Saturday 30 July 2016

TUWE MAKINI NA KAULI ZETU.


Katika maisha haya tunayoishi, wapo watu wenye tabia ya kutishia wenzao baada ya mizozo mbalimbali.
Yupo anayemtishia mwenzake eti asipoangalia atamuua, mwingine anamtishia kumnyima kitu fulani iwe fedha, chakula na kadhalika.
Kwa wengine matishio wanayotoa ni hasira tu wala hayamaanishi maamuzi ya kweli.
Kwa maneno ya mitaani huwa wanasema ``anamtishia nyau.
Huku wengine wakichukulia matishio mengine ni utani, hebu sikia kisanga hiki ambapo familia imejikuta ikisambaratika kisa mume kamtishia nyau mkewe kwamba atamuacha kama hakuwa makini.
Kisa hiki kanisimulia mama mwenyewe yaliyomkuta ambapo sasa anaishi na mume mwingine na tayari wamezaa mtoto mmoja.
Baba huyu (mume wa pili wa mama huyu), ni mume wa mtu mwenye familia yake inayoishi hapa hapa jijini.
Naam, ilikuwaje? Kwa mujibu wa simulizi ya mama huyu, aliwahi kuolewa na mwanaume mmoja wakazaa watoto wawili, msichana na mvulana. Mama akiwa anakaa nyumbani, huku mume akihangaika na biashara.
Mara kwa mara mume huyu akiwa anamwambia mkewe kuwa iko siku atamwacha.
Tishio hili, kwa mujibu wa mkewe lilikuwa linamkera sana. (hata hivyo binafsi siamini bwana yule alikuwa anasema vile bila sababu.
Lipo jambo ambalo mke huyu alinificha).
Naam. Baada ya mke kutafakari kwa muda, eti akaamua kutafuta chumba sehemu nyingine kwa siri bila mumewe kujua.
Baada ya kukipata, akatafuta mzozo ili apate mwanya wa kuondokea. Huku na huko akamvizia mume akiwa anakula na kumuuliza; hivi hilo tishio kwamba iko siku utaniacha lina maana gani? Mume akahamaki na kusema; unadhani utani? Nitakuacha kweli, wanawake mbona tele, hujui mke mmoja anakinaisha? Maneno hayo kwa mujibu wa mama huyu yalimchefua kweli kweli. Lilizuka zogo la kishoka ambapo (mama aliamua kwenda kulala. Asubuhi mume akaenda kazini kwake hadi jioni.
Huku nyuma mama akafungasha vitu vyake akavipeleka kwenye makao yake mapya, kisha kurejea ili amsubiri mume amuage. Ilikuwa ni kichekesho kitupu.
Bwana kurejea nyumbani alimkuta mke akiwa sebuleni huku kashika tama (mkono shavuni). Mume kuuliza kulikoni ``nilimjibu nimesubiri nikuage, si umekuwa ukiniambia iko siku utaniacha? Sasa hivi naondoka, siwezi kuvumilia kuachwa heri nikuache wewe mapema, watoto wako nakuachia pia japo huyu wa pili ni mdogo, kwa heri ya kuonana? Mpenzi msomaji, hivi ndivyo mama huyu alivyoondoka kwa mumewe kama alivyonisimulia mwenyewe.
Bwana yule hakuamini macho wala masikio yake akabakia ameduwaa asijue la kusema.
Pengine alikuwa akijutia kauli yake ya kumwacha mkewe siku moja. Kwa mujibu wa mama huyu kule makao mapya akatafuta sehemu ya kupikia vyakula (mamantilie) akafanikiwa na ndipo akampata mzee mmoja aliyekuwa mteja wake na katika mazungumzo ya mara kwa mara wakawa wapenzi na sasa mzee huyu amempangishia chumba eneo jirani na anakofanya kazi. Na siku mama huyu ananisimulia kisa hiki walikuwa wote na mzee pamoja na mtoto wao.nilipotaka kujua mume wa awali wa mama huyu yuko wapi niliambiwa tayari alishafariki. Pia mmoja wa watoto (yule mdogo) naye aliugua akafariki ambapo yule mkubwa ameolewa na ameshazaa.
Mwanamama huyu anasema amejaribu kumsaka bintiye huyo bila mafanikio. Yasemekana baba yake kabla ya kuaga dunia aliagiza kuwa mtoto huyo asipewe mamake kutokana na ukatili aliomfanyia wa kumuacha huku bado alikuwa anampenda kwa dhati. Hakika, Maisha Ndivyo yalivyo.
Jamaa alifikiri anatishia nyau kumbe yakawa ni kweli. Kisa hiki kinatukumbusha kuwa makini na kauli tunazotoa midomoni mwetu kwani zingine ni mauti kwetu.
Hata hivyo yawezekana mama na baba wa familia niliyogusia hapo juu, wote walikuwa na matatizo Fulani ambayo hayakuwa dhahiri.
Mume kumtishia kumwacha lazima lipo jambo alilokuwa akifanya mkewe lisilompendeza.
Na mke huyu pengine naye alishamchoka mumewe hivyo kutafuta sababu za kutengana au kuachana.
Huwezi kujua. Nyumba za watu zimeficha mengi.
Utaona baba na mama wakicheka pale wanapokuwa na wageni sebuleni, lakini wakiondoka huo moto unaowaka humo ndani ni balaa tupu. Wengine hawalali chumba kimoja au kitanda kimoja. Wengine tokea wanaingia garini kwenda kazini hadi wanafika hawaongei, hawacheki.
Maisha gani hayo?
Tumrudie Mungu abariki nyumba zetu.
Kwani amri kuu aliyotuachia `upendo tupendane`, tumeiweka kando. Turejeshe upendo ili amani na utulivu vitawale maisha yetu.

