Thursday 31 March 2016

KUPOTEZA HISIA..

“Nimepoteza hisia za kumpenda, zimepotea na zimepotea kabisa.
Simpendi kabisa mke wangu na hata sifahamu kama kweli niliwahi kumpenda; nashangaa na sihitaji kuwa naye tena, sijisikii chochote linapokuja suala na hisia zangu kwake naamini ndoa imefika mwisho” Jerry aliongea kwa mshangao mbele ya mkewe.

Mkewe naye akajibu kwa kusema “hata sielewi tumefikia vipi hatua hii.
Tunaongea mara chache sana na hata tukiongea hatuongei jema lolote, (machozi yanaanza kumiminika kwenye mashavu) ni kulaumiana, kudharauliana, kusutana, kila mmoja anampuuza mwenzake, ndoto zimeyeyuka na hakuna ladha ya maisha.
Hapa nina maumivu makali.
Hivi inawezekana mtu ukashindwa kabisa kumpenda mtu ambaye alikuwa bila yeye maisha hayana maana?

Hali kama hii huwakuta wanandoa wengi na watu wengi walio katika mahusiano; haijalishi ni miaka mingapi au mlikuwa mnapendana kiasi gani na bila kujifahamu vizuri na kutumia busara na hekima kumaliza hili tatizo ndoa au mahusiano huweza kujikuta yameangukia kwenye shimo lefu mno.

Kila ndoa ina positive na negative moments, mwanandoa mmoja akiwa anamwangalia mwenzake kwa negatives tu itafika mahali ataanza kuji – withdraw na kujiweka mbali na automatically ataanza kujisahau kuwa caring. Wakati mmoja anajiweka mbali na mwenzake huyu mwingine huanza ku-panic na kuanza kutoa lawama kwamba hupendwi. Wanavyozidi kusuguana ndivyo wanazidi kusababisha mafuriko ya lawama emotionally na matokeo ni kuwa disconnected katika emotions na feelings.


Kuna utafiti kuhusiana na positives na negatives kwenye suala la ndoa na mahusiano na kutoa jumuisho kwamba quality ya emotions ilizonazo kwa mwenzi wako ni muhimu sana.
Ni simple lakini muhimu sana katika mahusiano.

Kama positives zitakuwa nyingi kuliko negatives unavyomchukulia mwenzi wako basi mahusiano yatakuwa bora sana, haleluya Kubwa!
Na kama negatives zitakuwa nyingi kuliko positives katika hisia kwa mwenzi wako basi shughuli nzito inakuja mbele yenu!

Ukweli ni kwamba negatives moja huhitaji positive tano ili kufanya balance ya ndoa au mahusiano kuwa katika hali nzuri (feelings).
Hii ina maana ukimbomoa mwenzi wako mara moja basi inabidi umjenge mara tano zaidi ili ku- balance ule uharibifu umefanya mara moja.
Kila negative moja unahitaji positive tano ili emotions na feelings za mapenzi yenu kurudi kuwa katika hali ya kawaida.


Wednesday 30 March 2016

NI MUHIMU PIA..

Ulipooa au kuolewa kulikuwa na sababu na pia ulifanya commitment kuhakikisha unatumia muda wako wote wa maisha yako na yeye milele na milele au hadi kifo kitakapowatenganisha.


Kama unataka kuwa na mume mzuri anayehakikisha anakutunza wewe na watoto wako na ana ku-treat vizuri au kama unataka kuwa na mke ambaye siku zote mambo ni safi kila siku, basi unahitaji ku-invest vilivyo kwenye ndoa yako.
Jitahidi kumpa romantic life kila iitwapo leo, kufanya juhudi kukitunza kile ulichaonacho, kwani usione vinaelea vimeundwa na wewe pia unaweza kukiunda chako kikaelea, uwezo unao na muda ni sasa.
Ili ndoa iwe imara unahitaji kutumia muda wako na nguvu zako ili maisha yawe safi wewe na mpenzi wako.

Kuna vitu tunaviita vidogo sana ambayo ni muhimu sana katika kila ndoa yenye furaha na afya, hivi vitu havilengi kufanya mapenzi (tendo la ndoa) moja kwa moja



Hivi ni vitu muhimu na havitakiwi kuachwa kwa kila ndoa imara na yenye afya na ndoa imara na yenye afya huleta raha si kwa wahusika tu bali kwa familia nzima kwa jamii inayowazunguka na taifa pia.

Ni vitu gani hivyo vidogo Muhimu?

Kumpa mgusu wa kimwili mwenzako,

Kumshika kwa mikono yote (holding),

Kumkumbatia.

Kuongea pamoja au kumsikiliza mwenzanko dakika 10 au 15 kila siku.

Kuongea na mwingine kumsikiliza mwenzake kila siku kunajenga ukaribu na kuaminiana, na kupeana mguso wa kimwili kila usiku na asubuhi husaidia kila mmoja kujiona ni wa thamani kwa mwenzako.

Inakuwaje hapo?
Je, umewahi kusikia kitu kinaitwa "Njaa ya ngozi"

Basi, njaa ya ngozi ni mwitikio wa kihisia kutokana na kukosa kuguswa kimwili.
Binadamu huhitaji kiwango fulani cha kugusana ngozi kwa ngozi kila siku ili kuishi na kukosa hicho kitendo basi ngozi hupata njaa na matokeo yake mtu hudhoofika.

Njaa ya ngozi ndiyo inayosababisha sana wapenzi kutaka kufanya tendo la ndoa
Katika milango mitano ya fahamu, kugusa ndiyo mlango pekee wa fahamu unaojulikana kuwa ni muhimu kuliko yote, kitaalamu umuhimu wa kuguswa (touch) huzidi ule wa chakula.
Kuguswa ni mlango wa kwanza wa fahamu kujitokeza wakati wa mtu anazaliwa na huwa mlango wa mwisho wa fahamu wakati mtu anakufa.
Na kuna wana ndoa wengi sana wanapata njaa ya ngozi bila wao kujijua hapa hatuzungumzii kufanya mapenzi bali tunazungumzia nonsexual touching kama vile kukumbatia, Mguso wa mtekenyo.

Kuguswa (touch) ni moja ya muhitaji muhimu ya Binadamu hivyo Hakikisha kila siku unampa mpenzi wako Mguso wa kimahaba iwe kumpa busu huku umemshika au umemkumbatia.


Kitu kingine kidogo muhimu ni nini?
Kitu kingine muhimu ni kwa mwanamke kuwa na vivazi vinavyoacha mwili wazi ukiwa chumbani.

Tafuta chupi ambazo zinavutia kwa mume wako kukuangalia mkiwa wawili tu hata kama hamjapanga kufanya mapenzi hiyo inampa hamu na kujiona anakuhitaji zaidi kila siku.
Kuna wanandoa ambao kwao kuwa mikao ya hasara hasara na uchi chumbani ni mwiko, hapo mnajinyima raha mwenyewe.

Friday 25 March 2016

JIAMINI..

Fikiria wewe ni mwanamke na upo uchi mbele ya kioo chumbani,
Je, unapenda vile unajiona nywele, pua, matiti, tumbo, hips, mapaja, sehemu za siri?
Kama unajiona upo beautiful hongera mikono juu kabisa, na kama huridhiki pole hujiamini.Mwanaume huweza kusimamisha uume kila dakika 15 akiwa amelala usiku na mwanamke huweza kutoa majimaji (lubrication) kwenye uke wake kila dakika 15 akiwa amelala.

Binadamu ni wanyama pekee ambao hamu ya kufanya mapenzi au kufanya mapenzi (sex) si kwa ajili ya kuzaliana tu bali kupena raha ya kimahaba (sexual pleasure)

Pia Clitoris (kisimi) ni kiungo pekee katika mwili wa mwanamke kipo kwa ajili ya kumpa raha ya mapenzi, hakuna kazi nyingine ni hiyo tu.

Raha ya sex kwa mwanamke si katika uke tu kama alivyo mwanaume kwa uume wake bali ni zaidi ya hapo yaani mwili mzima.

Data zinaonesha kwamba wanawake ambao wamepatwa na matatizo ya ut wa mgongo (spinal cord injuries) na hawawezi kuhisi kitu chochote kuanzia kwenye kiuno kushuka chini bado wana uwezo wa kufika kileleni
Sababu kubwa ni kwamba ubongo hupokea hisia (feelings) za kusisimuliwa kimapenzi kupitia njia zingine nje ya uti wa mgongo hasa mwanamke anapochezewa matiti au kissing nk.
Hii ina maana mwanamke mwili mzima ni single sex organ tofauti na wanaume wanaowaza kwamba ili mwanamke afurahie mapenzi ni lazima uhakikishe unachimba vizuri Gold kule bondeni.

Quality ya mapenzi katika ndoa si mara ngapi mnafanya kwa siku au kwa wiki au kwa mwezi au kwa mwaka bali ni kuridhishana au kuridhika kwa wahusika kutokana tendo lenyewe.

Jamii inawadanganya wanawake kwamba wakiwa na sura fulani, au uzito fulani watakuwa wazuri katika mapenzi.
Thubutu, Mwanamke yeyote akiwa uchi mwanaume yeyote humuona ni mrembo na huchanganyikiwa kabisa.
Haina haja kuzima taa au kutaka giza eti kwa kuwa matiti yako ni makubwa mno au madogo sana, au mwili umenenepa sana au mwembamba sana, au ngozi upo tofauti na unavyodhani.
Ukiwa uchi tu mwanaume hukuona bonge na beautiful woman.

Pia jamii inapotoshwa kwamba kitendo cha mwanaume kusugua uke kwa uume wake kwa kila aina za style ni tendo linalompa mwanamke raha ya mapenzi.

Ukweli si wanawake wote hufikishwa kileleni kwa uume kuwa ndani ya uke tu (clitoral and viginal stimulation) bali kwa mwili mzima kama single sex organ na pia kuandaliwa kwa muda unaotakiwa.

Jamii imezungukwa na tamaduni zinazofanya mwanamke kujiona akiwa na shape Fulani au size Fulani ndipo atafurahia sex kitu ambacho ni kweli kwani ili mwanamke afurahie sex kwanza lazima ajifahamu mwenyewe na kuufurahia mwili wake kama ulivyo kujiamini kuhusu self esteem na body image yake.

Kuna asilimia zaidi ya 50 ya wanawake huwadanganya waume zako kwamba wamefika kileleni kitu ambacho si kweli ili mambo yaishe.
Kwa nini wanadanganya?
kwa sababu wanaume wengi huwa hawawaandai vizuri so anaona afahadhari aone amefikishwa maana lengo la wanaume wengi huwa kumfikisha mwanamke kileleni na si kumpa raha ya mapenzi.

MIGOGORO YA NDOA,HUATHIRI AFYA.

Kuolewa au kuoa ni kitu kingine na kujenga ndoa ni kitu kingine.
Ndoa yenye furaha huwa haijengwi siku ya ndoa au siku ya harusi au siku ya kuvalishana pete tu bali hujengwa kila iitwapo leo.

Ndoa inapokuwa na mgogoro mara nyingi (si zote) wanandoa huathirika zaidi na mara nyingi mwanamke huonekana ni makini na kuelekeza juhudi nyingi ili mahusiano yaendelee na kuwa yenye afya njema

Migogro mingi ya mahusiano (Ndoa au uchumba) mara nyingi mwanamke ndiye huathirika zaidi.
Wanaume hata kama ndoa ina mgogoro bado huonekana wapo physically fit na mentally fit kabisa nakuendelea kujichanganya na wenzao kama vile hakuna linaloendelea ktk ndoa zao wakati wanawake ndoa ikiwa na tatizo basi kwa kumwangalia tu unaweza kupata ujumbe kamili achilia kukoswakoswa kugongwa na magari.

Why?
Wanawake na wanaume hutofautiana sana jinsi ya kukabiliana au kuchimbua (ku-process) hisia (feelings), tukuto (emotions) zinazotokana na mgogoro uliopo.
Wanaume huweza kuvumilia tukuto na hisia zao bila kutegemea mwanamke au kuegemea kwa mwanamke, hii ina maana kwamba mwanaume hujikana, hujiondoa, huwa hajali, hu-withdraw hisia zake au kujisikia kwamba ana mgogoro na matokeo yake haathiriki sana.

