Tuesday 18 August 2015

ZINGATIA HAYA ILI UWE NA NDOA IMARA

FUNGUO ZA KUJENGA NDOA IMARA NA MAHUSIANO YA KUDUMU


USIKAE NA DONGE MOYONI

Kitu kizito kuliko vyote kukibena duniani ni DONGE MOYONI.

Pia unaweza kuathirika zaidi na kile umeweka moyoni kwani mwenzako anaweza kuwa hajui.

Kuweka vitu moyoni bila kuvitoa au kuzungumza na mwenzi wako huweza kuathiri afya na amani.


Kawaida kama una hasira hakikisha unazimaliza mapema na kuelewana na mwenzi wako kabla jua halijazama na kama ni usiku hakikisha unaenda kulala huku umeshalitoa donge lako.

FAHAMU KWAMBA HONEYMOON SIYO MAISHA YA NDOA

Kuna tofauti kubwa kati uchumba, Honeymoon na maisha ya ndoa, uchumba na Honeymoon hupewa moto kemikali ambazo zimo ndani yetu. Hatua ya pili ambayo ni ndoa yenyewe hapa tairi linakutana na barabara ili kuweka wazi uimara na udhaifu. Katika ndoa ni majukumu na kuwajibika na familia iliyoanzishwa, wakati uchumba na Honeymoon ni kuburudishana.

MUNGU KWANZA
Kumweka Mungu kwanza katika ndoa, huleta furaha ya kweli (joy) faraja na ulinzi. Kumweka Mungu kwanza maana yake mume na mke wanaishi kwa utii na amri za Mungu mwanzilishi wa ndoa wanaomba pamoja na kuwa na mahusiano yanayoongozwa na Mungu. Kwa vipimo vya kibinadamu huwezi kuwa na furaha siku zote kwa safari ndefu kama ya ndoa furaha ya kweli hupatikana kwa kumuweka Mungu namba moja.



MFAHAMU MWENZI WAKO NA KUJIFAHAMU WEWE MWENYEWE

Baada ya mapenzi ya Honeymoon kwisha wanandoa huwa na mgodi wa kuanza kuchunguzana na kufahamiana. Wakiwa Honeymoon wanandoa huona kila kitu shwari, wakianza maisha ya ndoa kila mmoja huanza kuona makosa kwa mwenzake hata Kirusiyo hiyo ni nafasi ya wanandoa kufahamiana ni nafasi nzuri ya wanandoa kusifiana, kutumia muda pamoja, kupeana zawadi, kusaidiana kazi ndogo ndogo za nyumbani, kubusiana na kukumbatiana (touch)


KUWA MSIKILIZAJI MZURI

Binadamu ana asili ya kupenda kuongea zaidi kuliko kusikiliza, kusikiliza kuna maana zaidi kuliko kuongea, wanaume Huongea ili kitu kifanyike na mwanamke Huongea kuchangia wazo na hisia zake. Kuna wakati kila mwanandoa anahitaji kusikilizwa wanaume ni vizuri kuwasikiliza wake zao wanapotoa mawazo yao na hisia zao. Mwanamke huongea maneno 45 elfu kwa siku, na mwanaume 15 elfu, ni nani anahitaji kusikilizwa zaidi?


KICHEKO

Wanandoa wanahitaji kuwa na kicheko siyo kuwa serious kila wakati kutaniana kusikopitilizwa huongeza furaha katika ndoa pia ni zawadi kutoka kwa Mungu. Wanandoa ni muhimu kuwa na wakati ambapo wanaweza kukaa pamoja na kuwa na kicheko iwe ni kuangalia TV na kusimuliana hadithi ambazo zinawafanya mcheke ni vizuri wanandoa kucheka wakiwa wao wenyewe au wakiwa pamoja na watu wengine. Kicheko huleta raha katika ndoa.


JIFUNZE KUKUBALI KWAMBA UMEKOSA NA KUOMBA MSAMAHA

Binadamu wote tunafanya makosa na wakati mwingine hayo makosa huumiza tunaowapenda. Lazima tukumbuke wakati tumekosa tunahitaji tuombe msamaha. Usizunguke (indirect way) bali be straight sema “Nisamehe au I am sorry”. Pia usibadili topic au kuanza kusifia ili usiombe msamaha.


Pia tunahitaji kufahamu kwamba wenzi wetu si mara zote wapo perfect kama ulivyo wewe (imperfect).

Pia ni vizuri kufahamu kwamba ndoa ni kazi inayoendelea na siyo mwisho wa safari.


MHESHIMU, USIMDHARAU

Kumdharau mwenzi wako wakati mwingine huwa kitu rahisi sana. Mwanzo wa mapenzi hata kama kuna hitilafu mara nyingi huitilii maanani, una minimize, lakini baada ya honeymoon kwisha utaona na kukumbuka/ Tambua mambo mengi ambayo huyapendi na unaweza kuanza kupambana nayo na kumdharau mwenzi wako.

Kumdharau mwenzi wako ni kama mmomonyoko ambao ni sumu kwenye mahusiano.

Mwanandoa mwenye busara hawezi kumuaibisha mwenzi wake bali ataongea kwa hekima na kumaliza tofauti zozote kwa upendo.

Kawaida angalia uwezo wake na si udhaifu wake.


USICHUJE (filtering)

Usimchekeche na kumbandika jina la kudumu kwamba mara zote yupo vile:

Sentensi zinazoanza na haya maneno uwe makini sana
Kila siku unafanya KirusiiKirusii…………………..

Mara zote nakwambia lakini………………

You never……………………

You always……………………

Mara nyingi Ukitokea msuguano wengi huanza kulalama kwa kutumia hayo maneno huwa na maana kwamba unafanya the same mistake over and over na anakupa hicho kibandiko kama jina la mkosaji wa kila siku.

Si kweli kwamba unaweza kufanya makosa yaleyale kila siku, muda wote miaka yote.


WEKA MKAZO KWENYE UWEZO NA SI UDHAIFU

Mwanamke na mwanaume wapo tofauti siku zote na ni mpango wa Mungu kuwa tofauti ili kwa tofauti tuweze kusherehekea uumbaji wa Mungu na ili mke na mume waweze kila mmoja kumridhisha mwenzake.

Huwezi kuwa na mwenzi ambaye ana udhaifu mwingi kuliko uwezo na ukiona ana udhaifu mwingi kuliko uwezo basi tatizo ni wewe si yeye.

SEMA NAE..!!

Kuongea suala la tendo la ndoa (sex) katika ndoa au kwa mume wako au kwa mke wako ni moja ya topic ngumu sana chini ya jua au katika uso wa dunia.
Kama utakuwa na maongezi au mawasiliano kuhusiana na suala la sex katika ndoa yako maana yake mtakuwa wazuri katika hiyo department.
Wanandoa wengi ambao wamekuwa na tabia ya kuongea kuhusu maisha yao ya sex kwa uhuru na ukweli wamekuwa na maisha mazuri chumbani kwako kwani si rahisi kufahamu mwenzako anahitaji kitu gani hadi umwambie.
Kuwa wakimya kuhusiana na kuongea kuhusu sex na mke wako au mume wako husaidia kuwa wajinga zaidi na wakati mwingine kutoridhishana sawa na uhitaji wa mwili wako au feelings zako.
Hatari kubwa zaidi ni pale wanandoa wanaposhindwa kuongea wenyewe na matokeo yake kutoridhika na kutoridhika ndiko husaidia kukwetua njia ya mmoja au wote kuanza kuangalia nje (kuchepuka)
Firikia wewe ni mwanamke una vitu mume wako akifanya basi huwa unajisikia kusisimka na mwili kuanza kutoa kuwa juicy na kutamani sana sex na mume wako.
Kwa nini usiwe huru ukamwambia kwamba unapenda iwe hivi:
Mwambie!

WAKATI NIMESISIMKA
Natamani mume wangu uwe na wewe unatoa sauti au na wewe uwe unaongea,
Napenda uwe unaongea maneno matamu ya kimapenzi,
Napenda mume wangu nini unakipenda kwenye mwili wangu,
Napenda uniguse (touch) na kunichezea namna hii (onesha),
Napenda ufanye hivi kwenye chuchu na matiti yangu,
Napenda unitazame usoni,
Napenda unichezee kisimi namna hii (mwambie unapenda afanye kwa kutumia nini na namna gani)
Napenda ufanye hivi kwenye G- spot,
Napenda kuchezea uume wako hivi nk

WAKATI WA SEX
Napenda na wewe uwe unaguna na kutoa sauti za kimahaba au uongee maneno matamu na elezea namna unafurahia au unajisikia kuwa ndani yangu,
Napenda uendelee kunibusu namna hii,
Endelea kusisimua kisimi changu namna hii (eleza kwa kutumia nini)
Natamani tunapoanza tuanze kwa mlalo huu na baadae tumalize kwa mlalo (love making position) hii,
Natamani uanze kwa kasi au msuguano wa polepole na baadae haraka zaidi namna hii,
Nioneshe kama na wewe unafurahia,
Nk

UNAPOFIKA KILELENI
Napenda upunguze kasi na kuniacha au napenda uongeze kasi unapoona nakaribia kufika kileleni,
Napenda unikumbatie na kunibusu nk

BAADA YA KUMALIZA SEX
Napenda sana uendelee kubaki ndani yangu hadi tulale usingizi nk,
Napenda unikumbatie huku tunalala,
Napenda angalau mkono wako au mikono yako ibaki mwili mwangu huku tunalala,
Natamani tuendelee kupiga story,
Natamani uendelee kunibusu.
Kumbuka huu ni mwongozo tu kwani kila mwanamke ana mahitaji yake kutoka kwa mume wake jambo la msingi ni kwamba jisikia huru kuongea na mume wako nini unahitaji kabla, wakati na baada ya sex.
Usisubiri eti utafaidi sana sex baada ya kumaliza kusomesha watoto au hadi mfanikiwe maisha au hadi umalize miradi Unafanya kwani itafika Mahali utakuwa na pesa na muda ila energy huna.

NI KUWEKANA WAZI TU.

Kawaida linapokuja suala la mapenzi opposite attract na the same repel kwa maana kwamba mara nyingi huwa tunavutiwa na strength za mwingine kwa kuwa hufanana na weakness zetu.
Watu ambao hutuvutia sana ni wale ambao huonesha strength katika maeneo ambayo sisi tupo weak.
Ukikutana na mtu wa jinsia tofauti na wewe na mkawa pamoja kwa muda mrefu pamoja na ukavutwa kutokana na strength zake ambazo zinakubaliana kwenye weakness zako penzi huzaliwa na baadae inaweza kuwa ndoa.

Ndoa ni kuwekana wazi.
Wakati Bwana harusi na Bibi harusi wanaposimama mbele ya Mhubiri kanisani na kutoa ahadi zao kwa Mungu na wageni wote walioalikwa huwa wanaahidiana kwamba
“Ninakuahidi kukupenda na kukunyenyekea kwa muda wote wa uhai wetu”

Hii ina maana kwamba maharusi huwa wanakazia kwamba kwa kuwa nakubali kiapo chako na unyenyekevu wako kwangu leo basi nitajifunua kwako mzimamzima kuanzia sasa si kimwili tu bali kisaikolojia pia kwani hadi hapa nimejidhihirisha/nimejifunua kwako katika upande ule wa mazuri tu (strength) kuhusu mimi.
Sasa kwa kuwa tunaoana nitajiweka wazi kwako mzimamzima na nina imani kubwa na wewe kwamba utaendelea kunipenda kama nilivyo.
Ndoa ni kuwekana wazi, ni kila mmoja kujidhihirisha kwa mwenzake kama alivyo pamoja na weaknesses zake.
Vitu vyote ambavyo vilikuwa vimejificha wakati wa uchumba hadi honeymoon basi kuanza kwa ndoa vyote huwa mezani juu kwa kila mmoja kuona.
Na hapo ndipo kwenye mtihani wa kwanza wa wanandoa wapya.
Honeymoon siyo residence ya kudumu ya ndoa, baada ya honeymoon (na wengine hata wakati wa honeymoon) wanandoa wapya hushikwa na mshangao wa partner anavyobadilika na kuwa kama mwingine kabisa.
Ukweli ni kwamba unapoona partner wako anaonekana kama mwingine tofauti na yule wa wakati wa uchumba, ukweli ni kwamba sasa matching inaanza, kufahamiana kikwelikweli kunaanza na wenye hekima na busara huwa makini katika kukabiliana na hizo tofauti na kuendelea kusherehekea hizo tofauti kwa upendo na kuvumiliana kwani huwezi kumbadilisha na kumbadilisha ni kupoteza muda wako.

JE,STYLE IPI NI NZURI?

Linapokuja suala la mwanamke kupata mimba (ujauzito) kuna mijadala mingi ipo kuhusiana na mlalo upi unafaa kwa ajili ya kutengeneza mtoto.
Hata hivyo hakuna mlalo ambao unajulikana au kushauriwa kwamba ndio unafaa duniani hata hivyo kuna maswali mengi ambayo huhusiana na suala zima la tendo la ndoa na kupata mimba.