Niwatakie Jumapili njema.

JINSI YA KUIJENGA NDOA YAKO.


Kujenga ndoa kuna fanana sana na kujenga jengo lolote kama nyumba tunazoishi.
Kwanza unaanza kwa kuwa na michoro mizuri (plan) na hatimaye unajenga jengo lenyewe.
Ndoa ni mahusiano ya juu sana kwa binadamu ni maamuzi ya ku-share moyo, akili, mwili; vyote kwa pamoja.

Katika kujenga jengo lolote suala la vifaa haliwezi kukwepeka kwani ndivyo husaidia jengo kusimama na ndoa ni hivyo hivyo kuna tools ambazo lazima utumie katika kujenga ndoa imara.

Kabla ya kununua hizo tools za kutumia kujenga ndoa kumbuka kwamba wewe na mwenzi wako wote mpo timu moja na lengo si kushindana kwani hatuhitaji mshindi bali tunahitaji kufanya kazi kama timu.
Ndoa si nani anashinda bali ni wanandoa wote kuelekeza nguvu kusukuma au kuvuta kama kuelekea upande mmoja.
Katika ndoa si lazima ushinde kila mgogoro unapojitokeza na wewe kuwa sahihi kuliko mwenzio bali ni kusaidiana na kumtanguliza mwenzako.

Kifaa cha kwanza ni:-

1. KUWASILIANA.
Ni muhimu kuwa na mwasiliana ya pamoja kila siku. Tunapozungumzia mawasiliano tunaenda katika nyanja zote zinazomuhusu mtu pamoja na kuhusisha milango yote mitano ya fahamu yaanu kuguswa, kunuswa, kusikia, kuonana na kuonja hahaha!
Hapa ni mawasiliano ya kihisia, kiakili, kimwili na kiroho

Kihisia- jitahidi kutiana moyo kati yenu na pia fahamu kwamba katika kuwasiliana ni asilimia 7 tu ni maneno asilimia 93 ni jinsi ya tone ya sauti yako na body language. Jinsi unavyoonekana wakati mwenzako anaongea na sauti yako unavyojibu huwasilisha hisia zako kwa mwenzi wako hivyo uwe makini kuhakikisha humuumizi. Watu wanapanda gari wote kwenda kazini na hawaongei hadi wanafika na hata wakiongea majibu ni mkato tu, kihisia hapo kuna jambo.

Kiakili: -je, kuna gazeti umesoma na kuna kitu kimekufurahisha nawe wataka mwenzi wako ajue?
Mweleze basi. Je, una story yoyote unataka kumsimulia mkeo au mumeo msimulie basi.

Kimwili: -mpe miguso mingi tu ambayo si ile ya chumbani wakati unataka ile kitu. Mkumbatie, mbusu, mshike mkono, unampompa mguso (touch) maana yake unamjali na touch ni hitaji la msingi la binadamu. Kama mnaweza oga pamoja it is so fun and so nice.

Kiroho:- kuna wanandoa wengi husahau kushirikiana katika mambo ya kiroho hata kama wapo imani moja. Unahitaji kumuombea mwenzi wako, na pia unahitaji kuomba pamoja kama wanandoa hii husaidia kuinua mahusiano yenu. Imba pamoja nyimbo za kumsifu Mungu. Soma Neno kwa pamoja na kila mmmoja kushiriki kutafakari.

2. KUBARIKI
Mbariki mwenzi wako kila iitwapo leo.
Anza leo kutoa maneno ya baraka kwa mume wako au mke wako hata kama hukuzaliwa familia ambayo imekuridhisha kumbariki mwenzako.
Mpe sifa anazostahili kwa mambo mazuri anafanya, inawezekana anafanya kazi kwa juhudi, anapika vizuri, anakutunza vizuri, anakupenda, anakuridhisha kitandani, mwambie “asante, nakupenda, pole sana, ubarikiwe, unapendeza nk.
Hata kama wewe ni mgumu mno kutoa neno la baraka basi anza leo kwa neno lolote dogo unaloona mwenzi wako amekufanyia.

