Friday 26 February 2016

WANANDOA WALIO IMARA.

Wanandoa imara au waliofanikiwa katika ndoa yao ni wale ambao wanaweza kukaa pamoja na kujadili tofauti zao katika namna ambayo huwezesha kujenga ukaribu kimapenzi zaidi.

Wanafahamu jinsi ya kukubaliana na kutokukubaliana, wanafahamu namna ya kuhakikisha kutokukubaliana hakusababishi maafa kwenye maeneo mengine ya mahusiano yao.
Si kweli kwamba tunaolewa au kuoa ili kuchukuliana katika migogoro hata hivyo kutofahamu namna ya kupambana na migogoro huweza kusababisha kutofanya vizuri katika mambo mengine ambayo ndo sababu za kuoana.

Kukwepa migogoro au kukwepa kuongea pamoja eti kunaweza sababisha mgogoro mzito si hekima wala busara kwani njia bora ni kuwa wazi kuongea pamoja ili kujadili tofauti au kutokuelewana kunakojitokeza ili wanandoa waweze kufahamiana zaidi.

Kwa lugha nyingine si rahisi mke kufahamu mume anapenda chakula gani bila kuongea kwanza, pia haina maana kukaa kimya kwa kuwa mke anapika chakula usichopenda basi atabadilisha na kukupikia chakula unapenda. Si rahisi mume kukupeleka outing kama hamuongei.

Wapo wanandoa ili kuepuka migogoro huacha kuongea na kuwa kimya, ni muhimu sana wanandoa kufahamu utafiti wa ndoa imara unasemaje.
Kila ndoa imara kwa wastani ina maeneo 10 ambayo wanandoa hawafanani au hawawezi kukubaliana au kwa lugha nyingine hawataweza kufikia muafaka maishani mwao.

Kwa nini hizi ndoa imara pamoja na tofauti 10 na bado zinaitwa ndoa imara?

Jambo la msingi au siri kubwa ni kwamba wanandoa wanafahamu namna ya kukabiliana na hizo tofauti na kuishi nazo, kupendana pamoja na kutofautiana na zaidi kila mmoja anamuelewa mwenzake na kukubaliana kihisia na kuchukua nafasi yake kama ni yeye.

Wanandoa imara hufurahia na kusherehekea tofauti zao na hufarijika kwa kuwa sasa anamfahamu mwenzake, anajua eneo ambalo wapo tofauti then wanaaendelea kupendana huku kila mmoja akifahamu namna ya kukabiliana na hizo tofauti.

Hawa wanandoa imara wanafahamu wazi kabisa kwamba hata kama watabadilisha partners bado watapata matatizo mapya katika maeneo ya kutokukubaliana, kuwa tofauti na kwa huzuni kubwa kazi kubwa itakuwa ni mizigo waliyotoka nayo kwenye ndoa zao za kwanza kama vile watoto nk ndiyo maana kwao talaka haina sauti wala nguvu na huwa haizungumzwi, ni neno lililofutwa katika maongezi.
Zaidi ya kukabiliana na tofauti na kutokukubaliana pia ni muhimu sana kusherehekea/kumbatia mabadiliko.
Wakati tunaoana huwa tunaahidi kukaa pamoja hadi kifo kitakapo tutenganisha hata hivyo huwa hatuahidi kubaki vilevile bila mabadiliko yoyote, tunahitaji kukua, kuongezeka skills, kwa wabunifu na wazuri zaidi kila siku zinavyozidi kwenda.
Kuna mambo mengi tunaweza kujifunza kadri siku zinavyozidi kwenda kama vile kusema asante, kuomba msamaha.
Hivyo inawezekana kujifunza tabia njema ambazo zinaweza kujenga ndoa na kuziacha tabia mbaya ambazo zinaweza kuharibu ndoa.

posted from Bloggeroid

Thursday 25 February 2016

SIRI ZA KUWA MWANANDOA MZURI.

Ili kuwa mwanandoa mzuri kimapenzi unahitaji kufahamu kwanza tofauti zilizopo kati ya mwanamke na mwanaume.
Kile wewe unapenda kufanyiwa ukiwa chumbani na mwanandoa mwenzako wakati mwingine ni tofauti sana na yeye anapenda wewe umfanyie.
Wanaume siku zote tupo tayari kwa sex any time anywhere, ni kama wote ni ma-genius kwenye eneo la sex.
Bahati mbaya ni kwamba wanaume wengi akishaambiwa sasa ni wakati wa faragha; moja kwa moja full speed kwenye genitals za mke wake na baada ya dakika moja akishapima maji na kuona kuna umande haijalishi ni kiasi gani anaingia bila hata maandalizi ya kutosha eti kwa kuwa yeye umeme umeshawaka.

Je, kwa nini maandalizi ya tendo la ndoa (foreplay) ni muhimu sana kwa mwanamke?

Kuna logic ya kisayansi kwa nini mwanamke huchukua muda mrefu sana ili kusisimka kimapenzi ukilinganisha na mwenzake mwanaume.
Mwanaume ambaye akisisimka uume wake ambao ni kama tube yenye wastani wa inches 6 tu huweza kusimama (dinda) baada ya damu kujaa. Kwa mwanaume rijari au mwenye afya njema kawaida huchukua dakika 2 tu tangu amesisimka na kuweza kufika kileleni.
Kwa upande wa mwanamke eneo ambalo huhitaji kujaa damu ili asisimke ni kubwa zaidi kwani huchukua muda mrefu damu kujaa katika genitals (lower pelvic area) na matiti au tuseme mwili mzima wa mwanamke ni one single sex organ hivyo huhitaji muda mrefu zaidi ili kusisimka.
Kama mwanamke ana mood nzuri ya sex au tuseme ubongo upo wired vizuri kwa sex basi humchukua kati ya dakika 10 hadi 15 kusisimka na kuwa tayari kwa sex.
Cha kushangaza ni kwamba tafiti nyingi zinaonesha kwamba wanandoa wengi huchukua dakika kati ya 10 hadi 15 kwa tendo zima la sex.
Hii ina maana mwanamke anapokuwa amesisimka mume huwa anakuwa alishamaliza na anakoroma na matokeo yake mke huachwa akiugulia kwa hamu ya kutaka zaidi na matokeo yake mwanamke hujikuta hajatosheka na hajafikishwa pale anahitaji kufika.

posted from Bloggeroid

UNA NDOTO GANI KUHUSU NDOA YAKO?

Wapo wanandoa ambao ndoa yao ipo kwenye hatari kwa kuwa hawana vision au dreams za ndoa yao au mahusiano yao yaweje au iwe na pattern ya aina gani.
Wanaingia katika ndoa au mahusiano huku wakiwa hawana picha kamili ya ndoa yao itakuwa vipi na wengine hali ni mbaya kwa kuwa mume anatofautiana na mume kwa kila wanalofanya au tenda na kuwaza.
Hii haijalishi wamesoma kiasi gani au hawajasoma kiasi gani, haijalishi wana uwezo kifedha kiasi gani au ni masikini kiasi gani bila maono ya ndoa waliyonayo ni kuangamia.
Bila maono au ndoto ndoa huwa mfano wa wajenzi wawili wa nyumba moja huku kila mmoja akiwa na ramani yake.
Mwingine ana ndoto au maono ya kuhakikisha anakuwa karibu na mwenzake (closeness/intimacy/romance) na akipata hivyo kwake ndo maana ya kuridhika na ndoa, mwingine ndoto zake au maono yake ni kila kitu kifanywe kwa wakati wake bila kukosea na maono au ndoto za kuwa na watoto 12 na akipata hivyo basi kwake ndo kuridhika na ndoa.
Kwa kuwa kila mmoja ana maono ambayo ni yake peke yake basi kutotimizwa kwa hayo humfanya kujiona yupo frustrated na ndoa.

Bila kuwa na maono au ndoto ya ndoa yako, maono ambayo yanakuwa shared na mwenzi wako huweza kupelekea kuanza kuwekeza energy kidogo sana kwenye ndoa yako.

Hapa tunazungumzia maono ambayo ni correct kwani kuwa na maono ambayo si correct ni sawa na kutokuwa na maono kwani huwa kama vipofu na kipofu akimuongoza kipofu mwenzake wote huishia kwenye shimo na kupotea


Mithali 29:18
Mahali pasipo na maono, watu huangamia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.

posted from Bloggeroid

HUWA HATUYAFANYII KAZI.

Kama unavyosikia kwamba siku za leo ndoa nyingi huishia katika talaka huku zikiacha uchungu kwa wanandoa wenyewe na watoto ambao wanakuwa confused na jambo lililotokea kwa wazazi wao. Usikubali hili litokee kwako haijalishi ndoa yako ipo katika wakati mgumu kiasi gani au ipo katika afya njema kiasi gani au kwanza ndo unafikiria suala la kuoa au kuolewa.

Huwezi kuwa Engineer au Doctor au successful business man/woman over night, lazima uwekeze muda na juhudi ya kutosha ili ufike hapo hata ndoa ni hivyo hivyo kwamba ni kazi huwezi ukakaa na kuishi kizembezembe ukawa na ndoa nzuri.
Jambo la msingi ni kufuata tips ambazo kila siku tunakumbushana ili kufanyaia kazi katika ndoa yako hebu leo tuangalia suala la mawasiliano.

Tafiti nyingi zinaonesha kwamba wanandoa wengi katika nchi zilizoendelea kama Marekani na Canada huweza kuwa na mawasiliano (kuongea pamoja) ya wastani wa dakika 17 kila week.
Kama kwa wiki mke na mume wanaongea kwa dakika 17 tu je ni zinatosha kuweza kuelezea au wasilisha matatizo unayokutana nayo? Hamu, hofu au vitu vinavyofukuta ndani ya moyo wako kuhusu mume wako au mke wako kama vile masuala ya sex? Bila kuwasiliana kinachofuata ni frustration kujaa ndani yako na huweza kuathiri ndoa.
Je, kuongea kwa dakika 17 tu unaweza kuwasiliana topic ngumu ambayo inatakiwa kuongelewa openly na kwa muda wa kutosha?
Kutokana na kuhangaika na maisha mke na mume huishia kuwa kama polisi wa barabarani anayeongoza magari ndani ya nyumba zao.
Wengi hukiri na kuongea kwamba wanataka kuwa na muda na wake zao au waume zao hata hivyo hujikuta muda wao mwingi wanatumia kufanya mambo mengine na si kuongea na waume zao au wake zao.

“Hii ni kumaanisha kwamba kufahamu jambo siyo kulitenda”

Kufahamu kwamba unahitaji muda wa kuongea na mke wako au mume wako ni vitu tofauti na kutenda jambo la msingi ni kutenda siyo kuongea na kuahidi tu.
Kama kuongea na mume wako au mke wako ni number one priority basi inabidi uweke kwenye kitabu chako au ratiba yako suala la kuongea na mume wako au mke wako liwe namba moja na utekekeze.

Huo ni ukweli na unauma kama kupigwa msumari kichwani.
Tunasema mdomoni linapokuja suala la ndoa na vitu vingine, ndoa ni namba moja na tunaishia kutumia muda wetu kufanya mambo mengine.
Kuipa ndoa kipau mbele au kuyapa mahusiano yako na yule umpendae first priority ndiyo siri kubwa ya kurudisha maongezi mazuri na muhimu yanayokosekana mkiwa pamoja.

posted from Bloggeroid

Tuesday 23 February 2016

UKIWEZA KUMPA RAHA HIZI MKEO,UTAKUWA NA NDOA YENYE AMANI SANA.

