Friday 25 March 2016

WANAWAKE HUJISAHAU.

Tatizo kubwa la wanawake wakiwa kwenye mahusiano (ndoa au uchumba) ni kwamba huwa wanasahau mahitaji yao na kujikuta wanavutwa na kuhusika zaidi na mahitasji ya wengine au wapenzi wao kihisia na kisaikolojia.

Challenge kubwa inaowakabili wanawake wote duniani wakishaiingia kwenye mahusiano ni uwezo wa kuimarisha sense of self, kujitambua, kujiamini, na kuanza na wao kwanza kabla ya mpenzi hasa linapotokea suala la mgogoro.
Wakati mwanamke hu-expand mwanaume hu-contract.
Kama ilivyo nguvu ya centripetal amabyo huhusika kuvuta kitu katikati (mwanaume) na nguvu ya centrifugal ambayo huhusika kuvuta kitu pembeni (mwanamke) kutoka katikati ndiyo ilivyo kwa mwanamke na mwanaume kwani mwanaume mara zote hurudi kwenye centerpoint hupungua, husinyaa, huongea kidogo, huongea kwenye point, wakati mwanamke yeye hupanuka kutoka katikati kwenda pembeni, huongea sana hata kama si point, huvutika kuongeza maongezi.

Ndiyo maana wanaume hulaumiwa sana linapokuja suala la mawasiliano kwani mwanamke na mwanaume wanapoongea mwanamke hu-expand maongezi na mwanaume hui-contract na kuongea kwenye point.

Kawaida mwanaume hufikiria kwanza (kwa ndani) kile anataka kuongea ili kujua kama ni point, wakati mwenzake mwanamke huendelea kuongea tu na anapoongea inamsaidia kuijua point,
Hii ina maana mwanamke huongea iliajue point na mwanaume hujua point ili aongee.

Bila kujua hii tofauti basi mwanaume asiyejali anaweza kusikitika sana kumsikiliza mpenzi wake na kuona alikuwa anaongea pumba au pointless na amempotezea muda wake au kuendelea kubishana kwamba mwanamke haongei point au kumkatisha kwa kuwa anachoongea hakielewiki.

Mwanaume anayejali husikiliza kwanza hata kama mwanamke anaongea kitu ambacho anahisi hakieleweki hata hivyo baadae ataelewa na mwanamke anajisikia mwanaume anamjali na kumsikiliza na maisha yanaenda

No comments:

Post a Comment