Wakati huohuo mwanamke yeye kwanza ni mtu wahisia na tukuto (feelings & emotions ) tatizo likitokea hujihusisha zaidi, huji-engage, hujitoa (dedicate), huji-commit kupata solution, hujiuliza maswali wengine watasemaje? huwaza zaidi kuhusu yeye na mpenzi wake na jinsi ya kusaidia mgogoro uishe, matokeo yake huathirika zaidi na hudhoofisha afya yake na kuweza kukumbwa na magonjwa kama shinikizo la damu, stress, depression, stroke, magonjwa ya moyo nk.

MWANAMKE AFANYEJE?
Jambo la msingi ambalo mwanamke anaweza kufanya ndoa inapokuwa katika mgogoro ni kumuomba Mungu ampe hekima, busara na ushindi ili ndoa iwe katika mstari kwani ni jaribu na lazima ushinde, kila ndoa bora imejaribiwa na kuonekana imara, usione vinaelea vimeundwa.

Pia mwanamke anahitaji kuwa positive, kwamba anaweza na kwamba bado ndoa ipo, mume ni wake na aendelee kumpenda na kutamkia mambo mazuri mume wake kuliko kuwa na mtazamo negative.
Pia mwanamke anahitaji kujiamini kwamba chanzo cha furaha yake ni Mungu hivyo hakuna binadamu anaweza kuondoa furaha yake hadi aamue mwenyewe.

WANAWAKE HUJISAHAU.

Tatizo kubwa la wanawake wakiwa kwenye mahusiano (ndoa au uchumba) ni kwamba huwa wanasahau mahitaji yao na kujikuta wanavutwa na kuhusika zaidi na mahitasji ya wengine au wapenzi wao kihisia na kisaikolojia.

Challenge kubwa inaowakabili wanawake wote duniani wakishaiingia kwenye mahusiano ni uwezo wa kuimarisha sense of self, kujitambua, kujiamini, na kuanza na wao kwanza kabla ya mpenzi hasa linapotokea suala la mgogoro.
Wakati mwanamke hu-expand mwanaume hu-contract.
Kama ilivyo nguvu ya centripetal amabyo huhusika kuvuta kitu katikati (mwanaume) na nguvu ya centrifugal ambayo huhusika kuvuta kitu pembeni (mwanamke) kutoka katikati ndiyo ilivyo kwa mwanamke na mwanaume kwani mwanaume mara zote hurudi kwenye centerpoint hupungua, husinyaa, huongea kidogo, huongea kwenye point, wakati mwanamke yeye hupanuka kutoka katikati kwenda pembeni, huongea sana hata kama si point, huvutika kuongeza maongezi.

Ndiyo maana wanaume hulaumiwa sana linapokuja suala la mawasiliano kwani mwanamke na mwanaume wanapoongea mwanamke hu-expand maongezi na mwanaume hui-contract na kuongea kwenye point.

Kawaida mwanaume hufikiria kwanza (kwa ndani) kile anataka kuongea ili kujua kama ni point, wakati mwenzake mwanamke huendelea kuongea tu na anapoongea inamsaidia kuijua point,
Hii ina maana mwanamke huongea iliajue point na mwanaume hujua point ili aongee.

Bila kujua hii tofauti basi mwanaume asiyejali anaweza kusikitika sana kumsikiliza mpenzi wake na kuona alikuwa anaongea pumba au pointless na amempotezea muda wake au kuendelea kubishana kwamba mwanamke haongei point au kumkatisha kwa kuwa anachoongea hakielewiki.

Mwanaume anayejali husikiliza kwanza hata kama mwanamke anaongea kitu ambacho anahisi hakieleweki hata hivyo baadae ataelewa na mwanamke anajisikia mwanaume anamjali na kumsikiliza na maisha yanaenda

UMUHIMU WA KUPEANA ZAWADI KTK NDOA.

Mwanamke anahitaji alama za upendo kutoka kwa mwanaume.
Mwanaume anapompelekea mwanamke (mkewe) zawadi hii hudhihirisha kwamba mwanamke ana thamani na anamjali, mfano zawadi ya maua huonesha kwamba mwanamke ni mrembo na ana uzuri ambao mwanaume anaukubali.

Iwe zawadi kubwa au ndogo zote hutoa maana halisi ya mapenzi, humsaidia mwanamke kufahamu kwamba yeye ni mwanamke special, na kumpa zawadi mwanamke ni njia ya kumpa heshima na thamani ambayo mwanamke huhitaji kutoka kwa mume wake.

Kuna alama nyingi ambazo huonesha kwamba unampenda mke wako moja ni kumpa zawadi mbalimbali kama maua au kadi yenye ujumbe unaoelezea hisia zako kwake nk.
Ni muhimu mwanaume kuwa creative na innovative katika kuhakikisha penzi linazidi kunawiri kila iitwapo leo katika ndoa yako na unajitahidi kutoa hisia zako original pale unampa zawadi au kumwandikia text message (sms) yoyote, kitu cha msingi afahamu kwamba kuna mwanaume anayemjali.

Wanaume wengi huwa wanakuwa wataalamu na wajuzi sana wa kuwapelekea wapenzi wao zawadi motomoto na kadi zenye maneno matamu matamu mwanzo wa mahusiano (uchumba au ndoa) na baada ya muda wanaachana kabisa na hiyo tabia, hili ni kosa kubwa sana ktk masuala ya ndoa, kutoa zawadi hakuzeeki wala ku-expire hudumu na kudumu na kudumu, ni njia muhimu sana ya Kuonesha unamjali mke wako.

Kama ni mwanamke unakumbuka lini mpenzi wako amekuletea zawadi?
Na kama ni mwanaume je, unakumbuka ni lini umempelekea mke wako zawadi?
Eti haya mambo yamepitwa na wakati!
Shauri yako!
Usione vinaelea vimeundwa!

Wanawake wengi kwenye ndoa au mahusiano hujisikia na kujiona hawapendwi na waume zao, hujisikia wanaume hawawajali, ukiangalia kwa undani moja ya sababu ni mwanaume ameacha kumpa zawadi hata ndogondogo, au maneno mazuri (notes) au kadi kama alivyokuwa anafanya mwanzo na kwa sababu ulikuwa unampa na umeacha anajiona humpendi tena, si ulikuwa unampa? sasa imekuwaje? unampelekea nani tena? maana ulikuwa na tabia ya kutoa zawadi.

Kiwango cha attention unayompa mke wako ni alama muhimu ya Kuonesha upendo wako kwake.

Mwanamke hujisikia anapendwa na kwamba unamjali pale mwanaume:-
Unampompa zawadi iwe ndogo au kubwa,
Unapompa zawadi ya kadi yenye maneno mazuri yanayoelezea hisia zako kwake,
Unapomhudumia kwa kumjali,
Unapomsikiliza yeye na kujiona anasikilizwa,
Unapojitolea kumsaidia kazi ndgondogo na mambo ambayo anajisikia upo na yeye,
Unapompa plan za mambo mbalimbali mnayotaka kufanya pamoja kama familia iwe "outing", likizo, business n.k,

Pale unapomuuliza anavyojisikia hasa baada ya kazi au unapohisi emotions zake hazipo sawa,
Unapochukua muda wa ziada kuwa naye na kuwa kwa ajili yake,
Unaposhirikiana naye ktk huzuni au tatizo huku ukimfariji na kumkumbatia,
Unapompa nafasi ya kujisikia huru kwako hata kudeka (si wote)
Unapogundua kwamba amevaa amependeza mavazi na nywele na kumpa sifa anazostahili.
Unapom-surprise na zawadi au notes na
Unapompigia simu ukiwa umesafiri na kumuulizia anaendeleaje na jinsi gani utakuwa unaongea naye na kuwasiliana naye.

Thursday 24 March 2016

HAMU YA MAPENZI KUPUNGUA KTK NDOA.

Unapoona au kuhisi hali hii kutokea,
Jambo la msingi napenda kukukumbusha tu kwamba unatakiwa kufanya yale ulikuwa unafanya pale mwanzo kama vile:-

Je, unakumbuka namna mlikuwa mnapeana kisses na hugs pale mwanzo?

Tafuta muda na uwe na muda wa kumfurahia mwenzako kwa kumpa ladha za mabusu kwenye lips zake.

Maandalizi ya moto wa mapenzi huanzia nje ya chumbani hivyo ni busara kuhakikisha unakuwa connected na mke wako kwa kuwa na mawasiliano mazuri kimwili, kiroho na kimoyo.

Je, mnapomaliza sex huwa inakuwaje?

Kama huwa unazama kwenye usingizi na kumwacha mke wako bila kuendelea kuwa mwilini mwake na kumweleza namna unajisikia na raha unayopata na namna unavyompenda, Kumbuka wakati kama huu ni muhimu kuwa karibu zaidi kuliko mwanzo wa maandalizi ya kufanya mapenzi.

Je, unaendelea kuwa mwanafunzi wa kujifunza na kuwa mbunifu chumbani kwako?

Je, unajua mke wako anasisimka zaidi kwa kumfanyia vitu gani?
Vumbua maeneo yote anayoweza kusisimka kwani huwezi kufanya kile kile kila siku na akajisikia kusisimka na excited kwani si vibaya sana mke wako kufahamu kwamba mkiingia chumbani anajua utafanya 1, 2, 3, 4 kama kawaida yako.
Pia fahamu anaposema nimeridhika kwake ina maana gani.
Zaidi kumbuka unavyoendelea na ndoa mambo hubadilika, kuna masuala ya kazi, majukumu, maisha nk na kuna wakati mke huchoka, huwa na nguvu, hukasirika, huweza kutokea huzuni na misiba nk hii ina maana kuna aina mbali mbali za sex tofauti na siku ya honeymoon wakati ule wote lengo na mitazamo ulikuwa kupeana raha na kila mmoja alikuwa na matarajio makubwa sana.
Kuna wakati mke wako atajisikia hamu kubwa ya kufanya mapenzi na kutamani kila kinachotembea akirukie, hapa inabidi ujue upepo umevuma ili apewe perfect sex, fireworks na jitahidi kuwa connected na yeye then atafurahia hata kufika kileleni mara mbilimbili, hapo kazi kwako!
Kuna wakati mmoja atakuwa anahitaji kubwa la sex na mwingine hana hiyo hamu na Jifunze kwamba mnaweza kupeana sex ya chapuchapu (quickie) na mwingine kuridhika na mwingine kuendelea na ratiba zake.
Inawezekana pia wewe ukawa huna mood ya sex lakini mke wako anakuhitaji.
Hapa huhitaji kung’ang’ania iwe kama ile ya jana.
Pia kuna wakati mke wako au wewe mmoja atakutana na shida au huzuni na mmoja atahitaji kumfariji mwenzake na hakuna kitu muhimu na kizuri kama mmoja aliyehuzunishwa kujikuta yupo kifuani na kuzungukwa na mikono ya mwenzi wake huku akipata maneno ya faraja na hata kushirikiana mwili hata katika huzuni (comfort sex).
Utakuwa hatua moja mbele kama utafahamu aina za sex katika ndoa na sababu zake na pia kufahamu kwamba lengo la sex wakati mwingine si kufika kileleni bali kuwa connected.
Pia uwe mwepesi kuweka wazi matarajio yako kwani mke huhitaji kuandaliwa kiakili kabla ya kuingia chumbani hivyo kama kuna migongano, mvurugano au jambo ambalo lipo pending bila kupewa ufumbuzi basi linapewa ufumbuzi kabla ya kuingia chumbani.
Kwa hapo Naamini unaweza kuwasha upya moto wa mahaba chumbani kwako na mwenzi wako kama mwanzo.

HII HUMFANYA MUME AWE NA RAHA CHUMBANI.