Wanawake wengi japo siyo wote, husisimka na hupandwa na wazimu wa kimahaba wakichezewa chuchu zao na visimi.(kinembe)

Chuchu za mwanamke mara nyingi husisimka ikiwa zitatomaswa vizuri na kwa upendo, kwa kutumia mikono,lips za mdomo na ulimi kupekecha pekecha ncha za chuchu na kuzimung'unya kwa mfano wa mtu anayemung'unya pipi hivi,Na mwanamke akianza kusisimka ncha za chuchu huwa zinasimama (dinda) na kuwa ngumu na kufanya matiti yawe kama yamesimama,Hali hiyo ya matiti kusimama na kuchomoza hujitokeza pia kwenye uke.

Ambapo mashavu ya uke hupanuka na kutengeneza msisimko wa ajabu huku kisimi kikisimama na kumwaga ute laini ambao kazi yake ni kuutelezesha uume wakati unaingia.

Jinsi mume anavyokutomasa mpaka unatoa huo ute niliousema,ukitokwa na huo ute mwanamke unakua katika hali mbaya sana,unakuwa katikati ya kifo na uhai kiasi kwamba hata mwanaume akiingiza tu kidole kisha kikatelezeshwa na huo ute utasikia raha sana ingawa kukojoa itakuwa bado.

Sasa mtu wa aina hii ili ukojozwe,Kwanza lazima mume ajue G-spot yako ilipo kisha aichezee kwa kuimassage kwa vidole vyake viwili na muda huo huo awe anachezea kisimi chako kwa kukitekenya awe kama anaichora namba nane kwa ulimi kukizunguka kisimi kwa kuichora namba nane mara kadhaa.. ingawa kwa wenye kinyaa.hawawezi hasa mwanamke kama ana tabia za uchafu.


G spot ipo kama sentimita tano hivi ndani ya uke ipo sehemu ya juu ya kuta za uke.

 Usione aibu kama mzee haijui muelekeze G spot ilipo,mwambie aitekenye hivi"mwambie akuingize taratibu na kwa upendo kidole au vidole vyake viwili ndani ya uke,kisha awe kama anaibomyeza na kuisugua sehemu ya ndani ya uke,hiyo niliyoisema ambayo iko sentimita tano ndani ya uke kwa juu Sehemu ambayo ukiigusa utahisi kama sponji hivi, hapa sasa vile vidole au kidole huko ndani anakuwa anavitumia kuibonyeza kwa style ya kuitekenya G spot, Anakuwa anafanya kama vile anamuita mtu kwa ishara ya mkono.

 Kitendo hiki kitakuwa kikimtekenya mwanamke mpaka anajisikia kama mkojo unataka kutoka lakini hautoki hapa ndipo wengine huchukua uume uliosimama vizuri na kuanza kukipiga piga kisimi na kukisugua kwa kichwa cha uume,hali hiyo akiifanya vizuri itakufanya wewe mwanamke sio tu kukojoa kawaida bali pia umwage maji mengi.Kama hii ya kukipigapiga kisimi na kusugua itakuwa ngumu basi mwanaume unaweza kuwa unakichovya kichwa cha uume kwenye kuta za uke huku ukikitumbukiza mpaka usawa wa kichwa tu na kuuchomoa hapo akifanya mara mbili,tatu mchezo huo mke atakojoa kwa fujo sana na kukamua mpaka tone la mwisho.

Mapenzi ni sanaa na ni muhimu kujifunza kila wakati ili kuifanya ndoa yako iwe na kitu kipya kila siku.

Niwatakie siku njema.


posted from Bloggeroid

Thursday 18 February 2016

KUDANGANYA KUFIKA KILELENI.

Kila mmoja naamini amesikia tetesi au fununu kwamba wanawake huwa wanadanganya kwamba wamefika kileleni.
Ni kweli hili jambo lipo; wanawake wengi wameshawahi kuwadanganya wanaume zao zaidi ya mara moja na wengine ni kamchezo kao ka mara kwa mara, hata wewe unayesoma hapa inawezekana usiku ulimdanganya kwamba umefika kileleni kumbe usanii mtupu.
Swali la kujiuliza hivi kwa nini wanachukua uamuzi wa kudanganya kwamba wamefika kileleni wakati si kweli?
Lazima kutakuwa na sababu za msingi kwani wanawake ni viumbe wanaojua kupenda kuliko wanaume na kama kuna sababu za msingi hii ina maana hawastahili kulaumiwa.

Katika dodosa dodosa akina dada wengi na akina mama wengi sababu kubwa zinazopelekea wawadanganye wanaume zao kwamba muziki umejibu kwanza ni kitendo cha kutopenda waume zao wajisikie kuwa discouraged kwani wakati mwingine wao wanawake huwa wanakuwa wamechoka na wanapenda love making sessions iishe na njia sahihi ni kuonesha kwamba wamefika kileleni.
Kama wewe ni mwanaume upo kwenye ndoa fikiria umejitahidi kufanya kila unaloweza kumfanya mke wako ajisikia kupenda sex? (umemsaidia kazi, na umefanya kila unaloweza ili ajisikia unampenda) ile mnaenda kitandani mke wako anakwambia:
“Mimi nimejichokea hivyo fanya tu, ukimaliza niambie”
Utajisikiaje?
Kuna tofauti gani kati ya ku-romance jiwe na mwanamke ambaye anakukabidhi sex organ na yeye analala usingizi?
Si afadhari akudanganye kwamba yupo na wewe na amefika kileleni haraka kumbe ni fake?
Naamini umepata jibu!

Pia wapo wanawake ambao wanakiri kwamba waume zao huwa hawaridhiki kimapenzi hadi mke afike kileleni, hivyo faking ni njia sahihi ya kumfanya mume aridhike na mwanamke asichoke.
Sababu nyingine ni kwamba mwanamke anapomuhitaji mume wake kwa sex si mara zote anahitaji kufika kileleni, wakati mwingine mke huhitaji ukaribu wa kimapenzi, hata hivyo wanawake wengi huamini kwamba kuwa na mtazamo kama huo inaweza kumfanya mwanaume asijisikie vizuri na njia sahihi ya kumfanya mwanaume wa aina hii afurahi ni kumdanganya kwamba amefika kileleni.
Pia wapo wanawake ambao si kawaida yao kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa inawezekana ni skills kidogo kutoka kwa waume zao au namna walivyo.
Wanawake hawa hupenda sana waume zao wajisikie wanaweza na wanawaridhisha na hakuna njia nyingine zaidi ya faking.
Kama mwanaume atakuwa na focus kubwa kwa ajili ya kumfanya mwanamke afike kileleni badala ya kumpa raha ya mapenzi, basi uwezekano wa mwanamke kudanganya huongezeka.
Mwanamke hujiona amempa mume disappointment kubwa mno kama hajafika kileleni kwani anaona juhudi ya mume wake, hivyo faking is the true name of the game.
Kudanganya kwamba amefika kileleni huweza kuwa sanaa nzuri sana kwa mwanamke smart ambaye anafahamu namna ya kucheza aina hii ya maigizo.
Atambana mwanaume wa watu, atatoa miguno ya kimahaba, atapumua kwa ndani, atabadilisha sura na uso, atajivuruga kwenye pillow kisanii na kijiografia hadi mwanaume aingie mjini.
Wanawake wataendelea kudanganya tu kwamba wanafika kileleni na wanaume hawawezi kufanya chochote zaidi kwa kuendelea kufurahia tu.
Kama ukigundua kwamba mke wako anakudanganya kwamba amefika kileleni jambo la msingi si kulaumiana bali kuzungumza au kujadiliana na kufahamu sababu zinazofanya mfungane kamba kiasi hicho na kama inawezekana nini kifanyike ili kuwa na kitu halisi.
Mapenzi ni sanaa na kwenye sanaa kuna actors.

posted from Bloggeroid

Tuesday 16 February 2016

KUMWANDAA MWANAMKE KUWA MWILI MMOJA 2.

Je, ni makosa gani ambayo wanaume hufanya katika kumuandaa mwanamke?

1. KUWA NA HARAKA.
Wanaume wengi huwa na haraka ya tendo la ndoa bila kuzingatia umuhimu wa kumuandaa muhusika kwanza.
Wanawake hutumia muda mrefu ili kusisimka ndiyo maana unahitaji kutumia muda bila kuwa na haraka ili uweze kumsisimua na zaidi kuwa na sex nzuri na yenye kuridhishana.
Ni vizuri kutumia muda wa kutosha kumuaandaa na kama unaweza hata kumfikisha kileleni hata kabla ya kumwingilia.

2.KUKOSA KUJUA SEHEMU MUHIMU ZA KUCHEZEA.
Zaidi ya matiti, shingo na midomo (lips) na kisimi wanaume wengi hawajui ni sehemu zingine zipi ambazo wanawake huwasisimua zaidi.
Kuna sehemu zingine ambazo mwanamke akiguswa anaweza kusisimka haraka zaidi.
Tumbo, matako, mapaja, nyuma ya shingo, mabega, mgongo, sehemu iliyopo kati ya uke na nyuma

Hizi sehemu ni muhimu sana kwake kuguswa wakati wa kumuandaa.
Pia lazima uwe mtundu kuweza kusoma lugha yake na jinsi nini anakifurahia na nini hafurahii wakati wa maandalizi.

3. KUWA BUBU BILA KUONGEA MANENO MATAMU YA KUMSIFIA.
Wakati wa tendo zima la kufanya mapenzi wanawake wanategema mwanaume awe anaongea si kuwa bubu na kuongea huanzia kwenye maandalizi na kama wewe ni fundi wa kuongea basi hutachukua muda mrefu kuhakikisha moto umewaka.
Kuna maneno matamu, kwenye mapenzi maneno matamu yapo ya aina mbili, kwanza ni dirty words (mfano uke kwa jina jingine unaitaje vile au uume kwa jina jingine unaitaje vile) na pili maneno ya kumsifia juhudi yake au alivyo na umbo zuri. Dirty words husaidia kumsisimua na kumpa nyege zaidi na maneno ya sifa husababisha atoe juice zaidi.

4.KUBUSU KWA KINYAA AU BILA USTAARABU.
Wakati unambusu usiache mimate kila mahali uwe mstaarabu pia usioneshe kwamba una kinyaa katika kubusu baadhi ya sehemu ambazo yeye anapenda umbusu, huyo ni mke wako na yeye wewe ni mwili mmoja, yeye ni wewe na wewe ni yeye, hivyo unaruhusiwa kubusu sehemu yoyote ndiyo maana usafi ni jambo la kwanza kabisa katika mapenzi.

posted from Bloggeroid

KUISHI NA MWANAMKE.

Kuishi na mwanamke kunahitaji mwanaume kuwa makini na jinsi unavyoishi naye pamoja na unavyoongea naye na mawasiliano yote kwa ujumla.
Mawasiliano ni ufunguo kwa mwanamke kumfurahia mume wake.
Ukiongea na mke wako kama mwanamke mrembo naye atajiona ni mrembo ukiongea na mke wako kama vile ni jimama lililopitwa na wakati ni kweli anajiona amezeeka na kupitwa na wakati.

Jambo la kwanza msifie kwa jinsi anavyoonekana (physical appearance) yaani nguo alizovaa, nywele, viatu na hata perfume, anyway vitu hivi anavaa kwa ajili yake na wewe pia.
Kwa kumpa compliment basi atakuwa na confidence na kwamba umevutiwa na atajisikia vizuri. Suala la nguo ni kitu muhimu sana kwa mwanamke ndiyo maana hata wenyewe kwa wenyewe huweza kupeana sifa,
je wewe mwenye mali naamini si zaidi?
Unavyozidi kumsifia mwanamke kwa mwonekano wake, jinsi anavyofanya vizuri kitandani, jinsi alivyo, tabia njema na kila kitu anafanya naye atajitoa zaidi kuhakikisha anakupa huduma za uhakika.
Jambo la msingi hapa unaanda akili yake kwa ajili ya kuwa mwili mmoja baadae.

