Wednesday 15 July 2015

MAMBO YA KUEPUKA WAKATI WA MIGOGORO YA NDOA.

Hapo kila mtu kivyake, Kila mtu mbabe, kila mtu anajiona hana kosa, hakuna kuongea, hakuna kugusana hata unywele; Ndoa ina raha yake hata mkosane vipi bado mnalala pamoja, hata hivyo kwa nini msijadili pamoja na kupata jibu then muendelee na kujirusha kama kawaida.

Kila mahusiano ya ndoa hukumbwa na migogoro ya hapa na pale, inaweza kuwa wakati wa raha au wakati wa shida kwa kuwa ni binadamu migogoro huja yenyewe hadi kifo kitakapowatenganisha.
Kitu cha msingi ni kufahamu kwa nini kuna mgogoro au tatizo, na umesababishwa na nini na ni njia ipi itumike kutatua hilo tatizo na zaidi kusameheana kwa pamoja na kusahau.

Tafiti nyingi zinaonesha kwamba mawasiliano mazuri kwenye mahusiano ya ndoa huongeza;
Utamu wa mahaba,
Kuaminiana na
Kusaidiana,
Na mawasiliano ovyo huweza kuharibu kabisa uimara wa ndoa na kujenga kutokuaminiana na zaidi ndoa kwenda ndivyo sivyo.
Kuna mambo ambayo tunapofanya kwenye ndoa huwa tunaona kama vile tunatatua tatizo kumbe ni kinyume chake, hebu angalia wewe ni lipi kati ya yafuatayo umekuwa unayafanya na pia kama unaweza badilisha huo mtazamo au njia ili kuimarisha mahusiano yako na huyo umpendaye.

Moja ya mwanandoa kukwepa tatizo au mgogoro:

Badala ya kujadili tatizo lililopo kuna watu huamua kubaki kimya tu kana kwamba tatizo litayeyuka lenyewe kama barafu.
Na wakati huohuo kutokana na tatizo au mgogoro mtu anakuwa na mawazo kiasi kwamba unajua kuna jambo linamsuta kwenye mawazo na moyo wake.
Hadi tatizo au mgogoro ukue sana ndipo kwa hasira mtu anapasuka.
Kuogopa eti tutabishana sana isiwe sababu ya kuacha tatizo liwe linakaa tu, ni jambo la busara kuelezena ukweli na kulimaliza tatizo na yule ambaye amekosea akubali na mwenzake amusamehe kwani hakuna aliye mkamilifu asilimia mia, bali kwa udhaifu wetu tunasaidiana na kukamilishana hivyo kuwa wazi na kuliezeza tatizo au mgogoro na hatimaye kupata suluhisho ndiyo dawa kamili si kubaki kimya.
Pia wapo wanandoa ambao tatizo likitokea anakataa katakata kabisa kuongea na anaweza kusema hilo tutaongea kesho na kesho anakwambia kesho, then kesho hadi inakuwa mgogoro mzito.

Kujilinda:

Badala ya kufungua moyo na kumuelewa mwenzako wewe unakataa kusababisha tatizo mbaya zaidi unakwepa kwamba kuhusika katika hilo tatizo au mgogoro.
Hapo badala ya kutatua tatizo unaongeza zaidi kwani mwenzio kwanza atajisikia kwamba hujamsikiliza na pia umemdharau kwa kujiona wewe huna kosa.
Matokeo yake tatizo au mgogoro utaendelea kukua na kufukuta.
Kitu cha msingi hata kama unahisi huhusiki basi msikilize mwenzako na jaribu kuangalia umehusika vipi kusababisha mgogoro au tatizo lenyewe kuliko kukimbilia kujilinda kwamba hijahusika.
Wanaume (siyo wote) hapa ndo panatukamata sana huwa tunajiona huwa hatukosei na wakati mwingine hata kosa au tatizo likitokea, sisi tunaona si kosa wala tatizo.
Wanawake ni watu wa hisia zaidi (emotional) na sisi tupo logical.
Inaweza kuwa kwako mwanaume si tatizo ila kwa mwanamke ni tatizo hivyo msikilize na angalia wewe umehusika vipi na zaidi shiriki ili kupata suluhisho na uhakikishe kila mmoja ameridhika.

