
Mzazi kutumia jina lake kumaanisha watoto wake wote kama vile baba anarudi kazini na watoto hawapo na mtoto anayempenda anaitwa Ben na badala ya kuuliza watoto wapo wapi yeye anauliza “akina Ben wako wapi?”

Tumia muda mwingi na mtoto mmoja.
Kuonesha upendo wa dhahiri kwa mtoto mmoja nk nk nk.

3.Je, mtoto ambaye anajisikia hapendelewi na mzazi au wazazi hujisikiaje?

Mtoto anakuwa na wakati mgumu sana kujikubali na kujipenda mwenyewe kwa kuwa anaamini mzazi/wazazi hawampendi na anaweza kuwa na tatizo sugu la kutojiamini (chronic low self-esteem)
Mtoto hujiona duniani hakuna haki na kwa kuwa hatendewi haki na yeye anaweza kuanza kutowatendea haki wengine.

4.Je, mtoto anayependwa anaweza kupata madhara yoyote?

Ukweli ni kwamba hata mtoto ambaye anajiona anapendwa pia anaweza kupata tatizo la kukosa kujiamini kwani anakuwa too much spoiled.
Kwa kuwa anapendwa basi atajitahidi kufanya zaidi kwani anaamini asipofanya kila kitu juu anaweza kupoteza kuendelea kupata upendeleo hivyo kama ni shule atajitahidi kupata grades za juu, kama ni tabia atajitahidi asikasirike nk na matokeo yake atakuwa hajiamini na anaweza kupota msongo mawazo.

Mtoto anayependelewa anaweza kuwa si mzuri sana linapokuja suala la wenzake wa rika moja au walimu au watu wengine kwenye maisha kwani kile kitendo cha kujiona anapendelewa na wazazi au mzazi humpa kakiburi Fulani.

Mtoto anayependwa hujiona yeye ndo mzuri na huwa hakosei hata hivyo maisha hayako hivyo na matokeo yake atakuwa na wakati mgumu mbele ya maisha hasa llikija suala la kupambana na matatizo.

Hasara ya kumpendelea mtoto mmoja huendelea hadi kwa wajukuu na inaweza kuleta matatizo na migogoro kwa kuwa wajukuu wa watoto wote huanza kuzozana kwa kuwa mmoja wa wazazi wao alikuwa anapendwa zaidi na babu au bibi.


5.Je, kwa mume na mke ni tatizo?

Ndiyo kunaweza kutokea mgogoro kati ya mke na mume hasa kwa mtoto mmoja kupendelewa na mzazi mmoja, kwa mfano baba anampa fedha nyingi zaidi mtoto mmoja anayempenda bila kujali ni mdogo kuliko wenzake, mama akiona au kusikia naye huja juuu kitendo ambacho kitafanya ndoa iwe katika mzozo.

6.Je, unaweza kuepuka vipi kumpendelea mtoto mmoja?

Kwanza wewe mzazi jikubali kwamba wewe ni binadamu na kwamba katika watoto wako mmoja anakubalika kwako zaidi kuliko wengine.
Wasikilize watoto wengine ambao wanakwambia unampendelea mwenzao na usijilinde, wasikilize na anza kufanyia kazi yale wanasema (kuacha kumpendelea mmoja)

Gundua utofauti wa kila mtoto na kile anapenda kufanya (characteristics, skills, interest) na mhudumie kutokana na vile anavipenda.

Usiwalinganishe au kumsema mmoja kwa sababu ya mwingine kwani kila mtoto yupo tofauti, sentensi kama “mwenzako Ben akirudi shule anafanya homework yake vizuri na anamaliza wewe hadi ulazimishwe!”
Ni kweli amekosea hata hivyo kila mtoto yupo tofauti na kila mtoto anatakiwa kuambiwa kama yeye na si mwingine.
Kama unanunua zawadi ni vizuri kununua zawadi zinazolingana siyo mmoja unanunua zawadi ya Tsh. 100,000 na mwingine Tsh. 20,000
Tumia muda vizuri na sawa kwa watoto wote.

