Friday 12 February 2016

UPENDO KATIKA NDOA.

Kumpenda mtu ni uamuzi na ni kazi inayoendelea kila siku hivyo basi kila siku kuna mambo ambayo unapaswa kufanya.
Yafuatayo ni muhimu sana kufanywa kila siku ili kuhakikisha upendo katika ndoa yako unakuwa katika kiwango kinachofanya ujisikia kweli nina mwenzangu anayenijali na kunipenda.

1. Tumia dakika angalau 10 kuwa pamoja (quality time) bila kuingiliwa na watoto, TV, Simu nk, huu ni muda tofauti na mkiwa mmelala au mnakula chakula pamoja.
2. Mbusu kila unapoodnoka nyumbani asubuhi, unaporudi nyumbani na unapoenda kulala na wakati wowote mchana ukipenda.
3. Mwambie "Nakupenda"
4. Mkumbatie mara kadhaa kwa siku (zisipungue 6)
5. Cheka pamoja
6. Usimlaumu mwenzako bila sababu za msingi
7. Fanya jambo lolote linaloonesha unampenda na kumjali
8. Mpe maneno yanayomtia moyo na pia mpe sifa pale amefanya vizuri
9. Uwe mwema kwake.

posted from Bloggeroid

No comments:

Post a Comment