Mitazamo ni suala muhimu sana inapokuja issue ya kumfanya mume wako ajisikie raha na wewe chumbani.
Kuna tofauti kubwa sana na pana sana kati ya mwanaume na mwanamke na tofauti kubwa hujiweka wazi katika suala la mapenzi.
Namna ya kuwasiliana kimapenzi (love/affection) kwa mwanaume na mwanamke kuna tofauti kubwa.
Kawaida mwanamke huweza kujisikia kusisimka kwa maongezi (kile anasikia), wakati mwanaume ni mwili (kile anaona).
Pia ili mwanamke ajisikie vizuri kimapenzi katika mwili wake hupenda kujiona au jisikia yupo connected kwanza na mume wake wakati huohuo ili mwanaume ajisikie connected ni pale tu atakapojisikia raha kimwili kwanza.
Hii ina maana kwamba mwanamke anayehitaji kumfurahisha mume wake kimapenzi atatakiwa kufahamu mapema kwamba ili kujisikia connected na mume wake anatahitaji kujiweka wazi kimwili ili mume awe rahisi kuwa connected kwake hata kama kanuni inagoma.
Lengo si kwako mwanamke kumkwepa mumeo bali wewe kujitoa kwake na hii itafanya mume wako ajisikie raha zaidi na kwenda extra mile kwa kila eneo la maisha yenu na kwamba anakuhitaji kila wakati wewe tu.
Mwanamke hujisikia kusisimka pale mume wake akimnong’oneza maneno matamu sikioni mwake na wakati huohuo mwanaume hujisikia msisimko wa ajabu pale mke wake anapompapasa mwilini mwake kwa ngozi yake laini na kujikuta Mr.x wake anaanza kutoa maamuzi ambayo hajatumwa afanye.

Je ni kweli mwanaume ana sehemu kiungo kimoja tu cha kumsisimua kimapenzi?

Si kweli kwani kama mwanamke na mwanaume ana sehemu na ana utajiri mwingi wa sehemu ambazo mwanamke akimgusa basi anaweza kujisikia raha kwa mguso anaoupata.
Hata hivyo kila mwanaume ni tofauti na ana namna ya kumsisimua kimapenzi na anayejua ni yeye kwa wewe mwanamke kuwa mvumbuzi kwa kumuuliza na ujanja wako tu.

Monday 14 March 2016

SEX WAKATI WA UJAUZITO.

Wakati wa ujauzito wanawake wengi hukosa hamu ya tendo la ndoa hivyo mwanaume unahitaji kuwa na mawasiliano mazuri ili mambo yaende vizuri.

Je, Mwanamke mwenye mimba anaweza kuendelea na tendo la ndoa?

Hakuna ushahidi wa kisayansi unaothibitisha kwamba tendo la ndoa kwa mwanamke mwenye mimba ya hatua yoyote ya ujauzito inaweza kumuathiri mwanamke mwenyewe au mtoto tumboni.
Hata kama kunatokea miscarriage bado sayansi inathibitisha kwamba chanzo huwa si sababu ya tendo la ndoa wakati mwanamke ana mimba, bali sababu zingine kabisa.
Tafiti nyingi zimefanywa kwa kufuatilia wanawake ambao waliendelea na tendo la ndoa huku wakifika kileleni (orgasm) na wale ambao hawakuwa wanafika kileleni wakati wa tendo la ndoa, na wale ambao hawakufanya kabisa tendo la ndoa muda wote wa ujauzito.
Matokeo yalionesha kwamba wanawake wote walizaa watoto ambao hawana tofauti yoyote kiafya.
Hivyo tendo la ndoa ni salama kabisa muda wote wa ujauzito.

Je, ni wakati gani huruhusiwi tendo la ndoa wakati wa ujauzito?

Ni pale tu mwanamke anapojisikia kuwa na bleeding au maumivu yoyote au leakage ya majimaji yajulikanayo kitaalamu amniotic fluid.
Mwanamke mwenye mimba haruhusiwi kuingiza upepo (by forcing) kwenye uke wake kwani husababisha kitu kinaitwa Air bubble kitendo ambacho kinaweza kusababisha kifo kwa mwanamke mwenyewe au mtoto tumboni kwani hu-block mishipa ya damu. Wapo wanaume huwa na mchezo wa kubusu huku wanapuliza huko bondeni kabla ya kuanza kusex.
Pia kama mmoja ya wanandoa ana magonjwa ya zinaa (STD) haruhusiwi tendo la ndoa hadi daktari athibitishe kwamba amepona ama sivyo anaweza kusababisha mtoto tumboni aambukizwe.

Pia ifahamike kwamba si wanawake wote wakiwa na mimba hupenda tendo la ndoa wengine huwa hawapendi kabisa.
Utafiti unaonesha pia kwamba mwanamke mwenye mimba hukosa hamu ya tendo la ndoa miezi mitatu (3) ya kwanza, kisha hupenda sana tendo la ndoa miezi mitatu inayofuata na Pia miezi mitatu ya mwisho hukosa tena hamu ya tendo la ndoa kwa sababu ya saikolojia ya kusubiri mtoto kuzaliwa.
Ingawa uzoefu unaonesha kwamba mwanamke mwenye mimba husisimka haraka na kufika kileleni mapema sana kwa sababu damu huwa nyingi sana kuzunguka uke na hivyo kuwa sensitive zaidi kuliko akiwa hana mimba, pia ni dhahiri kwamba mwanamke anayefurahia tendo la ndoa wakati ana mimba hupata utamu wa uhakika.

Kitu cha msingi pia ni kuzingatia mikao au milalo wakati wa tendo la ndoa kwani mwanamke mwenye mimba anahitaji mikao au milalo ambayo haikandamizi tumbo lake.
Hakikisha mnakuwa na communication nzuri kuhusiana na suala la tendo la ndoa ili kila mmoja aweze kuwa msaada kwa mwenzake.

Sunday 13 March 2016

MISINGI YA NDOA.

Wataalamu wa masuala ya ndoa (marriage experts) walikaa pamoja kujadili misingi muhimu ya ndoa ambayo wanandoa wakiifuata ndoa zao zitakuwa imara na zenye afya hadi kifo kitakapowatenganisha.
Misingi hiyo imeinamia zaidi kwenye imani ya Kikristo, ingawa mtu yeyote bila kufuata dini yake anaweza kuifuata na bila shaka ndoa yake itakuwa ya tofauti.

Kuna mambo mengi sana muhimu ya kufanya katika ndoa ili ndoa iwe imara na yenye mafanikio, hawa wataalamu walichambua yale ya msingi tu ambayo yakifuatwa basi vitu vingine muhimu katika ndoa inakuwa ndani yake.
Tumeshayaongea sana haya mambo hapa hii inaweza kuonekana kama kurudia, hata hivyo kuna kitu muhimu na kipya unaweza kukipata hapa.

Je, ni Misingi ipi hiyo?

1. MUNGU KUWA KIONGOZI WA NDOA.
Ndoa ambayo inaendeleza, ongeza, imarisha na kufurahia mahusiano na Mungu itakuwa na picha kamili ya Mungu.
Kila mwanandoa atakuwa na uhusiano mzuri na Mungu na atajitahidi kuishi katika maadili ya dini na matokeo yake dhambi itakaa mbali na dhambi kukaa mbali basi upendo wa kweli wa kimungu huongoza ndoa.

Ndoa yenye msingi wa Dini huwa na maombi na maombi ni mawasiliano ya wanandoa na Mungu, hivyo kwa kuwa na connection kati ya Mungu na wanandoa, Mungu atakuwa anaipa stabilization ndoa yao kila wanapokutana na tatizo, shida au jaribu.

Unajua kuna siku shetani huwa anaamua kumpaka matope mmoja ya wanandoa ili asipendwe (unajisikia kutovutiwa na mwenzako), ni kwa maombi tu unaweza kuharibu kazi za aina hii za shetani si pesa, wala elimu wala ujanja.

Kwenye ndoa kuna good times na bad times na Mungu huweza kuwapitisha wanandoa vizuri kama wanamtegemea yeye, hilo halina ubishi ni amini na kweli.

2.UPENDO WA KUJITOA.
Maisha ya binadamu ni safari ndefu, si sahihi kwamba siku zote ndoa itakuwa na mapenzi yaleyale ya motomoto, au kupendana kule kule kama mwanzo, kiwango cha mahaba kupanda tu graph kila iitwapo leo; si kweli, kutokana na kuwa na malezi tofauti na mambo mengine inawezekana ndoa kupita kwenye wakati mugumu sana, kuna stress, kuna kukata tamaa, kuna business kufilisika, na kuna wakati tu inatokea mume na mke kila mmoja hampendi mwenzake bila sababu, hivi vyote vinahitaji watu wenye Upendo wa kujitoa ili kurudi kwenye mstari.
Katika ndoa conflict na disagreement hutokea bila upendo wa kujitoa basi ndoa haiwezi kufika popote.
Kwenye ndoa hakuna mtu perfect wote bado tuna tumia Learner driving license kwa maana kwamba tunaendelea kujifunza na kutoa efforts za kuhakikisha ndoa inakuwa na afya na inaendelea kudumu na kudumu na kudumu.

Kuna utafiti ulifanywa kwa wanandoa waliopata talaka, asilimia 40 walisema wanatamani kurudi kwenye uhusiano wao wa kwanza, hii ni kuthibitisha kwamba wangekuwa na upendo wa kujitoa basi wasingeamua kuomba talaka zao kwani kuna watu ambao conflict kidogo tu, tuachane!

Hawana dogo na wengine sasa kuoa na kuolewa ni kama shopping!

3. MAWASILIANO.
Utafiti unaonesha kwamba watoto wadogo wa kike wamebarikiwa sana (talented) na uwezo wa kuongea na lugha kwa ujumla , huweza kuongea haraka na mapema kuliko watoto wadogo wa kiume.
Hiyo tabia huendelea hadi wanapokuwa watu wazima na kwa maana hiyo wanawake na wanaume lipokuja suala la kuongea na mawasiliano kwa ujumla kuna tofauti kubwa.
Inajulikana kwamba wanawake huongea maneno kati 40,000 hadi 50,000 kwa siku wakati wenzao wanaume huongea maneno 15,000 hadi 25,000 kwa siku.
Hivyo basi wanawake ni viumbe wanaohitaji mwanaume kuuongea ili na yeye aongee hayo maneno yake, ndiyo maana kwa mfano kama umetoka kazini basi mwanamke anapenda sana umwambie mambo mbalimbali kama vile unafikiri kitu gani, nini kilitokea kazini, watoto wameshindaje, unajisikiaje kuhusu yeye mwanamke nk.
Wakati huohuo wanaume hujisikia sawa tu hata asipoongea chochote akifika nyumbani kutoka kazini matokeo yake mke anakuwa bored na hayo ni mawasiliano mabovu.
Wanaume kushindwa kuelezea hisia zao kwa wake zao ni kitu kinachowaumiza sana.

Panga muda maalumu kwa ajili ya maongezi ya maana na mke wako hata kwa kuwa na matembezi au outing.
Hata hivyo wanawake wanapaswa kufahamu kwamba kuna wanaume ambao hawawezi kuwa kama wanavyotaka wao kwani ndivyo walivyo.
Mume wako hataweza kukutimizia mahitaji yako yote kwani hakuna mwanaume duniani ambaye anaweza kumpa mwanamke vyote anavyohitaji, ndiyo maana hata wewe mwanamke mwenyewe hupo perfect mia kwa mia.

Kumbuka

Unapowasiliana na mume au mke;
Badilisha kile ambacho kinaweza kubadilishwa
Elezea kile ambacho anaweza kukielewa
Fundisha kila ambacho anaweza kujifunza
Patanisha kile ambacho anaweza kukubaliana
Rudia kile ambacho anaweza kukiimarisha.

Thursday 10 March 2016

AINA HII YA UKAGUZI KTK NDOA

Utaniambia leo ulipitia wapi na ulikuwa na nani!Kila mtu duniani ana siri zake binafsi na kuwa wakati hapendi mtu yeyote ajue ila ni yeye na Mungu wake.
Si siri tu bali hupenda kuwa mwenyewe na kujiamulia mambo yake mwenyewe kwa kadri anavyotaka.
Unapokubali kuoana na mwanaume au mwanamke maana yake unaruhusu kuanza maisha ya pamoja (sharing) katika hisia, emotions, kazi, kitanda, bafu, harufu, nguo nk.
Hata hivyo hii haina maana kwamba tunawajibika upande mwingine yaani mume au mke kujua kila kitu kwani kila mmoja huhitaji kuwa na siri au kufanya kitu mwenyewe.

Hapa ninazungumzia vitu ambavyo ni vizuri havina uhusiano na tabia mbaya kama ulevi au kukosa uaminifu.

Hata hivyo wapo wanaume zetu au wake zetu hutaka kujua kila kitu tunachofanya na kila mahali tulikuwa zaidi ya mama zetu walivyokuwa wanatuchunga wakati watoto.