3. KUSHIRIKIANA.
Shirikiana mambo mengi katika maisha kwa kadri mnavyoweza.
Kuwa pamoja katika muda, mawazo, kucheza, kutazama TV program pamoja, kikombe cha kahawa au chai pamoja, kusafisha nyumba pamoja, kuendesha baiskeli pamoja., kula chakula sehemu pamoja, kufanya vitu mmoja anapenda pamoja nk.
Mnapotumia muda pamoja husaidia kuwaunganisha zaidi na kuwa kitu kimoja.

Kifaa cha nne ni:-

4.KUITIKIA BILA KULAUMU KWANZA.
Usibishe, itikia kwa kukubali kwanza. Jinsi unavyoitikia kuna elezea zaidi kuliko vitendo wakati mwingine.
Je, kama mume wako au mke wako amechelewa kurudi nyumbani, na hajapiga simu, huwa una respond vipi. Kitu cha msingi si kurukia na kuanza kulaumu bali kwanza kumsikiliza na kujua sababu ni ipi kuliko kulalamika na kuanzisha moto au zogo la nguvu.

"Ndoa haijengwi wa vitu tunavyonunua dukani tu, bali hujengwa kwa upendo kwanza"

Friday 29 July 2016

UWEZO WA UUME UBADILIKA.


Hakuna ubishi kwamba utendaji kimapenzi kwa mwanaume hupungua kufuatana umri unavyoongezeka.

Umri unavyoongezeaka hata kiwango cha homoni za testosterone hupungua na jinsi kiwango cha homoni kinavyopungua mwanaume huchukua muda mrefu kuweza kusisimka na baada ya kusisimka hutumia muda mrefu kusimamisha au kudindisha na si hivyo tu bali hutumia muda mrefu kufika kileleni na kubwa kuliko yote ni kwamba akisha fika kileleni huchukua muda mrefu zaidi kusimamisha tena ili kufika kileleni kwa mara nyingine.
Pia umri huweza kupunguza kiwango cha mbegu anazotoa pamoja na ubora wake.

Pia mwanaume anapozeeka huweza kupunguza uwezo wa utendaji wa kibofu chake cha mkojo, tafiti zinaonesha kwamba mrija wa mkojo huwa dhaifu kadri mwanaume anavyoongezeka umri pia misuli ya kibofu hupunguza uwezo.

Kubwa kuliko zote ni suala la mabadiliko ya uume kadri miaka inavyongezeka na kawaida huwa na mabadiiko makubwa mawili.

Mwonekano (Appearance)

Kichwa cha Uume hubadilika rangi yake kutokana na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenda huko chini.

Pia nywele (pubic hair) huweza kuanza kupotea hii ni kutokana na homoni ya testosterone kupungua.
Kwa hiyo ukifika umri huo usishangae kuwa na massive deforestation au kuota kipara ukaanza kutafuta mchawi nani.

Kimo (size)
Kuongezeka uzito au kujazia eneo la kiuno au chini ya tumbo ni jambo la kawaida kwa mwanaume anapoongezeka umri kwa sababu mafuta hujaa maeneo ya chini ya tumbo (abdomen).
Kadri fat inavyojaa maeneo ya tumbo kwenda chini husabaisha shaft ya uume kujaza fat ambako husababisha urefu wa Uume kupungua.

Pia mwanaume mwenye kitambi (obesity) huweza kuuzika uume wake kwa fat inayokuwa deposited kwenye tumbo lake na anaweza kuongeza urefu wa uume hadi inch moja kama ataamua kupunguza uzito.

Kwa ufupi ni kwamba kama mwanaume mwenye miaka 30 huweza kusimamisha uume wake na kuwa na urefu wa inches 6 basi akifikisha miaka 60 au 70 uume wake unaweza kupungua na kuwa na urefu wa inches 5 ikisimama.

Thursday 28 July 2016

MPE MKEO KILE ANAKIHITAJI.


Kila mwanamke ana sehemu ambazo husisimka zaidi na kupelekea kunyegeka na kuwa na hamu na kutana tendo la ndoa, mwanaume Unahitaji kujua ni sehemu ipi mke wako husisimka zaidi ukizingatia kwamba kila mwanamke ana sehemu yake. Mwanamke mwingine akiguswa viganja vya mikono tu chini analowa kabisa, na mwingine ukigusa matiti mtakosana maana unamuumiza. Mwanaume mtundu katika mapenzi hujua mke wake anasisimka na kuwa hoi akichezewa wapi.
Ukishafahamu ni sehemu ipi na inafanywa vipi ili asisimke basi huna budi kutumia muda wako wa foreplay kumpa bibie tamutamu yake hadi aridhike kwamba ana mwanaume anayemjali na si kurukia tu kule chini na kuanza kuchimba dhahabu bila hata kujua mgodi wenyewe upoje.