Jambo la pili ni muhimu sana kumuuliza jinsi alivyoshinda hasa ukikutana naye jioni baada ya kazi.
Hata hivyo unatakiwa kuwa makini sana na jibu la swali kwani kama alikuwa na siku mbaya anaweza kukumwagia kopo zima la worms. Pia unatakiwa kuwa na tactics za kuhakikisha unabadilisha mambo mabaya anayokwambia na kuwa mazuri au kubadilisha somo.
Kumbuka lengo lako ni kutaka kutengeneza mazingira ya yeye kuwa na mood nzuri kwa ajili ya kuwa mwili mmoja.

Jambo la tatu hakikisha anajifahamu jinsi unavyojisikia kuhusu yeye na pia ni jinsi gani unajisikia vizuri kufanya mapenzi, tendo la ndoa au kuwa mwili mmoja na yeye.
Kama umezoea kuwa na utaratibu unaojirudiarudia unatakiwa kubadilisha. Ikiwezekana kuanzia sasa kila touch mwilini mwake kuanzia mwanzo hadi mwisho hakikisha unamwambia unavyojiskia raha. Hakikisha amejifunza na anafahamu unavyojisikia unapombusu, mkumbatia, mpenda, mshika, mnusa, muonja nk zaidi mhakikishie jinsi unavyojisikia akikupa mahaba.

Jambo la nne hakikisha unamsifia mbele za watu au mbele za rafiki zako na zaidi sana ukiwa chumbani hakikisha unamuandaa hadi yeye analilia wewe kumuingia ili kuwa mwili mmoja hiyo ina maana kwamba utakuwa umemuandaa vya kutosha, tumia mwendo wa kobe na si cheater.

Jambo la tano, hujawahi ambiwa na mke wako kwamba “ hujawahi nipeleka hata Bagamoyo tu: hii ina maana kwamba anataka siku moja upange muwe na outing ya uhakika wewe na yeye tu, maana yake anataka romance. Hivyo fanya kweli maisha ni sasa!

posted from Bloggeroid

KUMWANDAA MWANAMKE KUWA MWILI MMOJA.

Kumwandaa mwanamke kuwa mwili mmoja huanza kwa maneno, ongea kile ambacho kitamfanya damu yake kuwa hot.
Pia matendo huweza kufanya kitu cha maana zaidi kuliko maneno, wakati unampa maneno mguse kwa kupalaza kwenye mwili wake wanawake husisimka kwa kuguswa wakati wanaume kwa kuona; tembeza mkono kama mawimbi unapoongea au kutoa zile hadithi zako za kumtengeneza mood, huku ukiwa karibu kiasi cha nywele zake kugusa uso wako.

Wakati wa maongezi mguse kwa wororo anza kuingilia himaya yake (siyo sehemu za siri – private parts) bali private space.
Unaweza kugusa mkono wake au kuondoa kitu chochote kwenye nywele zake au uso wake (hata kama hakipo we si unajua unafanya kitu gani) au unaweza kushika mikono yake (au vidole ) na kufanya massage kiaina kwa kutumia vidole vyako.

Anza kumsifia jinsi alivyo ukianza na nguo au kitu chochote amevaa (hapo ndipo ugonjwa wa wanawake wengi ulipo) sifia sura yake na vile alivyo kama vile nywele, kucha, lips na vingine unavyovijua wewe, sifia kwa uhakika na kiukweli anyway ni kweli ur wife is so beautiful ndo maana upo naye hapo.

Jihusishe naye zaidi kwa kumgusa katika njia ambayo si ya kuashiria unataka sex pia kwa hatua kama hii usithubutu kumbusu yeye bali yeye ndo atakuomba umbusu.

Maongezi yako yanatakiwa sasa kuwa ya kimahaba zaidi, tumia sexy words, mwambie unavyojisikia kihisia,ongea kwa ulaini ili akuelewe kirahisi, unapoongea mnong’oneze kwenye makisio yake kama vile unamwambia siri hata kama mpo chumbani wawili tu.
Wakati unamnong’oneza sogeza zaidi lips za mdomo wako kwenye masikio yake na kugusisha na kumpa kabusu ka kiaina halafu achia ili kumruhusu yeye kujiachia kwako zaidi na kukung’ang’ania zaidi.
Ukiona anakuegemea zaidi ongeza kabusu kengine kwenye sikio huku ukimwambia maneno matamu na yanayovutia ya kimahaba.
Ukiona joto lake linazidi sasa usifanye kosa anza kusambaza mikono yako na kumgusa kila eneo la mwili wake lakini usiguse matiti, au chini (sehemu za siri) bali tumbo, mgongo, shingo, mikono, miguu, kidevu nywele nk.

Anza kusambaza busu lako kuanzia kwenye lile sikio, shingo, kinywa huku yeye akiendelea kukuinamia na wewe unaendelea kumpoa soft kisses baada ya hapo naamini moto maji yataanza kuchemka kiasi kwamba kupoa itakuwa kazi nzito na ukiona hakuna kitu anza square one.

posted from Bloggeroid

Saturday 13 February 2016

KUMWAGA MAJI..

Wapo wanawake ambao akifika kileleni (G- spot stimulation) huweza kutoa fluid mfano wa mkojo kupitia urethra, huwa na sweet smell, huweza kujaa hata kikombe cha chai na huruka umbali wa futi hata 8 na kugonga ukuta wa chumba.

Huu si mkojo na ni haki ya kuzaliwa ambayo mwanamke amepewa na muumba wake hasa linapokuja suala la kufurahia mapenzi na mumewe.
Pia haya maji maji huitwa Amrita au Divine Nectar, au Fountain of Youth huu si mkojo hata kama hutoka kupitia njia ya mkojo ya kawaida.

Hiki ni kitu cha kawaida kwa mwanamke yeyote ambaye anapata mapenzi ya kweli na kukubali na kuachia hisia zake na kufahamu mwili wake unavyofanya kazi akisaidiana na mpenzi wake.
Hii fluid huweza kutokea pia hata pale mwanamke akifurahi jambo lingine na si lazima iwe mapenzi tu.

Kila mwanamke anayo potential ya kutoa haya maji maji ila ni pale tu atakapojifunza ku-surrender mwenyewe na kuwa na furaha ya kweli.

Mwanamke huweza kufikishwa kileleni kimapenzi kwa kusisimuliwa kisimi, uke au G- spot.

Tofauti ya mwanamke kufika kileleni kwa kuchezewa kisimi ni kwamba ile raha huja ghafla kama vile mwanaume anapofika kileleni, wakati kufika kileleni kwa uke au G-spot mwanamke hujisikia raha kama mawimbi kwenda mwili mzima.

Ndani ya uke sehemu ya juu ndani ya ukuta kati ya kufunguka kwa uke na cervix kuna eneo ambalo huitwa G spot.

Hili eneo huweza kukua na kuhama ambalo wengi huliita ni sacred spot kwa mwanamke huweza kutunza kumbukumbu na hisia za kuumizwa (hurts and pains), infections, abortion, sexual abuse, magonjwa na kitendo cha kutotaka sex na kama hakuna healing huweza ku-shut down na kushindwa kutoa hii fluid

Ili mwanamke aweze kutoa fluid ni lazima hili eneo liweze kuponywa au kuwa activated upya na mwanaume.
Activation hufanywa kwa mwanaume kumfanyia massage zaidi ya mwezi kwa muda usiopungua nusu saa kila wakifanya mapenzi huku mwanaume akimpa mke wake au mpenzi wake gentle and compassionate love making.

Muwe na siku njema kwa leo.

posted from Bloggeroid

KUAMSHA UPYA MAPENZI.

Kawaida mahusiano ni kama kujenga nyumba ambayo ujenzi wake hudumu na kudumu hata kama ipo siku utaamua kuishi kwenye hiyo nyumba bado utaendelea na kufanya repair kila siku na kila mara.

Hivyo basi, ili ndoa yako iwe tamu na kuteka nafsi ya yule unampenda basi hakikisha huu mwezi unafanyia kazi mambo Yafuatayo;

1.MAPUMZIKO YA PAMOJA.

Inatakiwa kujadili na kupata muda wa kuwa peke yenu, hii inawezekana ikawa mara mbili au tatu kwa mwezi, hata kama mna watoto wengi kiasi gani lakini faraja inayotukuka katika mapenzi ni kuwa pamoja. Tafuteni siku maalum ambayo mtatulia, mtajadili mambo yenu kwa usiri na mtatenda chochote kinachostahili, hapa mtashangaa kuona mnatengeneza penzi ambalo kwa muda mrefu mlikuwa hamjalipata.
Watu wanaokaa pamoja wakajifungia sehemu kwa zaidi ya masaa matatu manne si rahisi kuwa na kisirani, kwa vile kwa kukaa hivi kila mtu anakuwa na muda mzuri wa kumrekebisha mwenzake.

2.KUTAFUTA RAHA KATIKA MWILI.

Unatakiwa uwe mwepesi wa kuzigusa sehemu zinazomsisimua mwenzako hii inapendeza ikawa ni siku zile zile mnazoziteua kukaa pamoja, hata kama siku hiyo hamkuwa na ahadi za kutenda mambo yoyote ya kuchosha lakini ukishapita katika sehemu mbili kati ya 29 zenye raha basi ujue umetengeneza mapenzi mapya.

3.KUONDOA WOGA.

Hili nimekuwa nikilipigia kelele siku nyingi kwamba mpenzi wako hustahili kumwogopa, japokuwa kuna mila kama hizo ambazo mumeo unaweza ukamuona kama baba, hii si mbaya lakini ubaba huu uwe na mipaka na inapofikia wakati raha inahitajika basi kila vurumai lazima zitumike.
Yapo mambo mengi sana ambayo unaweza kufanya ili kuhakikisha penzi na yule umpendaye linazidi kuwa na fukuto kubwa zaidi kama vile kupeana zawadi, kuhakikisha unaongea maneno yanayomtia moyo na kumsifia vitu anafanya nk.


posted from Bloggeroid

Friday 12 February 2016

KUUMIZWA KWENYE MAPENZI.

Binadamu yeyote ameumbwa na asili ya uwezo wa kuponya maumivu au kuumizwa hisia zake.
Kama imetokea umeachwa na mpenzi wako ambaye ulitegemea mnaweza kuwa na maisha ya pamoja baadae usiogope.
Kwanza mshukuru Mungu kwa kuwa amekuacha sasa kuliko kukuacha baada ya kufunga ndoa.
Kitendo cha kuachwa na mchumba au mtu ambaye mlikubaliana kuwa wachumba na hatimaye ndoa kweli huumiza sana.

Wala usiogope maumivu ya kuumizwa na mapenzi, ogopa moyo ambao hauwezi kupenda tena.
Mara nyingi tunapoumizwa katika mapenzi au mahusiano tunapata maumivu makali sana na wengine hushindwa hata kwenda kazini, wengine hushindwa kupata hata usingizi kwa siku kadhaa, wengine huamua kuchukua uamuzi wa hata kupigana na kushitakiana kwa kupotezeana muda hata hivyo ni kwa sababu ya maumivu.
Wengine huweka nadhiri kwamba hawatapenda tena nk.
Kitu cha msingi kwanza ni kukubali (admit) kwamba upo kwenye maumivu na kwamba umeumia.
Hata ufanyeje huwezi kukimbia maumivu kwenye mapenzi, utaendelea kupambana hizi hisia upende usipende.
Ukiumizwa umeumizwa haijalishi utaamua kuwa kama mtoto kuumia na kuachia au kuwa ngangari kwa kubaki na maumivu ndani.

Kitu cha pili baada ya kubali umeumizwa ni kuachilia ile hali kwa kufanyia kazi kama unaweza kulia machozi lia sana kwani kulia machozi huleta relief na kujisia mwepesi then endelea kufurahia na kuona ni jambo la kawaida na pia wewe si mtu wa kwanza kuachwa na kuumizwa kwenye mapenzi.