Kudhani ni kawaida yake:

Kuna wakati tatizo au mgogoro ukitokea, wapo ambao huanza na sentensi kama zifuatazo,
“Kila siku upo hivihivi”
au
"siku zote huwa hunisikilizi”
au
“Hiyo ni kawaida yako”
au
“Nilijua tu utasema hivyo”
Usilete mambo ya nyuma kueleza kwa mwenzio tatizo au mgogoro uliopo, badala ya kutatua tatizo unaliongeza zaidi.
Kitu cha msingi mpe mwenzako nafasi aeleze jambo na pia husiku katika kuangalia chanzo cha tatizo ni nini siyo kurukia na kutoa hitimisho hata bila kujua jambo zima lipoje kisa unakumbukumbu ya makosa yake ya nyuma.
Mwenye kujenga ndoa ni wewe na mwenye kuibomoa ni wewe, usione watu wanadumu na ndoa zao, kitu cha msingi wanakuwa makini kusikiliza na kuhusika katika kutatua matatizo kwa kushirikiana bila kujali matatizo au makosa yaliyopita.

Kujiona mkamilifu
Kwa kuwa wewe ni binadamu hata kama umesoma au upo smart sana kwenye ndoa kuna siku unakosea tu, na pia ukubali kukosolewa na kukubali kukosa ili usamehewe pia.
Wapo wanandoa ambao yeye siku zote yupo sahihi na mwenzake ndo mkosaji.

Kumsoma mwenzako:

Wapo wanandoa hujiona wao wanafahamu na kujua kutafsiri hata mambo ambayo mwenzake anawaza au anafanya.
Au ukifanya kitu anatafsiri anavyojua yeye.
Kwa mfano; ukichelewa nyumbani kurudi, anakwambia humjali au humpendi, Usipimpigia simu anasema humjali au humpendi, au ukikataa tendo la ndoa kwa sababu unajisikia umechoka anasema humjali.
Kitu cha msingi fahamu tatizo au sababu ni nini kwa kuongea na mhusika ndipo utoe maamuzi yako.

Kutokusikiliza:

Kuna wanandoa ambao mwenzake akianza kumueleza tatizo hata kabla hajamaliza anadakia na kuanza kubwabwaja anachojua yeye, badala ya kusikiliza point zilizomo kwenye hicho anaambiwa.
Ni vizuri unapoongea na mke au mume na kama amekuomba aongee na wewe baada ya kuona kuna tatizo ni vizuri kumsikiliza kwa makini kuliko hata unavyomsikiliza bosi wako kazini, kwani usipomsikiliza mke au mume na mgogoro ukawepo hata kazini unaweza kufanya madudu.

Kulaumiana:

Kuna watu ambao style yao ni kwamba tatizo likitokea tu yeye ni kulalamika na kulaumu mwenzake, bila hata kuchunguza vizuri chanzo na kiini cha tatizo.
Hujiona kukiri udhaifu ni kujishusha sana mbele ya mwenzake, kama ni mwanaume atalalamika na kujiosha kwamba yeye hahusiki (ingawa anajua amehusika ila mfume dume) na badala yake kesho anakuletea zawadi ili yaishe, huko siyo kutatua tatizo bali ni ujanja tu.
Tathmini hali ya tatizo kwa pamoja na shirikiana kumaliza tatizo.
Tumia tatizo au mgogoro kama nafasi (stepping stone) ya kuweza kutengeneza ndoa kufikia viwango vya juu zaidi.

Kuonekana mshindi;

Kama kila tatizo likitokea wewe ndo unataka kuonekana upo sahihi na mshindi ujue unadhoofisha mahusiano ya ndoa yako.
Kila mara tunapokutana na matatizo lengo ni kutaka kushirikiana kutatua na zaidi kufikia muafaka huku kila mmoja akimheshimu mwenzake.
Unapong’angania au kulazimisha kwamba mwenzako ndo amekosea hapo unaumiza hisia zake na kuumiza hisia za mpenzi wako ni kitu kibaya sana.