UBUNIFU
Wanawake wengi katika ndoa na mahusiano hulalamika sana hasa kutokana na kukosa msisimko wa mapenzi wakati wa faragha. Wanalalamika kwa kuwa wanaume kila siku hutoa kitu kilekile, anakubusu, anakugusa kidogo na akiona chini kumelowa tayari anachomeka kama anapigilia misumari na ikiingia tu anapigilia akiona tayari huyo amemaliza na kuondoka zake.
Wanawake wanapenda surprise na kusisimuliwa katika njia mpya, mwanamke anahitaji kitu kipya baada ya muda, anahitaji sex position mpya, anahitaji busu jipya, anahitaji kunyonywa kupya na anahitaji kusikia neno jipya kwenye masikio yake.
Ni juu yako wewe mwanaume kujifunza mbinu mpya na kuwa mbunifu kitandani, wanaume ndivyo tulivyo tunahitaji kuwa wabunifu, fanya kitu kipya ambacho kitamfanya mwanamke ajisikie ana mwanaume ambaye anazijali na kuzijua hisia zake na hatimaye ndoa itakuwa ni yenye amani sana.

NI MUHIMU KWENU MLIOOLEWA.


Ni vizuri kama mwanamke kufahamu kuwa "Uume"

Mara zote upo tayari, Uume huwa haufuati ratiba (schedule), ukweli Uume haujui hata ratiba ni kitu gani na hufanywa vipi pia Uumr una kumbukumbu ndogo sana.

MFANO:
Wewe na mume wako mlikuwa na wakati mzuri sana usiku wa jana (love making) na kila mmoja aliridhika na kujiona ametosheka. Asubuhi wewe mwanamke unaamka mapema na kuamua kufanya usafi chumbani huku mumeo bado amelala. Unaamua kuvaa tu T-shirt bila bra ndani na katika inama matiti yanaonekana kuchezacheza ndani ya T-shirt uliyovaa kiasi cha kumvutia mumeo ambaye anaamua kuamka na kuja kukupa hug kwa nyuma na unagundua bila shaka kwamba Uume wake umeshaanza kutroti na hauoneshi dalili kwamba umelala.
Unajiuliza
“Tulifanya sex jana usiku tu, sijaoga bado, nimevaa ovyo, hivi mume wangu ana tatizo gani kunitaka tena asubuhi hii yote wakati anafahamu ninafanya kazi?”
Ukiongea na wanandoa ambao huridhishana watakwambia kuna kitu kinaitwa ‘spontaneity or quickies, chapuchapu, kimoja cha haraka nk”
Kwa kuwa mwanaume huvutiwa na kile anaona, ile kumuona mke wake na headlights, au katika chupi yake au akitoka kuoga na khanga yake kwa tukio kama hilo mume anaweza asijali atachelewa kanisani au kazini au mkutanoni kwani anakuwa ameshaigusa trigger na kwake kinachofuata ni kutoa risasi.
Wapo wanawake ambao wameamua kuwapa waume zao sex wiki mfululizo wakiamini kwamba itasaidia kuwafanya waume zao kupunguza uhitaji wa sex hata hivyo wiki inayofuata mume anakuwa na nyege ya juu kuliko wiki iliyopita.
Hawajajua "Mr.Uume" yeye hana tatizo kwani huwa hatunzi kumbukumbu za nini kilitokea jana au wiki iliyopita anachojua yeye ni sasa na anatunza smile lake kila iitwapo leo.
Mwanaume ni mwanaume na atabaki mwanaume na moja ya sifa ya mume ndani ya ndoa ni ule uhitaji wa sex kwa namna ya tofauti.
Kama ulihitaji mtu ambaye atafanya mambo kama unavyohitaji wewe kimapenzi basi ulitakiwa kubaki single, lakini umeoana na mwanaume ambaye ana mahitaji tofauti na wewe na moja ya mahitaji muhimu kwake ni sex.
Pia ieleweke kwamba kuna siku mume anaweza kuamka akiwa na full erections, anaweza kuku-approach na wewe ukakataa, hata hivyo kukataa kwako hakuwezi kupunguza hamu yake ya kukuhitaji wewe kimwili.
Kuna wakati hitaji la sex kwa mwanaume huwa mfano wa kitu cha urgent, anahitaji sexual release, kama ni bunduki yake basi huwa inakuwa ipo loaded na risasi ya mwisho imeshawekwa kwenye chamber, na jicho limeshawekwa kwenye target huku trigger imeshavutwa nyuma ili iweze kuruhusiwa hivyo kukataliwa kwake huwa ni kitu frustrating na hujiona ni loser.