Haina haja kuanza kukataa kwamba hukupenda au hukuwa katika upendo wa ndani na huyo aliyekuumiza.
Ulimpenda kwa sababu kulikuwa na sababu ya msingi na kitendo cha mahusiano kuharibika hii haina maana kwamba ulipenda vibaya au ulifanya jambo baya.
Kupenda mtu ni process ambayo ilikupasa wewe kuwa mtu anayependa, na hivyohivyo hata kama umeumizwa jambo la msingi ni kuendelea kujipenda mwenyewe na kujiamini kwamba wewe hukufanya kosa lolote na kwamba bado una nafasi kubwa zaidi ya kupata mtu wa kupendana na wewe upya.
Unatakiwa kuvaa positive focus kujipenda au kujikubali mwenyewe na baada ya hapo onesha upendo kwa wengine.
Kumbuka huwezi kupenda mtu then usipate maumivu hakuna kitu kama hicho, unavyopenda zaidi ndivyo mambo yakienda vibaya utapata maumivu makali zaidi.

Maumivu ni sehemu ya urithi wa mapenzi.

Huwezi kumbadilisha mtu mwingine, lakini unaweza kubadilisha jinsi unavyojihusisha na watu wengine.
Huwa Inachukua watu wawili kujenga na kuendeleza mzunguko wa mgogoro, lakini inamchukua mtu mmoja tu kumaliza mgogoro, kwa kufanya mabadiliko ndani yako unaweza kumaliza mgogoro, kuponya maumivu ya kuumizwa na wakati mwingine kurejesha upendo wa kweli kwa yule unayempenda.
Hofu, mashaka, na kukasirishwa huweza kubadilishwa na upendo na ushirikiano na hatimaye unapata suluhisho la tatizo na hatimaye peace of mind.

Una kila kitu kinachoweza kukuwezesha kuponya maumivu ya kuachwa na mpenzi, jiamini.

posted from Bloggeroid

MWANAMKE MLALAMISHI.

Binadamu ni kuimbe anayependa sana kulalamika iwe ofisini, kanisani, hotelini, kazini, sokoni, darasani, mikutanoni, msibani, harusini nk watu ni kulalamika tu.

Na kwa upande wa wanandoa mwanamke ndiye anajulikana sana kwa kuwa mtu wa kulalamika kiasi kwamba wanaume wengi huwa wanachoka na kuanza kujiuliza hivi mwanamke anahitaji kitu gani maana kila unachompa bado hakiwezi kumfanya asilalamike zaidi.

Je, ni tabia ipi huchukiza wanaume?

Ukiwauliza wanaume wengi kwenye ndoa asilimia kubwa watasema hawapendi kabisa tabia ya mwanamke kulalamika kwa kila kitu na wakati wote.

Kwa nini wanaume hawapendi mwanamke mlalamishi/mnung’unikaji?

Wanaume tangu utoto wao wamefundishwa kuwa tough, kuwa wavumilivu, kuwa unemotional, kuwa wanaume na zaidi kwamba tabia ya kulalamika si ya wanaume.
Matokeo yake wamekuwa watu dhaifu sana linapokuja suala la mtu mlalamikaji na hushindwa kuvumilia kuona mtu analalamika mnuda wote.

Wanaume pia ni watu wa ku-fix matatizo au kutoa solution na si kutafuta solution.
Mwanamke anapolalamika kwa mara ya kwanza humvuta mwanaume kuja kutatua tatizo na akiendelea kulalamika mwanaume hujisikia ameshindwa ku-fix hilo tatizo na hujiona failure mkubwa.
Kulalamika si njia njema ya kuuliza au kupata kitu kwa mwanaume bali ni njia bora ya kumfanya ajisikie vibaya.

Mwanamke mlalamishi ndani ya nyumba kwa mumewe muda wote hufanya mwanaume amuone ni takataka zaidi na kwamba hawezi kukufanya uwe happy na mwanamke usipokuwa happy maana yake mwanaume ameshindwa kazi ya msingi kabisa katika mahusiano.
Anajiona ni sawa na mwindaji anayerudi mikono mitupu nyumbani baada ya siku nzima ya kuwinda.

Wanawake wengi hutegemea sana mwanaume kuwa source ya furaha zao, huo ni mzigo mzito sana ambao mwanaume anaweza kuubeba.
Pia mwanamke unawajibika kabisa kujipa furaha mwenyewe kwanza, unapochukua jukumu la wewe mwenyewe kuwa mwanamke mwenye furaha na mumeo hujiona amefanikiwa sana hata kama hakufanya lolote kwa furaha uliyonayo na zaidi unapokuwa na furaha unaruhusu moyo wa mumeo kufunguka kirahisi kwako kuliko kuwa mwanamke mwenye uso usio na furaha kama vile ulilazimishwa kuolewa naye.

Pia kulalamika kunafanya mwanamke usiwe attractive, mwanamke unapolalamika kwa kila kitu na kila wakati mwanaume hukuona upo ugly na huvutii kabisa ndo maana wanaume wengi wanawatoroka wake zao kisa mwanamke ni mlalamishi na mwanaume anasema nimeshindwa kujua anataka kitu gani na pia nitawezaje kumfurahisha maana ni kulalamika tu kila siku.

Usiwe Chronic complainer maana kuwe na jua unalalamika, kusiwe na jua unalalamika.
kuwe na mvua unalalamika kusiwe na mvua unalalamika.
uwe na kazi unalalamika usiwe na kazi unalalamika.
Ukiwa mnene unalalamika ukiwa mwembamba unalalamika.
Uwe na mtoto unalalamika usipokuwa na mtoto unalalamika
Utaishi na nani?
Nani anataka mtu wa aina hii?
Jirekebishe!

posted from Bloggeroid

UPENDO KATIKA NDOA.

Kumpenda mtu ni uamuzi na ni kazi inayoendelea kila siku hivyo basi kila siku kuna mambo ambayo unapaswa kufanya.
Yafuatayo ni muhimu sana kufanywa kila siku ili kuhakikisha upendo katika ndoa yako unakuwa katika kiwango kinachofanya ujisikia kweli nina mwenzangu anayenijali na kunipenda.

1. Tumia dakika angalau 10 kuwa pamoja (quality time) bila kuingiliwa na watoto, TV, Simu nk, huu ni muda tofauti na mkiwa mmelala au mnakula chakula pamoja.
2. Mbusu kila unapoodnoka nyumbani asubuhi, unaporudi nyumbani na unapoenda kulala na wakati wowote mchana ukipenda.
3. Mwambie "Nakupenda"
4. Mkumbatie mara kadhaa kwa siku (zisipungue 6)
5. Cheka pamoja
6. Usimlaumu mwenzako bila sababu za msingi
7. Fanya jambo lolote linaloonesha unampenda na kumjali
8. Mpe maneno yanayomtia moyo na pia mpe sifa pale amefanya vizuri
9. Uwe mwema kwake.

posted from Bloggeroid

Thursday 11 February 2016

THAMANI YA NDOA.

Kama upo kwenye ndoa na upo kwenye tatizo kubwa, shida au mgogoro wowote na unajisikia kama ni wewe mwenyewe tu mwenye Matatizo ya ndoa, ukweli haupo mwenyewe kwa sababu kutokuwa na Matatizo hakufanyi ndoa kuwa imara bali ndoa huwa imara kwa sababu wanandoa wanajua jinsi ya kupambana na Matatizo kwa pamoja vizuri.

Ndoa imara na zenye afya zinajua jinsi ya kupambana na hali ngumu.
Ni kawaida kila ndoa kukutana na mambo magumu katika safari ya maisha duniani.
Wakati mnaendelea na mahusiano iwe uchumba au ndoa mnaweza kukutana na tuta kubwa la ugonjwa, kuachishwa kazi, kupoteza nyumba, kifo cha mmoja katika familia yenu kama vile wazazi, biashara kuyumba kabisa au kufirisika, hapo utafanyeje?
Tumesikia mara nyingi sana watu wakiwakimbia wapenzi wao au wake zao au waume zao pale moja ya hayo linapotokea.

Ukweli ni kwamba huwezi kujua ndoa yako au uchumba wako ni imara kiasi gani hadi pale utakapojaribiwa.

Matatizo yakitokea mara nyingi huweza kuvunja mahusiano vipande vipande mume huku na mke huko au wachumba kila mmoja kuachana na mwezake.
Lakini habari njema ni kwamba, wanandoa au wachumba ambao wanaweza kupita katika ugumu wowote pamoja kwa kushikamana kama super glue huwa na mahusiano imara yaliyoyoshikamana kwa nguvu za ajabu na kuwa na upendo imara kuliko mwanzo.

Wengi hujiuliza kwa nini hili litokee kwetu tu?
Kwa nini Mungu amenitupa kiasi hiki?

Ndoa si kunywa soda kila siku ukipata kiu, si kuwa na pesa kila siku, ndoa ni kazi, kazi inayohitaji kujitoa, hata hivyo matokeo ya kushirikiana pamoja hasa wakati wa shida kwa kushikamana bila kujali ugumu unaotokea ndoa huwa imara na yenye afya ya ajabu.

Wengine likitokea tatizo kwenye ndoa au uchumba solution ni kuacha na kutafuta mwingine, huo ni ujinga, kila binadamu ana Matatizo yake mapya kabisa na ovyo kabisa.

Jaribu kufikiria kwa nini ulimkubali na kuona anakufaa?

posted from Bloggeroid

HITAJI LA TENDO LA NDOA.

Wanawake hupenda kuguswa mwili mzima linapokuja suala la kusisimuana kimapenzi.
Ni mara chache sana wanaume hufahamu mwanamke anahitaji nini linapokuja suala la mapenzi na hata kama anafahamu basi akiingia chumbani baada ya muda kidogo anasahau na kuendelea kufanya kile anataka yeye.

Mwanamke anahitaji mwanaume mwenye mikono slow wakati wa kusisimuliwa na kuandaliwa kuwa tayari kwa tendo la ndoa, hata hivyo mwanaume akishakuwa amesisimka husahau na kuendelea kuwa na mikono mepesi kukimbilia sehemu muhimu ambazo mwanamke husisimka zaidi akidhani wote wanahitaji mwendokasi sawa.
Ni jukumu la mwanaume kufahamu mahitaji ya mwanamke wakiwa faragha hii ni kuhakikisha mwanamke anaridhika kupata kile anastahili.

Tendo la ndoa ni uzoefu wa tofauti kwa mwanamke na mwanaume pia, raha anayoipata mwanaume hasa akishasisimka ni hitaji kubwa la kutaka kuingiza na kutoa, kama vile nguvu ya kutaka kutoa risasi kwenye bunduki.
Mwanamke yeye akishasisimka na kuwa wet huwa na hitaji kubwa la kupokea, yaani hitaji la kutaka kitu kuingia ndani yake.

Kwa kuwa mwanaume huwa na nguvu hasa ya kutaka kutoa sperms ili kufika kileleni hivyo akishasisimka tu anatamani kuingiza na kutoa, wakati huohuo mwanamke akishasisimka huwa anakuwa na hamu kubwa ya kupokea, kuingiziwa kitu na kujaziwa hadi aridhike, hivyo basi kama mwanaume ana mwendokasi na kumaliza haraka hitaji la mwanamke kutaka kujaziwa raha inaweza isifike mahali panapotakiwa na matokeo yake hujisikia ametumiwa tu na mwanaume kufanikisha raha yake ya kuingiza na kutoa vitu vyake.


Jambo la msingi ni kuhakikisha mwanamke anaandaliwa na kupokea raha ya kutosha hata kabla mwanaume haja release na kumaliza raha yake.

Mwanaume anahitaji kuwa mtundu kuhakikisha anaanza kwanza na layers ambazo si sensitive moja baada ya nyingine huku akiwa na mikono slow ili kuhakikisha mwanamke anapata raha ya mwili mzima kabla ya kupokea kitu.