Kama mwanaume umeenda kazini, mkeo anataka kujua kwanza wakati unaenda kazini uliongea na nani, umefanya nini, umekula nini na nani, ulipotoka kazini ulipitia wapi, na mlikuwa na nani na atachukua simu ya mkono na kuanza kuangalia nani alipiga, nani alipigiwa na nani alikutumia sms na nani alitumiwa, ni kuchunguzana na kuulizana zaidi ya FBI.
Maswali mengi utafikiri ndoa ni mahakamani.
Mume anaogopa hadi kurudi nyumbani maana anaona ni usumbufu.
Kwani ni lazima ujue kila kitu?
Ukweli kama wewe ni mwanamke si lazima ujue kila kitu kuhusu mume wako, alikuwa wapi, alikuwa na nani, amefanya nini na ilikuwaje nk, kuna vitu ni non of your business.

Inawezekana unajua kutoka kazini hadi nyumbani huwa anatumia dakika 20 lakini sasa ametumia dakika 50, ile anafika nyumbani tu unambana na maswali ajieleze alikuwa wapi, alikuwa na nani, na analikuwa anafanya nini na ilikuwaje, inawezekana alipitia kwa rafiki zake aliosoma nao pia si lazima ujue kila kitu yeye ni mtu mzima si mototo tena, yaani anajisikia kama vile wewe ni mama yake kitu ambacho kinakupunguzia alama na anahisi hujiamini na pia msumbufu na humuamini.
Kama anataka kuishi na mtu anayetaka kujua kila kitu kuhusu yeye, basi angebaki kwa mama yake na si kuoana na wewe.

Ukweli si lazima ujue kila kitu kuhusu yeye, mwamini, mpende, mfurahie hata kama amechelewa kwa muda kidogo zaidi na alivyo kwambia.

UNAWAJIBIKA KWENYE NDOA YAKO?

Kuwajibika na kujitoa ni moja ya mahitaji muhimu sana ya mafanikio yoyote dunia leo.
Pia hakuna sehemu muhimu kwa kuwajibika na kujitoa kama kwenye ndoa na mambo ya familia.

Watu wanaoamua kuoana huwa wanawajibika na kuhakikisha wanajitoa kwa ajili ya uamuzi na uchaguzi wamefanya kwanza kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake ili kuhakikisha ndoa inaendelea.

Kila anayeingia kwenye ndoa huwa anakuwa amebeba limfuko la matatizo binafsi na kutokukomaa katika maisha ya ndoa (immaturity), hana uzoefu na kinachofuata ni kupata uzoefu mpya.
Hivyo partners wote wanawajibika kukutana na matatizo na kuyashughulikia hayo matatizo bila kulaumiana au kumlaumu mwenzake kwa matatizo just focus to the solutions kuliko ku-focus kwenye matatizo na kuanza kulalamikiana, ingawa hapa kuna wengine huwa kichwa ngumu anajiona yeye yupo sahihi siku zote na anaweza ku-ignore kila kile mwenzake anapendekeza ili ndoa irudi kwenye amani na usalama.


Kila mwanandoa anahusika na kuwajibika kwa ajili ya furaha yake, hisia zake na kila reactions, hakuna mtu atakufanya uwe happy ila ni wewe kwanza, kwani ukishinda umekasirika siku nzima au mwezi mzima au hata mwaka unapata faida gani?

Furaha ni matokeo ya kukomaa kwa mtu na kufahamu kwamba yeye mwenyewe ni chanzo cha furaha na simwingine.
Wewe ukiwa na furaha na wengine watakuwa na furaha.
Watu wenye furaha hutengeneza ndoa zenye furaha na watu wasio na furaha hutengeneza ndoa zisizo na furaha.

EPUKA KUTUMIA NENO HILI..

Naomba jiulize kidogo hivi ni mara ngapi kunapotokea mgogoro katika ndoa yako umekuwa unawaza au kutishia kwamba utaachana na huyo mume wako au mke wako?

Inawezekana unaishi katika wakati mgumu sana katika ndoa yako umeumizwa sana, umekatishwa tamaa sana, hupendwi, hakujali tena, umejawa na stress kiasi kwamba hata unapotamka kwamba afadhari kupata talaka na kujianzia maisha mapya kivyako huoni uzito wa neno talaka unavyolitamka.
Ukweli ni kwamba kwa maneno yetu tunayotamka tunaweza kuweka mustakabali wa maisha yetu ya baadae.
Maneno hushibisha nafsi sawa na chakula



Maneno tunayoongea yana uwezo wa ajabu ndani yake; yana uwezo kuponya au kuua au kuumiza, yana uwezo wa kutia moyo au kukatisha tamaa kabisa, yana uwezo wa kusema ukweli au kudanganya kwa uwongo wa ajabu, yanauwezo kutoa sifa au kulaumu, yana uwezo wa kubariki au kulaani nk.

Neno talaka ni neno lenye sumu na neno baya sana kulitumia katika ndoa yako na zaidi ya yote huweza kuumba kwenye akili na mawazo yako zaidi ya wewe unavyofikiria na kutoa matokeo sawa na mbegu iliyopandwa.

Unapotamka maneno mabaya kwa ndoa yako au katika maisha yako ya kila siku unamwaga sumu na ipo siku itakuwa kweli kwani kila unachopanda lazima utavuna.

Kawaida maneno tunayoongea kwenye ndoa zetu ni kama kioo kwa mwingine (mwanandoa mwenzako).
Ukisema nakupenda, mwenzako anajisikia vizuri na kujihisi kweli anapendwa;
Ukisema umependeza, atajisikia vizuri na kujiona amependeza;
Ukisema ndoa chungu, na mwenzako atajisikia ndoa chungu,
Ukisema nitakufa ni kweli utakufa kabla ya muda wako.

Hivyo ni vizuri kila mmoja kuongea maneno yanayojenga ambayo ni positive ili ndoa zetu zidumu.
Ukizoea kutamka neno talaka ni kweli usishangae siku ndoa inaishia kule unaitamkia hata kama ulikuwa unatania.
Ndoa haitaniwi!
Neno talaka inabidi lifutwe kwenye misamiati yako hasa baada ya kuoa au kuolewa

Duniani tuna watu wa aina tatu tu:
Kwanza wale wanafikiri chakuongea kabla ya kuongea
Pili wale wanafikiri cha kuongea huku wanaongea
Tatu wale wanaongea kwanza ndo wanafikiria nini wameongea
Wewe upo kundi gani na unatumia vipi uwezo wako wa maneno?

MWANAMKE KUKOSA HAMU.

Linapokuja suala la mapenzi, upendo na ndoa asilimia kubwa ya kila binadamu huwa na ndoto kubwa.
Hata hivyo hizi ndoto wakati mwingine huyeyuka pale mtu anapokutana na mambo ambayo ni kinyume chake mojawapo ni mwanamke au mwanaume uliyenaye kuwa baridi kabisa linapokuja suala la tendo la ndoa ukiongelea sex tu ni wa baridi na pia hafurahii kabisa tendo la ndoa.
Mwanamke kuwa wa baridi na kukosa kabisa hamu ya tendo la ndoa na kushindwa kabisa kufika kileleni au mwanamke kuwa baridi kuhitaji mapenzi, kukosa moto wa kutaka mapenzi.
Mambo mengi sana husababisha mwanamke kuwa na frigidity mojawapo ni:-
HATIA-Wapo ambao kutokana na malezi ya dini na jadi zao wamedumazwa na mafundisho kwamba sex ni uchafu na dhambi hivyo wakiingia kwenye ndoa bado hujisikia ni dhambi na uchafu pia mwanamke huwa na wakati mgumu sana kubadilisha gear na kujisikia sex ni haki yake na ni baraka ambazo Mungu amewapa wanandoa.

Pia huyu mwanamke anaweza kuwa na mzigo wa hisia na kuumizwa kama vile kubakwa au kunajisiwa wakati mtoto au kabla ya kuolewa hivyo akikmbuka tu mwili unakuwa barafu kuhusu sex.
Pia inawezeana mwanaume aliyenae anamuudhi sana na kumtesa na mwanamke hujisikia hatia kwamba amedanganywa kuingia kwenye hiyo ndoa na matokea ana freeze kabisa kuhusu sex.
Au inawezekana wameoana baada ya kudanganya wakat bado hawajaoana na kwa kuwa walidaganya na mimba ikapatikana na wakaozeshwa kwa nguvu sasa mwanamke haridhiki na mwanaume so anajisikia ama kauziwa mbuzi kwenye gunia hivyo hisia za mapenzi kwa mwanaume zimekufa.

HOFU, MASHAKA NA WASIWASIInawezakana mwanamke anapata hofu na mashaka au wasiwasi na kuumizwa (uke) na mwanamke hasa kama mwanaume yupo rough katika technic zake za mahaba.

Pia inawezekana uke ni mkavu kiasi cha kumuumizwa.
Pia kama mwanaume ana maneno ya kutisha na kukatisha tamaa wakati wa mapenzi au badala ya kuwa tender yeye anakuwa na hard.

Wanawake huwa na hofu hasa kutokana na mwanaume kuwa ignorant kwenye suala zia la tendo a ndoa kiasi kwamba wanamke hujikuta amejawa na hofu na mashaka kwani mwanaume hana uhakika na kile anafanya.

Wanaume wengi hujifanya wanajua kila kitu kumbe si hivyo na ukweli wanawake hujua zaidi na kwa kuwa wakionesha wanajua wataulizwa nani kakufundisha na matokeo yake ni balaa.
Pia wapo wanawake ambao hujiweka kwenye kundi la zero linapokuja suala la mahaba pia inawezekana ni kutokana na jinsi mwanaume anavyomkandia kwamba hajui.

Pia inawezekana mwanamke anatumia Tv, films, movies na media zingine kupima uwezo wake kitandani sasa akishindwa hujiona failure na matokea hukosa libido.
Dunia ina vipimo vyake ya kuonesha unajua sex hata hivyo hujaitwa kuja kwenye ndoa kujilinganisha na vipimo vya dunia (world sex performance standars) bali kumridhisha mumeo. Muhimu ni ku-focus kwa mumeo au mkeo na si kujilinganisha na masuperstar wa sex duniani.

Pia mwanamke anaweza kuwa frigidy pale anapokuwa na hofu hasa akiwa anahisi kuna watu wanawaona au wanachungulia au watoto wanawaona au watu wanasikiliza wakati wa sex hasa kutokana na mazingira ya chumba cha mahaba kilivyo, wanaume wengi huwa hawajali ila kwa mwanamke ni issue nzit sana ambayo huwezakufanya awe wa baridi.
Kumbuka privacy is a basic need to sex
Pia mwanamke anaweza kuwa frigidy hasa kama anakuwa na hofu ya kupata mimba hasa kama mimba yake huishia kwenye miscarriage, hivyo emotions zake huwa zimeumizwa kiasi kwamba zina overrule hamu ya sex na mwili kuwa baridi kabisa kuhusu sex.Pia inaweza kuwa ni stress, anxiety, depression.
Pia inaweza kuwa hofu ya kuambukizwa magonjwa ya zinaaa.

Nini tiba yake? Tiba halisi kama una tatizo la kuwa baridi kuhusu tendo la ndoa ni kuwaona washauri wa saikolojia au madaktari wa taaluma za wanawake na sex.

KUSHINDWA KUTOA HUDUMA.

Tunapozungumzia mwanaume kushindwa kitandani tuna maana kwamba ni mwanaume kutokuwa na uwezo kusimamisha uume ili kuweza kufanya tendo la ndoa kwa ufanisi unaotakiwa, au kuwahi kukojoa (immature ejaculation) au mwanaume kusimamisha uume kwa muda mrefu zaidi ya saa moja na kushindwa kurudi kwenye hali yake ya kawaida.

Kama mwanaume anaweza kumaliza tendo zima la ndoa kwa muda wa dakika 5 au chini ya dakika 10 na kuwa hana uwezo wa kuendelea tena basi hiyo ni dalili kwamba something is wrong.
Data zinaonesha asilimia 10 ya wanaume mahali popote wana tatizo hili,ulimwenguni kuna wanaume zaidi ya milioni 150 wana tatizo hili na pia kila mwanaume anaweza kukutana na tatizo hili angalau mara moja katika maisha yake.