Nikupe Tips za kukuhakikishia wewe mwanamke unakuwa na moto wa mapenzi chumbani.


1.Panga kabajeti kadogo baada ya muda fulani kwa ajili ya kununua kivazi ambacho unaamini ukivaa kinaweza kumvutia mumeo chumbani


2.Angalau kwa mwaka mara moja nenda kwenye social event yoyote na mumeo huku hujavaa chupi, usimwambie mumeo hadi muwe mmeshaondoka nyumbani na mnong’oneze sikioni na mwambie “honey unajua leo sijavaa chupi” utamfanya akuwaze siku nzima huku wewe mwenyewe ukisisimka mara kwa mara ukikumbuka chini ni empty!


3.Baada ya siku kadhaa “have fun” na mumeo chumbani unaweza kuwa naked kwa muda unaotaka wewe kwa ajili ya kufurahia reaction yake inakuwaje.

4.Tafuta aina mpya ya perfume ambayo siku ukijiweka basi ni siku ambayo unakuwa na mahaba ya uhakika na mumeo hivyo basi kila mara ukitaka maana yake unahitaji mahaba pia.

5.Jaribu kitu kipya kimoja baada ya muda fulani kwa ajili ya kumsisimua mume wako.

Wednesday 27 July 2016

KUWA NA UMRI MKUBWA.


Huwezi kugoma kutozeeka, ni muhimu sana kutarajia mabadiliko jifunze kukabiliana na hiyo hali au tarajia mabadiliko kwani mwanamke mwenye umri wa miaka 29 hawezi kuwa sana na mwanamke mwenye miaka 40 na mwanaume mwenye miaka 28 si sawa na mwanaume mwenye miaka 45.
Inawezekana wewe ni mwanaume na umeanza kupoteza nywele kichwani na inawezekana umeanza kujazia uzito wa ziada kwenye tumbo na una kakitambi ka kiana.
Ulizoea kuruka kirahisi sasa ni mzito huwezi kuruka tena, hapo sijakuuliza masuala chumbani na huo uume wako una behave vipi.
Inawezekana wewe ni mwanamke na umri ni kweli unaenda na huamini namna gravitational force inavyokuvuta kila kitu kushuka chini ya sakafu.
Unashangaa matiti yanashuka chini na kulala tofauti na zamani, uso nao unainama na kuweka wrinkles, unashangaa nywele zinakuwa ngumu na kuanza kupotea zenyewe bila taarifa, chini kunagoma kuwa wet hata baada ya kusisimuliwa kama ilivyokuwa kawaida yako kwani kwa maongezi tu kila kitu chini kulijibu.


MABADILIKO YA KIMAPENZI HUWA NI KAWAIDA KWA MWANAUME ANAPOONGEZEKA UMRI.

Kumbuka ulipokuwa teenager (siyo wote) ile kusoma gazeti ambalo ni romantic ulikuwa unasisimka, ile kumpita mwanamke mrembo mwili ulikuwa unasisimka.
Mwanzo wa ndoa yako, ukiona mke wako kapanda kitandani tu ulikuwa unasisimka na kuwa tayari kwa uume wako ulikuwa tayari ushajinyosha na unakugusa ceilings.
Inawezekana kutokana na mwili wako kusisimka kimapenzi haraka kumejenga tabia fulani kwako na kwa mke wako na siku mambo yakiwa tofauti mnaanza kuhaha kudhani kuna tatizo limejitokeza kumbe ni kawaida kwani ni kuongezeka kwa umri.
Inawezekana hata namna ya kuandaana ilikuwa ni one sided kwa maana kwamba mwanaume ndiye alikuwa anasisimuliwa kwa muda mrefu zaidi na mwanamke kwa muda mfupi.
Sasa umri umeongezeka na usipoandaliwa vizuri unaweza kujikuta uume unabaki soft muda wote bila kuleta mabadiliko yoyote kama kawaida yake.
Maana yake mwanaume anapoongezeka umri anahitaji direct penile stimulation kuliko zamani.
Ukweli ni kwamba mwanaume anapokuwa kijana hadi kuwa mzee ni mfano wa godoro jipya, ukilinunua huwa gumu na baada ya miaka kadhaa utaona kasheshe yake.
Pia mwanaume anapoongezeka umri anaweza kushangaa anamaliza sex bila kukojoa (ejaculate) kitu ambacho haikuwa kawaida yake, kwani older men kawaida hawahitaji kufika kileleni kama young men.
Hata hivyo hiyo ina faida kwa mwanamke kwani sasa mwanaume anaweza kufika mbali katika kumridhisha mke wake ndiyo maana umri unavyoongezeka mwanaume huwa mzuri zaidi kimapenzi.
Kama ni mwanamke Kumbuka kwamba si kushindwa kwako kama ukiona mume wako wa 40+ amemaliza nusu saa bila kufika kileleni, wala haina maana kwamba humvutii au hupendeza bali ni kuonesha kwamba mwili wake unazeeka.
Inawezekana ilikuwa kawaida yake akimaliza mara ya kwanza baada ya dakika 2 au 3 anaweza kurudi na kuanza upya kukupa mahaba wewe mke wake na sasa hawezi tena.