Kumbuka jinsi unavyozidi kuwa na watoto wengi ndivyo utakuwa na kibarua kigumu zaidi, kwani unahitaji kutafuta muda maalumu kwa kila mtoto na kugundua kipaji chake na kuhakikisha unakiendeleza sawa na watoto wengine.

Jambo la msingi ni kila mzazi kumpa (treat) kila mtoto sawa katika hali zote na juhudi za ziada zinahitaji katika mazingira ya nyumbani kuhakikisha watoto wote wanalelewa sawa na kila mmoja kujiona ana thamani sawa kwa wazazi mmoja mmoja na kwa pamoja.

Thursday 16 June 2016

NDOA IMARA NA ZINAZODUMU.


Ukiona kosa moja kwa mke wako au mume wako, hutakiwa kuliangalia na kuliwekea sura kamili au hutakiwi kulipa uhai badala yake lipe jina na liweke kando kwa kujaribu kulinganisha na uzuri wake au mambo matano mazuri kuhusu yeye(positive traits).


Kwa mfano unajikuta mume wako au mke wako amewaka hasira kwa jambo dogo tu hadi unahisi dunia umebadili mwelekeo, hata hivyo badala ya kuanza kufikiria hizo hasira zake Unachotakiwa kufanya ni kujiambia mwenyewe kwamba:

“ Ni kweli ana hasira hata hivyo ni mwanamke/mwanaume anayenijali, anayenipenda, anayewajibika, ni mbunifu na anajua kuniridhisha chumbani”.

Kumbuka strongest relationships ni zile ambazo partners wanaweza kujenga picha ya uzuri wa mwenzake (idealized/illusioned) kuhusu uwezo wake na si udhaifu.


Kwa kuufuta udhaifu au kuondoa mawazo kuhusu udhaifu wake na kuweka uwezo wake au uimara wake unahusanisha information muhimu za kufanya mke wako au mume wako awe mzuri zaidi na ukampenda zaidi.

Kwa miaka zaidi ya 100 hekima na busara iliyodumu na ambayo hata wengine wanaamini ni ile kwamba kinyume cha uzuri ni ubaya.

Hii ina maana kwamba Ukitaka kujua uzuri wa kitu basi unatafuta ubaya wake kwanza.

Ukitaka kujua furaha ni kitu gani au ina thamani kiasi gani unajaribu kumchunguza mtu mwenye huzuni kwanza.

Watoto ambao wanatumia madawa ya kulevya hutumika kujua namna ya kuwalinda watoto wasiotumia madawa ya kulevya wasijiingize kwenye hivyo vitendo.


Watoto ambao ni watoro shuleni hutumika kujifunza kuwafanya watoto wengine wawe na mahudhurio mazuri.


Linapokuja suala la ndoa si kweli kwamba ili kujifunza ndoa kuwa nzuri au kusiwe na talaka basi ni vizuri kujifunza ndoa ovyo au ndoa ambazo zimeishia kwenye talaka.

“Bad is not always the opposite of good”

Ukweli ni kwamba linapokuja suala la ndoa Ukitaka kujenga ndoa nzuri au imara unahitaji kujifunza kutoka ndoa imara na si ndoa ovyo au zile zimeishia kwenye talaka.

Vitu vinavyopatikana kwenye ndoa imara havina uhusiano na vitu vilivyosababisha ndoa ovyo kuwa ovyo kwani ndoa imara zina siri yake ambayo si kinyume cha ndoa ovyo.


Ndoa imara ni zile ambazo mwanandoa mmoja au wote huwa na picha kamili ya mwenzi wake, huwa na sifa ambazo amezijenga kwa mwenzi wake ambazo ukweli ni kwamba inawezekana kwamba mwenzi wake hana ila yeye huamini anazo na ni kuwa positive kwamba anamfaa.

Ndoa imara na zinazodumu ni zile ambazo mwanandoa huamini katika uimara au uwezo wa mke wake au mume wake hata kama huo uwezo hana.

Unaweza kuona kama ni utani au contradiction hata hivyo ndio ukweli.