Kumfikiria vibaya mwenzako:

Wapo wanandoa ambao udhaifu wa mwenzake katika jambo fulani anaupa kibandiko (label) cha kudumu.
Kwa mfano, mwanaume ambaye akivua nguo chumbani anaziweka mahali popote; mke wake anafikia uamuzi kwamba huyu ni mzembe na mvivu na anaachana naye kujadili na kumsaidia kuongea naye kuhusu hiyo tabia.
Au mwana mke ambaye kila tatizo likitokea anamuomba mume wajadili; na mume ana chukulia kwamba ni mtu msumbufu sana kila jambo kujadili.
Kitu cha msingi kila binadamu ana tabia imara na dhaifu; hivyo wewe ni mtu pekee ambaye unaweza kumsaidia kuondoa hizo tabia dhaifu kwa upendo na kushirikiana.

DALILI ZA NDOA INAYOELEKEA KUFA.

Jitahidi kuhakikisha unalinda moyo wako na moyo wa mpenzi wako; usije ukaupasua na kuuumiza.

Wanandoa wengi hujikuta wamefika mahali ambapo ndoa haiwezi kuwepo tena (talaka) na tatizo kubwa ni kwamba wengi hukaa bila kuchukua hatua zinazostahili (serious) wakati tatizo au mgogoro unapojitokeza ili kumaliza tatizo
Kutoshughulikia vizuri tatizo lolote kwenye ndoa hupelekea
Chuki,
Uchungu,
Kinyongo,
Kuumia hisia na
huweza kusababisha mwanandoa mmoja kujiondoa katika muungano wa kindoa uliopo
(kuanza kuishi kivyake katika kufikiria na kutenda).

Zifuatazo ni dalili mbaya sana ambazo zinaonesha ndoa inayoelekea kwenye kifo

KUFIKIRIA MAISHA KIVYAKO BILA MKE AU MUME KUMUHUSISHA
Ukiona unaanza kufikiria uzuri wa maisha utakavyokuwa bila mwenzi wako kwa maana kwamba kuwa na yeye unaona asilimia mia moja anakulostisha, au hana maana kabisa ni dalili kwamba hiyo ndoa inaelekea kwenye kifo cha ghafla.
Na kama unasongwa sana na mawazo kutaka kuishi mwenye au na mtu mwingine zaidi ya huyo uliye naye na kujiona utakuwa na amani zaidi basi unaelekea kubaya kwani inaonesha umeshapoteza nafasi yake ndani ya moyo wako na kitu cha msingi waone washauri wa mambo ya ndoa ili waweze kukusaidia.

MAMBO MABAYA NI MENGI KULIKO MAMBO MAZURI KWENYE NDOA YAKO
Kama mnajikuta ndoa yenu ina mambo mabaya mengi zaidi kama vile
kutokuelewana, k
ila mtu ana hasira,
mnapishana lugha kila mara,
hakuna kucheka wala kufurahishana na
mambo mazuri kama kucheka pamoja,
kufurahi pamoja,
kujisikia bila mwenzako siku haiendi
basi hiyo ni dalili kwamba hiyo ndoa inahitaji msaada na bila kuifanyia ukarabati basi itasombwa na mafuriko na hatimaye kufa.

UNAJISIKIA VIGUMU SANA KUWASILIANA NA MKE AU MUME WAKO
Je, unajisikia kupatwa na hofu au mashaka kuongea na mke au mume wako kuhusu matatizo ya ndoa yako au maisha yenu kwa ujumla?
Mawasiliano ndiyo njia pekee ya kuondoa stress za ndoa na maisha kwa ujumla na hatimaye kujenga ndoa yenye afya kwa wanandoa.
Kama mkiwa pamoja mnakuwa kimya bila kuongea chochote na hakuna dalili ya kutaka kuongea na mwenzako basi kuna tatizo kubwa sana, hasa kama ni tofauti sana na kawaida yenu hasa jinsi ilivyokuwa katika siku za kwanza wakati mnachumbiana.
Kama hujisikii vizuri kuwasiliana na mwanandoa mwenzio basi hiyo ni dalili kwamba tayari umekosa imani kwake na ndoa huwa inakuwa katika wakati mgumu kukiwa kauna kuaminiana (trust)
Pia kama wewe ni mtu wa mwisho kujua kitu chochote muhimu au kuzuri kuhusu yeye, basi hapo kuna tatizo kwani ni kawaida wanandoa kuelezana vitu vizuri vinavyotokea kwa mmoja wao.