Je, Baadhi ya milalo ni bora zaidi ya mingine linapokuja suala la kupata mimba?

ingawa kumekuwa na utafiti mdogo kuhusiana na hili suala bado utafiti umekuwa unaonesha kile hutokea wakati wa tendo la ndoa.
Katika zote missionary position (Mwanaume juu mwanamke chini huku wakiangaliana) inaonekana ndiyo inatoa uwezekano mkubwa zaidi kwa kuwa husaidia kuwa na deep penetration kuzihakikishia sperms zaidi ya mlango wa uzazi (womb).
Pia mwanamke kuingiliwa kwa nyuma (rear entry) huwezesha positioning ya sperms vizuri kama missionary position.

Je, kama mwanamke natakiwa kulala na si vinginevyo ili kupata mimba?

Wanasayansi wanasema ili kuondoa uwezekano wa sperms kushindwa kuogelea kutokana na gravity hasa mwanamke anapokuwa amekaa au simama juu ya mwanaume. Kama sperms zina afya hakuna tatizo ingawa kama sperms hazina afya mwanamke anashauriwa kulala wakati wa tendo la ndoa au hata baada ya tendo la ndoa ili sperms kufikia target.

Je kuna muhimu wowote kufika kileleni ili kupata mimba?

Ni dhahiri kwamba mwanaume ni vizuri afike kileleni (mshindo) katika process ya “baby making” ili kuhakikisha anazipa sperms speed inayotakiwa kufika kwenye target. Utafiti wa karibuni unaonesha pia mwanamke ni vizuri afike kileleni ikiwezekana wakati mmoja na mume wake kwani contractions zinapotokea husaidia sperms kufikia mji wa uzazi.

Je, kama ninataka mtoto wa kike au kiume mlalo gani unafaa?

Suala la milalo halina uhusiano na jinsia ya mtoto bali timing na frequency ndiyo muhimu kwa kusababisha jinsia ya mtoto.

KUNA TOFAUTI...!!

Wanandoa imara au waliofanikiwa katika ndoa yao ni wale ambao wanaweza kukaa pamoja na kujadili tofauti zao katika namna ambayo huwezesha kujenga ukaribu kimapenzi (intimacy) zaidi.

Wanafahamu jinsi ya kukubaliana na kutokukubaliana (disagreements), wanafahamu namna ya kuhakikisha kutokukubaliana hakusababishi maafa kwenye maeneo mengine ya mahusiano yao.
Si kweli kwamba tunaolewa au kuona ili kuchukuliana katika migogoro hata hivyo kutofahamu namna ya kupambana na migogoro huweza kusababisha kutofanya vizuri katika mambo mengine ambayo ndo sababu za kuoana.

Kukwepa migogoro au kukwepa kuongea pamoja eti kunaweza sababisha mgogoro mzito si hekima wala busara kwani njia bora ni kuwa wazi kuongea pamoja ili kujadili tofauti au kutokuelewana kunakojitokeza ili wanandoa waweze kufahamiana zaidi.

Kwa lugha nyingine si rahisi mke kufahamu mume anapenda chakula gani bila kuongea kwanza, pia haina maana kukaa kimya kwa kuwa mke anapika chakula usichopenda basi atabadilisha na kukupikia chakula unapenda. Si rahisi mume kukupeleka outing kama hamuongei.

Wapo wanandoa ili kuepuka migogoro huacha kuongea na kuwa kimya, ni muhimu sana wanandoa kufahamu utafiti wa ndoa imara unasemaje.
Kila ndoa imara kwa wastani ina maeneo 10 ambayo wanandoa hawafanani au hawawezi kukubaliana au kwa lugha nyingine hawataweza kufikia muafaka maishani mwao.

Kwa nini hizi ndoa imara pamoja na tofauti 10 na bado zinaitwa ndoa imara?
Jambo la msingi au siri kubwa ni kwamba wanandoa wanafahamu namna ya kukabiliana na hizo tofauti na kuishi nazo, kupendana pamoja na kutofautiana na zaidi kila mmoja anamuelewa mwenzake na kukubaliana kihisia na kuchukua nafasi yake kama ni yeye.

Wanandoa imara hufurahia na kusherehekea tofauti zao na hufarijika kwa kuwa sasa anamfahamu mwenzake, anajua eneo ambalo wapo tofauti then wanaaendelea kupendana huku kila mmoja akifahamu namna ya kukabiliana na hizo tofauti.

Hawa wanandoa imara wanafahamu wazi kabisa kwamba hata kama watabadilisha partners bado watapata matatizo mapya katika maeneo ya kutokukubaliana, kuwa tofauti na kwa huzuni kubwa kazi kubwa itakuwa ni mizigo waliyotoka nayo kwenye ndoa zao za kwanza kama vile watoto nk ndiyo maana kwao talaka haina sauti wala nguvu na huwa haizungumzwi, ni neno lililofutwa katika maongezi.
Zaidi ya kukabiliana na tofauti na kutokukubaliana pia ni muhimu sana kusherehekea/kumbatia mabadiliko.
Wakati tunaoana huwa tunaahidi kukaa pamoja hadi kifo kitakapo tutenganisha hata hivyo huwa hatuahidi kubaki vilevile bila mabadiliko yoyote, tunahitaji kukua, kuongezeka skills, kwa wabunifu na wazuri zaidi kila siku zinavyozidi kwenda.
Kuna mambo mengi tunaweza kujifunza kadri ziku zinavyozidi kwenda kama vile kusema asante, kuomba msamaha.
Hivyo inawezekana kujifunza tabia njema ambazo zinaweza kujenga ndoa na kuziacha tabia mbaya ambazo zinaweza kuharibu ndoa.

MTIMIZIE HITAJI LAKE..

Kazi si kuoana kazi ni kutimiziana mahitaji bila kuchoka!

Ndoa ni kazi.
Inayochukua muda, jitihada na commitment na wakati mwingine huhitaji professional counselling.
Kama umefika Mahali ambapo wewe na mume wako au mke wako hamuwezi hata kuwasiliana bila kuvurugana na umeanza kufikiria kuachana kama njia bora zaidi basi unahitaji msaada kwani kuachana bado si jibu la matatizo yote.
Katika ndoa mwanaume na mwanamke ni tofauti na kila mmoja ana mahitaji muhimu ambayo ni lazima mwenzake ayatimize na kutotimizwa hayo mahitaji husaidia kukwetua njia ya kila mmoja kutoridhika na mwenzake.
Kwa ufupi mahitaji muhimu ya mwanaume (yale anapenda mke wake amtimizie) ni kama ifuatavyo

HITAJI LA KURIDHISHWA KIMAPENZI (SEX).

HITAJI LA KUBURUDISHWA, RAHA, KUSTAREHE, KUPUMZIKA, NAFASI YA KUPUMUA, BURUDANI.
HITAJI LA KUWA NA MKE ANAYEVUTIA.
HITAJI LA KUWA NA AMANI NA UTULIVU.
HITAJI LA KUAMINIWA, KUHUSUDIWA NA KUHESHIMIWA.

Mahitaji ya mwanamke katika maisha ya ndoa (vile mwanamke anapenda mume amfanyie au kumtimizia) ni kama ifuatavyo:
HITAJI LA UPENDO, KUPENDWA, MAHABA NA HURUMA.
HITAJI LA MAONGEZI, MAZUNGUMZO, MISEMO, POROJO, KUSIMULIANA NA SOGA.
HITAJI LA UKWELI, UADILIFU, KUAMINIANA, UNYOFU, WIMA NA UWAZI.
HITAJI LA UHAKIKA WA KIFEDHA, AMANA KIFEDHA, UHAKIKISHO KIFEDHA, ULINZI KIFEDHA, USALAMA KIFEDHA, UTHABITI NA AMANI KIFEDHA.
HITAJI LA KUJITOA KWA AJILI YA FAMILIA.

Kwa ufafanuzi ni kwamba mwanamke hupenda mume akimaliza kazi jioni kwanza ajithidi kuwahi nyumbani ili ale chakula (supper/dinner) na mke na watoto, akae na mke na kuongea masuala ya familia kama watoto, matumizi ya fedha nk na hupendelea baba kutumia muda na watoto na mke na si kuangalia TV.
Mume naye hupenda anaporudi kazini mke ampe angalau dakika 15 apumue ndipo aanze kuuliza maswali na kuelezea siku ulivyokuwa na ikifika muda wa kulala mke aanzishe kwamba anahitaji tendo la ndoa.

NI PENZI AU PESA?

Huwezi kuongelea mapenzi bila kutaja suala la pesa. Wapo watu ambao wanaamini kuwa na pesa nyingi, nyingi kabisa za kutosha husaidia penzi kuwa imara na linaloridhisha.
Hata hivyo tumeona penzi la uhakika hata wakati pesa zikiwa hazipo au tumeona penzi la kweli hata katikati ya umaskini uliokithiri.
Hii haina maana kwamba pesa siyo muhimu, pesa ni muhimu sana. Na pesa ina umuhimu kwa kila mahusiano hata, hivyo inabidi ujiulize mwenyewe je, upo kwa ajili ya pesa au kwa ajili ya penzi la kweli.
Utakuwa mtu wa maana sana kama utakuwa unatazama na kuwekeza kwenye penzi la kweli na si pesa.
Pia ni vizuri kuwa makini na mtazamo wa mpenzi wako je yupo kwako kwa ajili ya pesa au kwa ajili ya penzi la kweli.
Mtazamo wake kuhusu pesa ni muhimu sana.

JE,UNATIMIZIWA MAHITAJI YAKO KTK MAHUSIANO?

MAHITAJI MUHIMU KATIKA MAHUSIANO YOYOTE YA KIMAPENZI

Ni kitu cha msingi sana kuhakikisha katika mahusiano mahitaji yako yanajulikana na kueleweka kwa mwenzako.

Mahitaji yako yakijulikana na kutekelezwa kawaida unajisikia vizuri na kujiona upo salama katika hayo mahusiano iwe ndoa au uchumba.

Partner wako hawezi kusoma mind (wanaume mara nyingi tunasoma magazeti na si nini mwanamke anawaza kichwani) na kujua mahitaji yako, ndiyo maana kuna wakati unahitaji wewe mwenyewe kumueleza ili aweze kukupa kile unahitaji, ingawa ni kweli wapo ambao wameshakata tamaa kabisa kwamba hata nikimwambia najua hatafanya, bado hilo si jibu kwani jambo la msingi ni wewe kuongea na mpenzi wako na kumueleza nini unahitaji kutoka kwake tena kwa busara na hekima au kwa upendo.

Mahitaji muhimu katika mahusiano ya ndoa yamegawanyika katika sehemu kuu tano nazo ni

1.Mahitaji ya kihisia.

2.Mahitaji ya Kimwili.

.3.Mahitaji ya kijamii

4.Mahitaji ya kiroho.

5.Mahitaji ya kiusalama.

Mfano wa muhitaji ya kihisia ni kama ifuatavyo

Hitaji la kusikia na kuambiwa unapendwa, una thamani kwa mpenzi wako, kujisikia wewe ni muhimu katika maisha yake, kujisikia wewe ni mali yake, hitaji la kujisikia unaheshimiwa wewe binafsi na yeye, hitaji la kujisikia mpenzi wako anakuhitaji zaidi ya kazi zingine unazofanya kama kulea watoto nk, hitaji la kujisikia wewe ni mtu wa kwanza kwake kwa kila kitu, kujisikia wewe ni mtu maalumu kwake, hitaji la kujisikia unaaminiwa, unakubalika na pia anakupenda na kukuhitaji, hitaji la kujisikia ana appreciate kwa jinsi ulivyo na unavyofanya nk

Mfano wa muhitaji ya kimwili ni kama ifuatavyo:

Hitaji la kuguswa (touched and caressed), kupata busu, kukumbatiwa, na kushikwa hata kubebwa akiweza, hitaji la kujiona unaruhusiwa kuwa naye katika faragha yake, kujisikia huru kuwa naye kimwili pale unapo muhitaji, kujisikia wewe ni sehemu yake pale mnapowasiliana na watu wengine, kutiwa moyo, kuwa na tendo la ndoa linalokuridhisha kama upo kwenye ndoa.

Mfano mahitaji ya kiroho ni kama ifuatavyo:

Hitaji la kuheshimiwa na kusaidiwa mambo yako ya kiroho, kuheshimiwa kwa tofauti za kiroho zilizopo.

Kuwa na wakati wa pamoja kuomba pamoja huku mmekumbatiana au kushikana mikono na kuwa kitu kimoja kwa Mungu wenu.

Mahitaji ya kihisia ni kama ifuatavyo:

Hitaji la kupenda na kupendwa.

Hitaji la kuwa mali ya mume wako au mke wako na kuwa na maana ya maisha pamoja naye.

Hitaji na kujiamini (self positive image)

Hitaji la kuwa na usiri yaani kuwa mwenyewe bila kuingiliwa.

Mahitaji ya kijamii ni kama ifuatavyo:

Hitaji la urafiki na mke au mume pamoja na wengine wanaowazunguka.

Hitaji la uhuru wa kujihusisha na masuala ya jamii bila kukatazwa na mke au mume.