Nina amini mke wangu ni caring, nina amini mke wangu ni sweetie, nina amini mke wangu ananifaa, nina amini mke wangu ni mzuri, nina amini mke wangu ni mchapa kazi, nina amini mke wangu ni mrembo, nina amini mke wangu ananifaa hata kama hizo sifa hana kwa kuwa naamini basi ninavyoamini ndivyo itakuwa na nitakuwa na furaha kuliko kuwaza vinginevyo.

NI VIZURI KUWA WAZI.


Kawaida linapokuja suala la mapenzi opposite attract na the same repel kwa maana kwamba mara nyingi huwa tunavutiwa na strength za mwingine kwa kuwa hufanana na weakness zetu.
Watu ambao hutuvutia sana ni wale ambao huonesha strength katika maeneo ambayo sisi tupo weak.

Ukikutana na mtu wa jinsia tofauti na wewe na mkawa pamoja kwa muda mrefu pamoja na ukavutwa kutokana na strength zake ambazo zinakubaliana kwenye weakness zako penzi huzaliwa na baadae inaweza kuwa ndoa

Ndoa ni kuwekana wazi.

Wakati Bwana harusi na Bibi harusi wanaposimama mbele ya Mhubiri kanisani na kutoa ahadi zao kwa Mungu na wageni wote walioalikwa huwa wanaahidiana kwamba
“Ninakuahidi kukupenda na kukunyenyekea kwa muda wote wa uhai wetu”
Hii ina maana kwamba maharusi huwa wanakazia kwamba kwa kuwa nakubali kiapo chako na unyenyekevu wako kwangu leo basi nitajifunua kwako mzimamzima kuanzia sasa si kimwili tu bali kisaikolojia pia kwani hadi hapa nimejidhihirisha/nimejifunua kwako katika upande ule wa mazuri tu (strength) kuhusu mimi.
Sasa kwa kuwa tunaoana nitajiweka wazi kwako mzimamzima na nina imani kubwa na wewe kwamba utaendelea kunipenda kama nilivyo.

Ndoa ni kuwekana wazi, ni kila mmoja kujidhihirisha kwa mwenzake kama alivyo pamoja na weaknesses zake.
Vitu vyote ambavyo vilikuwa vimejificha wakati wa uchumba hadi honeymoon basi kuanza kwa ndoa vyote huwa mezani juu kwa kila mmoja kuona.
Na hapo ndipo kwenye mtihani wa kwanza wa wanandoa wapya.
Honeymoon siyo residence ya kudumu ya ndoa, baada ya honeymoon (na wengine hata wakati wa honeymoon) wanandoa wapya hushikwa na mshangao wa partner anavyobadilika na kuwa kama mwingine kabisa.
Ukweli ni kwamba unapoona partner wako anaonekana kama mwingine tofauti na yule wa wakati wa uchumba, ukweli ni kwamba sasa matching inaanza, kufahamiana kikwelikweli kunaanza na wenye hekima na busara huwa makini katika kukabiliana na hizo tofauti na kuendelea kusherehekea hizo tofauti kwa upendo na kuvumiliana kwani huwezi kumbadilisha na kumbadilisha ni kupoteza muda wako.

LOVE MAY BE BLIND BUT MARRIAGE IS A REAL EYE-OPENER.

Wednesday 15 June 2016

TOFAUTI HUWA HAZIKOSEKANI.


Wanandoa imara au waliofanikiwa katika ndoa yao ni wale ambao wanaweza kukaa pamoja na kujadili tofauti zao katika namna ambayo huwezesha kujenga ukaribu kimapenzi (intimacy) zaidi.

Wanafahamu jinsi ya kukubaliana na kutokukubaliana, wanafahamu namna ya kuhakikisha kutokukubaliana hakusababishi maafa kwenye maeneo mengine ya mahusiano yao.

Si kweli kwamba tunaolewa au kuona ili kuchukuliana katika migogoro hata hivyo kutofahamu namna ya kupambana na migogoro huweza kusababisha kutofanya vizuri katika mambo mengine ambayo ndo sababu za kuoana.

Kukwepa migogoro au kukwepa kuongea pamoja eti kunaweza sababisha mgogoro mzito si hekima wala busara kwani njia bora ni kuwa wazi kuongea pamoja ili kujadili tofauti au kutokuelewana kunakojitokeza ili wanandoa waweze kufahamiana zaidi.

