Thursday 28 May 2015

NI MUHIMU KUZINGATIA HAYA,UNAPOCHAGUA MTU WA KUOANA NAE..

Suala la kuchagua mtu wa kuoana naye ni hatua rahisi ya muhimu katika process ya kuingia katika ndoa.
Jambo la msingi ni kuweka mkazo au msisitizo zaidi katika sifa za binadamu alivyo ndani yake kuliko kuangalia vitu alivyonavyo na anavyoonekana. Pia sifa za akili zake (mental) ni muhimu kuliko sifa za mwilini (physical).
Sifa za ndani za kibindamu si rahisi sana kubadilika kama sifa za nje na vitu alivyonavyo ambavyo hubadilika.
Pia tusisahau kwamba katika suala la kuchagua mke au mume wa kuishi naye katika ndoa suala la bahati lipo na hapa hakuna maswali.
Hata hivyo suala la kukubaliana kuoana na mwanaume au mwanamke ambaye ni cha pombe ukiamini mkioana ataacha au utambadilisha ni suala ambalo Unajidanganya.
Pia kwa mwanaume kuoana na mwanamke kwa sababu tu anaonekana mrembo na kupuuzia sifa zake mbaya, ni kujimaliza mwenyewe.
Tumia muda kufahamu maisha ya nyuma ya mtarajiwa wako, fahamu namna mahusiano yake ya zamani yalikuwa, isije kuwa bado yanaendelea.
Kwani kupuuzia vitu vya msingi kama hivi unaweza kujikuta unalipa gharama kubwa ya maisha yako.
Tafuta kama kuna vitu mnafanana ambavyo wewe unapenda kufanya kwani migogoro mingi huanza pale kila mmoja anapofanya kile anakipenda na mwenzake hapendi.
Na ndoa hujengwa na kushikwa na vitu vidogo sana katika maisha ya hao wawili.
Je, vile wewe vinakuchekesha na mwenzako hucheka?
Je, mnapenda vitu vinavyofanana?
Ndiyo maana ndoa za Hollywood huwa hazidumu kwa sababu mkazo ni kwenye vitu na sura (material things) ambavyo havina sehemu katika kufanya ndoa kuwa imara.
Kabla hujakubaliana kuoana na huyo mtu unatakiwa kujiuliza, hivi ni kweli ninampenda kweli huyu mtu kuliko mtu yeyote duniani?

Tuesday 26 May 2015

NI MUHIMU KUFIKIRIA HAYA,KABLA YA KUAMUA KUACHANA.

Kwa wewe ambaye umeoa au kuolewa na upo unafikiria kuachana na mwenzi wako.

Fikiri upya uamuzi wako.
Fikiria hao watoto mlionao, Fikiria nyakati zote nzuri mlizokuwa nazo pamoja kama mke na mume, Fikiria sehemu tofauti ambazo mlitembelea pamoja, marafiki wazuri mliokuwa nao wote wawili kama mke na mume.
Iepuke talaka kwa gharama zote, sababu zinazokufanya uamue kuachana na huyo mume wako au mke wako zinaweza kuwa ndizo zitakazokuwa sababu mara nyingine tena mbele ya safari kama utaamua kuoa au kuolewa tena.
Sasa unaachana na Jeffy kwa kuwa umechoka na tabia zake za kulewa sana pombe, au kukutaka sex mara nne kwa siku na next time unaweza kujikuta unaachana na John kwa kuwa anakupiga mingumi usiku kucha na yeye sex kwa mwaka mara moja.
Inawezekana unataka kuachana na Aziza kwa sababu ni msumbufu na anakusema hata kwa vitu vidogo, hata hivyo unaweza kujikuta unaachana na Mary baadae kwa sababu si mwaminifu katika fedha.
Sasa utaishia wapi na hiyo project ya kuachana na kila unayeoana naye?
Ukiangalia kwa makini kinachobadilika ni tabia na mhusika tu ila wote ni binadamu na binadamu asiye na kasoro bado hajazaliwa hadi leo.