Mahitaji ya kiusalama ni kama ifuatavyo:

Hitaji la kujisikia salama na hatari yoyote.

Hitaji la kujisikia salama kwamba mahitaji yote katika ndoa yanatimizwa.

NI VIZURI KUBADILISHA MAZINGIRA.

Kubadilisha mazingira au eneo au mahali ni jambo la msingi sana kwa ajili ya wanandoa kufurahia ukaribu kimapenzi (intimacy).
Inajulikana kwamba kwa wanandoa kwenda mbali na nje ya nyumbani kwao kama Motel huweza kuwafanya kupata msisimko mkubwa na tofauti wa kimapenzi.

Sababu za msingi ni kwamba:
Kunakuwa na privacy kwa wahusika yaani mke na mume wanaweza kuvaa wanavyotaka.
Pia kunakuwa na uhuru kwani mkiwa sita kwa sita unaweza kupiga kelele, unaweza kuugulia kimapenzi, mnaweza kucheza, kucheka bila majirani wala watoto kuwasikia.

Hakuna kuingiliwa na kitu chochote kama ndugu kuwatembelea au watoto kuwaita kwa ajili ya kitu chochote. Pia kama simu zimezimwa ndo mnakuwa dunia yenu wenyewe.

Zaidi na kubwa kuliko yote ni kwamba wanandoa huwa mbali na masumbufu ya maisha kama vile kupika, kuangalia watoto, kutembelewa na ndugu au majirani nk.

Ukiona suala la tendo la ndoa linakupa maumivu kwa maana kwamba hakuna anayeridhika au wewe mwenyewe huridhiki ufahamu kwamba na ndoa yako itakuwa na maumivu.
Hata hivyo hujachelewa kurekebisha mambo, anza sasa.
Wanandoa wengi hujikuta katika wakati mgumu wa kuwa karibu kimapenzi, inawezekana mmoja au wote hujisikia wamechoka muda wote, au wanajisikia msongo wa mawazo au basi tu hakuna mwenye hamu na mwenzake, no feelings.
Haitakiwi kuwa hivyo, naamini ingekuwa hivyo wala msingekubaliana kuoana.

UMECHOSHWA NA SEX?

Je, unajisikia frustrated linapokuja suala la sex katika ndoa yako?

Ukweli lazima uongelewe na kuna ulazima wewe unayesoma sasa hivi kujibu na kuwa mkweli.
Kama jibu lako ni NDIYO basi swali la pili ni kwa nini upo frustrated?
Hebu tuangalia sababu kubwa tatu za msingi

Kwanza inawezekana umekuwa na matarajio yasiyo halisi,

Pili inawezekana kuna uchoyo na ubinafsi au umimi,

Na tatu inawezekana humuelewi mwenzi wako.

Hapo ndipo kwenye source ya matatizo ya mume na mke chumbani kama kungekuwa hakuna unrealistic expectation usingekuwa unakuwa disappointed na hali ya mapenzi na mume wako au mke wako

MATARAJIO YASIYO HALISI
Baadhi ya njia za kukuwezesha kuondoa matarajio yasiyo halisi na kuondoa frustration ni pamoja na kuondokana na matumizi ya mikanda ya ngono ambayo wanandoa wengi hutumia eti kujifunza.
Hii ni pamoja na kuangalia pornography.
Video za ngono hazielezei maisha halisi ya mapenzi katika ndoa na kuangalia kunakufanya ujiweke katika kundi la failures kwani hakuna mwanamke ambaye yupo na afya njema kihisia anaweza kufanya kama wanavyofanya Wanawake wa kwenye mikanda (porno) kwani wao wanafanya business na wanaigiza.
Porn stars wao wanatengeneza pesa kwa kuigiza na kuwakamatisha wanaume wenye tama na ni laana ya mapenzi (intimacy).
Biblia inafundisha kutoa ndiyo msingi kwa ajili ya kufurahia mahusiano ya ndoa. Ili kufurahia tendo la ndoa kwanza huanza kwa upendo wa kweli na upendo wa kweli ni kwanza kumpa au kufanikisha mahitaji ya mwenzi wako kwanza na wewe baadae.

UCHOYO NA UBINAFSI
Kama wewe ni mchoyo, mbinafsi (selfish), maisha yako yatakiwa balaa, huwezi kukwepa kuwa na frustrations linapokuja suala la sex na mwenzi wako.
Kwani mzunguko wa maisha yako ni kujipa raha wewe tu na kila kitu kuvutia kwako na si mwenzi wako.
Mtazamo wa aina hii ni adui na huweza kuharibu ukaribu wa mapenzi baina ya wanandoa.
Kuwa karibu kimapenzi (intimacy) kwa wanandoa huweza kusababisha kuwa na sex inayoridhisha na pia maisha bora kwa kila mwanandoa.
Jambo la msingi unahitaji kubadilika kabla kuharibu ndoa yako, kwanza jikubali kwamba wewe ni selfish na anza kumpa priority mke wako au mume wako kwanza.
Pili lazima uwajibike kwa yule unampenda yaani mke wako au mume wako na kubali kubadilika inawezekana.
Na mwisho confess kwamba umekosa na sasa unaanza plan mpya maisha mapya.

KUTOMWELEWA MWENZI WAKO
Sababu kubwa ya wengi kuwa frustrated na ndoa kimapenzi ni suala la kutomfahamu vizuri mke au mume.
Ukiwa na mtazamo kwamba mke wako au mume wako ana mahitaji sawa ya kimapenzi kama wewe basi hilo tayari ni tatizo kubwa.
Mungu alituumba tofauti kati ya mwanamke na mwanaume na lazima mahusiano yetu yakubaliane na hiyo design ambayo Mungu aliiweka.
Kumbuka mahitaji ya mwanamke na mwanaume ni tofauti na ni muhimu kila mmoja kutimiziwa mahitaji yake.
Mwanamke huhitaji LOVE na mwanaume huhitaji RESPECT..

WEWE NI AINA GANI?

Kila mwanamke ana mtazamo wake tofauti kuhusiana na ndoa yake. Kuanzia wale wanaokuwa makini kuhusu mume hadi wale ambao hajali lolote.

Je, wewe ni mwanamke yupi kati ya hawa?

MKE MLEAJI.
Mume akiwa na hitaji lolote hulitimiziwa. Mume akiwa mgonjwa ajue chicken soup hakosi.
Anakuwekea love note kwenye bag lako la kazini au lunch yako ya kubeba kazini. Anafanya kazi zote za nyumbani kama kuosha vyombo na kufua nguo bila malalamiko.
Pia anajua mume anachoka na kazi hivyo jambo la msingi ni kuhakikisha nyumbani kuna amani hivyo mke wa aina hii hujichosha na kazi.
Wanawake wa aina hii huchoka sana na kutoa kwa waume zao kila kitu kwa jina la amani.
Tatizo la mke wa aina hii akiamua kugombana anagombana kwelikweli.

MKE KAMA MAMA..
unamtengenezea breakfast ya nguvu mumeo asubuhi, unahakikisha unamkumbusha ratiba za mambo anatakiwa kuhudhuria.
Unamkumbusha kumeza dawa alizopewa na daktari.
Unapanga nguo zake za kazini kila siku.
Unahakikisha anakula chakula tena balance diet hata kama hataki vegetables unahakikisha anakula.
Unafanya yote hayo kuhakikisha unamtunza.
Na wanaume wenye mke wa aina hii wakati mwingine hufurahia kwa kuwa wanaume wengi hupenda kutunzwa ingawa wakati mwingine huudhika Kutokana na tabia zao za kukefyakefya kama mama na hakuna mume anayependa kuoa mke ambaye ni kama mama yake.
Mke ni mke na mama ni mama na haipaswi kuchanganywa.
Tatizo la mke wa aina hii humzoesha vibaya mume kiasi kwamba anakuwa tegemezi na mke hujikuta mume amekuwa kama mtoto mwingine.

MKE KAMA BINTI..
Ni mwanamke ambaye hawezi kufanya vitu mwenyewe au peke yake.
Hawezi hata kubadilisha bulbu, hawezi hata kuwasha Computer au TV mpya kuifanya ifanye kazi.
Kulipa bills bila msaada wa mume, hawezi kufan bank hadi mumewe awepo. Kila anachofanya anajiona hawezi hadi mumewe awepo.
Anakuwa kama vile ni binti ambaye anahitaji directions zote kutoka kwa baba yake.
Mke wa aina hii huvumiliwa sana mwanzo wa mahusiano hata hivyo mahusiano yanavyozidi kwenda mume hujiona ni usumbufu.
Wanawake wa aina hii inawezekana wakati watoto walikuwa neglected na hawakupata attention kutoka kwa wazazi wao hivyo hujikuta hajiamini kila analofanya.

MKE BOSI..
Mke wa aina hii huweza kumpa mume orodha ya vitu anatakiwa kufanya, mume hupewa taratibu za kusaidia kazi za nyumbani. Huweza kutoa amri za nani awe rafiki wa mume wake au la. Anampa mume kikomo cha muda anatakiwa kutazama Tv au kujihusisha na masuala ya sports na rafiki zake.
Wanawake wengi wa nchi zilizoendelea wapo kwenye kundi hili.
Hii tabia huondoa uhuru wa mwanaume na hivyo anaweza kuwa disconnected kwani mwanaume huhisi anaondolewa heshima yake ya kuwa mwanaume.

MKE SUPER..
mwanaume hafanyi kazi yoyote ya nyumbani kama kupika na kufua labda mwanaume aamue mwenyewe.
Anahakikisha watoto wanapata kila wanachohitaji.
Hapa haijalishi mke wa aina hii ana kazi yenye kipato kuliko mume wake au la.
Mwanamke wa aina hii huchoshwa na kazi kiasi kwamba anakosa na usingizi.
Pia mwanamke wa aina hii huweza kujihisi mume hana appreciation kitu ambacho kinaweza kumfanya ajisikia hana furaha na matokeo yake anaweza asiwe na mawasiliano mazuri na mume.

MKE KILA KITU NI MTOTO/WATOTO..
Wakati mwingine kuwa mzazi huongeza stress katika ndoa.
Na tatizo kubwa ni kwamba baada ya mwanamke kuwa na mtoto hujikuta mume hana nafasi tena kwake.
Mke hujikuta ana hitaji kubwa la kutumia muda au uwezo wake kwa mtoto kuliko mume.
Wanawake wa aina hii hutumia muda wote kwa ajili ya kuhudumia watoto na ni wapo wonderful kuitwa mama ingawa husahau kuhusu mume.
Ukweli ni kwamba hakuna ubaya wa kuwa na watoto, jambo la msingi ni kuwa na muda na mtoto na pia kuwa na muda na mume.

NI HATARI KUWA NA NDOA ISIYO NA MAONO.

Wapo wanandoa ambao ndoa yao ipo kwenye hatari kwa kuwa hawana vision au dreams za ndoa yao au mahusiano yao yaweje au iwe na pattern ya aina gani.
Wanaingia katika ndoa au mahusiano huku wakiwa hawana picha kamili ya ndoa yao itakuwa vipi na wengine hali ni mbaya kwa kuwa mume anatofautiana na mke kwa kila wanalofanya au tenda na kuwaza.
Hii haijalishi wamesoma kiasi gani au hawajasoma kiasi gani, haijalishi wana uwezo kifedha kiasi gani au ni masikini kiasi gani bila maono ya ndoa waliyonayo ni kuangamia.
Bila maono au ndoto ndoa huwa mfano wa wajenzi wawili wa nyumba moja huku kila mmoja akiwa na ramani yake.

Mwingine ana ndoto au maono ya kuhakikisha anakuwa karibu na mwenzake (closeness/intimacy/romance) na akipata hivyo kwake ndo maana ya kuridhika na ndoa, mwingine ndoto zake au maono yake ni kila kitu kifanywa kwa wakati wake bila kukosea na maono au ndoto za kuwa na watoto 12 na akipata hivyo basi kwake ndo kuridhika na ndoa.
Kwa kuwa kila mmoja ana maono ambayo ni yake peke yake basi kutotimizwa kwa hayo humfanya kujiona yupo frustrated na ndoa.

Bila kuwa na maono au ndoto ya ndoa yako, maono ambayo yanakuwa shared na mwenzi wako huweza kupelekea kuanza kuwekeza energy kidogo sana kwenye ndoa yako.

Hapa tunazungumzia maono ambayo ni correct kwani kuwa na maono ambayo si correct ni sawa na kutokuwa na maono kwani ni sawa na kuwa vipofu na kipofu akimuongoza kipofu mwenzake wote huishia kwenye shimo na kupotea.


Mahali pasipo na maono, watu huangamia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.

Wednesday 12 August 2015

NI MFANO HUU..

Mke mtiriri anafahamu namna ya kumfanya mume wake kuwa tayari kwa ajili ya tendo la ndoa pia ni kweli kwamba mume mtiriri anafahamu namna ya kumfanya mke wake kuwa tayari kwa ajili ya tendo la ndoa.

Kitu kinachoshangaza (au bahati mbaya) ni kwamba Malaya (wanaume na wanawake) ndio wanaojua kushawishi vizuri linapokuja suala la sex kuliko wanandoa.