Nini husababisha?
Ili uume uweze kusimama lazima damu iende kwa wingi huko na kusababisha kuwa mgumu na kusismama na kuwa tayari kwa huduma.

Sababu kubwa ya mwanaume kushindwa kusimamisha uume wakati wa tendo la ndoa mara nyingi huwa ni mawazo.

Pia Inawezekana ni dalili ya ugonjwa mwingine kama Diabetes.
Mwanaume anaweza kuwa na hofu kwamba hawezi vizuri sex na hii hupelekea kutojiamini na hatimaye uume kushindwa kabisa kusimama.
Pia Inawezekana ndoa ina matatizo na kupelekea kichwa kuwa na limzigo la mawazo na hatimaye kushindwa kabisa kusababisha utendaji wa kazi huko south pole.

Inawezakana mwanaume amefiwa na mtu wa karibu aliyekuwa anampenda.
Kuchoka
Pia stress
Kuwa na hatia ya kitu chochote.
Inawezekana mwanamke aliye naye havutiii kabisa
Kufilisika biashara au kufukuzwa kazi hupelekea kuwa na mawazo.
Kupungukiwa homoni zinazowezesha uume kusimama hasa umri ukienda sana.
Matatizo ya mirija ya damu kushindwa kusafirisha damu kwenda sehemu zote za mwili, hii uweza kusababishwa na magonjwa kama BP na arteriosclerosis.
Kuvuta sigara
Magonjwa ya nerves
Kufanyiwa upasuaji hasa ule wa prostate

Wanaume ambao huonekana labda ni maarufu sana katika fani zingine bado likija suala la kitandani ni kitu kingine hivyo mwanamke anatakiwa kujua kwamba lazima atoe ushirikiano wa kutosha kwani mwanaume anahitaji kutiwa moyo na mwanamke aliyenaye kwani Inawezekana ni mawazo kichwani mwake ndo hupelekea kushindwa.

Je, unaweza vipi kuepuka hili tatizo?
Hakuna kitu kinachoshushia mwanaume hadhi mbele ya mwanamke kama hili tatizo hivyo basi mwanaume akiona hili tatizo linajitokeza mara kwa mara kwanza ajiamini na kuangalia linaweza kuwa nini kimesababisha kama ni msongo wa mawazo inahitaji kwenda kwa washauri (counselling) na kama ni suala la kimatibabu awaone madaktari.

WENYE TABIA HII..

Kukefyakefyani nini?
Ni kitendo cha kutafuta makosa na kuendelea kulaumu, kulalamika, kusumbua, kutesa, kuchokoza , kuudhi, kushutumu, kuleta mzozo ndani ya wanandoa.
Mara nyingi wanawake ndiyo wenye hii tabia ingawa imegundulika kwamba wapo wanaume wenye tabia hii katika ndoa.

Pia kukefyakefya ni kitendo cha kumsumbua mwanaume kwa maswali, au kumtuma kitu au kumwambia afanye kitu kama vile ni bosi wa kihindi na mfanyakazi wake au mama na watoto wake wakati ni mke na mume ndani ya nyumba.

Inawezekana mume wako anatabia ya kuacha bathroom kuwa chafu baada ya kutumia, akila anaacha meza na vyombo ovyo na vichafu, Inawezekana huwa anatupa nguo ovyo na kusambaa sakafuni utadhani chumba cha watoto wa shule, Inawezekana anakaa tu huku anazidi kunenepeana kama wachezaji wa sumo, au anaangalia TV kama vile ana mkataba na vituo vya TV na umekuwa unamwambia kubadilika lakini habadiliki na umeona dawa nikuendelea kumsema.

Au umekuwa ni mwanamke mwenye maswali hata yasiyo na kichwa na miguu tangu asubuhi wewe ni kuuliza tu nakuendelea kuuliza.
"Unamuuliza, je Ulitoa zile takataka, ulilipa ile bill, umetengeneza lile dirisha, umemwambia fundi kuhusu tatizo la umeme hata hajajibu umeshampachika swali lingine"
Kawaida wanaume huwa hawapendi kuambiwa nini cha kufanya.

Kwa nini kukefyakefya si vizuri?
Kwa sababu husababisha mwanaume kukwazika, kwani hujiona yeye ni mtoto na mke ni mzazi au mama, Hakuna mwanaume anapenda mke wake kuwa kama mama yake mzazi.
Mwanaume hujisikia haheshimiwi na mkewe.

Mwanaume hujisikia kushambuliwa na kudharauliwa nakujiona hafai

Kwa nini wanawawake hupenda tabia ya kukefyakefya?
Wanaume hawafanyi vile wanawake wanawaambia wafanye.
Pia wanawake hudhani kwa kurudia kukumbushia na kusutana basi mwanaume atafanya.
Wapo wanawake wamekulia mazingira ambayo mama zao walikuwa ni watu wa kukefyakefya kwa baba zao hivyo basi nao wanaamini hiyo ndiyo njia pekee ambayo wanaume wanaweza kufanya yale wanasema au wanataka wafanye.
Wengine ni asili yao kufanya hivyo.

Nini matokea ya tabia ya kukefyakefya?

Mwanaume huanza kumkwepa mke wake na kuchelewa kurudi nyumbani au kujibakia ofisini au kazini au kupitia sehemu hadi ahakikishe akirudi nyumbani mke amelala.
Mwanaume anaweza kuanza tabia mbaya za ulevi au kukosa uaminifu katika ndoa
Mwanaume huanza tabia ya kutosikiliza mke wake kwani anamchuja (filter) kwamba huyu ni tabia yake kukefyakefya so msumbufu.
Kuchokana katika ndoa maana hakuna ukaribu (intimacy) pamoja na mawasiliano kuwa ovyo maana mume sasa uwa si msikilizaji mzuri.
Mwanaume hukosa hamu na huyo mwanamke mwenye hii tabia.

Je, mwanamke afanyeje asiwe na tabia ya kukefyakefya?

Kwanza mwanamke lazima akubali kwamba yeye na mume wake wapo tofauti na azikubali tofauti, akubali upungufu uliopo na kuchukua maisha kama yalivyo.
Siku mwanaume akifanya vizuri ampe appreciation.
Lazima mwanamke awe positive kama mwanaume amefanya alichoambiwa afanye kwa maana kwamba usilaumu, shutumu, au kukasirika au kumfanya aonekane stupid.
Kawaida Hakuna kitu kibaya duniani kinachofanya tuone kitu ni kibaya bali ni jinsi tunavyofikiri.
Shirikisha hisia zako kwake kama ungekuwa wewe kila siku unaambiwa kama mtoto mdogo ungejisikiaje.

Inawezekana mumeo huchelewa kurudi nyumbani au kukupa sababu eti anapitia sehemu kumbe anakwepa tabia yako ya kukefyakefya.


Ni afadhari kuishi pembe ya darini kuliko kukaa katika nyumba pana pamoja na mwanamke anayekefyakefya
(Mithali 19:9)

ANAHITAJI MUDA WA KUPUMZIKA KWANZA.

Wanaume hupenda kuwa wenyewe muda fulani hasa akiwa amerudi nyumbani kutoka kazini au akiwa anatatizika na jambo lolote.
Hivyo basi inawezekana wewe kama mwanamke ndani ya ndoa umezoea mume akirudi kutoka kazini unamkaribisha home kwa kumpiga maswali na kuanza kumueleza kila aina ya matatizo na karaha ambazo zimetokea siku hiyo bila kumpa hata muda wa yeye kupumzika kidogo.

Sina maana kwamba mumeo akirudi nyumbani ule jiwe bila kumpokea au kumuuliza kazi ilikuwaje, nazungumzia suala la kutompa muda angalau dakika 15 kupumzika kabla hujaanza kutoa maswali yako na matatizo yako.

Pia naamini dunia ya sasa wote wanawake na wanaume tunafanya kazi iwe ofisini au shambani hata hivyo tukifika nyumbani kila mmoja hujitahidi kumweleza mwenzake nini kimeendelea au kupeana taarifa mbalimbali za familia ukweli ni kwamba bado mwanaume huhitaji dakika kama 15 kabla ya kujiunga na familia.

Kumbana maswali na kumwambia matatizo na shida tangu anaingia mlangoni si jambo zuri sana kwa mwanaume kwani hujisikia anaishi na mama yake na si mke wake maana mama yake alizoea kumbana maswali tangu anaingia nyumbani kutoka shule.
Kama angekuwa anataka kuishi na mama yake basi asingekuoa wewe bali amekuoa wewe kwa sababu wewe ni tofauti na mama yake.

Baada ya kuchoshwa na kazi, na boss, au wateja au foleni za magari njiani anapowahi nyumbani anachohitaji akifika nyumbani ni busu na hugs kutoka kwa mke wake then aoge na kupumzika kidogo kama dakika 15 hivi ndipo atakuwa tayari kujibu maswali ya mkewe na kuendelea na story zingine pia.

Mpe muda wa kurelax akishafika nyumbani kwani kumbana maswali punde tu anaingia nyumbani kunaweza kusababisha yeye kuchelewa home kwani hujisikia ni usumbufu.
Akishakuwa tayari ameridhikana muda wake kuwa kwenye hilo cave unaweza kuona anaanza kuzungumza mwenyewe then anza kumpa hayo maswali yako.
Pia akigundua wewe ni msumbufu, hata siku ukiwa na point za maana anaweza kupuuzia maana umezoea kuchonga sana akiingia tu mlangoni hata kabla hajafika chumbani.

HUWAUMIZA SANA.

Je umemchoma mara ngapi mumeo au mchumba wako?
Ni ukweli usiopingika kwamba hata wanaume huumia sana hisia zao na mtu pekee mwenye uwezo wa kupooza maumivu ni mpenzi wake yaani mke au mchumba yake, Je inakuwaje pale inatokea mke au mchumba ndo anakuwa chanzo cha maumivu ya hisia za mwanaume?
Ni muhimu sana mwanamke (mke au mchumba) kuepuka haya;-

Kumwambia kwamba hana thamani yoyote na kwamba hana lolote na hakusaidii lolote. Hata kama unaongea ukiwa na hasira kumwambia mwanaume yeyote kwenye mahusiano kwamba hana maana unaweza ukajutia. Ni busara kama una hasira na unajiona huwa unakuwa huna break kwa maneno unaongea baki kimya.

Kumfananisha yeye na mwanaume mwingine ambaye amefanikiwa iwe pesa au maisha kwa ujumla. Usimwambie mumeo au mchumba wako kwamba mbona mke wa fulani au mchumba wa fulani amenunuliwa hiki au kile na yeye hawezi, hiyo ni kashfa. Atakwambia uende ukaolewe naye kama wewe ni mchumba na kama ni mke atakwambia nenda kaishi naye au unawasha moto ambao kuuzima unahitahi magari ya fire ambayo tena yanakuja bila maji.

Usimwoneshe kwamba husikilizi pale anaongea hasa anapoongelea jambo lolote analoliona ni la msingi. Hata kama kama anachoongelea unaona kwako ni upuuzi jitahidi kuonesha kama unamsikiliza ikiwezekana hata kuuliza maswali kutokana na anachoongea. Ukimsikiliza atajisikia wa maana na anaweza kuongea na wewe mambo mengi ya msingi.

Usifanye utani (hasa kwa kutumia wanaume wengine hasa utani unaomdhalilisha yeye) hata kama unatumia utani ukiongelea mwanaume ambaye ni rafiki yake. Maana akiumizwa hisia zake kumbuka kutibu ni gharama kubwa sana. Kwani kwa maneno wengine wamevunja ndoa na uchumba.

Kutoa sababu kila mara mumeo anapotaka kufanya mapenzi na wewe, hii ni pamoja na kuwa mwanamke mwenye huzuni mara zote, hakuna furaha wala kutabasamu kila wakati mwanamke ni malalamiko, huzuni na gubu, unafikiri kwa nini aliondoka kwa mama yake na baba yake kama si kukasirikiwa kila mara.
Amekuchagua wewe ili uwe faraja na akiwa na wewe anajisikia raha kama hivyo basi ni afadhari asirudi nyumbani au atumie muda wake na mtu mwingine usidhani eti kwa kukasirika au kuonesha uso wa huruma na huzuni ndipo mwanaume atakuona wa maana au kukuhitaji na kukubembeleza zaidi, ukweli anajiona hawezi kukupa furaha na hivyo afadhari awe na kitu kingine badala yako, who cares hata TV anaweza kuona inamfaa kama si kwenda kuangalia mechi za ligi kuu Uingereza.