Kumbuka!
Mwitikio wa kusisimuliwa kwa mapenzi kwa mwanamke ni mzunguko unaohusisha saikolojia, mazingira na homoni pia anaweza kuathiriwa sana na hisia, mawazo, lugha, utamaduni na sababu za kibaolojia, hivyo kitu cha msingi ni kuhakikisha kabla ya kufika mbali ana hamu na anatamani tendo la ndoa.


posted from Bloggeroid

NDOA NI MFANO WA MBIO NDEFU.

Ndoa inafanana sana na ukimbiaji wa mbio ndefu (marathon) na hutoa matokeo mazuri sana pale wanandoa wanapofahamu kwamba mbio za ndoa yao si mbio fupi.
Sababu kubwa inayofanya wakimbiaji wa mbio fupi kushindwa kukimbia mbio ndefu ni kwa sababu akili zao wameziweka au zimezoeshwa kukimbia mbio fupi tu na si zaidi ya hapo.
Mawazo yao kichwani ni mita 100 tu na kuwaambia wakimbie mita 1000 husababisha kushindwa hata kabla hawajakimbia kwa sababu ya mindset zao na mazoezi na malengo ya taaluma zao.
Hatujawahi kusikia mkimbiaji maarufu wa mbio fupi (ameweza kupata medali ya mbio ndefu, ni vigumu mno.

Kwa nini ndoa nyingi huishia njiani?
Ndoa nyigi (si zote) huishia njiani kwa sababu wanandoa huanza safari ya ndoa kwa kuwa wakimbiaji wa mbio fupi badala ya mbio ndefu yaani marathon.
Hujawa na mawazo ya furaha muda mfupi badala ya kuangalia mbali zaidi miaka 100 ijayo.
Akiumizwa kidogo au kukutana na tatizo kubwa au shida nzito au jaribu kubwa hujiona kama hastahili kuumizwa na pia kama mwenzake anampenda basi amisha ya ndoa ni raha na mstarehe.

Mkimbiaji mzuri wa marathon hawezi kuacha kukimbia akipata maamivu kwenye miguu, au kuchoka au kushikwa na misuli au kukumbana na hali mbaya ya hewa jua kali au baridi kali huwa hakati tamaa huendelea kukimbia huku akivumilia kwani lengo ni kuhakikisha anamaliza hadi mwisho.

Wanandoa wengi huamini kwamba kama umempenda mtu basi ndoa itakuwa rahisi na mteremko kama nyikani kwenye mawindo, waulize wanandoa wote ambao wamekaa kwenye ndoa zaidi ya miaka 10 acha miaka 50, wote watakwambia walipitia hatua zote za kukutana na matuta, siku za giza nene, siku ambazo hujisikia kama mume au mke hafai tena kwa kuwa lengo ni mbio ndefu ndoa zao bado zina Baraka hadi leo.

Usiwe mkimbiaji wa mbio fupi, anza kujizoeza kuwa mkimbiaji wa mbio ndefu za ndoa yako.
Wakati unakimbia marathon kuumia au maumivu ni kitu cha asili hakikwepeki kilichopo ni kupambana tu.
Bila kuwa na maumivu huwezi kumaliza marathon na bila kumaliza marathon huwezi pewa medali.

Kuachana na kumkimbia mwenzako si jibu kwani hata ukae mwenyewe bado utakutana na shida acha zile za upweke na Ukisema utafute mwanaume/mwanamke mwingine huyo ndo atakupa shida mpya kabisa ambazo zitakupeleka ground zero tena.

posted from Bloggeroid

MFANYE MWENZIO KUWA NAMBA 1

Kila mmoja anapoacha baba na mama na kuanza maisha mapya na yule amempendaye, basi huwa amefanya uamuzi ambao ni wa maana na busara sana.
Mambo huwa ovyo sana, na huwa inakatisha tamaa sana unapoona mtu ambaye ulichukua uamuzi wa kuishi naye maisha yako yote anabadilika na kuweka vitu vingine kuwa namba moja badala yako.

Mwanaume au mwanamke anapoweka kitu kingine kuwa msingi kwake, kitu cha maana kwake, namba moja kwake na kutumia muda wote na uwezo wake wote kwa ajili ya hicho na mke au mume kuwa kitu cha pili yaani namba mbili.
Bila kumuweka mwenzi wako kuwa namba moja ujue hakuna kitu unaweza kununulia kwa pesa hapa duniani kikamridhisha na kuona unamjali na kumsikiliza.
Kwani hujasikia wanawake wengi ambao waume zao ni watu maarufu na wenye pesa wanalalamika kwamba bado hawahitaji pesa au vitu, wanachohitaji kupata muda na kupewa nafasi ya kwua pamoja, kusikilizwa na kujiona wanaume wanawajali.

Wapo wanaume ambao business ndo kimekuwa kitu cha kwanza kwake na mke anakuwa ziada na hata hudiriki kutoa pesa au vitu ili mke aridhike na kuona anamjali. Hii haina maana usifanye business ila lazima mke apewe muda wa pamoja na wewe na yeye kuwa muhimu.
Wapo ambao utadhani walizaliwa na TV na akiwa na TV mke au mume si lolote, TV anakuwa mke au mume.

Wengine hujikuta wanahangaika na kazi za kanisa (kazi za kanisa zingine si kazi za Mungu) fahamu ukristo wa kweli ni ule kanisa kuanzia nyumbani kwa mke na mume kuwa na amani ya kweli na maisha ya upendo kwa kutanguliza na kumjali mwenzako.
Wengi kazi za ofisini ndo zimekuwa mume au mke, Kumbuka kazi zipo ulizikuta na utaziacha mume au mke ni namba moja.

Wengine watoto ndo wamekuwa wa maana kuliko mume au mke nao pia wamewakuta na watawaacha wenyewe na maisha yenu, watoto wanahitaji upendo lakini isiwe wao wakasababisha mke au mume awe wa mwisho katika kusikilizwa.

Bila mume na mke kila mmoja kumpa nafasi ya kwanza mwenzake basi itakuwa ngumu sana kuwa na ndoa bora kama Mungu alivyopanga.

posted from Bloggeroid

MAHUSIANO YENYE AFYA.

Kuwa na mahusiano yenye afya kwenye ndoa au uchumba huhitaji nguvu za ziada wakati mwingine.
Hakuna kitu kizuri kama kuwa na mahusiano bora.
Pia hakuna kitu kizuri kama kupendwa na Yule unayempenda.

Hata hivyo kazi inahitajika kuhakikisha mapenzi yanadumu na kudumu kwani kuna milima na mabonde.
Pia bila kuvumiliana, kuchukuliana na kumtanguliza mwenzako kwa kusameheana na kutiana moyo bado mahusiano yanaweza kufika mahali yakashindikana.


posted from Bloggeroid

HATUA ZA RAHA NA VIKWAZO KTK TENDO LA NDOA.

Huanzia kwenye ubongo kwanza!Uumbaji wa Mungu ni wa ajabu sana hasa linapokuja suala la mahusiano Kati ya mwanamke na mwanaume katika ndoa.
Ili kuridhishana kimwili kati ya mwanamke na mwanaume jambo la msingi ni kufahamu vizuri hatua kamili ambazo ili tendo la ndoa likamilike lazima zifuatwe na hasara zake.

Hata hivyo wakati mwingine wanandoa hujikuta katika mgogoro katika eneo lingine la ndoa na matokeo yake masuala ya kitandani pia huwa ovyo na zaidi kuanza kulalamikiana kila mmoja akimlaumu mwenzake.
Kawaida tendo la ndoa hupitia hatua tatu muhimu ambazo ni vizuri kila mwanandoa kufahamu na pia ni muhimu kufahamu kwamba kila hatua huwa na vikwazo vyake na hili lisipozingatiwa unaweza kujisikia wewe tu ndiye unayepunjwa kwenye ndoa.

Hizi hatua tatu muhimu kila moja ina uwezo wake na mzunguko wake binafsi na vikwazo vyake.
Hatua ya kwanza ni hamu ya tendo la ndoa na ili kupata hamu ya tendo la ndoa lazima ubongo uhusike kwani kwenye ubongo kuna mfumo maalumu wa fahamu (neural) ambao kutokana na hali iliyopo mtu hujisikia hamu.

Hatua ya pili ni kusisimka hii ni hatuas ambayo baada ya kuwa na hamu damu huweza kusambaa sehemu muhimu kama vile matiti, uke au uume kwa ajili ya kuhakikisha sex inafanyika.

Hatua ya mwisho ni kufika kileleni hii hutokana na kukaza kwa misuli ya uke au uume na kutoa raha isiyoelezeka na baada ya hapo ni kama mwisho ya furaha ya tendo lenyewe.

Nini vikwazo vya hatua hizo muhimu?

Wasiwasi, hofu, mashaka, woga, kuogopa na uadui hupelekea mtu kukosa hamu ya tendo la ndoa.
Fadhaa zozote kuhusu sex hupelekea kukosa kusisimka na kuwa tayari kwa mapenzi pia ku-concentrate kwenye skills na techniques au style za sex kuliko kufurahia tendo lenyewe hupelekea kushindwa kufika kileleni.

Kumbuka utendaji wa sex katika ndoa huonesha hali ya ndoa nzima katika mambo yote kwani mara nyingi ndoa ikiwa na mgogoro hata tendo la ndoa huwa ni bora liende, si kuridhishana bali wajibu na ukweli unabaki kwamba sex katika ndoa huelezea ndoa ipoje.

Kama kuna mgogoro ambao haujapata jibu au kutokuelewana katika ndoa basi mfumo mzima wa sex hubadilika.

Je, unajisikia raha na hamu kubwa na kusisimka kwa ajabu kama zile siku za kwamba wakati mnaoana?
Je, jinsi unavyoridhika na tendo la ndoa ni sawa na ulivyokuwa unategemea? Au ni kama wajibu na si kupeana raha?
Ukweli unao mwenyewe.

Uzoefu unaonesha jinsi wanandoa wanavyozidi kuishi pamoja; tendo la ndoa huwa zuri zaidi na la kuridhisha zaidi kuliko mwanzo au miaka ya mwanzo.

posted from Bloggeroid

ULIMI HUWEZA KUJENGA AU KUBOMOA NDOA YAKO.

Maneno yetu huweza kubomoa ndoa kama mmomonyoko wa udongo!Utafiti unaonesha kuwa mtu mmoja kawaida huwa na maneno 5,000 ambayo hutumia kila siku kuongea kuhusu mawazo, hisia, matukio na mahitaji mbalimbali ya mawasiliano ya kila siku.

Na hayo maneno ambayo binadamu huongea kila siku yana nguvu ya ajabu mno hata kuweza kuponya au kuumiza, kutia moyo au kukatisha tamaa, kusifia au kulaumu, kuleta uhai au kuleta kifo, kuimairsha au kudhoofisha, kuleta ukweli au kuleta uwongo, kubariki au kulaani.

Pia maisha tunayoishi ni matokeo ya kile unaongea, hivyo basi kufanikiwa kwako au kushindwa kwako katika maisha au mahusiano mara nyingi ni matokeo ya matumizi ya kinywa chako.

Pia tafiti nyingi zinabainisha kwamba kinachoelezea mafanikio na kushindwa kwa mahusinao (ndoa) si uzuri wa mapenzi au kufanana kwa wahusika au kufanana kwa vitu wanavyovipenda au uchumi au umaskini au kiwango cha elimu cha wahusika bali ni maneno wanayoongea kila mmoja kwa mwenzake.

Wapo wanandoa ambao huongea maneno ambayo ni death sentence kwa ndoa zao au ni maneno yenye mtazamo hasi kwa kila jambo katika ndoa au mahusiano yao au kila kinachoongelewa wao huchuja na kuweka katika msimamo wa negatives.
Kumbuka maneno ya aina hii yasipobadilika huwa mfano wa seli za kansa kiasi kwamba huendelea kumomonyoa ndoa au mahusiano kama mmomonyoko wa udongo na huishia kuiua kabisa ndoa.