Kitu maalumu ni kwamba wanawake wana faida kubwa zaidi ya wanaume linapokuja suala kuanzisha romantic encounter yoyote,Kwani ni rahisi mno kutabiri au kukisia, kujua au kufahamu kile kinaweza kumsisimua kimapenzi mwanaume ndani ya hata dakika 5.
Wakati si rahisi wakati mwingine kutabiri ni namna gani unaweza kumfanya mwanamke awe turned on chini ya dakika 5.

Kinachomsisimua mwanamke mwezi huu kimapenzi kinaweza kuwa hakina maana yoyote mwezi unaofuata, ndiyo maana mwanaume mwenye busara ni mbunifu kufahamu nini mke wake anahitaji kimapenzi ili aweze kumridhisha.
Kwa kuwa anasisimka sana akishikwa matiti au kisimi au G-spot, au yeye kuwa juu, au ukimfanyia massage au busu mwili mzima mwezi huu basi na mwezi ujao atasisimka au mwaka mzima ukifanya the same atasisimka; utachanganya mambo!

Wakati mwanaume kusisimka kimapenzi ni sawa na uhusiano wa kufuli na ufunguo wake,kwani ili kufungua kufuli lake lililofungwa ni rahisi mno kwani anachohitaji mwanamke ni kuwa na ufunguo halisi wa kufuli la mumewe.
Mara nyingi ukitumia kufuli la kuwa uchi au nusu uchi mwanaume anakuwa turned on.

Hata hivyo linapokuja suala la mwanamke ukweli ni kwamba kufuli lake ni complex hata kama unao ufunguo halisi wa kufungua hilo kufuli lake, hii haina maana utafungua kirahisi kwani lazima uwe na funguo aina tofauti tofauti kutokana na mood, mazingira nk ili kufungua kufuli hilohilo moja.

Hivyo mwanaume mwenye busara hubeba funguo zote ambazo zinahitaji kwa ajili ya kufungua kufuli moja la mwanamke kutokana na siku au mwezi au mazingira au mood.

Hii ina maana mwanaume ili mambo yawe sawa (mwanamke asisimke na kuwa tayari kwa mapenzi) unahitaji kuwa na lundo la funguo tofauti kufungua kufuli lake moja la mwili wake vinginevyo utakuwa unavunja mlango na kuingia ndani ya nyumba yake na matokeo yake ni yeye kujisikia maumivu au kuwa bored.

NI MFANO HUU..

Mke mtiriri anafahamu namna ya kumfanya mume wake kuwa tayari kwa ajili ya tendo la ndoa (seduce) pia ni kweli kwamba mume mtiriri anafahamu namna ya kumfanya mke wake kuwa tayari kwa ajili ya tendo la ndoa (turned on).

Kitu kinachoshangaza (au bahati mbaya) ni kwamba Malaya (wanaume na wanawake) ndio wanaojua kushawishi vizuri linapokuja suala la sex kuliko wanandoa.

Kitu maalumu ni kwamba wanawake wana faida kubwa zaidi ya wanaume linapokuja suala la kuanzisha romantic encounter yoyote,Kwani ni rahisi mno kutabiri au kukisia, kujua au kufahamu kile kinaweza kumsisimua kimapenzi mwanaume ndani ya hata dakika 5.
Wakati si rahisi wakati mwingine kutabiri ni namna gani unaweza kumfanya mwanamke awe turned on chini ya dakika 5.

Kinachomsisimua mwanamke mwezi huu kimapenzi kinaweza kuwa hakina maana yoyote mwezi unaofuata, ndiyo maana mwanaume mwenye busara ni mbunifu kufahamu nini mke wake anahitaji kimapenzi ili aweze kumridhisha.
Kwa kuwa anasisimka sana akishikwa matiti au kisimi au G-spot, au yeye kuwa juu, au ukimfanyia massage au busu mwili mzima mwezi huu basi na mwezi ujao atasisimka au mwaka mzima ukifanya the same atasisimka; utachanganya mambo!

Wakati mwanaume kusisimka kimapenzi ni sawa na uhusiano wa kufuli na ufunguo wake,kwani ili kufungua kufuli lake lililofungwa ni rahisi mno kwani anachohitaji mwanamke ni kuwa na ufunguo halisi wa kufuli la mumewe.
Mara nyingi ukitumia kufuli la kuwa uchi au nusu uchi mwanaume anakuwa turned on.

Hata hivyo linapokuja suala la mwanamke ukweli ni kwamba kufuli lake ni complex hata kama unao ufunguo halisi wa kufungua hilo kufuli lake, hii haina maana utafungua kirahisi kwani lazima uwe na funguo aina tofauti tofauti kutokana na mood, mazingira nk ili kufungua kufuli hilohilo moja.

Hivyo mwanaume mwenye busara hubeba funguo zote ambazo zinahitaji kwa ajili ya kufungua kufuli moja la mwanamke kutokana na siku au mwezi au mazingira au mood.

Hii ina maana mwanaume ili mambo yawe sawa (mwanamke asisimke na kuwa tayari kwa mapenzi) unahitaji kuwa na lundo la funguo tofauti kufungua kufuli lake moja la mwili wake vinginevyo utakuwa unavunja mlango na kuingia ndani ya nyumba yake na matokeo yake ni yeye kujisikia maumivu au kuwa bored.

MAPENZI..a.k.a MAHUSIANO.

Je, umewahi kujiuliza ni nini siri ya mahusiano yanayodumu kwa muda mrefu, miaka nenda rudi na wahusika wakawa na furaha na kicheko bila unafiki?

Jitahidi kufanya yafuatayo naamini mahusiano yako yatakuwa imara na yenye afya

Hakikisha unasifia zaidi kuliko kulaumu.
Ukiwa na rafiki zako hakikisha unaongea mambo 2 au 3 mazuri kuhusu mpenzi wako au mke wako au mume wako.
Kumbuka kwamba kufanya vitu kila mtu kwa tofauti ni kitu cha kawaida kwani kuna njia nyingi sana za kumenya kiazi au kukunja nguo.

Hakikisha mnakuwa na muda wa pamoja na mpenzi wako.
Kama hujaoa au kuolewa hakikisha unaoana na mwanaume au mwanamke ambaye unapenda kumsikiliza na anavyoongea.
Kumbuka ndoa wakati mwingine ni kitanda cha maua ya waridi na wakati mwingine ndoa ni kitanda cha miiba.

Kumbuka zawadi nzuri sana kwa watoto wako ni kumpenda mama yao.
Pia kumbuka kuhakikisha unajihusisha vizuri na kazi ndogondogo za nyumbani kama ni mwanaume kama vile kufua nguo, kusafisha nyumba nk.

Ukiona kuna uwezekana wa kuzipiga kikwelikweli basi hakikisha mnapigana mkiwa uchi! Serious!
Kubali, kutokukubaliana.
Usitamke kabisa neno talaka
Usiende kulala huku umekasirika labda iwe ni saa tisa usiku na umechoka huwezi kufanya chochote.


Mawasiliano mazuri ni ufunguo wa ndoa na mahusiano yako.
Usisahau kusema “Nakupenda”
Uwe na kimbelembele cha kusema “Nimekosa nisamehe’
Hakikisha ndugu (inlaws) wanakaa mbali na ndoa yako

Usilinganishe ndoa yako au mahusiano yako na wengine kwani unachokiona nje haina maana kinaweza kupatikana ndani.

Hakikisha si kitanda kilekile, milalo ileile, chumba kilekile, nyumba ileile, wakati uleule wa kufanya mapenzi na mke wako au mume wako kwani tofauti huleta maana.
Mwisho!
Uhusiano wako na Mungu ni muhimu sana katika mahusiano, Mungu ndiye mwenye upendo hivyo unavyozidi kuwa karibu na Mungu ndivyo unavyozidi kuwa na upendo na mtu unayejua kupenda.
Mafanikio ya ndoa yoyote yanauhusiano mkubwa sana na uelewa kuhusu Mungu ni nani katika maisha yako.
Usipuuze ...

TENDO LA NDOA NI ZAWADI SI HAKI.

Mungu alitoa sex kama zawadi kwa waliooana.
Ametoa zawadi ya sex ili kutufundisha kuhusu yeye na uhusiano wake na sisi.
Utendaji wa sex ni picha ya muunganiko kwa kutoa vyote (vile tulivyo) kwa mwenzako (mke au mume) na pia ni picha ya kumkubali kumpokea mwenzako (wote) kama alivyo kwako.

Kuna faida wazi kabisa kwa uhusiano wa tendo la ndoa kwa mke na mume kama vile afya ya mishipa, kupunguza maumivu, kufanya MP kuwa stable, kupunguza depression (unyonge wa kihisia), kupunguza (stress) msongo wa mawazo na kuongeza kuridhika kwa mahusiano ya ndoa.

Mungu anawapa uhuru wanandoa kunywa na kufurahi raha ya mapenzi kila mmoja kwa mwenzake kama wanandoa, hata hivyo sababu za kiroho na kisayansi haziwezi kutumika kama silaha ya mwanandoa mwingine kumthibiti mwenzake.
Uwezo wa kimapenzi kati ya mke na mume bado ni zawadi ambayo tunatakiwa kupeana bure na kwa kupenda na kwa moyo wa furaha (kutoa na kupokea kila mmoja kwa mwenzake katika ndoa).
Pale mwanandoa mmoja anapokuwa na mtazamo kwamba tendo la ndoa ni haki basi kunakusinyaa kwa aina fulani katika mahusiano huanza kujitokeza.
Mke hawezi kuwa na raha ya mapenzi katika ndoa kama mume atakuwa ni mtu wa kulazimisha na kutaka kwa nguvu kama haki yake (demanding) na pia si raha sana pale mke anapotoa tendo la ndoa kwa sababu anawajibika kutoa hata kama hakuwa tayari.

Tendo la ndoa linaloridhisha (great sex and satisfying sex) ni pale kila mwandoa anakuwa amejiadabisha kutoa kwa uhuru mwili wake kwa mwenzake.
Unapotoa kwa uhuru mwili wako kwa mume au mke wako na kupokea mwili wake kwa uhuru unaipa ndoa kitu sahihi cha asili yake na Mungu hufurahia na kutoa kibali.


UUME KUSHINDWA KUSIMAMA.

Ni matatizo ya uume kushindwa kusimama (kudinda) kiasi kinachotakiwa ili kufanikisha kuingia ndani ya uke wakati wa tendo la ndoa, au ni kitendo cha uume kusimama kwa muda unaotosha kuhakikisha mwanamke ameridhika na tendo la ndoa.

Matatizo ya uume kushindwa kusimama wakati wa tendo la ndoa ni tatizo la kawaida kwa wanaume wambao umri umeenda sana, kiukweli wanaume wengi hii hali imewahi kuwatokea na hii haina maana kwamba wanamatatizo ni mpaka hii hali iwe ni ya muda mrefu na kinatokea mara kwa mara hapo ndipo litakuwa tatizo.

Kama tatizo linazidi kujirudia linaweza kuharibu kujiamini kwa mwanaume na matokeo yake linaweza kuanza kuwa tatizo la kudumu na pia kuharibu uhusiano wako na yule umpendaye hasa kwa yeye kutoridhika na huduma yako.

Tangu kale tatizo la uume kushindwa kusimama lilikuwepo na mara nyingi lilikuwa linahusisha akili au mawazo kichwani mwa mwanaume na wengi walikuwa wanashauri kwamba
ni mwanaume kuondoa hofu,
kutulia na baadae hali itarudi yenyewe.
Kwa sasa tuna madaktari ambao wanashauri kwamba tatizo si kichwani peke yake bali linaweza kuwa ni la kimwili zaidi.

Njia ya kawaida ya kujua kama una tatizo la kimwili kwa uume wako kushindwa kusimama ni kwa mwanaume kutafiti je, wakati wa usiku ukilala unasimamisha mara ngapi kwani ni kawaida mwanaume hata mtoto wa kiume kusimamisha uume mara 3 hadi 5 kwa usiku mmoja.
Au wakati wa kuamka asubuhi ukiona uume umesimama basi wewe kimwili upo fiti kabisa na inawezekana tatizo la kushindwa kusimamisha ni la kisaikolojia zaidi.

Kukojoa mapema au ugumba hauna uhusiano na kushindwa kusimamisha uume kwani mwanaume anayeshindwa kusimamisha uume anaweza kutoa mbegu ambazo zinaweza kurutubisha yai na mtoto akazaliwa.
Vilevile mwanaume anayekojoa mapema akipewa msaada wakisaikolojia anaweza kutumia muda mrefu ndipo aweze kukojoa.

Nini husababisha jogoo kushindwa kuwika:?