NI VIZURI KUKAGUA MSINGI.

Katika kujenga au kusimamisha jengo lolote duniani kawaida kuna taratibu ambazo ni sharti zifuatwe ili jengo lisimame, liwe imara na lidumu.

Tumekuwa tukishuhudia majengo mengi yakiporomoka hii ni kutokana na kutofikia viwango hasa uzembe wakati wa kufanya ukaguzi wa ujenzi tangu msingi.
Pia hata kama jengo likiimarishwa juu wakati msingi ni ovyo au haujafikia viwango bado jengo zima lipo hatarini na haliwezi kufika mbali kwa sababu msingi hautaweza kuhimili kila aina ya dharuba, mitikisiko, upepo na wakati mwingine hata mvua.

Tunaporudi kwenye suala la mahusiano wakati wa uchumba ndiyo wakati wa kuchunguza msingi, ni wakati wa kufanyia inspection msingi kuhakikisha ni kweli una standards zinazotakiwa kuhakikisha jengo linadumu karne hadi karne.

Mtu unayechagua kuoana naye na kujenga maisha yako yaliyobaki hapa duniani ni vizuri akawa na imani, values, interest, standards, mitazamo unayoridhika nayo na kufikia uamuzi wa kukubali kupitisha hati ya kusaini kwamba msingi umefikia viwango vinavyotakiwa (engagement ring) ingawa bado unaweza kuahirisha ujenzi ukigundua kwamba bado jengo linaweza lisisimame kwani kuachana katika uchumba ni kiroho na pia afadhari kuvunja uchumba kuliko Ndoa.
Ni busara kuvunja msingi kuliko kumaliza jengo la ghorofa 25 then linavunjwa.

Wakati unaendelea na inspection ya msingi kama unaona kuna dalili na umethibitisha kwamba nyufa zilizopo zinaweza kusababisha jengo lisisimame, deal with it!,
Usifanye terrible mistake kwani kufikiria kwamba nitaishi naye hata kama ana matatizo hayo au hata kama hili ni tatizo ambalo nitasaidiana naye hadi nambadilisha; thubutu! kawaida hatuwezi na hatutaweza kumbadilisha mtu hata kama upo smart namna gani au una skills za ajabu za kushawishi, suala la ndoa na mapenzi ni gumu utajuta!

Binadamu ni wazuri sana kwa kutoa ahadi hasa katika mapenzi,ingawa ahadi nyingi ni kwa ajili ya kukupata wewe hivyo ni juu yako wewe kuamini kama kweli atakununulia gari wakati kazi hafanyi na mvivu, hana tatizo na dini yako wakati haitambui dini yako, atakupenda milele wakati juzi ulikutana naye ana kwa ana amekaa na rafiki yako katika mkao wa hasara uliotikisa moyo wako kiasi kwamba ile picha ikikurudia unajisikia he is the wrong person.
Anakwambia anakumiss wakati huohuo kuwasiliana na wewe hadi umkumbushe maana hakuna cha simu wala sms wala email wakati simu anayo.
Hapa unafanya uamuzi wa aina yake katika maisha yako na watu wanaweza kukushauri ila mwamuzi ni wewe.
Pia hata kama umeachwa na mchumba inawezekana huo ni muujiza wa kumpata aliyesahihi kwako hivyo usiumize kichwa.

“Don't cry for a man who's left you, the next one may fall for your smile.”

MAHUTAJI MUHIMU KWA MWRNZA WAKO.

Kama ni mwanandoa ambaye unataka kuwa na ndoa yenye furaha, inaweza kuwa ndiyo kwanza unaanza maisha ya ndoa, au unaweza kuwa upo kwenye ndoa kwa muda mrefu na ndoa ipo hali mbaya kiasi kwamba unajuta kwa nini upo kwenye ndoa au inawezekana wewe ni mmoja ya wanandoa ambao wanafurahia kuwa kwenye ndoa na unapenda kujifunza zaidi na kuwa na ndoa yenye kumpa Mungu utukufu zaidi.

Jambo la msingi ni kwamba unaweza kuijenga ndoa imara kama tujifunze kufahamu mahitaji ya mwenzako na kuyatumia.

Bila kutimizwa kwa haya mahitaji muhimu wanandoa wengi hujikuta katika matatizo makubwa baina yao.
Mahitaji ya mwanaume na mwanamke ni tofauti hivyo basi kila mmoja anahitaji kuwa makini kujua upande mwingine unahitaji kitu gani na si kuhitaji tu bali kutimiza.

Mahitaji matano muhimu ya mwanaume katika ndoa
Kuridhishwa kimapenzi (sex)
Mtu wa kuandamana naye
Mke anayevutia
Msaada nyumbani,
Kuwa na mwanamke anayemuhitaji (depend on him)

Mahitaji muhimu ya mwanamke katika ndoa
Upendo,
Mtu wa kuongea naye
Uwazi na ukweli
Kutimiziwa hitaji la fedha
Mwanaume anayejali familia
Kwa mwanandoa kukosa moja ya hayo mahitaji muhimu huweza kutengeneza kiu ambayo lazima ipate maji.
Baada ya mwanandoa kukosa mahitaji hayo muhimu anaweza kushawishika kuanza kutafuta kutimizwa nje ya ndoa yake.

NB:
Hata kama mwanandoa mmoja anashindwa kutimiza mahitaji muhimu kwa mwenzake kutoka nje ya ndoa bado si jibu au jawabu kwenda kukipata kile unakosa.
Njia sahihi ni kukaa pamoja na kuelezana kwa upendo kila mmoja kueleza kile anakosa na kuendelea kuijenga ndoa kwa pamoja kwani huko nje kuna foxes ambao kama si kuweza kukutafuna mzima mzima basi unaweza kuangamiza familia nzima.

WANANDOA WENYEWE KWANZA.

Wakati mwingine hata ndoa ambazo huonekana nzuri huweza kushindwa na zile zinazoonekana mbaya hudumu.

Zipo ndoa ambazo wawili huishi kwa mipaka hadi unashangaa sasa kwa nini inaitwa ndoa, kwa mfano mume au mke anatakiwa kuongea kwa mahesabu kwani akikosea neno anaweza kumkasirisha mwenzake na nyumba ikawa haikaliki na hakuna ladha kabisa kuongea na partner wake matokeo yake hata wakiwa wawili hakuna cha maana cha kuongea na kila mmoja hujibakia bubu kwani hujiona ni bora kuwa bubu kuliko ukaongea na ukawasha moto usioweza kuuzima.

Na mwingine hataniwi hata akifika nyumbani kutoka kazini si mama si mume au watoto wanajua kwamba baba amerudi au mama amerudi kila kitu sasa ni moto.
Swali la kujiuliza je, kwa nini uwe hivyo na unapata faida gani kuwa hivyo? kwa nini familia iwe na nyoka mtu?
Pia wapo wanandoa ambao huwa hawakubali kushindwa hasa pale kukiwa na tofauti ya mawazo au kutoelewana kati yao.
Kila siku wewe ndiye upo sahihi na kila siku mwenzako ndiye anakosea, haiwezekani binadamu wawili wakaishi pamoja na kila siku mara zote mmoja ndo anayekosea, huo si ustaarabu na ni ubabe tu.

"Ijulikane kwamba ndoa hurekebishwa kwa kuanza na wanandoa wenyewe, wanaweza kwenda kwa wazazi au marafiki au majirani au mchungaji, au padre au washauri maarufu wa ndoa au mtu yeyote mwenye utaalamu wa kushauri masuala ya ndoa, kama wanandoa wenyewe hawataki kujirekebisha na kuweka mambo sawa tangu chumbani mwao, mawazo au ushauri wa wengine hauwezi kupenya kwenye maisha yao ya ndoa na kuleta mabadiliko".

posted from Bloggeroid

NI UPI MTAZAMO WA NDOA YAKO.?

Moja ya tatizo la kawaida kwa ndoa za sasa ni mtazamo wa wanandoa kuamini kwamba ndoa yao haitafika popote au siku moja itashindikana au mmoja wa wanandoa kuwa na wazo kwamba siku moja ataondoka zake au wote kuwa na mtazamo kwamba siku moja nitaondoka na kuanza kivyangu upya.

Ukiwa na wazo la kushindwa ni hakika utashindwa vizuri sana kwani muda wote utakuwa unaangalia matatizo yote (negatives) ambayo yanakuwa alama kwamba sasa kushindikana kumeanza.
Yaani kwa kuwa una mawazo kwamba siku moja ndoa itashindwa basi akili yako hujipanga kusubiri dalili za kushindikana hata wewe mwenyewe kujua.

Wapo wanandoa wanaweza kusimama juu ya paa na kukiri kwamba ndoa zao ni za furaha hata hivyo ukichunguza kwa makini siri ya furaha yao si kwa sababu hawakutani na matatizo au shida au mambo magumu bali ni kwa sababu ya mtazamo wao kwamba wao ni mke na mume hadi kifo kitakapowatenganisha na zaidi sana wanajua sanaa ya kusuluhisha matatizo katika ndoa yao kwa kuanza na wao wenyewe kila mmoja kuamini kwamba anaweza kubadilika kwanza na kuleta mabadiliko na siyo kunyosheana vidole au kila mmoja kujiona yupo right all the time.

Inawezekana wewe unayesoma hapa sasa hivi ni mmoja ya wale ambao likitokea tatizo nyumbani na mumeo/mkeo basi ni kununa tu eti kwa kuwa siku moja utaondoka zako! Au kwa sababu una mipango yako kabambe na murua kabisa ya kumuacha mwenzio kwenye mataa hata hujafikiria watoto na huo uamuzi wako ambao ni kujifaraji tu kwani kuondoka si jibu la mambo yote bali ni njia nzuri ya kwenda kuanza kukutana na tatizo jipya na kubwa zaidi.

Kwani wewe ndo mtu wa kwanza kukutana na tatizo kama hilo kwenye ndoa?
Si kweli, badala ya kuchangamka na kupenda kwa moyo wako wote wewe unafikiria kuondoka au kudhani sasa mwisho wa ndoa umefika.

Eti tupo tofauti sana hatuwezi kuishi pamoja tena! Kwani ni nini kilikuvutia hadi ukakubali kuoana naye? Eti siku hizi simpendi kabisa! Lini umeanza kutompenda? Si umeamua mwenyewe kutompenda kwani love is a choice, wewe mwenyewe umeamua kutompenda na kweli humpendi ukichagua kumpenda utampenda.

Eti mke wangu ni mchafu sana! Unataka kumuacha kwa sababu ni mchafu? Mbona wakati wa uchumba alikuwa mchafu na ulikuwa una ignore! Nani mchafu kama si wewe uliyechumbia mwanamke mchafu, leo badala ya kutunza kilicho chako king’ae unataka kukimbia?

Unapoingia kwenye ndoa huku ukiwa na ufahamu au mtazamo kwamba ndoa ni hadi kifo kitakapowatenganisha hapo tayari umepiga hatua kubwa sana na mbali kukuhakikishia ndoa yako inadumu na kuwa ya furaha kwa sababu unakuwa tayari kukubali kurekebisha kila tofauti zinazojitokeza kwani unajua huyu ni mwenzi wangu na kuna umuhimu wa kuishi kwa furaha kila wakati.

Ukiingia kwenye ndoa huku unategemea kushindwa ni kweli utashindwa vizuri sana na ukitegemea kufanikiwa na kuwa na ndoa ya furaha ni kweli utakuwa na furaha na zaidi utajifunza njia ya kuwa na furaha na utakuwa moja ya wanandoa wenye furaha duniani.


posted from Bloggeroid

Tuesday 8 March 2016

SEX KABLA YA NDOA..!

Sex kabla ya ndoa si sahihi na msimamo wangu ni kwamba kabla ya ndoa sex ni dhambi na kuna athari kubwa sana zinazopelekea kutokuaminiana na zaidi kusababisha ndoa kuanza kufa mapema.
Sipendi kuhukumu na kuwa mzungumzaji sana kwenye issue muhimu na personal kama hiyo, hata hivyo naweza kukushauri uende kwa kiongozi wako wa dini na muulize kama atakukubalia sex kabla ya ndoa na akikubali urudi uniambie ili nami niongee naye.