Kama ni mwanaume unahitaji kuongea maneno mazuri kwa mke wako kwa kadri unavyotaka awe.
Acha kuongea na kuendelea kusisitiza yale anafanya vibaya, jifunze kumsifia kwa mfano:-
“Mke wangu ni mzuri, mke wangu unapendeza, mke wangu una akili, mke wangu unanifaa, mke wangu ni mwanamke wa tofauti duaniani hakuna kama wewe, mke wangu ni mtamu, mke wangu una uwezo na hekima ya ajabu”

Na mwanamke naye ni hivyo hivyo lazima uongee maneno ya kujenga ndoa si kubomoa kama vile:-
“Eti mume wangu ni mbishi, mume wangu hunisikilizi, mume wangu hunijali, mume wangu huna akili, mume wangu huna lolote, mume wangu siku hizi hunivutii, mume wangu hanipendi nk”

Maneno unayotimia kwa mwenzi wako yanaweza kuumba hisia za furaha, upendo, ukaribu, sifa, kutia moyo, kufariji, kumpa nguvu, kumuinua pia maneno yako yanaweza kuumba hisia za maumivu na hasira na hatimaye kutoana ngeu.

posted from Bloggeroid

Wednesday 10 February 2016

HUATHIRI AFYA.

Kuolewa au kuoa ni kitu kingine na kujenga ndoa ni kitu kingine.
Ndoa yenye furaha huwa haijengwi siku ya ndoa au siku ya harusi au siku ya kuvalishana pete tu bali hujengwa kila iitwapo leo.

Ndoa inapokuwa na mgogoro mara nyingi (si zote) wanandoa huathirika zaidi na mara nyingi mwanamke huonekana ni makini na kuelekeza juhudi nyingi ili mahusiano yaendelee na kuwa yenye afya njema ( ingawa si wote)

Katika migogoro mingi ya mahusiano (Ndoa au uchumba) mara nyingi mwanamke ndiye huathirika zaidi.
Wanaume hata kama ndoa ina mgogoro bado huonekana wapo physically fit na mentally fit kabisa nakuendelea kujichanganya na wenzao kama vile hakuna linaloendelea ktk ndoa zao wakati wanawake ndoa ikiwa na tatizo basi kwa kumwangalia tu unaweza kupata ujumbe kamili achilia kukoswakoswa kugongwa na magari.

WHY?
Wanawake na wanaume hutofautiana sana jinsi ya kukabiliana au kuchimbua (ku-process) hisia (feelings), tukuto (emotions) zinazotokana na mgogoro uliopo.
Wanaume huweza kuvumilia tukuto na hisia zao bila kutegemea mwanamke au kuegemea kwa mwanamke, hii ina maana kwamba mwanaume hujikana, hujiondoa, huwa hajali, hu-withdraw hisia zake au kujisikia kwamba ana mgogoro na matokeo yake haathiriki sana.

Wakati huohuo mwanamke yeye kwanza ni mtu wahisia na tukuto (feelings & emotions ) tatizo likitokea hujihusisha zaidi, huji-engage, hujitoa (dedicate), huji-commit kupata solution, hujiuliza maswali wengine watasemaje? huwaza zaidi kuhusu yeye na mpenzi wake na jinsi ya kusaidia mgogoro uishe, matokeo yake huathirika zaidi na hudhoofisha afya yake na kuweza kukumbwa na magonjwa kama shinikizo la damu, stress, depression, stroke, magonjwa ya moyo nk.

MWANAMKE AFANYEJE?
Jambo la msingi ambalo mwanamke anaweza kufanya ndoa inapokuwa katika mgogoro ni kumuomba Mungu ampe hekima, busara na ushindi ili ndoa iwe katika mstari kwani ni jaribu na lazima ushinde, kila ndoa bora imejaribiwa na kuonekana imara, usione vinaelea vimeundwa.

Pia mwanamke anahitaji kuwa positive, kwamba anaweza na kwamba bado ndoa ipo, mume ni wake na aendelee kumpenda na kutamkia mambo mazuri mume wake kuliko kuwa na mtazamo negative.
Pia mwamke anahitaji kujiamini kwamba chanzo cha furaha yake ni Mungu hivyo hakuna binadamu anaweza kuondoa furaha yake hadi aamue mwenyewe.

posted from Bloggeroid

HUATHIRI AFYA.

Kuolewa au kuoa ni kitu kingine na kujenga ndoa ni kitu kingine.
Ndoa yenye furaha huwa haijengwi siku ya ndoa au siku ya harusi au siku ya kuvalishana pete tu bali hujengwa kila iitwapo leo.

Ndoa inapokuwa na mgogoro mara nyingi (si zote) wanandoa huathirika zaidi na mara nyingi mwanamke huonekana ni makini na kuelekeza juhudi nyingi ili mahusiano yaendelee na kuwa yenye afya njema ( ingawa si wote)

Katika migogro mingi ya mahusiano (Ndoa au uchumba) mara nyingi mwanamke ndiye huathirika zaidi.
Wanaume hata kama ndoa ina mgogoro bado huonekana wapo physically fit na mentally fit kabisa nakuendelea kujichanganya na wenzao kama vile hakuna linaloendelea ktk ndoa zao wakati wanawake ndoa ikiwa na tatizo basi kwa kumwangalia tu unaweza kupata ujumbe kamili achilia kukoswakoswa kugongwa na magari.

Kwanini?
Wanawake na wanaume hutofautiana sana jinsi ya kukabiliana au kuchimbua hisia (feelings), tukuto (emotions) zinazotokana na mgogoro uliopo.
Wanaume huweza kuvumilia tukuto na hisia zao bila kutegemea mwanamke au kuegemea kwa mwanamke, hii ina maana kwamba mwanaume hujikana, hujiondoa, huwa hajali, hu-withdraw hisia zake au kujisikia kwamba ana mgogoro na matokeo yake haathiriki sana.

Wakati huohuo mwanamke yeye kwanza ni mtu wahisia na tukuto (feelings & emotions ) tatizo likitokea hujihusisha zaidi, huji-engage, hujitoa (dedicate), huji-commit kupata solution, hujiuliza maswali wengine watasemaje? huwaza zaidi kuhusu yeye na mpenzi wake na jinsi ya kusaidia mgogoro uishe, matokeo yake huathirika zaidi na hudhoofisha afya yake na kuweza kukumbwa na magonjwa kama shinikizo la damu, stress, depression, stroke, magonjwa ya moyo nk.

MWANAMKE AFANYEJE?
Jambo la msingi ambalo mwanamke anaweza kufanya ndoa inapokuwa katika mgogoro ni kumuomba Mungu ampe hekima, busara na ushindi ili ndoa iwe katika mstari kwani ni jaribu na lazima ushinde, kila ndoa bora imejaribiwa na kuonekana imara, usione vinaelea vimeundwa.

Pia mwanamke anahitaji kuwa positive, kwamba anaweza na kwamba bado ndoa ipo, mume ni wake na aendelee kumpenda na kutamkia mambo mazuri mume wake kuliko kuwa na mtazamo negative.
Pia mwamke anahitaji kujiamini kwamba chanzo cha furaha yake ni Mungu hivyo hakuna binadamu anaweza kuondoa furaha yake hadi aamue mwenyewe.

posted from Bloggeroid

WANAWAKE HUWA HIVI.

Tatizo kubwa la wanawake wakiwa kwenye mahusiano (ndoa au uchumba) ni kwamba huwa wanasahau mahitaji yao na kujikuta wanavutwa na kuhusika zaidi na mahitasji ya wengine au wapenzi wao kihisia na kisaikolojia.

Challenge kubwa inaowakabili wanawake wote duniani wakishaiingia kwenye mahusiano ni uwezo wa kuimarisha sense of self, kujitambua, kujiamini, na kuanza na wao kwanza kabla ya mpenzi hasa linapotokea suala la mgogoro.
Wakati mwanamke hu-expand mwanaume hu-contract.
Kama ilivyo nguvu ya centripetal amabyo huhusika kuvuta kitu katikati (mwanaume) na nguvu ya centrifugal ambayo huhusika kuvuta kitu pembeni (mwanamke) kutoka katikati ndiyo ilivyo kwa mwanamke na mwanaume kwani mwanaume mara zote hurudi kwenye centerpoint hupungua, husinyaa, huongea kidogo, huongea kwenye point, wakati mwanamke yeye hupanuka kutoka katikati kwenda pembeni, huongea sana hata kama si point, huvutika kuongeza maongezi.

Ndiyo maana wanaume hulaumiwa sana linapokuja suala la mawasiliano kwani mwanamke na mwanaume wanapoongea mwanamke hu-expand maongezi na mwanaume hui-contract na kuongea kwenye point.

Kawaida mwanaume hufikiria kwanza (kwa ndani) kile anataka kuongea ili kujua kama ni point, wakati mwenzake mwanamke huendelea kuongea tu na anapoongea inamsaidia kuijua point,
Hii ina maana mwanamke huongea iliajue point na mwanaume hujua point ili aongee.

Bila kujua hii tofauti basi mwanaume asiyejali anaweza kusikitika sana kumsikiliza mpenzi wake na kuona alikuwa anaongea pumba au pointless na amempotezea muda wake au kuendelea kubishana kwamba mwanamke haongei point au kumkatisha kwa kuwa anachoongea hakielewiki.

Mwanaume anayejali husikiliza kwanza hata kama mwanamke anaongea kitu ambacho anahisi hakieleweki hata hivyo baadae ataelewa na mwanamke anajisikia mwanaume anamjali na kumsikiliza na maisha yanaenda

posted from Bloggeroid

ONYESHA UPENDO HUU KWA MKE WAKO.

Mwanamke anahitaji alama za upendo kutoka kwa mwanaume.
Mwanaume anapompelekea mwanamke (mkewe) zawadi hii hudhihirisha kwamba mwanamke ana thamani na anamjali, mfano zawadi ya maua huonesha kwamba mwanamke ni mrembo na ana uzuri ambao mwanaume anaukubali.

Iwe zawadi kubwa au ndogo zote hutoa maana halisi ya mapenzi, humsaidia mwanamke kufahamu kwamba yeye ni mwanamke special, na kumpa zawadi mwanamke ni njia ya kumpa heshima na thamani ambayo mwanamke huhitaji kutoka kwa mume wake.

Kuna alama nyingi ambazo huonesha kwamba unampenda mke wako moja ni kumpa zawadi mbalimbali kama maua au kadi yenye ujumbe unaoelezea hisia zako kwake nk.
Ni muhimu mwanaume kuwa creative na innovative katika kuhakikisha penzi linazidi kunawiri kila iitwapo leo katika ndoa yako na unajitahidi kutoa hisia zako original pale unampa zawadi au kumwandikia text message (sms) yoyote, kitu cha msingi afahamu kwamba kuna mwanaume anayemjali.

Wanaume wengi huwa wanakuwa wataalamu na wajuzi sana wa kuwapelekea wapenzi wao zawadi motomoto na kadi zenye maneno matamu matamu mwanzo wa mahusiano (uchumba au ndoa) na baada ya muda wanaachana kabisa na hiyo tabia, hili ni kosa kubwa sana ktk masuala ya ndoa, kutoa zawadi hakuzeeki wala ku-expire hudumu na kudumu na kudumu, till death do us apart, ni njia muhimu sana ya Kuonesha unamjali mke wako.

Kama ni mwanamke unakumbukani lini mpenzi wako amekuletea zawadi?
Na kama ni mwanaume je, unakumbuka ni lini umempelekea mke wako zawadi?
Eti haya mambo yamepitwa na wakati!
Shauri yako!
Usione vinaelea vimeundwa!