Ili uume usimame na kuwa imara kwa tendo la ndoa huhusisha
Ubongo,
Mishipa ya fahamu,
Homoni,
Mishipa ya damu na
kitu chochote kitakachoingilia huu mfumo, basi kitendo kizima kinapatwa na tatizo.
Kawaida husababishwa na:
Magonjwa kama vile Kisukari, pressure (mgandamizo wa damu), moyo.
Matatizo ya damu kushindwa kuzunguka vizuri kwenye mwili.
Kiwango kidogo cha homoni za testosterone.
Matatizo ya uti wa mgongo
Kuharibika kwa nerves kutokana na upasuaji.
Tiba za madawa kama vile BP (Blood Pressure), matibabu ya moyo, ulcer.
Dawa za usingizi, na dawa za kutibu stress.
Kuvuta sigara, pombe, na madawa ya kulevya aina zote.
Mawasiliano ovyo na mwenzi wako
Stress, hofu, mashaka, na hasira
Matazamio au mtazamo tofauti kuhusu tendo la ndoa, badala ya kupata raha (plessure) mwanaume anakuwa anahisi kama ni kibarua au kazi (task)

Je, kama jogoo anapenda kuwika mara kwa mara bila utaratibu?

Hii huwapata sana ma-teenager wenye miaka kuanzia 15 - 20 na hili ni suala la kisaikolojia tu na huwa inawatokea sana wakiwaza kuhusu mapenzi au kumuona msichana anayevutia inaweza kuwa njiani, darasani au mahali popote na huo ni utoto tu ukikua hiyo hali utaacha.

Je, ni jinsi gani mtu anaweza kuondokana na hili tatizo?

Kwa wanaume wengi mfumo wa maisha ndio unatakiwa kubadilika.
Achana na sigara, pombe na madawa ya kulevya
Pumzika muda wa kutosha na kurelax
Fanya mazoezi na pia chakula bora ili damu iwe inazunguka vizuri mwili mzima hadi huko kwenye uume.
Pia uwe na mke mmoja au mpenzi mmoja kwani hofu ya kupata UKIMWI na magonjwa ya zinaa wengi husababisha hata jogoo ashindwe kuwika.
Uwe wazi kuongea na mpenzi wako linapokuja suala la mapenzi kama huwezi nenda kwa washauri wako, hata hivyo kwa nini ushindwa kuongea na mpenzi wako sasa wewe mwanaume gani unashindwa kuongea na mpenzi wako.
Pia wanaume ambao wana matatizo kuongea na wapenzi wao feelings zao kuhusu mapenzi huwa mbali na wanapata shida sana kuelekeza matatizo yao kuhusu kiwango cha ufanyaji wa tendo la ndoa hivyo hubaki amekumbatia tatizo lake na matokeo yake ndo jogoo analala tu wakati anatakiwa kuwika.
Pia kuna dawa ambazo unaweza kutumia ingawa unahitaji msaada wa dakatari kama vile viagra,
cialis,
levitra
Uwe mwangalifu usibugie hizo dawa bila ushauri wa Daktari kwani kama una matatizo ya BP unaweza kufia kufuani mwa mtu.

Kama tatizo la uume kushindwa kusimama umegundua linatokana na dawa unazotumia ni vizuri kumuona daktari akakushauri kitu cha kufanya kuliko kukatisha (kuacha) kutumia dawa kwa ajili ya tendo la ndoa wakati dose hujamaliza.

Ni hadi iweje ili kumuona Dakatari au mshauri?

Pale unapoona juhudi zako hazizai matunda na jogoo anazidi kugoma kuwika.
Pale unapoona dawa unazotumia ndiyo sababu ya jogoo kushindwa kuwika.
Ukiona tatizo linajitokeza hasa baada ya kufanyiwa surgery kwenye viungo vyako vya uzazi.
Pale unapoona uume unashindwa kusimama na wakati huohuo unapata maumivu ya mgongo (back pain), maumivu ya tumbo au mabadiliko katika mkojo (haja ndogo).

Tuesday 11 August 2015

TATIZO LA KUWAHI KUFIKA KILELENI..mwisho

Mwanaume kuwahi kumaliza (Premature Ejaculation - PE) ni jambo muhimu linalomhusu mke na mume, karibu mwanaume mmoja kati ya wanawaume watatu mmoja huwa na tatizo la kuwahi kumaliza mapema.
Nitatumia Neno PE kumaanisha mwanaume kuwahi kumaliza mapema au kwa kingereza (Premature Ejaculation)
Kwa njia zingine kuwahi kumaliza kwa mwanaume ni kitu ambacho kimejificha kwani huwezi kumtambua mwanaume ambbaye ana PE kwa kumwangalia sura, pia ni mara chache sana au ni ngumu sana kwa wanaume kupeana story za mambo kama haya wakiwa wenyewe kwani mwanaume huhofia kuonekana si lolote kwa wenzake (kupoteza ego) sana sana anayejua ni mke wake ambaye anajua inamuathiri kiasi gani na kupata usumbufu kiasi gani kwani wapo wanaume ambao hata huruma hana ile kumaliza tu basi usimguse.

Kwa kuwa hakuna mwanaume anapenda kuwa na PE hii ina maana kwamba kuwa na PE siyo huathiri mwenendo wa sex tu bali hupelekea kuathiri maeneo yote ya maisha kwani mwanaume akiwa na hili tatizo huogopa kushiriki na matokeo yake huwa mtu mwenye masumbufu na mpweke na baadae hukosa ujasiri na huathiri maisha kwa ujumla hadi taaluma yake.

Mambo mengine ya msingi ambayo yanaweza kukusaidia mwanaume ni jinsi ya kutumia akili na mawazo.

Amua kwamba utaweza kuthibiti hiyo hali, jiamini, jitolee, uwe na imani ile ya kuhamisha milima na kwamba wakati umefika unataka kubadilisha uwezo wako katika tendo la ndoa.

MAZOEZI
Pia ni muhimu kuwa mtu wa kufanya mazoezi, kama una misuli ambayo hata kama ulikuwa unakojoa (urinate) ukashindwa kuziba mkojo ghafla basi hii ina maana misuli yako ya PC imelegea na jambo la msingi ni kujifunza kuikaza kwa kufanya mazoezi.
Kuwa na misuli ya PC iliyokaza ni siri kubwa katika kufanikisha furaha ya mapenzi kwa mume na mke.
Nini Imani Potofu kuhusiana na PE?

Eti PE ni kitu ambacho huwezi kuthibiti.?

Ukweli ni kwamba unaweza kuthibiti na mwanaume yeyote anaweza kujifunza kuthibiti PE kama vile ile njia alitumia kubana mkojo wakati mtoto na sasa akilala hakojoi ovyo kitandani.

Eti PE huathiri wanaume wenye umri mkubwa.?

Ukweli ni kwamba PE huathiri wanaume wa umri wowote, ingawa wanaume wenye umri mkubwa huwa na tatizo na kushindwa kusimamisha na hutumia muda mrefu ili uume usimame na kuwa tayari kwa tendo la ndoa.

Eti PE huweza kusababisha kuwa na matatizo ya kuchelewa kusimamisha.?

Ukweli ni kwamba huwezi kukojoa bila uume kusimama hii ina maana kuliacha tatizo kwa muda mrefu kunaweza kupelekea kuwa na matatizo ya jogoo kushindwa kuwika kabisa.

Eti PE haiwezi kuathiri maisha yako ya kimapenzi na mke wako.?

Ukweli ni kwamba kama una experience PE wakati unafanya mapenzi kawaida unakuwa umejawa na mawazo kwamba unaweza kumaliza mapema na matokeo yake huwezi kufurahia sex na huwezi ku-relax, pia mke wako anaweza kuwa haridhiki na matokeo yake atakuwa anakwambia kichwa kinauma kila siku ukitaka kuwa mwili mmoja hahaha!

Eti PE haiwezi kuathiri kujiamini kwako.?

UKweli ni kwamba kila mwanaume huwa anapenda kuwa mzuri kitandani, PE na kutomfikisha mke pale anahitaji kufika ni sababu tosha ya kupoteza confidence zako.

Eti PE huathiri wanaume wachache sana?

Ukweli ni kwamba wanaume wengi ni wahanga wa hili jambo kuliko watu wanavyodhani.
Hivyo si wewe unayesoma hapa ndo unahusika, huko nje kuna wanaume wengi tu wanakumbana na hii kasheshe, ila wengi wamechukua hatua na kuondokana na hili tatizo.

Eti ukiwa na PE huwezi kubadilika kabisa hivyo ishi nayo ni kilema chako.?

Ukweli ni kwamba kukubali kwamba ni kilema chako ni kosa kubwa sana.
Kufikiria hivyo ni kosa ambalo litakufunga wewe na mpenzi wako kwenye jela ya wale ambao ni wapweke wakati wapo kwenye ndoa.
Siri kubwa ni wewe kuweza kuthibiti PE (piga ua lazima uweze, kama wengine wanaweza kwa nini wewe ushindwe?)
Ukifanikiwa unaweza kuwa ni mwanaume smart sana kitandani ambaye hajawahi kutokea kwani utakuwa ni mwanaume unayejali, uliyejifunza na kugundua feelings zako na hisia zako na jinsi ambayo huwa unasisimka kwa muda wote kitandani na hii itakupa ujasiri wa kuwa mwanaume kiongozi kitandani na kila mwanamke huhitaji mwanaume kiongozi na ambaye ni caring.

TATIZO LA KUFIKA KILELENI HARAKA..2

Kawaida baada ya mwanaume kuwa na tabia ya kumaliza haraka kinachofuata ni kuanza kukwepa sex kitu ambacho inakuwa ngumu zaidi kudhibiti tatizo, mwanaume akiwa anauwezo wa kuthibiti kumaliza mapema pia huweza kuwa na hamu zaidi ya kufanya mapenzi.

Wengine hutumia njia ya kuondoa mawazo kujihusisha na tendo lenyewe kwa kuwaza vitu vingine hata hivyo hapo ni kujinyima raha na huweza kupelekea vitu kuwa ovyo zaidi.
Si vema kuhamisha mawazo yako kutoka kwenye akili zako wakati wa tendo la ndoa kwani ni sex muunganiko wa roho, mwili na nafsi.
Jambo la msingi ni kuwa na ufahamu wa viwango tofauti vya msisimko wa kimapenzi kuhusiana na kiungo chako (uume).
Unatakiwa kujua ni namna gani unajisikia unapokaribia kufikia hatua ambayo hakuna kurudi nyuma (ejaculatory inevitablility kifupi EI).

Ukishakuwa umefahamu unavyojisikia kuelekea point of No return hapo haitakuwa vigumu kufanya marekebisho ambayo yatakuruhusu kubaki umesisimka lakini bila kumaliza (kukojoa).

Kusisimka kimapenzi huwa ni mzunguko wa hatua 4 muhimu ambazo kwanza ni kupanda kwa mdadi, huu ni wakati ambao kupumua huongezeka, uume husimama (hudinda), hatua ya pili ni kilimani, hii ni hatua ambayo uume huwa umebaki umesisimka kwa kiwango cha juu, hatua inayofuata ni hatua ya tatu ambayo ni kumaliza au kukojoa, na hatua ya mwisho ambayo kupumua hurudi kama kawaida na uume hurudi na kuwa kawaida.
Ufunguo muhimu katika kuthibiti kumaliza mapema ni ku-maintain hatua ya pili yaani kubaki hapo kilimani bila kupiga risasi hata kama umelenga vizuri na unajisikia kuachia, hapa ndipo panahitaji imani na kujikana maana huwa ni kuelekea kwenye raha kamili ya sex kwa mwanaume, ila kumbuka uliye naye anahitaji uendelee zaidi.

Nini kifanyike kuthibiti hii hali?
Usitumie drugs au kilevi eti ndo unaweza kuthibiti hii hali, vitu kama hivi huweza kukupa interference na kupunguza uwezo wa kuelewa wakati muhimu wa wewe kuthibiti kumaliza mapema.
Kwanza jikubali, wanaume wengi huamini kwamba sex ni kwenye uume tu na pia kufanya mapenzi ni pale uume ukiingia kwenye uke tu.
Kufikiria hivyo ni tiketi ya moja kwa moja ya mwanaume kuwahi kukojoa au kumaliza.

Kufanya mapenzi kunakoridhisha (best sex) ni pamoja na kupeana mahaba, romance kuanzia juu kichwani kwenye nywele hadi kwenye kucha za vidole miguuni.
Mwanaume anayejifunza kujipa raha kimapenzi kupitia sehemu zote zinazompa raha (chuchu, lips, shingo, midomo, ulimi, nk) huweza kurelease tension kupitia hizo sehemu na kutosubiri sehemu moja tu yaani uume ndo iwe sehemu ya kupata raha ndo maana huweza kukojoa mapema.
Ni kwamba mwanaume anakuwa amefunga outlet zingine na kubaki na uume tu hivyo ni rahisi kufikia point ya no return tena kwa haraka mno.
Ukishajifunza kupata raha ya mapenzi (sexual pleassure) kuanzia nywele kichwani hadi kucha miguuni maana yake mwili mzima unachukua raha ya mapenzi badala ya uume peke yake na matokeo yake utabaki ndani ya mke wako kwa muda mrefu.

Kujipa raha ya mapenzi ya mwili mzima ni njia ya ku-relax na kurelax ni moja ya njia muhimu za kujipa good sex.
Kwa mfano kuoga pamoja kwanza au kufanyiana massage kwanza kabla ya kuanza kwa tendo la ndoa husaidia mwanaume kurelax na zaidi kuupa mwili mzima sexual pleassure matokeo yake ni kufanya mapenzi kwa muda unaotosha na bibie kuridhika.