Monday 11 July 2016

WANATOFAUTIANA KTK SUALA LA KUFIKA KILELENI.


*Je, kufika kileleni kwa mwanamke anapofanya mapenzi ni tofauti na mwanaume?

Tafiti nyingi zimefanyika na mojawapo ni ile iliyoruhusu Wanawake na wanaume wote kuandika vile wanajisikia wanapofika kileleni na baadae wakaruhusu watu wengine wasome na wapendekeze nani ameandika kati ya mwanamke au mwanaume hata hivyo ilikuwa vigumu kwa wasomaji kufahamu maelezo yaliyoandikwa yameandikwa na mwanaume au mwanamke.
Hii ina maana kufika kileleni kwa mwanaume na mwanamke huhusisha uzoefu unaofanana.
Hata hivyo kuna tofauti ya uzoefu wa kufika kileleni kwa Wanawake na hata mwanamke mmoja na hii tofauti hutokana na aina ya kusisimuliwa ili kufika kileleni kuanzia kisimi, uke, G-spot, matiti n.k

*Je, ni kweli kwamba kinachomfikisha kileleni mwanamke huyu ni tofauti na mwanamke yule?


Ni kweli, na pia hata mwanamke huyo mmoja kinachomfanya asisimuliwe kufika kileleni leo ni tofauti na wiki ijayo na mwezi ujao na hata miaka matano au kumi ijayo.
Wapo wanaopenda kusisimuliwa G-spot na wengine hawataki, wapo wanaopenda kusisimuliwa kisimi wengine hakuna lolote, wapo wanaopenda kusisimuliwa uke na wengine hawataki. Wengine matiti au masikio au shingo nk kila mmoja au hata huyo mmoja uliyenaye anatofautiana kutokana na mzunguko wake wa siku kwa mwezi.
Kama tunavyopenda vyakula tofauti na nguo tofauti na usisimuliwe wapi kwa mwanamke kufika kileleni ni tofauti.
Kuamini kwamba kumsisimua mwanamke Mahali fulani ndipo huweza kumfikisha kileleni bila kuwasiliana naye wakati mwingine huweza kuwa kero.

*Je, mazoezi ya kukaza misuli ya uke huweza kuongeza uwezekano wa mwanamke kufika kileleni kirahisi?

Mazoezi hayo ni muhimu mno. Uwezo na uimara wa misuli ya PC (puboccoccygeus) unahusiana mno na mwanamke kufika au kufurahia tendo la ndoa.
Wanawake ambao hawawezi kufika kileleni kirahisi wana misuli ya PC iliyodhaifu (loose).
Mwanamke anayeweza kufika kileleni kwa kusisimuliwa kisimi ana misuli imara hata hivyo mwenye misuli imara zaidi ni yule anayeweza kufika kileleni kirahisi kwa uke wake.


Wanawake huwa na tofauti za kufika kileleni kutokana na aina ya kusisimuliwa pamoja na sababu zingine kama vile anavyojisikia huo wakati, na kiwango cha homoni.
Si suala la kubonyeza button na mwanamke akafika kileleni. Kufika kileleni si conditioned reflex.
Mara nyingi lengo la mume katika sex ni kuhakikisha mke anafika kileleni je kuna tatizo kuwa na mtazamo kama huo?
Kawaida tunapozungumzia maisha huwezi kukwepa kuweka malengo.
Linapokuja suala la sex ni kweli kwamba wanaume huwa goal-directed na Wanawake huwa pleasure-directed.
Tatizo huja pale watu wameshindwa kufahamu hiyo siri na hasa wanaposhindwa kuwasiliana na wapenzi wao.
Mwanamke anaweza kufika kileleni kwa kusisimuliwa sehemu zingine za mwili kama vile masikio nk hivyo bila kuwasiliana inaweza kuleta shida kwani we are all unique.

FANYA JITIHADA KUIFANYA NDOA YAKO KUWA MPYA.


Baada ya muda katika ndoa kila kitu kinaweza kuwa katika ratiba isiyobadirika, huwa vilevile, routine, predictable, uniform, sare jana juzi, leo na kesho maongezi ni yaleyale, ratiba ya kuwa mwili mmoja ni vilevile hakuna kipya na hakuna raha.