Maisha ni matamu sana kiasi cha kuyapoteza kwa kupeana talaka.
Wanaume wote duniani wanafanana pia wanawake wote duniani wanafanana , na sote ni binadamu.
Waingereza wanamsemo usemao "better the devil you know than the angle you don’t" tumia ubongo.
Wapo wanandoa ni wazembe kiasi ambacho huacha kutumia kila alichonacho kuhakikisha ndoa inarudi kwenye mstari, kukimbilia talaka si jibu bali ni kumsukuma tatizo mbele na matokeo yake utakuja kukutana nalo tena mbele ya safari.
Hata kama kuna mtu amekuahidi kwamba ukiachana na huyo uliyenaye basi yeye atakufanya uwe mtu mwenye furaha, hatakuumiza wala kukuacha, ni mwongo na anakudanganya kwani katoka sayari gani na binadamu gani.
Anaonekana anakufaa kwa kuwa huishi naye ukianza kuishi naye utajikuta umeruka mikojo na kukanyaga..


Jiulize mwenyewe upya.
Hivi kweli nimetumia uwezo kiasi gani kuhakikisha mwenzi wangu anajua namna tunahitaji kuirudisha ndoa yetu kwenye mapenzi upya kama tulivyoahidiana siku tunaoana?
Je, ni kweli nimefanya kila linalowezekana kusamehe na kusahau?
Je, ni kweli tunataka kuachana na kupeana talaka kwa sababu za msingi?
Kabla ya kuwasiliana na ndugu zako, rafiki zako, washauri wako, wanasheria au wachungaji wako Jaribu kukaa mwenyewe, na mwenzako kujadili upya na kwa upendo namna ya kutatua tatizo lenu na hakuna anayejua shida ya ndoa yako isipokuwa wewe na mwenzi wako.
Usifanye kwa haraka ukiamini unaingia kwenye uhuru.
Dawa ya kuachana au talaka ni kusamehe bila masharti.

Sunday 17 May 2015

MWAMBIE MPENZIO UNACHOTAKA WAKATI WA SEX..

Kuongea suala la tendo la ndoa (sex) katika ndoa au kwa mume wako au kwa mke wako ni moja ya topic ngumu sana chini ya jua au katika uso wa dunia.
Kama utakuwa na maongezi au mawasiliano kuhusiana na suala la sex katika ndoa yako maana yake mtakuwa wazuri katika hiyo department.
Wanandoa wengi ambao wamekuwa na tabia ya kuongea kuhusu maisha yao ya sex kwa uhuru na ukweli wamekuwa na maisha mazuri chumbani kwako kwani si rahisi kufahamu mwenzako anahitaji kitu gani hadi umwambie.
Kuwa wakimya kuhusiana na kuongea kuhusu sex na mke wako au mume wako husaidia kuwa wajinga zaidi na wakati mwingine kutoridhishana sawa na uhitaji wa mwili wako au feelings zako.
Hatari kubwa zaidi ni pale wanandoa wanaposhindwa kuongea wenyewe na matokeo yake kutoridhika na kutoridhika ndiko husaidia kukwetua njia ya mmoja au wote kuanza kuangalia nje (kuchepuka)
Firikia wewe ni mwanamke una vitu mume wako akifanya basi huwa unajisikia kusisimka na mwili kuanza kutoa kuwa juicy na kutamani sana sex na mume wako.
Kwa nini usiwe huru ukamwambia kwamba unapenda iwe hivi:

WAKATI UMESISIMKA....
Mwambie hivi Natamani mume wangu na wewe uwe unatoa sauti au na wewe uwe unaongea,
Napenda uwe unaongea maneno matamu ya kimapenzi,
Napenda mume wangu nini unakipenda kwenye mwili wangu,
Napenda uniguse (touch) na kunichezea namna hii (onesha),
Napenda ufanye hivi kwenye chuchu na matiti yangu,
Napenda unitazame usoni,
Napenda unichezee kisimi namna hii (mwambie unapenda afanye kwa kutumia nini na namna gani)
Napenda ufanye hivi kwenye G- spot,
Napenda kuchezea uume wako hivi nk

WAKATI WA KUHONDOMOLA..
Mwambie mpenzi Napenda na wewe uwe unaguna na kutoa sauti za kimahaba au uongee maneno matamu na elezea namna unafurahia au unajisikia kuwa ndani yangu,
Napenda uendelee kunibusu namna hii,
Endelea kusisimua kisimi changu namna hii (eleza kwa kutumia nini)
Natamani tunapoanza tuanze kwa mlalo huu na baadae tumalize kwa mlalo (love making position) hii,
Natamani uanze kwa kasi au msuguano wa polepole na baadae haraka zaidi namna hii,
Nioneshe kama na wewe unafurahia,n.k

UNAPOFIKA KILELENI
Mwambie mpenzi Napenda upunguze kasi na kuniacha au napenda uongeze kasi unapoona nakaribia kufika kileleni,
Napenda unikumbatie na kunibusu nk

BAADA YA KUMALIZA KUHONDOMOLA..
Mwambie mpenzi Napenda sana uendelee kubaki ndani yangu hadi tulale usingizi nk,
Napenda unikumbatie huku tunalala,
Napenda angalau mkono wako au mikono yako ibaki mwilini mwangu huku tunalala,
Natamani tuendelee kupiga story,
Natamani uendelee kunibusu.