Wanawake wengi kwenye ndoa au mahusiano hujisikia na kujiona hawapendwi na waume zao, hujisikia wanaume hawawajali, ukiangalia kwa undani moja ya sababu ni mwanaume ameacha kumpa zawadi hata ndogondogo, au maneno mazuri (notes) au kadi kama alivyokuwa anafanya mwanzo na kwa sababu ulikuwa unampa na ueacha anajiona humpendi tena, si ulikuwa unampa? sasa imekuwaje? unampelekea nani tena? maana ulikuwa na tabia ya kutoa zawadi.

Kiwango cha attention unayompa mke wako ni alama muhimu ya Kuonesha upendo wako kwake.

Mwanamke hujisikia anapendwa na kwamba unamjali pale mwanaume:-
Unampompa zawadi iwe ndo au kubwa,
Unapompa zawadi ya kadi yenye maneno mazuri yanayoelezea hisia zako kwake,
Unapomhudumia kwa kumjali,
Unapomsikiliza yeye na kujiona anasikilizwa,
Unapjitolea kumsaidia kazi ndgondogo na mambo ambayo anajisikia upo na yeye,
Unapompa plan za mambo mbalimbali mnayotaka kufanya pamoja kama familia iwe "outing", likizo, business n.k,

Pale unapomuuliza anavyojisikia hasa baada ya kazi au unapohisi emotions zake hazipo sawa,
Unapochukua muda wa ziada kuwa naye na kuwa kwa ajili yake,
Unaposhirikiana naye ktk huzuni au tatizo huku ukimfariji na kumkumbatia,
Unapompa nafasi ya kujisikia huru kwako hata kudeka (si wote)
Unapogundua kwamba amevaa amependeza mavazi na nywele na kumpa sifa anazostahili.
Unapom-surprise na zawadi au notes na
Unapompigia simu ukiwa umesafiri na kumuulizia anaendeleaje na jinsi gani utakuwa unaongea naye na kuwasiliana naye.

posted from Bloggeroid

JE,NDOA INAKUCHANGANYA

Je, unapita katika ndoa ngumu hata unawaza sijui kesho itakuwaje?
Kila siku ikipita unaona afadhari ya jana kwa kwani ndoa ni ngumu, ipo ovyo, kupigana kila wakati, kitu kidogo basi mzozo mkubwa huzaliwa, nyumba ni moto, ni kudharauliana tu na visa kila iitwapo leo?

Kwa tabia mbaya alizonazo partner wako unajilaumu hata kwa nini ulichukua uamuzi wa kuoana naye.
Kila ukimtazama sasa hana mvuto kabisa, amechuja, ni mbaya na havutii, hapendezi tena na anakutia kichefuhcefu unatamani mlale vyumba tofauti au asafiri miaka isiyojulikana.

Unaanza kufikiria kuachana ndiyo njia rahisi na kwamba ni permanent solution.
Wakati huohuo mawazo yako na akili yako na moyo wako na nguvu zako zote umeelekeza nje, kwa partner mwingine ambaye unaamini kwa moyo wako kwamba ni mzuri, mtamu, yupo single, independent, loving, romantic, caring na ukiwa na yeye basi maisha yatakuwa matamu zaidi.

Hata umeamua kubadilisha marafiki ili kukubaliana na nafsi yako kwamba ukiwa na hao marafiki wapya ambao ni single na wenye tabia mpya kama yako basi dunia itakupa kile unahitaji.

Ukweli ni kwamba mambo si rahisi kama unavyofikiria.
Pia ni kweli mawazo kama haya (mawazo ya kujenga nyumba kwa mabua) huwapata wengi sana kwenye ndoa zetu.
Hebu vuta pumzi, pumua upya na jikusanye na kuanza kufikiria upya hata kama ndoa unaona haina ladha, imekuwa upside down, umeshindikana na haina mwelekeo ukweli bado unaweza kuirudisha kwenye siku zake za honeymoon.

Wakati unaendelea kufikiria jinsi utakavyokuwa unajirusha na partner wako mpya katika viwanja mbalimbali, please fikiria kwanza watoto wenu (mtoto), pata picha jinsi utakavyowaambia watoto kwamba wewe na mwenzako mmeachana na wao sasa wanaishi na mzazi mmoja.
Fikiria jinsi ya kugawana picha zilizomo kwenye Album yenu ya harusi, Fikiria mtakavyoanza kugawana mali.
Fikiria utasema nini kwa Mungu maana uliahidi mbele zake na mbele za wandamu kwamba utaishi na hii ndoa hadi kifo kitakapowatenganisha.
Fikiria familia, ndugu, marafiki nk
Na cheti cha ndoa je, rings je?

Je, bado unamawazo ya kuachana naye?
Una uhakika hakuna mambo mazuri kwake kuliko mambo mabaya?
Usije kuwa unataka kubadilisha seat kwenye meli ya MV Bukoba ukaishia kuzama ziwa Victoria.

Naamini unadhani kwa sura aliyonayo huyo partner 2 basi hutapata matatizo au migogoro yoyote.
Ukweli ni kwamba hata ukipata partner mpya kinachobadilika ni sura tu matatizo ni yaleyale kwani wote ni binadamu na ndoa imara si kukimbia matatizo bali kukabiliana nayo na kujifunza na kuendelea mbele.
Je, umeshaomba ushauri kwa kiongozi wako wa dini naye akashindwa? washauri wa mambo ya ndoa nao wakashindwa?

Tafiti zinaonesha wengi walioamua kuachana na kuanza ndoa mpya baada ya muda hukutana na matatizo makubwa zaidi na magumu zaidi kuliko yale ya kwanza na hutamani kama wangerudi kwenye ndoa zao za kwanza.

Kitakachokusaidia ni kubadilisha mtazamo siyo kubadilisha ndoa na ukweli ni kwamba ni rahisi kubaki kwenye ndoa kuliko kuanza ndoa mpya.

posted from Bloggeroid

SI LAZIMA UJUE KILA KITU.

Kila mtu duniani ana siri zake binafsi na kuna wakati hapendi mtu yeyote ajue ila ni yeye na Mungu wake.
Si siri tu bali hupenda kuwa mwenyewe na kujiamulia mambo yake mwenyewe kwa kadri anavyotaka.
Unapokubali kuoana na mwanaume au mwanamke maana yake unaruhusu kuanza maisha ya pamoja (sharing) katika hisia, emotions, kazi, kitanda, bafu, harufu, nguo nk.
Hata hivyo hii haina maana kwamba tunawajibika upande mwingine yaani mume au mke kujua kila kitu kwani kila mmoja huhitaji kuwa na siri au kufanya kitu mwenyewe.

Hapa ninazungumzia vitu ambavyo ni vizuri havina uhusiano na tabia mbaya kama ulevi au kukosa uaminifu.

Hata hivyo wapo wanaume zetu au wake zetu hutaka kujua kila kitu tunachofanya na kila mahali tulikuwa zaidi ya mama zetu walivyokuwa wanatuchunga wakati watoto.

Kama mwanaume umeenda kazini, mkeo anataka kujua kwanza wakati unaenda kazini uliongea na nani, umefanya nini, umekula nini na nani, ulipotoka kazini ulipitia wapi, na mlikuwa na nani na atachukua simu ya mkono na kuanza kuangalia nani alipiga, nani alipigiwa na nani alikutumia sms na nani alitumiwa, ni kuchunguzana na kuulizana zaidi ya FBI.
Maswali mengi utafikiri ndoa ni mahakamani.
Mume anaogopa hadi kurudi nyumbani maana anaona ni usumbufu.
Kwani ni lazima ujue kila kitu?
Ukweli kama wewe ni mwanamke si lazima ujue kila kitu kuhusu mume wako, alikuwa wapi, alikuwa na nani, amefanya nini na ilikuwaje nk, kuna vitu ni non of your business.

Inawezekana unajua kutoka kazini hadi nyumbani huwa anatumia dakika 20 lakini sasa ametumia dakika 50, ile anafika nyumbani tu unambana na maswali ajieleze alikuwa wapi, alikuwa na nani, na analikuwa anafanya nini na ilikuwaje, inawezekana alipitia kwa rafiki zake aliosoma nao pia si lazima ujue kila kitu yeye ni mtu mzima si mototo tena, yaani anajisikia kama vile wewe ni mama yake kitu ambacho kinakupunguzia alama na anahisi hujiamini na pia msumbufu na humuamini.
Kama anataka kuishi na mtu anayetaka kujua kila kitu kuhusu yeye, basi angebaki kwa mama yake na si kuoana na wewe.

Ukweli si lazima ujue kila kitu kuhusu yeye, mwamini, mpende, mfurahie hata kama amechelewa kwa muda kidogo zaidi na alivyo kwambia.

posted from Bloggeroid

Tuesday 9 February 2016

USIWE NA MATARAJIO MAKUBWA.

Wakati wa uchumba noti zinatoka kirahisi, ukiolewa tu bajeti inabana!Baadhi ya wanandoa wapya mwaka wa kwanza wote huwa bado ni wakati wa honeymoon pia, kwa ndoa zingine unapoisha mwaka tayari tofauti huanza kujitokeza na kama si tofauti basi baadhi ya ahadi ziliahidiwa wakati wa ndoa huanza kuota mabawa.

Habari njema ni kwamba kati yao wanandoa hakuna aliye na kosa wote wapo sahihi kwa kuwa hakuna mzoefu wa ndoa wote wanaanza kupata uzoefu mpya hivyo tofauti lazima ziwepo ili wapate uzoefu.
Inawezekana wewe unapenda kusikiliza muziki kwa sauti ya chini na mwenzako anapenda husikiliza muziki kwa sauti kubwa kama vile ni Dj.
Inawezekana wewe unapenda kutazama movie kimya kimya ila yeye anataka kuielezea hadi kila hatua movie inavyoenda hadi inakuwa usumbufu na hakuna maana ya kuangalia hiyo movie. Inawezekana yeye anapenda sex kabla ya kulala na wewe unapenda sex kabla ya kuamka asubuhi sasa inakuwa vurugu maana hakuna maelewano.
Inawezekana yeye anapeda maombi (kuomba Mungu) kabla ya kulala wewe unapenda maombi kabla ya kuanza siku asubuhi.
Inawezekana kabla ya kuoana ulikuwa anajitahidi kujiweka portable lakini sasa amenenepeana kama kitimoto.

Matatizo mengi ya mwaka wa kwanza katika ndoa mpya huweza kuepukika kwa kupunguza matarajio juu ya mwenzako na juu ya ndoa yako na kwamba kila kitu kitakuwa kama unavyotaka wewe.
Pia usitegemee kwa kuwa anakupenda basi kila kitu atafanya na kuwaza kama unavyotaka wewe.
Punguza matarajio!

MFANO.
Jerry alikuwa mwema sana linapokuja suala la pesa wakati wa uchumba kabla hajamuoa Prisca
Alikuwa tayari kumnunulia zawadi yoyote, kitu chochote, na wakati mwingine alimpa pesa Prisca atumie anavyotaka yeye na afanyie kitu chochote anachojisikia kufanya kama vile kwenda saloon kujiweka sawa au kununua pamba anazotaka nk.
Baada ya kuoana ndani ya mwaka mmoja,Jerry amekuwa mchungu wa pesa hadi Prisca anahisi kama ni mwanaume tofauti na yule wa wakati wa uchumba.

Sasa ni mgogoro kila linapokuja suala la matumizi ya pesa na Jerry kila mara aamlaumu mkewe Prisca kwamba hajui kutumia pesa vizuri na anatumia ovyo kwa vitu visivyo na maana kama kwenda saloon kutengeneza kucha na nywele.