Inawezekana hawa wewe msomaji kile kinachotokea kwenye ndoa yako kinakupa wakati mgumu na unajiuliza hivi nitaishi bila kuridhika kiasi hiki hadi lini.

Hata hivyo kabla hujaanza kumlaumu partner wako ni vizuri ukajiuliza maswali yafuatayo huku ukitafakari kwa undani wewe mwenyewe bila kumnyoshea mwingine kidole

Hivi wakati mnachumbiana (let say dating) ni vitu gani ulikuwa unavifanya ili huyu partner wao aonekane yeye ni special kwako?

Je, hapa karibuni au wiki hii umefanya kitu gani kwa partner wako aonekane yeye ni special?

Je, unakumbuka ni kitu gani na lini mmekuwa pamoja na mmefanya kitu special na mkawa na wakati mzuri nje ya hapo nyumbani mnapoishi?

Je, ni mara ngapi mnakuwa wote kufanya kile kila mmoja anakifurahia kufanya?

Ukiulizwa utaje vitu vitano ambavyo partner wako anavipenda au anaviona vya maana sana katika maisha yake na kujisikia vizuri katika maisha unaweza kutaja? Na je umehusika vipi kuhakikisha anavipata?

Je, mume wako au mke wako yupo namba ngapi kwenye list yako ya vitu vya thamani duniani?
Haya maswali yakipata majibu yake inaweza kuwa njia sahihi kwako kuanza kutengeneza mahusiano yenye direction mpya kuelekea furaha na amani.
Najua mtu yeyote akikuuliza je, unampenda huyo partner wako jibu utakalo toa ni “ndiyo nampenda” hata hivyo ulivyo busy na kazi na watoto na kazi zingine ni dhahiri kwamba humpendi na kama unampenda basi hujaweka efforts zinazotakiwa.
Ni kweli hivyo vitu ni muhimu sana hata hivyo ndoa ni zaidi ya vyote, hata kama umekuwa unasema nitafanya hivyo karibuni hata hivyo karibuni yako sasa ni mwaka hakuna kitu.

Wakati uliokubalika ni sasa, sasa ni wakati wa kuwekeza kiasi cha kutosha kwa partner wako, na utatakiwa kurekebisha ratiba yako ili partner wako aingizwe kiuhakika katika ratiba yako ngumu.

Ukweli ni kwamba hata watoto hufurahia kuwa na wazazi wanaopendana kuliko wao kufurahia kuchezea gitaa linalotoa sauti nzuri au kufunga goli anapopelekwa na mzazi kucheza soka kuliko wazazi ambao hawapendani ndani ya nyumba.

Ndoa yako ni muhimu sana, na mke wako au mume wako ni muhimu sana kumbuka Mungu aliumba ndoa, kabla ya kazi na kabla ya watoto.

Saturday 9 July 2016

NI MWENZI WAKO,KUWA HURU NAE.


Kuongea suala la tendo la ndoa katika ndoa au kwa mume wako au kwa mke wako ni moja ya topic ngumu sana chini ya jua au katika uso wa dunia.
Kama utakuwa na maongezi au mawasiliano kuhusiana na suala la sex katika ndoa yako maana yake mtakuwa wazuri katika hiyo department.
Wanandoa wengi ambao wamekuwa na tabia ya kuongea kuhusu maisha yao ya sex kwa uhuru na ukweli wamekuwa na maisha mazuri chumbani kwao kwani si rahisi kufahamu mwenzako anahitaji kitu gani hadi umwambie.
Kuwa wakimya kuhusiana na kuongea kuhusu sex na mke wako au mume wako husaidia kuwa wajinga zaidi na wakati mwingine kutoridhishana sawa na uhitaji wa mwili wako au feelings zako.
Hatari kubwa zaidi ni pale wanandoa wanaposhindwa kuongea wenyewe na matokeo yake kutoridhika na kutoridhika ndiko husaidia kukwetua njia ya mmoja au wote kuanza kuangalia nje (kuchepuka)
Firikia wewe ni mwanamke una vitu mume wako akifanya basi huwa unajisikia kusisimka na mwili kuanza kutoa kuwa juicy na kutamani sana sex na mume wako.
Kwa nini usiwe huru ukamwambia kwamba unapenda iwe hivi:

Mueleze:-

WAKATI NIMESISIMKA
Natamani mume wangu uwe na wewe unatoa sauti au na wewe uwe unaongea,

Napenda uwe unaongea maneno matamu ya kimapenzi,

Napenda mume wangu uniambie nini unakipenda kwenye mwili wangu,

Napenda unigunise na kunichezea namna hii (onesha),

Napenda ufanye hivi kwenye chuchu na matiti yangu,

Napenda unitazame usoni,

Napenda unichezee kisimi namna hii (mwambie unapenda afanye kwa kutumia nini na namna gani)