Kumbuka huu ni mwongozo tu kwani kila mwanamke ana mahitaji yake kutoka kwa mume wake jambo la msingi ni kwamba jisikie huru kuongea na mume wako nini unahitaji kabla, wakati na baada ya sex.
Usisubiri eti utafaidi sana sex baada ya kumaliza kusomesha watoto au hadi mfanikiwe maisha au hadi umalize miradi Unayofanya kwani itafika Mahali utakuwa na pesa na muda ila nguvu huna,

NI NINI MAANA YA KUFIKA KILELENI..na JINSI YA KUFIKA..

Katika ndoa sex ni kitu kizuri kinachowafanya wanandoa kuwa mwili mmoja kwa maana ya kuwaleta karibu.
Jambo kubwa ambalo huleta raha ya kiwango cha juu kwa wanandoa wakati wa tendo la ndoa ni suala la kufika kileleni (orgasm)
Kila mwanandoa anaweza kufika kileleni Ingawa si kila mmoja, kufika kileleni kwa wengine si issue rahisi hasa kwa wanawake Ingawa kwa wanaume ni kitu rahisi hata kitendo cha mwanaume kuwa na penetration na kuingia kwa mke wake basi anaweza kujikuta anafika kileleni, Ingawa hilo haliwezi kumfanya mwanamke kufika kileleni.
Kufika kileleni ni nini?
Ni kitendo cha kufikishwa juu kabisa katika raha ya sex, msukumo wa kiwango cha juu wa raha ya tendo la ndoa ambalo huishia kumwacha muhusika ajisikie yupo relaxed na mwepesi. Kwa mwanamke kufika kileleni huwa kwa sekunde kadhaa ambazo huendana na kujisikia relaxed na msukumo wa kutamani kama kunyanyuka ili kupokea kitu au kutoa hata hivyo kama mwanamke ataendelea kusisimuliwa huweza kujikuta anafika kileleni tena Ingawa hii ni kwa wanawake wa umri fulani.

JE,KUNA AINA NGAPI ZA KUFIKA KILELENI KWA MWANAMKE?

Kimsingi kuna aina mbili za mwanamke kufika kileleni na hizi aina zinajikita kutokana na aina ya msisimko anaoupata (stimulation).

Kwanza ni kifika kileleni kwa njia ya kusisimuliwa kisimi chake (clitoral)

kwa mwanaume kukisisimua kwa kuchezea kwa njia Tofauti anazozijua au wanazoelekezana wakati wa tendo la ndoa.


Pili ni kufika kileleni kwa njia ya uke (vaginal).

hii mara nyingi hutokea kutokana na mwanaume kuingia na kutoka kwa mawimbi huku akigusa eneo la G-Spot
Uzuri ni kila aina ya kufika kileleni ina ladha yake na wanawake wenye uzoefu wa hizi aina wanafahamu Tofauti yake.
Ni wanawake wachache sana hufika kileleni kwa kitendo cha Uume kuwa ndani ya uke hata hivyo ni rahisi mwanamke kufika kileleni kwa kuchezewa kisimi/kinembe chake kwa namna zote (touching/rubbing or kissing)


Je, ni milalo ipi husaidia mwanamke kufika haraka kileleni?

Kwanza ni ule wa mwanamke kuwa juu ya mwanaume na pile ule wa mwanamke kulala kwa tumbo lake na mwanaume kumuingia kwa nyuma.

Je ni mambo gani yanaweza kuathiri mwanamke kufika kileleni?


1: Mara ngapi mwanamke anapata sex, ili mwanamke kufika kileleni anahitaji kuwa na sex ya mara kwa mara (use it or loss it). Mwanamke anapokaa kwa muda mrefu bila sex ndivyo anakuwa mgumu kusisimka na mgumu kufika kileleni period.


2: Lazima mwanamke awe relaxed na hana stress au tension. Ili mwanamke apate raha ya mapenzi ni lazima awe comfortable na mazingira yaliyopo na pia mahusiano au ndoa yake bila trust na mwenzi wake mwili unajifunga na ngumu kufungua.