Kuwa na uwezo wa kupumua vizuri (deep breath) hii haina maana kwamba wakati unafanya mapenzi huwa hupumui, la hasha bali upumuaji wako inawezekana si ule usiotakiwa kwani wanaume wengi huzuia kupumua wakiwa kwenye sex.
Wengine huogopa kusikika wanapumua tofauti, sex ni kazi kama kazi zingine sasa usipopumua unadhani kitatokea nini, ikiwezekana pumua huku unatoa visauti, achia kupumua usijivunge kwani unapoficha kupumua maana yake unakaribisha uume ukusaidie kupumua na njia sahihi kwa uume kupumua ni kukojoa mapema.
Wengi baada ya kujifunza kupumua kwa kujiachia wamefanya mabadiliko makubwa sana katika muda wa kuwa ndani bila kumimina risasi.
· .
Ukishajua kuutumia mwili mzima kuhusika na raha ya mapenzi pamoja na kupumua sasa inakuja technic nyingine ya kujipiga stop.
Unaweza kuwasiliana na partner wako jinsi ya kupeana signal kwamba nakaribia kile kituo ambacho nikifika sitarudi tena, hakuna break.
Unaweza kutoa uume nje huku ukiendelea kupumua na ukiona unapata zile feelings kwamba huwezi kukojoa basi unaweza kurudi na kuendelea tena, kiasi cha kujipiga stop na kuendelea ni uamuzi wa ninyi wawili mnaohusika hasa baada ya mke kuridhika.

Kwa wale ambao kufanya mapenzi kupo katika level nyingine (oral sex) wanaweza kutumia oral sex kuthibiti mwanaume kumaliza mapema kwa mwanaume kujipa stop akiona anakaribia kumaliza kwa oral sex hii ni baada ya kupata mafanikio hasa baada ya kuona sasa mwanaume anaweza kwenda mbali zaidi ya kawaida yake.

Pia aina ya milalo wakati wa mapenzi huchangia mwanaume kumaliza mapema, kwa mfano missionary position (mwanaume juu mwanamke chini) huu huwezesha mwanaume kumaliza haraka kuliko mwanamke kuwa juu na mwanaume chini, otherwise mwanaume ni vizuri ukafanya utafiti wako kujua ni mlalo gani huwa unajisikia kuchelewa kumaliza na mke wako kuwahi kufika kileleni.

Pia ni vizuri kufanya mapenzi bila kuwa mabubu,kufanya mapenzi huku mnaongea husaidia mwanaume kurelax (na mwanamke pia) na husaidia mwanaume kuchukua muda mrefu kumaliza
Kujifunza kuthibiti kumaliza mapema kunaweza kuchukua muda mrefu na mazoezi ya kutosha, unaweza kujisikia ksumbuka tu wakati unajitahidi kuthibiti hata hivyo kwenye nia njia ipo na wewe utaweza tu nakuamini.

Mwisho, kujifunza mwanaume kumaliza mapema kutampa mpenzi wako raha kubwa sana kimapenzi. Wanawake hupenda good sex ambayo ni leisure, playful, whole body, massage kwa wingi.
Na wanawake wengi hulalamika kwamba wanaume huwa na haraka tukiwa kwenye miili yao, tupo too much mechanical, tunakimbilia kule chini tuingize tumalize na tuishie zetu kwa usingizi, tuna focus matiti na maeneo ya uke tu.
Wanawake hujisikia mwili mzima ni uwanja wa kucheza kimapenzi na hushangazwa na wanaume kugundua visehemu kidogo tu katika uwanja mzima na kuvipenda.
Hata uume pia umeumbwa kwa ajili ya leisure, kuchezewa, mapenzi ya mwili mzima, massage ya mwili mazima ndipo sex, kuwa focused kwenye uume peke yake huweza kuupa uume mgandamizo ambao hupelekea kutoa risasi mapema.

Kimsingi kama wanaume wangekuwa wanafanya mapenzi kwa namna ambayo wanawake wanapenda basi kusingekuwa na malalamiko na wanaume wangekuwa na matatizo kidogo yanayohusiana na tendo la ndoa.

USIKOSE SEHEMU YA MWISHO..

TATIZO LA KUWAHI KUFIKA KILELENI..1

Baada ya kupeana mabusu na romance hadi kila mmoja anakuwa amesisimka kiasi cha kuwa tayari kwa kurushwa hadi kufika kileleni, ghafla baada ya msuguano mmoja tu mwanaume ameshamaliza na tayari hoi anageuka na kulala zake usingizi mzito wakati huohuo bibie bado kwanza ndo alianza kupata raha na sasa ameachwa kwenye mataa anazubaa akiugulia kukosa raha yenyewe.

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba baadhi ya wanaume huweza kufika kileleni haraka mno; dakika chache tu baada ya kuingiza uume kwenye uke, ingawa hii humpa mwanaume raha ya ajabu hata hivyo anaweza kumwacha mke wake katika kukatishwa tamaa na kutoridhika hasa kama ni mwanamke ambaye kufika kwake kileleni hutegemea msuguano wa uume kwenye uke wake.

Kawaida mwanaume huweza kuwa tayari kufika kileleni kila baada ya mipigo 50 (kuingiza na kutoka ndani ya uke) na wakati huohuo inachukua zaidi ya dakika 10 kwa mwanamke kufikia kileleni (siyo wanawake wote wengine huwahi).

Mwanaume anapokuwa hana uwezo wa kujizuia kukojoa mapema huweza kukosa kiwango cha raha ya kutosha anayostahili yeye mwenyewe na mke wake pia, vilevile hukosa raha halisi ya kuwa ndani ya mke wake kwa muda mrefu (mwili mmoja) na hapati zile hisia za ukaribu (intimacy), mapenzi na muunganiko ambao huweza kuwaunganisha wawili wapendanao kupitia tendo takatifu la ndoa ambalo Mungu alilifanyia ubunifu kwa ajili ya mwanaume na mwanamke duniani kuwa pamoja na kufurahia uumbaji wake.
Wanawake wengi huhitaji mume kukaa ndani ya uke kwa muda mrefu unaotosha kwa kadri wanavyohitaji raha na utamu wa hii zawadi ya mwili.
Na njia sahihi ya kuweza kufanikisha hili ni pale tu mwanaume anapokuwa na uwezo wa kuhimili kutokojoa mapema na kuwa na uwezo wa kuwa na hiari wakati gani aweze kukojoa au kutokukojoa.


Fikiria raha inayopatikana kwa mwanaume ambaye anaweza kumhakikishia mpenzi wake anapata raha kwa muda anaoutaka maana tendo la ndoa ni haki yake ya msingi ya kuzaliwa.

Kwa kujifunza unaweza kuwa na uwezo wa kufika muda mrefu vyovyote unataka na kukupa ridhiko la kimapenzi wewe pamoja na mpenzi wako.

Mwanaume anapokuwa kwenye mahaba asipokuwa makini huweza kufika mahali mambo yakawa matamu kiasi kwamba hakuna kurudi nyuma kwa maana kwamba lazima mwanaume akojoe, hana chaguo bali kumaliza hata hivyo kumbuka mke wako ni muhimu pia na mwitikio wa mapenzi kati yako na yeye ni tofauti, ili kumtanguliza yeye unahitaji kufanya kitu nacho ni kudhibiti kutowahi kukojoa kabla yeye hajaridhika.


Habari njema ni kwamba mwanaume yeyote pamoja na wewe unayesoma unaweza kujifunza na kuwa mwanaume anayeweza kufika kileleni wakati anaotaka yeye.
Naamini ni ndoto ya kila mwanaume kuwa mzuri katika mapenzi na kuhakikisha mke wake mpenzi anapata kile anastahili wakiwa faragha na zaidi kuweza kumfikisha mwanamke katika kiwango cha juu kabisa cha raha ya mapenzi ambayo ni ndoto ya binadamu yeyote duniani ambaye ana hisia kamili za kimapenzi.

Je, nini kifanyike kuweza kuthibiti kumaliza mapema?

USIKOSE PART 2...

Monday 10 August 2015

NI KUENDELEA KUJIFUNZA TU.

Tendo la ndoa au kufanya mapenzi (sex) kwa watu wawili wanaopendana (Ndoa) ni moja ya vitu vya asili duniani vinavyowapa wahusika raha ya ajabu ambayo bado lugha za kawaida tunazotumia binadamu hazitoshelezi kuelezea.
Ingawa ni kweli mwanamke na mwanaume wapo tofauti linapokuja suala la sex bado kujifunza na kuwa equipped kwa ajili ya sex ni muhimu.
Miili yetu ni complex machines ambazo zinahitaji kutumia Owners Manual kusoma mara kwa mara ili kuelewa na kuwa wazuri kuitumia.
Wakati wanaume hujisikia vizuri baada ya sex wanawake mara nyingi hupenda kujisikia vizuri ili wajishughulishe na sex.
Pia mwanaume akiwa amesisimka kimwili ndipo hujisikia kusisimka kisaikolojia mwanamke akisisimka kisaikolojia ndipo hujisikia kusisimka kimwili.
Sex yenye utamu wa kweli hutokana na kujiachia katika fahamu zetu na kutojiachia fahamu huweza kufanya blocking ambayo huweza kuiba hamu ya kufanya mapenzi.
Ni kweli kwamba ubongo wako ni most important sex organ na kwa ubongo tunaweza kuhusanisha mwili, nafsi na roho kuumba raha ya mapenzi ambayo haiwezi kusaulika katika maisha yote tunayoishi.
Hakuna binadamu anazaliwa anajua kila kitu, hivyo basi kujifunza ndiyo silaha ya kwanza kabisa ya kufahamu mwili wako na wa Yule umpendae una react vipi linapokuja suala la kufanya mapenzi.
Wala huhitaji kununua libido meter ili kuhakikisha kitanda chenu kinakuwa na moto mambo ya msingi ni kwamba:
Hakikisha kufanya mapenzi ni moja ya priority kati yako na mume/mke
Jifahamu mwenyewe kama vile unapenda kitu gani na wapi katika mwili wako
Mfahamu vizuri partner wako
Fahamu aina mbali mbali za style za kufanya mapenzi (sex position) hiyo hiyo kila siku inakuwa mazoea, muwe wabunifu.
Hakikisha mnapata suluhisho kwa matatizo kabla ya kwenda chumbani ( wakati mwingine jifunze kukubaliana kutokubaliana.
Hakuna kitu muhimu kama romance.
Afterplay ni muhimu kama foreplay- huwezi kumaliza mazungumzo bila kutoa hitimisho.
Hakikisha unaimarisha mawasiliano.
Pia kubali mabadiliko au kutafuta kitu kipya.

KWENU WANAWAKE.!

Kumfanya mume wako aridhike kimapenzi maana yake ni kufanya akuangukie kimapenzi zaidi.
Kufanya mapenzi kwa wanandoa ni njia nzuri ya kuwaunganisha kinafsi na kujipa raha na ukaribu.

Ukijifunza sanaa ya kumkaribisha na kuwa tender kwa mwenzako basi mnaweza kutengeneza bond ambayo ni strong na mume au mke atakufurahia siku zote za maisha yenu.
Kumfanya mwanaume awe na furaha kwa mke wake huonesha jinsi unavyompenda na pia inampa msukumo wa kuhakikisha anakuwa karibu na wewe kimahaba na kuwa na muda na wewe kama wapenzi.
Kuna vitu vingi ambavyo mwanamke huhitaji kufanya kwa mume wake hata hivyo kila mwanaume ana tofauti na mwingine na kila mwanaume ana ladha yake linapokuja suala la mapenzi au tendo la ndoa.

Hivyo ni jukumu la wewe mwanamke kujifunza na zaidi kufanya utafiti wa kutosha kujua mume wako anapenda kitu gani kwako na pia mwili wako upo sensitive wapi na zaidi jiografia yake.
usiniulize jiografia ya mume ni nini, sugua ubongo!

Kila mwanaume hupenda kuona mke wake akionekana sexy na nguo amevaa, inawezekana mpo wawili tu yeye na wewe, kwa nini usimtanie mzee na kinguo cha uhakika then pima libido meter yake itasoma vipi?
Kuna vinguo vya kuogea, kuna vinguo vya chumbani, kuna nguo za kuvaa ofisini au kazini nk kila nguo huvaliwa mahali pake.
Huwezi kuvaa nguo ya kazini chumbani!

Unajua kuchezesha sauti kuna raha yake kumfanya mwanaume joka litoke pangoni, siyo kila siku kulalamika tu, lawama tu, manung’uniko tu, acha hizo jaribu siku hata kama anakosea kila siku anza kumsifia hata kwa vitu vidogo tu, mpe asante, mkumbatie na kumpa romantic touch, uwe mbunifu.
Siamini kama kuna mwanaume ameoa mke ambaye siku zote ni kelele au kununa tu, au kulalamika tu au kuongea tu makosa na kusahihisha, kwa nini asikukwepe, hata kama anakosa siku zingine geuza udhaifu wake kuwa kitu kizuri au uwe na mtazamo positive.