Napenda ufanye hivi kwenye G- spot,

Napenda kuchezea uume wako hivi nk

WAKATI WA SEX
Napenda na wewe uwe unaguna na kutoa sauti za kimahaba au uongee maneno matamu na elezea namna unafurahia au unajisikia kuwa ndani yangu,

Napenda uendelee kunibusu namna hii,

Endelea kusisimua kisimi changu namna hii (eleza kwa kutumia nini)

Natamani tunapoanza tuanze kwa mlalo huu na baadae tumalize kwa mlalo (love making position) hii,

Natamani uanze kwa kasi au msuguano wa polepole na baadae haraka zaidi namna hii,

Nioneshe kama na wewe unafurahia,
Nk

UNAPOFIKA KILELENI
Napenda upunguze kasi na kuniacha au napenda uongeze kasi unapoona nakaribia kufika kileleni,

Napenda unikumbatie na kunibusu nk

BAADA YA KUMALIZA SEX
Napenda sana uendelee kubaki ndani yangu hadi tulale usingizi nk,

Napenda unikumbatie huku tunalala,

Napenda angalau mkono wako au mikono yako ibaki mwili mwangu huku tunalala,

Natamani tuendelee kupiga story,

Natamani uendelee kunibusu.
Kumbuka huu ni mwongozo tu kwani kila mwanamke ana mahitaji yake kutoka kwa mume wake jambo la msingi ni kwamba jisikie huru kuongea na mume wako nini unahitaji kabla, wakati na baada ya sex.

Friday 8 July 2016

FANYA HAYA KUMVUTIA MWENZI WAKO.


Wengi huwa wanajiuliza “nifanyeje ili mwenzangu awe na hamu au nimvutie?” ingawa unapenda sana mume wako awe na hamu na wewe jambo la msingi ni wewe kukaa chini kwanza na kujichunguza vile unajiona na kujisikia wewe mwenyewe.
Wewe mwenyewe unajionaje, unajiamini vipi na unavyovutia, unavyopendeza? kwani kama wewe mwenyewe hujioni unavutia basi inakuwa ngumu sana mume wako kuona unavutia.
Mahusiano mazuri kimapenzi na mume wako hayaji tu kwa kuwa mnakaa pamoja bali kwanza wewe mwenyewe unajisikiaje au unajiamini vipi kuhusiana na mwonekano wako.
Hatua inayofuata ni wewe na yeye kuanza kuongea pamoja kuhusiana na suala la mahusiano ya kimapenzi katika ndoa yenu.
Ni kawaida kwa wanandoa kuwa na up na downs zinazohusiana na tendo la ndoa hata hivyo kunapokuwa na ukame wa kimapenzi au ukaribu wa kimapenzi ni muhimu kwa wanandoa wenyewe kukaa chini na kuanza kujadili wapi pamepungua au kitu gani kinakosekana na si kuanza kulaumiana bali kila mmoja kuwa wazi kuelezea na kusema kile anahitaji katika mahusiano ili moto wa mapenzi urudi tena.

Je, kama mwanamke, unahitaji mume kuwa karibu na wewe kwa kukubusu mara kwa mara ua kukukumbatia mara kwa mara?

Je, unahitaji kushikwa mikono au mwili wako na mume wako mara kwa mara?

Je, kuna migogoro nje ya chumbani au kutokuelewana au una hasira kutokana mambo fulani fulani kitu kinachofanya mume wako kuwa mbali na wewe kihisia?
Nk
Ukijiuliza hayo maswali na mengine na kukaa na mume wako kujadili mnaweza kufika Mahali kila mmoja akafahamu nini wajibu wake ili kurudisha moto wa mapenzi chumbani kwenu.
Mawasiliano yaliyo wazi na yanayomruhusu kila mmoja kusema kile anahitaji ndiyo njia sahihi ya kurudisha ukaribu wa kimapenzi upya katika ndoa.
Baada ya kufahamu hatua tatizo lipo wapi weka plan na kuanza kufanyia kazi na hakikisha kila mmoja anakuwa positive kwa mwenzake bila kulaumiana.
SWALI

Ndoa yetu ina miaka 4 na tunafanya tendo la ndoa mara moja kwa miezi mwili. Kila siku usiku mume wangu husema kwamba amechoka na hawezi tendo la ndoa kwa kuwa alikuwa na siku ngumu hata hivyo nafahamu aina ya kazi alikuwa nazo mchana kwa kuwa tunafanya kazi pamoja.
Kinachonishangaza ni kwamba anasisimka sana akimuona mwanamke mtaani hasa kama anavutia.
Ninachojiuliza kwa nini mara zote anasema amechoka kwangu na je nifanyeje ili awe na hamu na avutiwe na mimi?
Mama B