3: Hii inamuhusu mwanaume ambaye anahusika na huyu mwanamke anayetakiwa afike kileleni Kwani anatakiwa kuwa caring na anayefahamu kumsisimua mwanamke asisimke kiasi cha kutosha na kumsaidia kufika kileleni kwa kusoma upepo unavyovuma.
Pia ni vizuri kwa mwanamke mwenyewe kujitambua na kufahamu mwili wake vizuri na zaidi kushirikiana na mume wake kuwa wazi kumweleza kile anaona kinampa raha na kitapelekea kufika kileleni.

Friday 15 May 2015

USIFANYE HAYA UNAPOKUWA FARAGHA NA MWENZI WAKO.

Unapokuwa kitandani na mpenzi wako kitu ambacho hupendi kitokee ni kumfanya ajisikie vibaya na kukosa hamu ya kuendelea na raha ya kufanya mapenzi.  Hata hivyo kuna watu si wastaarabu au ujinga tu hufanya mambo yafuatayo kwa makosa. 
Ni muhimu ukayafahamu na kutofanya ili mpenzi wako afurahie huo muda wa faragha yenu.

KUTOKUBUSU:
Amini usiamini wapo ambao hufanya mapenzi bila kubusiana (iwe katika maandalizi au wakati wa tendo lenyewe).
Unashauriwa kumbusu mpenzi wako na kama hujui namna ya kubusu ni vizuri kufundishana kwani mapenzi ni sanaa na kujifunza ni jambo la msingi

KUPIGA KABLA YA KUSISIMKA
Wapo watu ambao hupenda vionjo vya ajabu kama vile kufinya, kupiga kofi iwe mashavuni au matakoni, kumkaba kooni nk hata hivyo hivi vitu vinafanywa kabla ya muziki kukolea au kusisimka huwa ni usumbufu kwa anayefanyiwa kwani kwa kuwa mwili haujasisimka huwa anapata maumivu badala ya raha hakikisha mpenzi wako ammesisimka na yupo katika ulimwengu wa raha ya mapenzi ndipo umuume hilo sikio au shingo au bega nk.

KUACHA SEHEMU ZINGINE
Wapo watu hasa wanaume, anapomuandaa mpenzi wake anachojua ni matiti na bondeni kujua  kama kumelowa then kumuingiza mr happy wake na kumaliza kazi. Jambo la msingi ni kwamba mwili wote wa mwanamke ni kiungo cha mapenzi. Kuanzia nywele kichwani hadi kucha na unyayo mguuni huhitaji kusisimuliwa na utaratibu wa kweli matiti na uke ni vitu vya mwisho katika safari ya kumuandaa

UZITO WAKO
Wapo watu wamebarikiwa uzito na linapokuja suala la kufanya mapenzi sijui makusudi au mazoea huamua kuegesha uzito wao kwa mpenzi wake.
Please, fahamu kwamba unapo kuwa juu yake kama wewe ni mzito uwe mwangalifu unaweza kumfanya akakosa hata hewa au akapunguza uwezo wake wa kupumua na ukaharibu good time yafaragha

KUMALIZA HARAKA AU KUCHELEWA MNO
Hii inahusu sana wanaume
Mwanaume unahitaji kujizuia ili umalize katika wakati mwafaka sawa na uhitaji wakuridhishwa kwa mpenzi wako ukimaliza haraka utamwacha bibie hajaridhika, na kuchelewa sana bibie atajikuta amebebeshwa chuma.
Kuepukana na hili ni muhimu mwaume kutumia mda mwingi katika maandalizi (foreplay) hii itawasaidia wote wawili kujisikia raha

KUTOKUSEMA UNAKALIBIA KILELENI
Kutomwambia mpenzi wako kwamba unakaribia kileleni siyo ustaarabu ni vizuri kumwambia ili ajue mpenzi wako anastahili kufahamu kwamba unakaribia kufika kileleni

KUKAA KIMYA
Je, unapenda kusikia mpenzi wako anapata kitu kizuri toka kwako?
Kama unapenda basi naye anapenda mwambie kama anafurahia sio lazima iwe maneno bali hata kelele za kimahaba, hiyo itamtia moyo  na kuelimika zaidi katka suala la kelele za mahaba

Thursday 7 May 2015

CHUKI KWA MPENZI WAKO WA ZAMANI HAINA FAIDA..UNAPOTEZA MUDA..