Hata siku moja hujamchezea kifua au kidevu chake, mfanye ajisikie yeye ni mwanaume special.
Mwanamke anatakiwa kumlinda mumewe na maadui wote kiroho na kimwili lakini wakati mwingine mke hujisahau na kuzoea ndoa hadi mume ana fall in love kihisia na mwanamke mwingine (nyumba ndogo).

Hata hivyo inawezekana mume huwa haja fall In love na yule mwanamke bali ame-fall in love na hisia zile wewe humpi na akikutana na huyo mwanamke anajisikia raha na kupata kile love tank yake ndani ya moyo wake huhitaji hata kama mwanamke mwenyewe hampendi ila emotionally ameoza kwa huyo mwanamke na anajikuta anavutwa na yeye badala ya wewe kumvutia.

Saturday 8 August 2015

HII PIA NI MUHIMU MNAPOKUWA "FARAGHA"

Ili kuwa mwanandoa mzuri kimapenzi unahitaji kufahamu kwanza tofauti zilizopo kati ya mwanamke na mwanaume.
Kile wewe unapenda kufanyiwa ukiwa chumbani na mwanandoa mwenzako wakati mwingine ni tofauti sana na yeye anapenda wewe umfanyie.
Wanaume siku zote tupo tayari kwa sex any time anywhere, ni kama wote ni ma-genius kwenye eneo la sex.
Bahati mbaya ni kwamba wanaume wengi akishaambiwa sasa ni wakati wa faragha; moja kwa moja full speed kwenye genitals za mke wake na baada ya dakika moja akishapima maji na kuona kuna umande haijalishi ni kiasi gani anaingia bila hata maandalizi ya kutosha eti kwa kuwa yeye umeme umeshawaka.
Je, kwa nini maandalizi ya tendo la ndoa ni muhimu sana kwa mwanamke?
Kuna logic ya kisayansi kwa nini mwanamke huchukua muda mrefu sana ili kusisimka kimapenzi ukilinganisha na mwenzake mwanaume.
Mwanaume ambaye akisisimka uume wake ambao ni kama tube yenye wastani wa inches 6 tu huweza kusimama (dinda) baada ya damu kujaa. Kwa mwanaume rijari au mwenye afya njema kawaida huchukua dakika 2 tu tangu amesisimka na kuweza kufika kileleni.
Kwa upande wa mwanamke eneo ambalo huhitaji kujaa damu ili asisimke ni kubwa zaidi kwani huchukua muda mrefu damu kujaa katika genitals na matiti au tuseme mwili mzima wa mwanamke ni one single sex organ hivyo huhitaji muda mrefu zaidi ili kusisimka.
Kama mwanamke ana mood nzuri ya sex au tuseme ubongo upo wired vizuri kwa sex basi humchukua kati ya dakika 10 hadi 15 kusisimka na kuwa tayari kwa sex.
Cha kushangaza ni kwamba tafiti nyingi zinaonesha kwamba wanandoa wengi huchukua dakika kati ya 10 hadi 15 kwa tendo zima la sex.
Hii ina maana mwanamke anapokuwa amesisimka mume huwa anakuwa alishamaliza na anakoroma na matokeo yake mke huachwa akiugulia kwa hamu ya kutaka zaidi na matokeo yake mwanamke hujikuta hajatosheka na hajafikishwa pale anahitaji kufika.

NDOA SI YA MAJARIBIO.

Kuna ushauri mmoja tu muhimu sana kwa yule anaetafuta mchumba ili awe mke au mume nao ni kwamba usikimbilie au kuingia haraka bila kuchunguza kwamba huyo unaetaka kuingia naye kwani ukiingia hakuna haraka ya kutoka kwani ni shimo ambalo kutoka ni hadi kifo.
Kama wewe ni binti au msichana au mwanamke ambaye unatamani kuolewa jambo la msingi ni kuhakikisha umejua tabia kabla ya kuamua kuoana naye.
Na kama wewe ni mvulana au mwanaume ambaye unatamani kuoa jambo la msingi ni kuhakikisha unajua fika tabia ya huyo binti au mwanamke unateaka kumuoa.
Kuna mambo muhimu sana ambayo binadamu hufanya uamuzi na uamuzi wake huweza kuathiri maisha yake hapa duniani na maisha yake baada ya kufa, moja ya jambo ilo ni ndoa.
Ndoa si safari ya majaribio kwamba nikiingia haraka haraka basi hata kutoka nitatoka haraka haraka, usijidanganye!
Adhabu ya kuingia kizembezembe kwenye ndoa ni kuvumilia maisha ya huzuni na maumivu maisha yako yote yaliyobaki duniani na huyo utakaye oana naye.
Kabla ya kuoa au kuolewa tumia muda wa kutosha kutafakari majaribu, matatizo, shida na magumu yote ambayo hutokea kwa wanandoa na kwamba una uhakika mwanaume au mwanamke unayetaka kuingia naye kwenye ndoa ana hizo sifa ya kusaidiana na wewe kuhakikisha ndoa inakuwa kitu cha Baraka kwako.
Jiulize mwenyewe kama mwanamke au binti je, nina uwezo wa kimwanamke, stamina na tabia ya kuweza kubeba majukumu ya ndoa kwa uangalifu maisha yako yote ya ndoa?
Na kama ni mvulana au mwanaume jiulize je, ninao uwezo na tabia ya kuweza kuwa baba wa watoto na kichwa cha nyumba au familia na kuwa mwanaume bora kwa mke wangu maisha yangu yote yaliyobaki duniani na mwanamke naenda kumuoa?
Unaweza kuingia harakaharaka kwenye ndoa kwa kuwa unatamani kuolewa; kumbuka ukiingia kwenye ndoa hakuna kutoka wala hakuna haraka ya kutoka ni hadi kifo kitakapowatenganisha.

NI MUHIMU SANA HII KWENU WANANDOA..

Kwanza lazima nikiri kwamba wanaume wengi hujikuta wanasisimka pale mke wake akiwa hali ya utupu.
Mungu alituumba sisi wanaume kuitikia kwa kusisimka kwa mwili wa mwanamke akiwa hivyo, na wakati mwingine tunasisimka hata kama sex halikuwa wazo kichwani mwetu yaani mwili huamua kufanya kile ambacho hatujautuma.
Hivyo wanawake wote mlio kwenye ndoa ni vizuri kufahamu kwamba ukiona dalili za kusisimka usifanye conclunsion kwamba lengo la mume wako kuwa hivyo ilikuwa ni kutaka sex.

Pia ni vizuri kama mume kufahamu kwamba wenzetu wanawake hawawezi kusisimka kwa kuona mwanaume upo mtupu kama sisi wanaume tunavyosisimka kuona wake zetu wapo uchi.
Ukweli ni kwamba ni muhimu sana na vizuri sana kwa wanandoa kujifunza kufurahishana (mume na mke) kwa njia ya kuwa uchi kwani ni raha kwa mwili na afya ya ubongo.

Kwa nini mke na mume kuwa uchi ni suala muhimu?

Kwanza kuwa uchi ni mke na mume tu, hivyo kuwa uchi hujenga aina ya bonding kwani hakuna mtu unaweza kuwa uchi isipokuwa mke na mume,vinginevyo utakuwa kichaa!
Pia kama lengo ni skin contact huleta raha; basi jinsi ngozi inavyozidi kuwa kubwa kugusana na raha huongezeka maradufu kama mke na mume watakuwa uchi.

Je ni nyakati zipi wanandoa huweza kuwa uchi na kila mmoja kumfurahia mwenzake?

Wakati wa kulala
Wakati wa kuoga
Wakati ambao si kuoga wala kulala bali wawili chumbani (kucheza, kupeana joto nk)

KULALA PAMOJA
Kulala pamoja kama mume na mke ni jambo ambalo lipo kwenye mind zetu na ni jambo muhimu sana.
Suala si kulala kitanda kimoja na kuamka pamoja tu bali kulala pamoja uchi na kuwa na maongezi, kukumbatiana na kujenga ukaribu zaidi.
Utafiti wa karibuni unaonesha kwamba kulala pamoja (uchi) husaidia wanandoa kupeana homoni za pheromones (ambazo hufanya kazi ya kuimarisha bond kati ya mke na mume) hivyo kuwa uchi ni kujipa exposure kubwa ya kupeana pheromones na matokeo yake ni kujisikia mpo closer na more secure kama mume na mke na pia hizi homoni husaidia kujisikia una afya njema kimwili na kiakili.
Kama unajisikia aibu au mwoga kuwa uchi kwa mke wako au mume wako basi kuna tatizo kubwa.

KUOGA PAMOJA
Je, Unakumbuka ni lini ulioga na mume wako au mke wako pamoja?
Je, umeshakumbatiwa wakati wa kuoga?
Umeshawahi kumuogesha mwenzako au wewe kuogeshwa?
Wakati mwingine ukiona mke wako au mume wako anaenda kuoga mpe surprise kwa wewe kuomba muwe wote kwani kuna raha yake.

WAKATI AMBAO SI KUOGA WALA SI KULALA
Hii inaweza kuwa ni wakati kabla ya kulala usiku au asubuhi wakati unataka kuamka au kuondoka kitandani, unaweza kumkumbatia mume au mke kwa dakika kadhaa bila kuongea maneno yoyote, muhimu ni mwili kuwa na mawasiliano na kuwa one flesh.

Wanawake wengi huogopa sana hii kwa kuhofia kwamba hii inaweza kuwa janja ya mwanaume kutaka sex usiku kabla ya kulala au asubuhi kabla ya kuamka na wanaume huogopa sana hii kwa kuhofia kwamba mwanamke anaweza akagoma sex baada ya mwanaume kujikuta amesisimka na anahitaji sex.

Suala ambalo husumbua kwa mwanamke na mwanaume ni kwamba mke na mume wakiwa uchi akili ya mwanaume hufikiria sex na akili ya mwanamke hufikiria romance/intimacy na kila mmoja akiona haja yake haijatimizwa hujiona hajaridhika.

Jambo la msingi kwa mwanaume ni kukumbuka kwamba mke wako huhitaji kuguswa mwili wake mara kwa mara na si lazima iwe sex na hii hupelekea yeye kuwa na afya njema katika mwili na emotions zake na kukosa kupokea mguso wa kimwili husababisha asiwe na hamu ya sex.
Mwanamke kukosa ukaribu wa kimapenzi huathiri utendaji wa ubongo wake.

Pia jambo la msingi kwa mwanamke ni kukumbuka kwamba mume wako ana hamu kubwa sana ya sex na ingawa anaweza kuzuia kile angefanya hiyo haiwezi kumsaidia kuzuia anavyojisikia. Anapokuwa amepitiliza muda mrefu bila kutoa nguvu zake kupitia sex, ubongo wake huathirika pia kama wewe mwanamke unapokosa physical touch na ukaribu kutoka kwa mume wako. Hisia zake za kutaka sex si ubinafsi bali ni response ya ubongo wake kutokana na kitendo cha kukosa sex.

Jambo la kukumbuka kwa wote ni kwamba ni muhimu sana kila mmoja kujitoa kwa mwenzake na kumfahamu vizuri mwenzi wako na weka lengo kuhakikisha unatimiza mahitaji yake hata wewe usipotimiziwa mahitaji yako.
Wewe kutokuwa selffish ni baraka kwa mumeo au mkeo na wewe kutimiza mahitaji yake kutafanya na yeye atimize mahitaji yako.

Tukumbuke kwamba kuwa comfortable kuwa uchi kwa mume wako au mke wako ni faida kwako ndani na nje ya kuta za chumba chenu cha kulala.


Friday 7 August 2015

LUGHA MUHIMU KWENYE NDOA.

Ndoa ni kama Kambai nayounganisha (kuwafunga) wawili kuwa mmoja. Kamba ya ndoa imetengenezwa kwa kuunganisha nyuzinyuzi za upendo wa ahadi nne yaani mawasiliano, kujitoa, kumwelewa mwenzako na kumsamehe.

Wakati mwenzi wako anajisikia kuridhishwa kimapenzi hujiona salama kihisia na hujiona ulimwengu unampa vyote na atajitoa zaidi kuhakikisha anajitoa katika kiwango cha juu kwao kuimarisha upendo na mahusiano.

Na anapojisikia kutoridhishwa kabisa kimapenzi, hujisikia ni kama vile anatumika au unamtumia tu kufanikisha hitaji lako la mapenzi bila kupendwa na kwake ulimwengu unageuka kuwa mahali hatari kwake na husababisha hata vitu vingine ulivyompa kama nyumba, gari, fedha nk kuwa havina maana katika uhalisia wa maisha.

Mapenzi yana lugha kama zilivyo lugha za mawasiliano, utamu wa lugha ni pale unapoifahamu kuisikia na kuiongea, pia utamu wa mapenzi katika ndoa ni pale unapofahamu lugha ya mapenzi kusikia na kuongea.

Raha ya Kiswahili ni pale unapoongea Kiswahili na mswahili mwenzako, na kuongea vile vimaneno vitamu vinavyofanya ufurahi na kucheka na kujiona kweli Kiswahili kitamu. Je inakuwaje unapoongea Kiswahili na mtu anayeongea kihindi?