Kwa lugha nyingine si rahisi mke kufahamu mume anapenda chakula gani bila kuongea kwanza, pia haina maana kukaa kimya kwa kuwa mke anapika chakula usichopenda basi atabadilisha na kukupikia chakula unapenda. Si rahisi mume kukupeleka outing kama hamuongei.

Wapo wanandoa ili kuepuka migogoro huacha kuongea na kuwa kimya, ni muhimu sana wanandoa kufahamu utafiti wa ndoa imara unasemaje.
Kila ndoa imara kwa wastani ina maeneo 10 ambayo wanandoa hawafanani au hawawezi kukubaliana au kwa lugha nyingine hawataweza kufikia muafaka maishani mwao.

Kwa nini hizi ndoa imara pamoja na tofauti 10 na bado zinaitwa ndoa imara?

Jambo la msingi au siri kubwa ni kwamba wanandoa wanafahamu namna ya kukabiliana na hizo tofauti na kuishi nazo, kupendana pamoja na kutofautiana na zaidi kila mmoja anamuelewa mwenzake na kukubaliana kihisia na kuchukua nafasi yake kama ni yeye.

Wanandoa imara hufurahia na kusherehekea tofauti zao na hufarijika kwa kuwa sasa anamfahamu mwenzake, anajua eneo ambalo wapo tofauti then wanaaendelea kupendana huku kila mmoja akifahamu namna ya kukabiliana na hizo tofauti.

Hawa wanandoa imara wanafahamu wazi kabisa kwamba hata kama watabadilisha partners bado watapata matatizo mapya katika maeneo ya kutokukubaliana, kuwa tofauti na kwa huzuni kubwa kazi kubwa itakuwa ni mizigo waliyotoka nayo kwenye ndoa zao za kwanza kama vile watoto nk ndiyo maana kwao talaka haina sauti wala nguvu na huwa haizungumzwi, ni neno lililofutwa katika maongezi.
Zaidi ya kukabiliana na tofauti na kutokukubaliana pia ni muhimu sana kusherehekea/kumbatia (embrace) mabadiliko.
Wakati tunaoana huwa tunaahidi kukaa pamoja hadi kifo kitakapo tutenganisha hata hivyo huwa hatuahidi kubaki vilevile bila mabadiliko yoyote, tunahitaji kukua, kuongezeka skills, kwa wabunifu na wazuri zaidi kila siku zinavyozidi kwenda.
Kuna mambo mengi tunaweza kujifunza kadri ziku zinavyozidi kwenda kama vile kusema asante, kuomba msamaha.
Hivyo inawezekana kujifunza tabia njema ambazo zinaweza kujenga ndoa na kuziacha tabia mbaya ambazo zinaweza kuharibu ndoa.

MTAZAMO WAKO UKOJE?


Huwezi kuongelewa mapenzi bila kutaja suala la pesa. Wapo watu ambao wanaamini kuwa na pesa nyingi, nyingi kabisa za kutosha husaidia pesa kuwa imara na linaloridhisha.
Hata hivyo tumeona penzi la uhakika hata wakati pesa zikiwa hazipo au tumeona penzi la kweli hata katikati ya umaskini uliokithiri.
Hii haina maana kwamba pesa siyo muhimu, pesa ni muhimu sana. Na pesa ina umuhimu kwa kila mahusiano hata, hivyo inabidi ujiulize mwenyewe je, upo kwa ajili ya pesa au kwa ajili ya penzi la kweli.
Utakuwa mtu wa maana sana kama utakuwa unatazama na kuwekeza kwenye penzi la kweli na si pesa.
Pia ni vizuri kuwa makini na mtazamo wa mpenzi wako je yupo kwako kwa ajili ya pesa au kwa ajili ya penzi la kweli.
Mtazamo wake kuhusu pesa ni muhimu sana.

Saturday 11 June 2016

TABIA HIZI WAKATI MWINGINE ZINAKERA KTK NDOA.