KILA MMOJA KUKATAA KUHUSIKA NA MATATIZO AU MIGOGORO YA NDOA INAPOJITOKEZA
Kama kila mmoja anajilinda na kutothamini hisia za mwenzake hasa linapotokea tatizo na kuanza kumrushia mwenzake lawana kwamba ndiye muhusika na wote mnakuwa na msimamo huohuo, fahamu kwamba hapo ndoa inapitiliza hata tiba za uangalifu zinazopatikana ICU.
Ikiwa migogoro au matatizo yanapojitokeza kuna kuwa na kushindana kwa kila mmoja kukwepa kuhusika na badala ya kupata suluhisho mnajikuta mgogoro unazidi kuongezeka basi hiyo ni dalili kwamba sasa mmeanza kubusu kifo cha ndoa.

KUJIKUTA NI WEWE PEKE YAKO TU UNAHUSIKA KATIKA KUTATUA MIGOGORO AU MATATIZO YA NDOA.
Je, umekata tamaa, au kujisikia vibaya kuongea masuala ya matatizo ya ndoa yako kwa sababu mwenzako anakurudisha nyumba, au imefika mahali na wewe umeamua kunyamaza na kuachana kabisa na kujishughulisha na tatizo lolote katika ndoa na matokeo yake hakuna hata mmoja anajali tena kushungulikia matatizo ya ndoa?
Kama mpo kwenye matatizo na kila mmoja amenyamaza kimya katika kuhakikisha mnamaliza tatizo lililopo basi hii ndoa ipo ICU na kama mtabaki kimya bila kila mmoja wenu kuhusika ili kuhakikisha ndoa inarudi kwenye mstari basi ni kama bomu lililotegwa ardhini na siku mtu akikanyaga hakuna kitakachosalia.

TENDO LA NDOA
Kama mmoja wenu sasa hana hamu kabisa na tendo la ndoa, au wote kwa pamoja hamna hamu kabisa ya tendo la ndoa hiyo ni dalili kwamba somethings is wrong.
Kukosa faragha ya pamoja (intimacy and affection) itawafikisha mahali ambapo ndoa inaweza kufa au kuwa na ndoa isiyokidhi haja au kukosa kuridhishana inavyotakiwa.
Je mnaishi tu kwa sababu ya watoto ndo wamewafanya msiachane?
Kama ni ndiyo basi mnahitaji kupata msaada wa washauri wa mambo ya ndoa kwani hakuna tatizo lolote kwenye ndoa ambalo halina jibu.
Kama hakuna hamu ya mapenzi kwa mmoja wenu au wote maana yake hisia zenu zipo mbali sana na hiyo ni dalili kwamba kila mmoja anaenda njia yake.

KUBISHANA AU KUGOMBANA KWA KITU KILEKILE KILA MARA
Kama kubishana, kupishana, kugombana, kuanzisha zogo kila mara kunatokana na issue ileile moja bila kupata suluhisho basi hiyo ndoa imesimama haikui wala kuelekea kwenye uimara zaidi bali inatelemka kwenda kwenye shimo.
Kama hakuna kitu kipya kinatokea ili kupata ufumbuzi wa hiyo hali basi tafuta mshauri wa mambo ya ndoa ili awasaidie.
HITIMISHO
Hakuna tatizo la ndoa ambalo halina jibu hapa duniani kuna washauri wa mambo ya mahusiano na ndoa, wazazi ambao hupenda mafanikio ya watoto wao, kuna wachungaji ambao wana hekima na busara walizopewa na Mungu kwa ajili ya kuwashauri hivyo hata kama kuna tatizo kubwa namna gani jibu lipo na tiba ipo.
Anza kwa kuzungumza na mwanandoa mwenzako then ikishindikana nenda kwa watu mnaona wanaweza kuwasaidia, usiwe mbishi wala mbabe ndoa ni kuchukuliana na kuelewana.