Kuna watalamu na washauri ya mambo ya ndoa na mapenzi wameandika sababu nyingi sana zinazoelezea lugha halisi za mapenzi, wengine wanasema zipo 5, wengine 10, wengine 50, wengine 100 Mimi naona zipo sita ila moja (ile ya sita) ni muhimu kwa wote na ni msingi halisi wa ndoa na ni asili yake na kuizembea hiyo naamini inaharibu mtiririko wa lugha zote za hisia za mapenzi. Kuzijua hizi lugha sita na kufahamu ni zipi (ipi) mke wako au mume wako yupo basi ndoa inakuwa tamu kwelikweli, utamu halisi usio na hila, na utakiri kwamba kweli ndoa ni tamu.

Lugha za msingi za kuelewana katika ndoa kwa hisia za mapenzi ni kama ifuatavyo:-
1. Kuwa na muda na mwenzi wako
2. Kupeana zawadi
3. Kusaidia kazi/huduma
4. kumpa maneno ya kumsifia, kushukuru na kumtia moyo kwa kile anafanya
5. Mguso wa kimwili (wale wa mabusu na ma-hug kazi kwenu)
6. Mungu. Muhimu kuliko zote

Leo tutaongelea namba Moja

1. KUWA NA MUDA NA MWENZI WAKO.
Msingi wa kuwa na muda na mwenzi wako ni upamoja pamoja na kuwa kimawazo, kimwili na kiakili.

Kuwa na muda na mwenzi wako hatumaanishi kukaa pamoja kwenye sofa au makochi kuangalia TV; au movie hapo mnaipa time au muda wa pamoja TV au movie mnayoitazama siyo mwenzi wako.
Kuwa na muda na mwenzi wako ni kukaa pamoja na kumpa attention yote, anaongea na wewe unamsikiliza tena ninyi wawili tu, kutembea pamoja yaani mmeamua kwenda kutembea kwa ajili ya kwenda kutembea wewe na yeye tu si kwa sababu mnaenda kanisani au mnaenda kazini, kupeana muda wa pamoja ni kama vile kwenda kula pamoja (outing) ninyi wawili na mkifika hapo kwenye hoteli mnaongea kwa kuangaliana ninyi romantically.

Ukienda kwenye hoteli au sehemu yoyote watu wanaenda unaweza kula chakula au huduma zingine (outing) utajua tu wapenzi walio kwenye ndoa na wale ambao bado wachumba au dating couples, Guess what? Wachumba utakuta wanaongea kwa kuangaliana tena kwa karibu na vikolombwezo kibao na wanatamani wabaki hapo, tuje walio kwenye ndoa wanakula na kunywa kila mtu anaangalia kwake, wanaangalia kuta na watu na unajua wameenda kula na si kuwa na muda pamoja, halafu wana haraka sana, kidogo tu waaondoka kama vile wamelazimishwa kwenda outing.
Tuwe romantic jamani, tutaendelea kujadili zaidi huko mbele safari ya somo letu.

Ni kweli kila mtu anahitaji muda na mwenzi wake, lakini maajabu ni kwamba si kila mwanandoa ukimpa muda au kuwa naye kwake ndo anajisikia na kujiona unampenda kwani kwake kuwa na muda naye hakumgusi kama ukiwa unamletea zawadi, au unapo mpa maneno ya kumsifu kwa kitu amefanya, au kumshukuru na kumpa affirmation kwa kila anachofanya.

Kitu cha msingi ni wewe kuchunguza je mpenzi wangu anajisikiaje kwa kila mambo 5 ni lipi linamgusa sana na kujiona kwake ndo la msingi kuliko yote. Kama ni Kumpa muda ndo anajisia unampenda basi fanya makeke your baby ajipe raha.

Mbona tunapo date tunakuwa na muda pamoja huko tumepanga kukutana? Kwa nini baada ya kuoana watupeani time hata kama tunalala pamoja issue hapa ni kumpa muda ambayo katika masaa 24 hata kama ni dakika 20 tu mpe mpenzi wako na kama lugha yake ya mapenzi ni kuwa na muda na wewe basi utampatia sana na kama hufanyi ndo yale yale unampa zawadi ya gharama lakini bado anasema humpendi na love tank inazidi kuwa empty Hebu jaribu kufanya kweli uone kama mwenzi wako hajakwambia baba Fulani au mama Fulani siku hizi unanipenda sana, yaani umebadilika, acha kusema upo busy, gharama ya kusuruhisha ndoa unayoenda ICU ni mbaya sana kuliko huo ubusy.

Fanya yafuatayo katika suala zima la kumpa mwenzi wako muda wa pamoja hasa kama kwake kumpa muda ndo anajisikia unampenda
(a) Mwangalie usoni wakati anaongea atajua unamsikiliza
(b) Usimsikilize huku unafanya kazi nyingine, kama huwezi muombe akupe muda kidogo then utamsikiliza anachosema kuliko kuendelea kufanya kile unafanya huku unamsikiliza, utamuumiza sana
(c) Onyesha hisia kwa kile anakwambia, kama unahisia amekatishwa tamaa mwambia ukweli kwamba nahisi unajisikia umeumizwa au kukata tamaa, basi nitafanya hivi na hivi, changia kupata solution
(d) Hakikisha unajua anaongelea nini na anajisikiaje (body language)
(e) Usimkatishe anapoongea, sikiliza maana wengi huwa tunadhani tunajua hata alichokuwa anataka kusema hata kabla hajasema, eti nilikuwa najua utasema hicho tu

UMUHIMU WA MAWASILIANO KTK NDOA.

Mawasiliano katika Ndoa ni kama barabara ya njia mbili inayoruhusu magari kuingia na kutoka; yaani wanandoa wawili ambao mmoja akiongea mwingine anasikiliza na mwisho wanapata jibu la kudumu la tatizo lililokuwepo.
Mawasiliano mabovu husababisha kutokuelewana ktk ndoa na mahusiano ya aina yoyote.

Ni kitu cha kawaida kwa sasa kuona mabishano ambayo yanaanza asubuhi jua linaochomoza na kuendelea hadi jua linapozama jioni bila ufumbuzi.


Mabishano kama hayo yasiyo na ufumbuzi ni kama Bomu linalosubiri muda ili lilipuke.


Baadhi ya wanandoa hudhani kwamba kuacha tatizo bila kulizungumzia ni kutatua, hiyo si kweli na hali kama hiyo haileti afya ya ndoa bali ugonjwa na matokeo yake ndoto ambazo mtu alikuwa nayo kuhusu ndoa huyeyuka kama barafu lililokutana na jua la mchana.

Kanuni muhimu katika kuhakikisha ndoa inakuwa imara ni pamoja na kila muhusika kujitoa na kuelekeza jitihada za kuhakikisha kila siku anawekeza ili ndoa kustawi.

jambo la msingi ni kuwekeza katika mawasiliano bora

Mawasilinao katika ndoa au mahusiano yoyote ni kama gundi inayounganisha ndoa.


Na ikitokea hiyo gundi ikaacha kufanya kazi basi mahusiano au ndoa huanza kukatika vipande vipande, na ndoa bila kuwasiliano lazima itakufa.

Katika jamii nyingi za kiafrika watu hawapo wazi sana kujieleza kile anahitaji kutoka kwa mwenzake

Sema kile unataka bila kuzunguka.

Kama hujaridhika na style za sex za mpenzi wako sema ili ajue unataka kitu kipya, kama hujaridhika na chakula anachopika sema ili msaidiane na kuona inakuwaje, watoto, huduma kanisani maana wengine ni kanisani tu na mambo ya nyumba hana mpango, ndugu, kama hujaridhika na jinsi anavyotumia pesa sema ili ajue.

Kubaki kimya na kudhani atajua mwenyewe hata kama utahuzunika hatakuelewa eleza wazi ili kujenga ndoa yako.

hakuna njia nyingine zaidi ya ninyi wawili kuelewana na kukaa pamoja kupata jibu.

Kama unahitaji kitu Fulani kutoka kwa mwenzi wako sema nahitaji kitu Fulani, na kama kuna kitu Fulani anafanya wewe unaona kinakuletea shida mwambie kwa upole na moyo wa upendo na pia mwambie kwa nini unaona kinakuumiza kubaki kimya ni kama bomu ambalo linasubili muda na muda ukifika litalipuka.


Kama unahitaji muda wa kujibakia mwenyewe tu kufikiria mambo fulani fulani sema ili mwenzako ajue ila si kuwa mkali na kufukuza watu bila kusema kulikoni;

kuna wakati binadamu huhitaji awe yeye mwenyewe na Mungu wake, muhimu mawasiliano.


Huishi na malaika kwamba atajua kila kitu ambacho wewe unapenda au hupendi

Ndoa ni kujengana kila iitwapo leo


Na kama mwenzi wako anakasirika kwa kile umemwambia inawezekana hajakulewa so unahitaji kurudia kumwelekeza vizuri hadi aelewe kwa upendo na hekima.

Jinsi tunavyowasiliana tunatiofautiana kijinsia na kimalezi na ni muhimu sana kuwa makini kusoma lugha ya mawasiliano ya mpenzi wako.


Wanaume mawasiliano yetu ni ya moja kwa moja na wanawake mawasilino yao yanabebwa na hisia na wao ndo wanaoumizwa sana

Pia si busara kuongea na mpenzi wako kwa hasira kwani hasira wakati mwingine husababisha

Kulia machozi,

Kupiga au kupigana,

Kutupa vitu hata kama ni vya thamani kama simu za mikononi, vyombo nk,

na wengine hubaki mabubu na kushindwa kuongea.


Ndoa zote imara zina kitu kimoja kinachofanana nacho ni

Mawasiliano mazuri.

Na bila kupinga ndoa zenye matatizo nyingi matatizo huanzia kwenye

Mawasiliano mabaya.

Mawasiliano ni pamoja na

Kuwepo wakati wa maongezi,

Kumsikiliza mwenzi wako anapoongea,

na kusema kila unachohitaji kwa mwenzako.


Msingi Hasa wa Mawasiliano Katika Mahusiano Yoyote ni Katika Mambo Makuu Matatu

(a) Uwepo katika maongezi kwa mpenzi wako, upatikanaji wako pale mwenzi wako anataka kuongea kitu.

Wote mnahitajika kuwepo katika maongezi tena kwa kuhusika vizuri kwa lile linalozungumzwa.

Pia wewe unayetaka kuongea hakikisha mwenzi wako yupo tayari kukusikiliza siyo kulazimisha akusikilize wakati unajua anafanya kitu kingine muhimu tafuta muda muafaka.


(b) Msikilize kwa makini mwenzi wako na kama huna muda wa kusikiliza mwambie ni wakati gani utakuwa tayari na utasikiliza kwa makini kuliko kusikiliza huku unafanya kitu kingine.


(c) Husika katika mazungumzo au maongezi, hakikisha mwenzi wako anapata hisia kwamba unasikiliza na unajali pia unachangia kile anaongea na ongea kwa upendo, ukaribu kwani anayeongea ni mtu muhimu sana kwako hapa duniani.

Pia uwe wazi kueleza hisia zako na mawazo yako halisi kuhusiana na lile mnaongea


Mambo ya kufanya na kutokufanya wakati mnawasiliana
Lenga katika kutatua tatizo siyo kushinda mjadala au mabishano

Hakikisha unamsikiliza mwenzi wako vizuri na unaelewa ana maanisha kitu gani

kwani wanaume wengi hata kabla mke hajamaliza kuongea tayari tunadakia “nilikuwa najua unataka kusema hivyo”

Jieleze vizuri kama hujaelewa kuliko kujidai umeelewa then ukafanye sivyo

Heshimu mawazo ya mwenzako hata kama huwezi kupata jibu sasa kwa tatizo alilokwambia; kuliko kutoa majibu ambayo huishia kumkatisha tamaa mwenzako

Tumia muda mwingi kufanya maongezi kujadilia mambo unayodhani ni ya msingi kuliko kutumia muda mwingi kuongea kile ambacho si muhimu na kuacha kile ambacho ni muhimu

Kuwa mwepesi kusamehe na mwepesi kusahau pia, hakuna nafasi ya kitu kinaitwa "Nimekusamehe ila sitasahau."

Uwe mwangalifu lugha yako au maneno yako na body language kwani unaweza kuwa unaongea kitu kingine na mwonekano wako ni kitu kingine;

Ongea kile unamaanisha; wengi hupenda kulalamika badala ya kuongea kile anataka.

Usiende kulala kabla ya kutatua tatizo, Usilale na gubu au donge moyoni hakikisha umeliyeyusha kabla hujalala.

Usiongee na mpenzi wako kijeuri au kihuni au bila heshimu au kibabe hasa wanaume.

Usimlaumu mwenzi wako mbele za watu.

Unapotoa maamuzi yoyote usitoe kwa hasira

Usianze mjadala kwa kukumbushia mambo yaliyopita zamani hasa wanawake


Usidhani mwenzi wako anakuumiza kwa sababu hakubaliani na wewe inawezekana yupo sahihi hivyo mpe muda.