Ukweli ni kwamba mwanaume akiwa kwenye uchumba huwa anajitahidi sana kumfurahisha mwanamke ili avutike na hatimaye aoe na akisha oa anaanza kuwaza kuhusu watoto shule, kujenga nyumba, kuwekeza nk. na mipango mingie endelevu ya maisha.

Mwanamke anahitaji kupunguza matarajio otherwise awe na pesa zake mwenyewe kwa ajili ya mambo ya ziada.
Jambo la busara ni kuacha kuzozana kwa issues ndogo kama hizo jaribu kupunguza expectations na jenga familia.
Kumbuka hakua mtu anaweza kuondoa furaha yako au kukufanya ujione inferior hadi uamue mwenyewe so be you.

posted from Bloggeroid

MAHABA YA ASUBUHI.

Kama wewe upo kwenye ndoa basi utafiti unaonesha kwamba kufanya sex asubuhi hukuweka kwenye afya njema zaidi.

watafiti wanasema kwamba sex mara tatu asubuhi kwa wiki hupunguza uwezekano wa kupata heart attack, au stroke kwa nusu nzima na kufanya mapenzi mara kwa mara asubuhi huimarisha mzunguko wa damu na kupunguza blood pressure.

Kufanya mapenzi asubuhi husaidia kupunguza kupata kisukari kwani kwa kitendo hicho unaweza kuchoma idadi ya calories 300.

Pia sex asubuhi huweza kupunguza arthritis (maumivu kwenye viungo kama magoti nk) pia husaidia kuzalisha homoni za testosterone ambazo husaidia mifupa na mishipa kuwa imara.
Pia mahaba ya asubuhi pia husaidia nywele kung’aa na kunawiri vizuri pamoja na ngozi kwa kusaidia uzalisha kiwango kikubwa cha oestrogen na homoni zingine zinazofanana na hiyo.

Pia utafiti ulionesha kwamba wanawake ambao waume zao hawakutumia condom walikuwa ngangari linapokuja suala la stress na depression ukilinganisha na wale ambao waliuwa wanatumia condom wakati wa sex.

Pia watafiti wana onya kwamba mahaba ya asubuhi yasiwe yale ya kuchosha kwani yanaweza kusababisha kuwa na immune system dhaifu.

posted from Bloggeroid

HATUA MUHIMU ZA NDOA.

Binadamu yeyote aliyezaliwa na mwanamke mara nyingi maisha yake huathiriwa sana na muamuzi yake na uchaguzi anaofanya, na moja ya uchaguzi na maamuzi ni suala la ndoa.
Tangu wawili mume na mke wanapooana ndoa hupitia hatua mbalimbali hadi mmoja anapokufa na baadae mwenzake kufa baadae na ndoa kuwa historia.
Zifuatazo ni hatua muhimu ambazo ndoa nyingi hupitia si lazima ndoa ipitie kila hatua bali ni ukuleles cha hatua mbalimbali ndoa hupitia na kama upo kwenye ndoa unaweza kujua ndoa yako ipo stage ipi kati ya hizi nne muhimu.

1. MAHABA:
Wanandoa wote wamepitia hatua hii, kwani ndiyo hatua iliyowapa sababu ya kuamua kuoa kwa kupeana ahadi za kuishi pamoja hadi kifo kitakapo watenganisha.
Hapa maisha ni matamu, kupendwa ni kutamu na bila mwenzako (partner) maisha unaona hayana maana kabisa.
Kila mmoja yupo romantic ni raha.
Kila mmoja hutoa maneno matamu yenye Kuonesha mapenzi ya kweli kama vile "I mis you baby!" "You are mine", I love u nk, pamoja na kupeana vizawadi vya kila aina.
Hupeana ahadi za kushinda hata wanasiasa wanapongombea vyeo utasikia “nitakupenda milele‘, ‘hakuna mwanamke mzuri kama wewe‘, ‘hakuna mwanaume wa maana kama wewe”

Huwa kunakuwa na tofauti lakini tofauti hazionekani kwani humezwa na “fall in love”
Hata wakilala hukumbatiana kama wote ni mwili mmoja.
Wanandoa wengine hii hatua hudumu kwa muda wa kuanzia miezi sita hadi miaka mitano ya kwanza.

2. MAUZAUZA:
Katika hatua hii ya pili zile tofauti ndogondogo ambazo zilikuwa hazionekani sasa huanza kujitokeza na kwa mbali huanza kukera na kusumbua na kuudhi.
Vitu vile vile ambavyo Mwanzoni vilikuwa havina maana au vilikuwa havisumbui wala kuudhi sasa huanza kuudhi na kusumbua wanandoa.
Mmoja au wote huanza kulalamika kwamba mwenzake sasa hawi kama anavyotaka, hii ina maana sasa tofauti zinaanza kujitokeza na kuonekana.

Sasa spouse anaanza Kuonekana si perfect kama ulivyokuwa unadhani.
Ndoto za kuwa ulikuwa na bonge la partner zinaanza kuyeyuka kama barafu kwenye jua, unaanza kulinganisha na wengine.
Unaanza kujiuliza na kama kuna mtu alikushauri kwamba partner anatatizo unaweza kuanza kukumbuka ushauri wake hata kama hakuwa sahihi.
Wengine kwa hatua hii tu huanza kuwaza kuhusu talaka ingawa walio na hekima na hofu ya Mungu ndani yao huanza kuchukua hatua ili kupata solution.

3. MAJONZI, MATESO NA TABU

Hapa kama mtu ni mlevi basi hujikita nakuweka mizizi na hali kuwa mbaya zaidi.
Hapa wengine ndo huanza extra marital affairs, na wengine husikia maneno yanayoumiza kutoka kwa spouse wao kiasi kwamba hujiuliza hivi huyu ndo Yule nilikubali kuishi naye?

Ndoa huingia kwenye majonzi, majuto, mawazo, stress, BP, depression, kukosa usingizi, katakana, kudundana, ngeu, kulala mzungu wa nne, wengine vyumba tofauti.
Hapa ndo talaka nyingi hutokea, ni hatua ambayo imeumiza watoto wengi sana ambao walikuwa na wazazi wawili na kujikuta wakiishi na single parent.
Ndoa huwa katika mtihani, ndoa huwa katika maumivu makali kama ya jino ambayo huathiri mwili mzima.

Inaweza kutokea Mwanandoa mmoja akawa anataka talaka au ndiyo huyo mmoja analeta kasheshe zote na mwingine ndo anataka mambo yaishe na kupata suluhu.
Hapa ni mahali ambapo mwanamke au mwanaume anahitaji Kuonesha uwezo,hekima ubunifu, moyo mkuu, kutokata tama, kuwa imara, kusimama imara ili kuhakikisha anabadilisha machungu yote kuwa furaha, amani, na upendo na ndoa kuwa imara kuliko mwanzo.
Wengi wanaoachana (talaka) kwenye hii hatua wakioa mwanamke mwingine au kuolewa na mwanaume mwingine baada yamuda hujikuta anaingia kwenye matatizo yaleyale na kuanza kujiona ana mkosi au bahati mbaya kupata aina ileile ya partner, ukweli ni kwamba hajui jinsi ya kupambana na matatizo ili kupata solution.

4. KUAMKA, KUCHANGAMKA NA FURAHA MPYA
Kumbuka wote wanaoishia hatua ya 3 na kuamua kutengana si watu wabaya, bali tatizo kubwa ni kwamba walikosa tools au walikosa kujua tools zinazotumika kujenga ndoa imara.
Ndoa imara si ile isiyokutana na dhoruba bali ni ndoa ambayo inazishinda aina zote na dhoruba nakuendelea mbele kwa kasi ya ajabu.
Hata kama ndoa imekondeana na kubaki mifupa ambayo hata mtoto wa chekechea anaweza kuhesabu mifupa, bado inaweza kutiwa stake na kuwa nene ikapendeza zaidi kuliko mwanzo.
Ndoa si romance kama tunavyoangalia kwenye magazeti na TV ndoa ni maisha halisi pamoja na kukutana na setback na kuzigeuza kuwa viungo vitamu kuifanya ndoa kuwa na furaha, amani na upendo kila siku.

Kwenye hii hatua Mwanandoa huanza kuaminiana kuliko kawaida kwa sababu wanajuana na pia wametoka mbali na wamepitia mengi na wamejifunza.

NB:
Si lazima ndoa yako ipitie hatua zote 4 unaweza kuwa kwenye hatua ya kwanza miaka yako yote kama utaruhusu Kristo kuwa kiongozi wa ndoa yako kwani kama yeye anavyolipenda kanisa basi mume na mke wanahitaji kuishi kwa mfano wa Kristo na kanisa.

posted from Bloggeroid

NDOA NI MFANO WA "U"

Ndoa ni msingi wa jamii yoyote duniani.
Pia malezi ya watu katika jamii huanzia katika ndoa.
Hii ina maana katika ndoa bora tunapata taifa bora.

Linapokuja suala la ndoa mambo mengi hushangaza sana watu na wanandoa wenyewe.
Wengi hujikuta na mauzauza ya kushangaa yule alikuwa naye mbele ya kanisa na mbele za mungu kufungishana ndoa kuuthibitisha ulimwengu kwamba nimepaa liubav langu, na baada ya kukaa kwenye ndoa miezi, au mwaka au miaka anakuta ni mtu mwingine kabisa kwa tabia na kila kitu kama vile kabla ya ndoa alikuwa mwingine na baada ya ndoa ni mwingine.

Habari njema ni kwamba maisha ya ndoa yapo mfano wa U shape kwa maana kwamba wakati wanandoa wanakutana kabla ya kuoana upendo huwa juu sana na mahaba huwa katika kiwango cha juu, then yanakuja mauzauza na jinsi miaka inavyoenda basi huko mbele mahaba na upendo huanza kurudi na upanda juu tena kukamilisha umbo la U.
Hata kama ndoa yako inakukatisha tamaa namna gani bado tumaini lipo na kwa msaada wa Mungu unaweza kurudi na kukamilisha umbo.

posted from Bloggeroid

USIJARIBU KUMFANANISHA NA WENGINE.

Kuna wakati huwa inashangaza sana ukisikia yale wanandoa wanafanya au wanataka yafanyike katika ndoa zao.

Kama ni mwanamke basi una marafiki wanawake wenzako ambao waume zao inawezekana wana pesa nyingi kuliko mumeo, wamesoma kuliko mumeo, wana mali kuliko mumeo, wana akili kuliko mumeo, wanakuwa na muda zaidi na familia zao kuliko mumeo, wakivaa wanapendeza kuliko mumeo na pia wanabembeleza wake zao kuliko mumeo, au wana tabia njema kuliko mumeo au kama wewe ni mwanaume nawe una marafiki wa kiume ambao wake zao wapo hivyo.

Je, ni mara ngapi umemlalamikia mumeo au mkeo kwa kumlinganisha na wanaume wengine au wanawake wengine?
Inawezekana umemlalamikia mumeo au mkeo kwamba
“Mwenzako jerry amepunguza uzito wewe umebaki umenenepeana kama kitimoto kwa nini?
“Mwenzako George amenunua gari wewe nini kinakushida , wewe ni mwanaume gani?”
“Mwenzako mama Noel kila siku ukienda kwake nyumba safi wewe inakuwaje chafu namna hii”
Kama ni wewe utajisikiaje?
Hapa msipotoana ngeu au kuzuka zogo basi kati yenu mmoja hana baadhi ya homoni fulani fulani mwilini ndo maana kabaki kimya.

Kitu cha msingi ni kujikubali kwamba huwezi kupata kila kitu au mwenzako kuwa kama walivyo wengine kama vile umeoana na “mr right or mrs right”

Dunia itakuwa na ndoa za ajabu sana kama wote tungeamua kila tunachokiona kwenye ndoa zingine lazima tuwe nacho.
"Furaha si kuwa na kila kitu unachohitaji bali ni kuhitaji kile ulichonacho".


posted from Bloggeroid