Friday 15 May 2015

USIFANYE HAYA UNAPOKUWA FARAGHA NA MWENZI WAKO.

Unapokuwa kitandani na mpenzi wako kitu ambacho hupendi kitokee ni kumfanya ajisikie vibaya na kukosa hamu ya kuendelea na raha ya kufanya mapenzi.  Hata hivyo kuna watu si wastaarabu au ujinga tu hufanya mambo yafuatayo kwa makosa. 
Ni muhimu ukayafahamu na kutofanya ili mpenzi wako afurahie huo muda wa faragha yenu.

KUTOKUBUSU:
Amini usiamini wapo ambao hufanya mapenzi bila kubusiana (iwe katika maandalizi au wakati wa tendo lenyewe).
Unashauriwa kumbusu mpenzi wako na kama hujui namna ya kubusu ni vizuri kufundishana kwani mapenzi ni sanaa na kujifunza ni jambo la msingi

KUPIGA KABLA YA KUSISIMKA
Wapo watu ambao hupenda vionjo vya ajabu kama vile kufinya, kupiga kofi iwe mashavuni au matakoni, kumkaba kooni nk hata hivyo hivi vitu vinafanywa kabla ya muziki kukolea au kusisimka huwa ni usumbufu kwa anayefanyiwa kwani kwa kuwa mwili haujasisimka huwa anapata maumivu badala ya raha hakikisha mpenzi wako ammesisimka na yupo katika ulimwengu wa raha ya mapenzi ndipo umuume hilo sikio au shingo au bega nk.

KUACHA SEHEMU ZINGINE
Wapo watu hasa wanaume, anapomuandaa mpenzi wake anachojua ni matiti na bondeni kujua  kama kumelowa then kumuingiza mr happy wake na kumaliza kazi. Jambo la msingi ni kwamba mwili wote wa mwanamke ni kiungo cha mapenzi. Kuanzia nywele kichwani hadi kucha na unyayo mguuni huhitaji kusisimuliwa na utaratibu wa kweli matiti na uke ni vitu vya mwisho katika safari ya kumuandaa

UZITO WAKO
Wapo watu wamebarikiwa uzito na linapokuja suala la kufanya mapenzi sijui makusudi au mazoea huamua kuegesha uzito wao kwa mpenzi wake.
Please, fahamu kwamba unapo kuwa juu yake kama wewe ni mzito uwe mwangalifu unaweza kumfanya akakosa hata hewa au akapunguza uwezo wake wa kupumua na ukaharibu good time yafaragha

KUMALIZA HARAKA AU KUCHELEWA MNO
Hii inahusu sana wanaume
Mwanaume unahitaji kujizuia ili umalize katika wakati mwafaka sawa na uhitaji wakuridhishwa kwa mpenzi wako ukimaliza haraka utamwacha bibie hajaridhika, na kuchelewa sana bibie atajikuta amebebeshwa chuma.
Kuepukana na hili ni muhimu mwaume kutumia mda mwingi katika maandalizi (foreplay) hii itawasaidia wote wawili kujisikia raha

KUTOKUSEMA UNAKALIBIA KILELENI
Kutomwambia mpenzi wako kwamba unakaribia kileleni siyo ustaarabu ni vizuri kumwambia ili ajue mpenzi wako anastahili kufahamu kwamba unakaribia kufika kileleni

KUKAA KIMYA
Je, unapenda kusikia mpenzi wako anapata kitu kizuri toka kwako?
Kama unapenda basi naye anapenda mwambie kama anafurahia sio lazima iwe maneno bali hata kelele za kimahaba, hiyo itamtia moyo  na kuelimika zaidi katka suala la kelele za mahaba

No comments:

Post a Comment