Kuna wakati mwanandoa mmoja anajikuta yupo ndani ya ganda la yai kwa maana kwamba anajikuta anakabiliana na mke au mume ambaye anadhibiti, anayeamulisha, anapenda ufyate ulimi, anakukalia kooni, huna hiari yako na anakusimamia kila kitu.


Judy ni mmoja ya wanawake ambao wanatabia ya kufanya auditing hadi chumbani.

Kwanza mumewe huambiwa asahau tendo la ndoa siku za wiki (weekdays), labda Ijumaa usiku au Jumamosi usiku, pia watoto lazima wawe wamelala dakika 90 zilizopita na wawe kweli wamelala fofofo kwa kukaguliwa zaidi ya mara tatu na kuthibitisha kwamba kweli wamelala folilo kabla ya wao kuingia kwenye sita kwa sita.


Mume wake lazima ahakikishe ameoga kwa dakika 30, ahakikishe ametumia sabuni, kitamba (washcloth) na kupiga mswaki, akitumia dakika pungufu ya hizo lazima ataambiwa hajaoga akawa safi (amelipua) hivyo hawezi kupata unyumba (kama una hasira hapa nyumba haitoshi).

Pia mume anatakiwa ahakikishe anatandika taulo sehemu ambayo yeye Judy atalala wakati wa tendo la ndoa kitu kinachofanya eneo la kufanyia mapenzi kuwa dogo.


Anatakiwa kuhakikisha taa zimezimwa wakati wa tendo la ndoa na wanaenda kulala kabla ya saa nne usiku siku ya kupeana unyumba.

Pia kunatakiwa kusiwe na sauti ya binadamu au kitu chochote ndani ya mita 500 vinginevyo hakuna unyumba.

Ni kweli ni muhimu sana binadamu kuwa na taratibu lakini taratibu zingine badala ya kuwajenga wanandoa huwabomoa na kuwa vipande vipanda ambavyo kuvirudisha inakuwa ngumu maradufu.


Mume wa Judy itafika siku atasema “enough is enough”


Jeffy ni mwanaume ambaye kwake kila kitu ni utaratibu, akikwambia anapiga simu saa mbili kamili ni kweli atakupigia saa mbili kamili. Akikwambia atakuwa mahali fulani saa fulani, count him there. Jumamosi anakata majani kuzunguka nyumba yake na Jumapili jioni anaosha gari lake, kwa ufupi shughuli zake zinafanywa kwa mtindo wa saa.


Likija suala la tendo la ndoa na mke wake basi utaratibu wake ni kila baada ya siku tano, penda usipende mwanamke awe anataka au hataki period.

Kutokana na tabia za controlling wapo wanaume wamefanya wanawake kujisikia baridi kali mwilini kila mlango ukigongwa mume anapofika nyumbani kutoka kazini na kumfanya mwanamke kuwa turned off ile jioni na usiku mzima.


Hapa haijalishi umesoma au hujasoma, upo smart au ovyo, tajiri au maskini, kumbuka skills zinazokufanya ufanikiwe kazini kwako wakati mwingine ndo skills zinazofanya ushindwe masuala la chumbani kwako na mke wako au mume wako.

Tabia za kudhibiti na kutaka kila kitu kufanyika kwa umakini wa kupindukia (Control & Perfection) wakati mwingine huharibu mapenzi na ndoa badala ya kujenga.

ANA MTAZAMO GANI KUHUSU PESA?


Watu tunatofautiana katika mitazamo kuhusu fedha, baadhi huiangalia fedha kwa jicho la kutoa (giving) na wengine kwa jicho la kuitunza (saving) na wengine kutumia (spending)

Kama wewe ni kijana wa kiume au kike ambaye upo katika harakati za kusaka mwenzi wa maisha basi ni muhimu sana kuwa na makubaliano au kufahamu mtazamo wa huyo mtarajiwa kuhusu fedha.


Judy ni mwanamke ambaye mume wake Jeffy akipata mshahara huamuriwa akabidhiwe na anachofanya ni kugawa zile pesa na kuziweka kwenye bahasha tofauti tofauti, bahasha moja kwa ajili ya kununua chakula, bahasha nyingine usafiri, nyingine pango la nyumba, nyingine kununua nguo na nyingine sadaka kanisani na nyingine kwa ajili ya dharura.