Nikupe mfano wa kweli
Neema ni dada ninayemfahamu anaishi Kinondoni Dar es salaam na alimpata mchumba Jimmy mwanaume wa miaka 40 naye anaishi Msasani jijini Dar es salaam, wamekuwa wanaenda wote sehemu tofauti na kujiona ni kweli kuna kila dalili ya kuwa mke na mume.
Kwa kuwa Neema ana miaka 36 kumpata Jimmy kwake ni kitu adimu na alijipanga tayari kuolewa kwani muda unaenda na nguvu ya uvutano ilishaanza kuvuta kwenda chini.
Jimmy alikuwa akimshawishi Neema walale wote kitanda kimoja mara kwa mara na Neema alikuwa anagoma na kumuahidi wasubiri hadi siku ya harusi.
Hata hivyo miezi miwili baadae, Jimmy alimualika Neema kwenye sherehe ya rafiki zake huko Msasani (jumapili) na sherehe zilichelewa kumalizika kitendo kilichopelekea Jimmy kuondoka na mchumba wake (Neema) na kwenda naye kwake.
Walipofika kwake (Jimmy) walikaa kwenye sofa wakaweka movie wakaanza kuitazama na hatimaye Neema akajikuta yupo kifuani kwa Jimmy.
Movie ikanoga, mara wakaanza kuwekeana miguu kila mmoja juu ya mwenzake, mara kushikana mikono, mara kukumbatiana, hatimaye kisses zikaanza, miguno ya raha ya mahaba ikaendelea kujikoleza, joto la mahaba likapanda na romance ikanoga na hatimaye wakajikuta wameingia ulimwengu mwingine wa kurusha kila nguo waliyovaa kusikojulikana, kilichoendelea Naamini unajua……
Asubuhi Neema akajikuta kile amefanya si kile alipanga na akarudi kwao huku amejawa machozi na mawazo maana hata kupima walikuwa hawajaenda.
Siku iliyofuata ilikuwa Jumatatu Neema akaamua kumpigia simu Jimmy na hakupokea na akaanza visababu.
Jimmy aliacha kumpigia simu Neema na hata baada ya Neema kulalamika na kuuliza kwa nini hapigi simu tofauti na nyuma kabla ya kupewa zabibu, Jimmy aliendelea kujibu utumbo kama si pumba.
Baada ya hapo Jimmy alipotea kabisa kwenye uso wa dunia na mbele ya macho ya Neema kwa namna yoyote.
Kuona hivyo Neema akaamua kupiga kiguu na njia hadi kwa Jimmy na kwa kuwa hakutoa taarifa alichokikuta ni Jimmy yupo kifuani kwa mrembo mwingine.

Kwa asili wanaume huwa na respect ndogo sana kwa wanawake ambao wameshalala nao, so kama unataka ndoa kaa mbali na sex kabla ya ndoa.

posted from Bloggeroid

Saturday 5 March 2016

UPENDO WA NDANI..

Mapenzi katika ndoa huweza kugawanywa katika sehemu mbili yaani upendo wa ndani na upendo wa nje.

Tunapozungumzia upendo wa ndani tuna maana jinsi tunavyoonesha katika emotions kama vile tendo la ndoa, kuwa pamoja karibu (intimacy), pamoja kimawazo, kujieleza katika feelings, maneno matamu yanayoonesha kujali na kupenda, kupeana busu, kukumbatiana, kupeana zawadi nk.

Tunapozungumzia upendo wa nje huu hujikita zaidi katika huduma kama vile kupika chakula, kuzaa watoto, kujenga au kukarabati nyumba, kufua nguo, kupiga pasi nguo, kuogesha watoto na kazi (ajira) ambazo zinatupa vipato.

Hapo zamani (mababu na mabibi) wao upendo external ulikuwa na maana zaidi kuliko internal na kizazi cha leo ni kinyume chake.

Ndiyo maana ni rahisi sana leo kuishi kama mke na mume zaidi ya miaka miwili na ikafika siku mke au mume akamuuliza mwenzake
“je, unanipenda?”

Hata kama wamefanikiwa kujenga nyumba au kuwa na gari au familia na maisha mazuri kwa ujumla.

Kuuliza je, unanipenda ina maana something is wrong kwenye upendo wa ndani (internal) inawezekana ni tendo la ndoa (love making) au ukaribu kimapenzi (intimacy) au maneno ya kutia moyo na sifa kimoja au vyote havipo sawa.

Leo wanawake wanategemea sana mume alete zawadi kuliko kuleta mkate.
Mke anataka mwanaume ambaye anaongea maneno matamu na si anayefanya kazi nzuri tu.

Mwanaume kiasili ni bread winner na anapenda mke atambue kwamba kwa kazi anayefanya maana yake anampenda mke na familia sasa baada ya kazi kutwa nzima na kurudi nyumbani na mkate na mke akamuuliza
“Je, Unanipenda?"
Eti kwa sababu asubuhi wakati anaondoka hakuaga kwa busu na hug kwa mwanaume bado ni kitu kinachoshangaza.

Hata hivyo industrial revolution imeleta mabadiliko ambayo wanaume na wanawake wote sasa wanafanya kazi (mchanganyo wa duties na responsibilities za mke na mume) na leo tupo kwenye information society kwa maana kwamba information zina flow ajabu na kila mwanandoa anataka Mapenzi (romance/intimacy) bila kujali sana kazi anayefanya mwenzake.

Je, siri ya ndoa imara ni ipi?

Siri ya ndoa iliyobarikiwa na imara ni ile inayohakikisha upendo wa ndani unaenda sawa na ule wa nje, ni ile ndoa ambayo inachanganya tendo la ndoa na majukumu kuwa kitu kimoja na kukipa nafasi sawa.

Mwanandoa halisi ni yule ambaye leo anaweza kumsaidia mwenzake anayeumwa kwa kufuta matapishi yake na baadae akaendelea kumpa kisses za kutosha.

Mke halisi ni yule anayeweza kuwa mama mchana na kuwa mpenzi usiku chumbani na kumfurahia mume wake kimapenzi kwa kwenda mbele.
Ndoa iliyo imara ni ile ambaye wanandoa ni waaminifu katika kutekeleza uhitaji wa ndani na nje katika ndoa.


posted from Bloggeroid

SIRI KATIKA NDOA..

Ndoa ni institution ambayo ni takatifu na hujengwa kwa msingi wa kuaminiana.
Huu msingi wakati mwingine hujikuta una hofu ya kubomoka na kusambaratika kwa vitu vidogo vidogo kama suala la siri katika ndoa.

Siri katika ndoa huweza kuharibu msingi wa ndoa ambayo imejengwa vizuri na kuonekana mbele za watu ipo imara.
Ni kweli inawezekana mke wako au mume wako hatakiwi kujua kila kitu kuhusu wewe vile umefanya ana unajua kila siku inayopita duniani hata hivyo ukiangalia kwa undani zaidi siri unazoficha kwa mume wako au mke wako zinaweza kukupeleka pabaya.
Iwe siri nzuri au siri mbaya kumbuka kwamba inaweza kuweka madoa mabaya sana kwenye ndoa yako.

Jambo la kujiuliza ni je, kwa nini unaficha hizo siri?
Kumbuka kiapo, namna ulivyoahidiana wakati mnaoana kwamba ninyi ni kitu kimoja na kama unajikuta unajitahidi kuficha siri basi unaelekea kwenye big trouble.

Je, unaficha matumizi ya pesa?

Kumbuka siri katika ndoa mara nyingi ni hatari kwani itafika siku utaangukia pua, kwa mfano kama unaficha namna unatumia pesa na madeni yanazidi kuingiliana ipo siku wanaokudai watakuja kuuza nyumba ndipo mke au mume atajua kulikuwa na tatizo na utakuwa umeshachelewa!
Inawezekana unamficha mchumba wako kwamba huna mtoto wakati mtoto unaye, siku akigundua hata kama mmeoana miaka 5 au 10 gharama ya kurudisha trust itakuwa kazi ya ziada, Utajuta!

Inawezekana unaficha siri kwamba mtoto uliyenaye si wa huyo mume wako na umeamua kula jiwe, hata hivyo siku akigundua hapata tosha!

Je, ni siri kiasi gani unamficha mke wako au mume wako au mpenzi wako?

Kumbuka mahusiano ya kweli hujengwa kwa trust, kuficha siri ni moja ya bleach ya trust na zaidi kuliko yote hakuna siri duniani.

posted from Bloggeroid

Friday 4 March 2016

MWENDO WA POLE POLE HULETA RAHA ZAIDI.

Unachotakiwa kujua ni kwamba inches mbili za kwanza kwenye uke wa mwanamke ndiyo ina hold raha ya sex kwa mwanamke (ni sehemu yenye nerves za raha ya sex kuliko ndani ya uke.

Na kuna factors 3 muhimu za kuzingatia

MWENDO
Lazima uwe katika kipimo ambacho mwanamke anaweza kujisikia (feel).
Wanaume wengi hufanya makosa ya kwenda kwa nguvu kama mbio za hasira.
Hii ni kupoteza muda wakati mwingine otherwise iwe imefanywa for right time.
Kwa wanawake wengi isipokuwa muda mfupi kabla ya kufika kileleni suala la kutumia miguvu ni style ambayo huwaacha katika maumivu na boring kwani kawaida feeling za utamu wa tendo hupati.

Ngozi huweza kubeba feelings za sex mara 10 zaidi iwapo mwanamke atakuwa anasisimuliwa polepole.
Kufahamu siri hii kutaweza kukupeleka mbele zaidi na kukufanya mwanaume lovable kutimiza kile mke wako anahitaji.

Kumbuka ngozi yetu kama wanaume linapokuja suala la sex (uume) ipo nje na kavu ukilinganisha na mwanamke ambaye organs zake zipo ndani, wet na zipo nyororo kama ua la roses.
Huhitaji kuwa genius ili kufahamu jinsi unaweza kusababisha maumivu bila kwenda polepole.

Jinsi mwanaume anavyoumia akipigwa teke kwenye balls ni sawa na mwanamke kuumia wakati mwanaume akiwa rough ndani ya uke.
Weka akilini kwamba muda wote unapomuingia mke wako unatakiwa kuwa na movement polepole hatua kwa hatua kama vile unawasha moto ili aweze kupata feeling kwenye ngozi yake.
Hivyo hata kama ni ile ya Quickie au whole night mwanaume kumbuka kuwa passionate na loving huku ukiwa na self control kuhakikisha skin on skin ipo tender.

Iangalie sex kama riadha kwa kuanza polepole na baadae unaongeza mwendo kidogo na mwisho mwenda wa kufa mtu na kushinda hizo mbio.
Exception ya hii kanuni ni pale tu mwanamke anapokuwa ana nyege kuliko kawaida (very hot, wet, loose) na ana ugulia kwa hamu au kiu ya sex hivyo inabidi amalizwe kiu haraka iwezekanavyo.

PEMBE YA KUINGILIA
Angle muhimu kwa ajili ya kumpa raha na ridhiko katika kiwango cha juu kwa mwanamke kwanza ni muhimu kwa uume kucheza kiasi cha inches 1-1/2 hadi 2 ndani ya uke.
Pia fikiria mke wako amelala chali na wewe unamwangalia akiwa mbele yako na ukachukua saa na kuiweka juu ya uke wake basi pale inaonesha 12 (12 o'clock) ndipo kwenye vaginal orgasmic trigger.

Ili kumsisimua kiwango kinachotakiwa unahitaji ufahamu wa hili eneo na pia angle ambayo mwanaume anatakiwa thrusting.
Ndiyo maana love making position nzuri ni ‘Doggy Style', huu mlalo ni fantastic kwa sababu
Kwanza mwanaume anapofanya thrusting uume hugusa moja kwa moja kwenye vaginal trigger (G-spot)

Pili huwaruhusu mwanamke na mwanaume huwa huru kujielekeza kule kunasisimua zaidi, pia mwanamke anaweza kusaidiana na mwanaume kuwa na movement za mzunguko kwa mwanamke kuzungusha kiuno kutoka upande wowote chini, juu, pembeni au vyovyote anataka.

Tatu kunakuwa na uwezo wa kuthibiti kiasi gani uume uingie (deep or shallow)

Faida kubwa ya face to face ni kwamba inakuwa rahisi kwa mke na mume kubusiana na hii ni factor ambayo inatakiwa isichukuliwe kwa mzaha hasa pale anataka kufika kileleni.