MAPENZI yana siri kubwa. Kila mmoja ana ugonjwa wake wa kupenda. Wengine wanawapenda wapenzi warefu, lakini kuna kundi ambalo huchanganyikiwa zaidi kwa wafupi. Pamoja na mchanganuo huo, kuachwa inauma hata kama anayekutosa hukuwa na mapenzi naye.

Ile dhana tu ya kuachwa ndiyo hutesa watu. Kuna dhana kwamba anayeacha mara nyingi hujiona mshindi dhidi ya aliyemuacha. Na hiyo ndiyo sababu ya wengi kuumia wanapofungiwa milango ya kukatisha uhusiano ambao pengine hata hawakuwa na maslahi nao.

Watu wanaingia kwenye mapenzi na baadaye wanatengana. Wapo wanaobaki na amani, lakini wengine wanaendelea kuishi katikati ya chuki.
Husalimiani na mwenzi wako wa zamani, mbaya zaidi pengine huyo uliye na uhasama (bifu) naye, mmefanikiwa kupata mtoto pamoja. Usiangalie moyo wako, zingatia ukuaji wa mwanao.

Hapa nifafanue kitu kimoja kwamba sifundishi watu kuwakaribia wenzi wao wa zamani, la hasha! Nashauri kutowekeana uadui kwa sababu hauna maana.
Mtaalamu mmoja wa saikolojia ameandika: “Moja kati ya njia rahisi ya kupoteza muda wako ni kumchukia mwenzi wako wa zamani.” Binafsi nakubali, kwa nini ujenge bifu na mtu aliye nje ya mzunguko wako wa maisha?

Naweza kuelewa kwamba kumchukia mtu ambaye hayupo tena kwenye mzunguko wa maisha yako, ni kama hatua ya kujipa maumivu ya moyo au huzuni isiyo na sababu.
Ukimchukia mwenzi wako wa zamani, maana yake unaendelea kumhifadhi kwenye moyo wako. Aghalabu utakumbuka mabaya yake lakini kuna vipindi vichache ambavyo mazuri yake yatakujia.

Endapo kuna mambo yake mazuri yatakuja kwenye ubongo wako, yatakutesa. Utakumbuka namna alivyokujenga kimahaba, si ajabu utamkumbuka tena na kuanza kuhisi kumkosa.
Njia rahisi ni kuhakikisha moyo wako unakuwa mweupe. Unaachana na kumbukumbu zote. Funga ukurasa wa zamani na ufungue mpya. Maisha yaendelee, Siku Hazigandi, wazungu wanasema life goes on.

Hatari kubwa katika chuki yako kwa mwenzi wako ni kuendelea kujipa maumivu ambayo si ajabu yatakuja kukusababishia ujione wewe bila yeye ni sawa na kukabiliana na kifo.
Kinyume cha mapenzi siyo chuki. Ni kutojali (kupotezea). Yaani unapokosana na mwenzi wako, usianze bifu, badala yake anza kumpotezea na usimjali kwa chochote.

Tafsiri nzuri ya kumchukia mwenzi wako wa zamani maana yake bado unampenda na bado unahitaji kuendelea naye.
Watu wengi wanatangaza kuachana na wenzi wao lakini wanaendelea kudumisha ukaribu bila sababu za msingi, ingawa kuna uwezekano mkubwa mioyo yao ndiyo inayowatuma.

Kwa taarifa ni kwamba kitendo cha kuendelea kuwa karibu na mwenzi wako wa zamani, maana yake unakaribisha fursa ya wewe na yeye ya ama kukumbushia au kurejea upya kwenye mapenzi.
Tafsiri nyingine ni kwamba ile chuki ambayo wewe unakuwa nayo inatokana na ukweli kwamba unahitaji aje kwako lakini unaona wazi kuwa hana mpango nawe hata kidogo.

Ukweli ni kwamba wewe mwenyewe utajiona umebeba mzigo wa usumbufu kumchukia mpenzi wako wa zamani ambaye huna ukaribu naye.
Kwa mwanamke, nafasi kubwa kwake katika maisha yake, mara mnapoachana, atatengana na wewe kwa sababu maalumu. Ukionesha nia ya kuendelea naye, atarejea kwako kwa ari zaidi.

Unatakiwa kwenda mbele kukabiliana na matukio mapya ikiwa unaumizwa na machungu ya kuachana na mwenzi wako.