Mume akitumia pesa kutoka moja ya bahasha lazima aeleze ni bahasha ipi alichukua pesa, na amefanyia kitu gani, na risiti ziko wapi na change zipo wapi na duka gani alienda kununua na alikuwa na nani na ametumia usafiri gani na amelipa kiasi gani.

Jeffy hujikuta oppressed, frustrated na hawezi kuvumilia tena!


Je, unadhani hiyo ndoa itadumu kwa muda gani?


Kumbuka wengine hutumia pesa kama emotional agenda, kama kwenye huo mfano bahasha za Judy si bahasha tu bali ni mfuko anaotumia ku-mcontrol Jeffy.

Kuna watu walitembelea ndoa moja na ilikuwa ni summer time na joto lilikuwa limepanda nyuzi 40 centigrade.

Ikafika mahali watu wakawa wana sweat utadhani wapo ndani ya sauna wakati huohuo nyumba ilikuwa na viyoyozi vya uhakika ila vimezimwa kwa utaratibu kwamba hadi ifike tarehe iliyowekwa ndipo huwashwa.

Wanandoa walipoulizwa kwa nini kuzima wakati joto linatuua, wakawajibu tarehe tuliyoweka kuwasha viyoyozi haijafika bado na kuwasha sasa ni matumizi mabaya ya pesa.

Hawa wanandoa wanafurahia ndoa yao kwa kuwa wanamtazamo sawa kuhusu fedha na hakuna kulemba!

Kuna wanawake ambao kwao fedha za mume ni za familia, na pesa zake ni zake.

Hii ilitokea kwa Suzy na Simon wakati fulani ambapo Suzy alikuwa anafanya kazi na Simon naye alikuwa anafanya kazi.

Simon akipata mshahara, Suzy humkomalia na kupanga bajeti namna ya kutumia hizo fedha kwani anachojua ni kwamba mshahara wa mume ni wa familia na mshahara wake ni kwa ajili yake tu.

Hata Simon alipotaka kununua kitu kutokana na ule mshahara basi Suzy huja juu kwa kuanza kutoa lecture kwa Simon namna watoto wanavyohitaji nguo na vifaa vingine wakati huohuo yeye Suzy pesa anayopata kazini kwake anaila kisirisiri.

Mitazamo kama hii huweza kuharibu ndoa kwa kasi ya ajabu kama dhoruba.

Angalia kwa makini yule unategemea kuwa mke au mume anazielewaje fedha kama unaona mtazamo wake ni wa ajabu ajabu ushauri wangu ni kwamba fikiria kwa makini kabla ya kuchukua uamuzi wa kuwa naye.

NI KUJIDANGANYA.


Kuna usemi mmoja wa kingereza unaosema:

“Someone is better than no one”

Kwa maana kwamba wapo watu ambao (hasa wanawake wale ambao wanaona muda unaenda bila kuwa na mchumba au mpenzi wa kuwa naye katika maisha) huamua kushikana na bora mwanaume kwa imani kwamba ni heri kuwa na huyo mmoja (unfaithful, untrustworthy) kuliko kutokuwa na mwanaume yeyote.


Subiri kidogo nikwambie!

Kujiingiza kwa mwanaume ambaye moyo wako hauko radhi eti kwa sababu unataka na wewe uonekane una mpenzi au una mchumba au una mume ni kuumiza hisia zako.

Hata kama unaamini utafanikisha matakwa yako bila kuunganishwa emotionally, intellectually au affectionally utaishia kuumizwa.


Pia huyo someone ambaye unaona ni afadhari kuliko kuwa mwenyewe ni looser ambaye anakuzuia wewe kumpata anayefaa, kwa lugha nyingine huwezi kumpata mwanaume mwenye sifa njema kama utaendelea kukaa au kushikamana na huyo someone wako ambaye hata hivyo ana sifa ovyo.

Wengi wanajuta kwa sababu ya kuamini kwamba "someone is better than no one, hata hivyo waliokiri kwamba "no one is better than a relationship that lack respect" wanapeta.