Friday 29 July 2016

UWEZO WA UUME UBADILIKA.


Hakuna ubishi kwamba utendaji kimapenzi kwa mwanaume hupungua kufuatana umri unavyoongezeka.

Umri unavyoongezeaka hata kiwango cha homoni za testosterone hupungua na jinsi kiwango cha homoni kinavyopungua mwanaume huchukua muda mrefu kuweza kusisimka na baada ya kusisimka hutumia muda mrefu kusimamisha au kudindisha na si hivyo tu bali hutumia muda mrefu kufika kileleni na kubwa kuliko yote ni kwamba akisha fika kileleni huchukua muda mrefu zaidi kusimamisha tena ili kufika kileleni kwa mara nyingine.
Pia umri huweza kupunguza kiwango cha mbegu anazotoa pamoja na ubora wake.

Pia mwanaume anapozeeka huweza kupunguza uwezo wa utendaji wa kibofu chake cha mkojo, tafiti zinaonesha kwamba mrija wa mkojo huwa dhaifu kadri mwanaume anavyoongezeka umri pia misuli ya kibofu hupunguza uwezo.

Kubwa kuliko zote ni suala la mabadiliko ya uume kadri miaka inavyongezeka na kawaida huwa na mabadiiko makubwa mawili.

Mwonekano (Appearance)

Kichwa cha Uume hubadilika rangi yake kutokana na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenda huko chini.

Pia nywele (pubic hair) huweza kuanza kupotea hii ni kutokana na homoni ya testosterone kupungua.
Kwa hiyo ukifika umri huo usishangae kuwa na massive deforestation au kuota kipara ukaanza kutafuta mchawi nani.

Kimo (size)
Kuongezeka uzito au kujazia eneo la kiuno au chini ya tumbo ni jambo la kawaida kwa mwanaume anapoongezeka umri kwa sababu mafuta hujaa maeneo ya chini ya tumbo (abdomen).
Kadri fat inavyojaa maeneo ya tumbo kwenda chini husabaisha shaft ya uume kujaza fat ambako husababisha urefu wa Uume kupungua.

Pia mwanaume mwenye kitambi (obesity) huweza kuuzika uume wake kwa fat inayokuwa deposited kwenye tumbo lake na anaweza kuongeza urefu wa uume hadi inch moja kama ataamua kupunguza uzito.

Kwa ufupi ni kwamba kama mwanaume mwenye miaka 30 huweza kusimamisha uume wake na kuwa na urefu wa inches 6 basi akifikisha miaka 60 au 70 uume wake unaweza kupungua na kuwa na urefu wa inches 5 ikisimama.

No comments:

Post a Comment