KINA
kichwa cha uume hakikuumbwa kwa ajili ya kuweza kuingia kirahisi au kwa ajili ya mwanaume kufurahia sex bali kwa ajili ya kumuwezesha mwanamke kufurahia tendo la ndoa (awe crazy).

Hivyo basi kuingia kwako ndani yake kunatakiwa kuwa kitu kizuri kwake kujisikia.
Kuna baadhi ya wanawake huwa ngumu sana kufika kileleni kwa uke kusuguliwa na uume hata hivyo kama mwanaume anajua namna ya kutumia tool yake basi anaweza kuondoa hivyo vaginal climax barrier.

Kuanza kwa strokes za kwanza very slowly na shallowly!
Hii husaidia kwani mwanamke huhitaji kuingiliwa slowly, tenderly kama ua linavyofunguka asubuhi wakati wa kiangazi.
Kufungua kwa haraka huweza kusababisha ua kukauka.
Kuwa na haraka kuingia huweza kumuumiza hivyo kabla ya kuiingia ni vizuri kutumia kichwa cha uume kusugua polepole eneo zima kuanzia juu kwenye kisimi hadi urefu wote wa uke kwa nje.
Waingereza huita ni style ya “Sausage & Bun" au hii ipo designed kwa ajili ya kuwafikisha kileleni wanawake ambao hufika kileleni kwa njia ya kisimi tu.

Baada ya hapo unaweza kuwa na penetration ndani kidogo hata kama anakuomba uingie zaidi kwani wewe ndiye kiranja wa hicho kipindi si yeye.

Polepole ongeza kuingia ndani hadi mwisho na hapo unaweza kuongeza speed kwa kadri unavyojisikia na bila kusahau skills za kujizuia usimalize mapema.

Ukihisi anataka kufika kileleni unaweza kupunguza moto au kuchochea zaidi in full speed huku ukiwa na movement za aina tofauti.

posted from Bloggeroid

Thursday 3 March 2016

UPENDO HUU KATIKA NDOA..

Tumeona kwamba mwanamke anatakiwa (lazima) amheshimu mume ili mume naye ampende na matokeo yake kila mmoja aridhike na mwenzake na hatimaye kuwa na uhusiano mzuri idara zote.

Mke anahitaji mume anayempenda na kumuonesha upendo kuanzia asubuhi, mchana na jioni wakikutana mume anahitaji kuwa karibu na mke wake ili mke ajisikie anapendwa na hatimaye ajisikie relaxed na kuwa tayari hata kwa activities zingine usiku.

Je, mume kuwa karibu na mke wake ina maana gani?

Maana ya kuwa karibu kwa mke na mume ni kuambatana, shikamana, kushikana, ng’ang’aniana, fungamana, kaa jirani jirani, songamana, karibiana, kuwa pamoja (cleaving, cling or intimate)
Kuwa karibu ni kuungana uso kwa uso na kuwa mwili mmoja.
“Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe nao watakuwa mwili mmoja”.
(Mwanzo 2:24)

Katika uimbaji wa Mungu ni Binadamu peke yao ambao huweza kuwa karibu kimapenzi (sexual intimate) uso kwa uso.
Kuambatana kati ya mke na mume ni zaidi ya kuwa mwili mmoja.
Kuambatana kwa mke na mume ni kuwa karibu au mwili mmoja kiroho na kimwili.
Kama wewe ni mwanaume inakupasa ufahamu kwamba mke wako hufurahia na kujiona anapendwa na wewe pale unapomkaribia na kufanya ajione unataka kuwa karibu kwa namna unavyomtazama, unavyomgusa, unavyomkumbatia, unavyotabasamu na kumbusu na kumwambia NAKUPENDA.

Katika ulimwengu wa sasa ni rahisi sana kwa mke na mume kuchukuliwa na kuwa busy na kujisahau kujenga ukaribu ambao ndiyo msingi wa mwanamke kujisikia anapendwa na mume wake.
Wanandoa wenye busara huchukua dakika si chini ya 15 kila siku wakikutana jioni baada ya kazi; huhakikisha kila mmoja anajihusisha na mwenzake kwa ukaribu wa kimaongezi na sharing ya information za namna siku ilikuwa kwao wote na matokeo yao jioni na usiku vinakuwa exciting.
Mke akirudi anataka connections, anataka involvement na mume, anataka face to face talks na Mume akirudi kazini anataka kupumzika hata hivyo jambo la msingi ni mwanaume kuhakikisha anapata muda wa kutosha ili kufanya connection na mke na hasa kama unataka mambo yawe safi kuanzia jikoni, sebuleni hadi chumbani huo usiku pia usigande kwenye TV au Gazeti bila kuongea na mke wako na kusaidia kazi ndogondogo hapo nyumbani.
Kuna ubaya gani kama utakuwa unapiga story na yeye anaandaa dinner au na wewe unasaidia kupika (kama hamna wafanyakazi wa ndani)

KUMBUKA KUWA KARIBU NA MKE SI GHARAMA BALI MUDA:

Mke atafurahi kama mara kwa mara:
Utamshika tu mikono,
Utamkumbatia na kumbusu wakati wowote,
Unapokuwa affectionate bila wazo la sex,
Kufanya kitu kinachosaidia kuwa na “togetherness”
Pale unapomwambia unampenda, yeye ni mwanamke mzuri (mrembo).
Kumbusu mke kwa sababu unataka sex tu ni turn off.
Pale mnapoangaliana na kupeana story zinazowafanya kuwa na kicheko.
Unapotumia muda wa kutosha kuwa na yeye katika kazi ndogondogo kama kupika, kufua nguo, kuogesha watoto, kusafisha nyumba nk.
Pale unapomfanya ajisikie unafurahia kujadili vitu mbalimbali na yeye.
Pale unapoendelea kuongea naye, au mkumbatia na mbusu baada ya tendo la ndoa.

posted from Bloggeroid

Tuesday 1 March 2016

MUNGU AMEKUWA KIMYA KWAKO?

Kila mmoja wetu, mimi, wewe na yule tunakutana na milima na mabonde, nuru na giza katika maisha yetu ya kila siku.
Hata hivyo jambo moja kubwa ambalo linatoa tofauti kati ya mtu na mtu ni namna tunavyochukulia namna Mungu anahusika na maisha yetu.
Hata baada ya juhudi ya kuomba na kufunga, kujitoa na kujitakasa mbele za Mungu na kuishi maisha ya uaminifu na utakatifu bado Mungu amekuwa kimya katika kujibu maombi yetu au kukutana na mahitaji yetu ambayo ni kilio chetu kwake kila iitwapo leo.
Katika Biblia kuna maelezo yanayohusu Lazaro na dada zake Maria na Martha, rafiki wa karibu wa Bwana Yesu katika kijiji cha Bethania.
Lazaro aliugua na akawa serious (naamini alipelekwa hadi ICU) na wakatuma habari kwa Bwana Yesu ili aje amfanyie maombi na ndugu yao apone; hata hivyo Bwana Yesu ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa hii familia hata baada ya kupata habari aliendelea na ratiba yake kwa siku mbili zaidi.
Lazaro akafa!
Naamini tafsiri ambayo Maria na Martha walikuwa nayo ni kwamba Yesu alikuwa Hawajali na kuwaona hawana maana.
(Yohana 11:1-10)
Fikiria walivyojisikia Maria na Martha kwa kitendo au kwa ukimya ambao Bwana Yesu aliuonesha kwao?
Fikiria huzuni waliyokutana nayo familia hii huko Bethania kwa Bwana Yesu kukaa kimya kwa siku mbili zaidi hadi mpendwa wao akafa?

Je, Mungu amekuwa kimya kwako?

Pamoja na kuomba bado Mungu amekuwa kimya na umefika Mahali unakata tamaa na kumuwazia Mungu vibaya?
Mungu yupo kimya kwa sababu anataka kutenda muujiza katika maisha yako, anataka kukuonesha ishara ambazo zitakufanya umtukuze yeye maisha yako yote.
Inawezekana Mungu amekuwa kimya kujibu maombi yako ya kutaka kuwa na ndoa yenye amani,maombi yako ya kutaka kuolewa, kazi, ndoa, shule, fedha, watoto, familia, elimu nk hata hivyo jambo la msingi unatakiwa kuwa makini sana namna una behave katika kipindi kama hiki kwani ni wakati wako wa kumjua Mungu ili kupokea baraka.
Mungu anataka kukuonesha Mpango kamili wa maisha yake kwako.
Tunatakiwa kumuamini, kumpenda, kumtegemea, kumsadiki na kumngoja Bwana hata akiwa silent.
Fikiria namna walivyofurahi baada ya Yesu kumfufua Lazaro siku nne baada ya kufa? Matumaini na kukua kwa imani na kutukuza matendo makuu ya Mungu?
“Trust in God stays strong even when He is silent”

posted from Bloggeroid

UPENDO HUWA HIVI..

Mara ya kwanza ulipopendana na mume wako au mke wako au mchumba wako, kuwaza kuhusu yeye kulikuja kwenyewe automatically.
Ulitumia masaa mengi sana kumuwaza namna anavyoonekana, ukijiuliza atakuwa anafanya nini katika muda fulani, ulikuwa unarudirudia kuwaza na kujiuliza vitu vizuri ambavyo ungemwambia au kuongea naye wakati mkiwa wote, ulimtumia emails nzuri zenye maneno matamu, ulimtumia sms mara kwa mara kuonesha ulikuwa unamuwaza, uliandika hata barua nzuri kuonesha hisia zako na kwamba ulikuwa unamuwaza, ulihangaika kutafuta maneno matamu ambayo akiyasikia anafahamu kwamba zaidi ya kumpenda ulikuwa unamuwaza.
Na hata usiku ulimuota (ndiyo maana ulikuwa unamwambia usiku hukulala) yeye kwa sababu ulikuwa unamuwaza kuliko kitu chochote.
Ikafika Mahali ukakiri kwamba;
“Siwezi kuacha kukuwaza wewe!”
Hata hivyo kwa baadhi ya wapendanao (inawezekana hata wewe unayesoma hapa ndicho kinachoendelea katika ndoa yako) baada ya kuoana mambo huanza kubadilika kwani mwanamke sasa amempata mwanaume aliyekuwa anamuhitaji; na mume ameshapata trophy ambayo alikuwa anaiwinda miaka yote, sasa kazi ya kuwinda amemaliza, mission accomplished, job done, malengo yametimia.
Miali ya ukaribu wa kimapenzi inaanza kuwaka kwa udhaifu mkubwa na kilichokuwa kinasukuma kumuwaza sasa kinapoa, sasa unaweka malengo katika kazi na taaluma yako au marafiki, au mambo unayoyapenda wewe binafsi na baada ya muda unaanza kuacha kutimiza mahitaji ya mke wako au mume wako.
Hata hivyo bado ukweli unabaki palepale kwamba ndoa imemuongeza mtu maalumu katika maisha yako na hii haitabadilika na kama uwezo wako wa kufikiri unashindwa kumweka mtu aliyeongezeka katika mawazo yako ili kumpa nafasi basi unakoelekea ni hatari.
Kama hujifunzi kumfikiria/kumuwaza mke wako au mume wako basi unaweza kuishia pabaya, inaweza kufika birthday yake usijue, inaweza kufika anniversary ya ndoa yenu na usikumbuke na ukalaumiwa kwamba humfikirii yeye bali wewe mwenyewe.
Utakosa opportunities nzuri za kuweza kuonesha upendo wako kwake.
Kuonekana huna wazo lolote kuhusu mke wako au mume wako ni adui mkubwa wa kudumisha moto wa ukaribu wa kimapenzi katika ndoa.
Mwanamke siku zote ana hamu ya kufahamu namna mume wako anavyomuwaza na hii humfanya kujisikia anapendwa.
Je, ni mara ngapi au ni muda kiasi gani umekuwa kuitumia kuwaza namna unaelewa na zaidi unavyoweza kuonesha upendo kwa mume wako au mke wako?
Je, ni tukio gani (birthday, anniversary, holiday) ambalo sasa unaandaa ili kuonesha unamuwaza na unamkumbuka?
“Great marriages come from great thinking”

posted from Bloggeroid