Tuesday 14 July 2015

UCHUMBA-1

Kutokana utafiti ambao umefanywa unaonesha kwamba moja ya mambo ya msingi ambayo kila kijana anahitaji ni Ndoa ya Kudumu ukiacha ongezeko la kufeli kwa ndoa nyingi.

Wakati huohuo moja ya uamuzi wa maana sana katika maisha ya binadamu ni kuamua nani atakuwa mume wako au mke wako na huu uamuzi ndiyo utakufanya uweze kuishi maisha ya namna gani katika ndoa yako na pia kuathiri kabisa mfumo wa maisha yako kuwa raha au kuwa karaha

Watu wengi katika maisha wamekuwa wakilaumu upande mwingine iwe mke wake au mume wake kwamba ndiye sababu ya kuvunjika kwa uhusiano au ndoa yao.
Hii si sawa, muhusika mara nyingi ni wewe kwani asilimia 99 ni jinsi ulivyompata huyo mtu ambaye amesababisha ndoa yako au uhusiano kuvunjika.

Mtu anayestahili kupewa lawama zote ni wewe.

Kama hujaolewa au ndio upo kwenye process za kuolewa au kuoa,Fahamu kwamba hakuna jambo muhimu maishani mwako kama huo uamuzi unaotaka kufanya, unaweza kukupa furaha ya maisha au uchungu wa maisha hapa duniani.

Unahitaji kutumia
akili zako zote,
maombi yako yote,
uwezo wako wote na
kila resource ulizonazo
kwani hapa makosa hayana nafasi kabisa

Wala usikubali kumuoa huyo binti au kuolewa na huyo kaka eti kwa sababu:

Watu wanasema Mbona hujaolewa au kuoa!
Au ndugu zako, au mchungaji, au wazazi wako au rafiki zako wamekwambia!
Au kwa sababu umeona muda unakwenda!

Amua mwenyewe na jichunguze kama upo tayari na kama mtu unayetaka kuwa naye anakupa uhakika unaoridhika nao wewe mwenyewe.

Kumbuka it is easy to reshape the mountain siyo mtu, kwa hiyo kama kuna tabia fulani ambayo unaiona kwa mtu unayetaka kuoana naye na hujaridhika nayo Please fikiri zaidi ya mara mbili.
Na kama unaweza give time au fikiri mara nyingi zaidi.

Mara nyingi wanaosema watawabadilisha matokeo yake wao ndo wamebadishwa

Hapa huhitaji kuwa blind kwa sababu ya fall in loves, bado unahitaji kuwa na akili timamu kumfahamu zaidi huyo unataka kuoana naye kabla love haijawafanya kuwa blind au otherwise muwe blind maisha yenu yote.

MAWASILIANO KATIKA NDOA.

Mawasiliano katika Ndoa ni kama barabara ya njia mbili inayoruhusu magari kuingia na kutoka; yaani wanandoa wawili ambao mmoja akiongea mwingine anasikiliza na mwisho wanapata jibu la kudumu la tatizo lililokuwepo.
Mawasiliano mabovu husababisha kutokuelewana ktk ndoa na mahusiano ya aina yoyote.


Ni kitu cha kawaida kwa sasa kuona mabishano ambayo yanaanza asubuhi jua linaochomoza na kuendelea hadi jua linapozama jioni bila ufumbuzi.


Mabishano kama hayo yasiyo na ufumbuzi ni kama Bomu linalosubiri muda ili lilipuke.


Baadhi ya wanandoa hudhani kwamba kuacha tatizo bila kulizungumzia ni kutatua, hiyo si kweli na hali kama hiyo haileti afya ya ndoa bali ugonjwa na matokeo yake ndoto ambazo mtu alikuwa nayo kuhusu ndoa huyeyuka kama barafu lililokutana na jua la mchana.

Kanuni muhimu katika kuhakikisha ndoa inakuwa imara ni pamoja na kila muhusika kujitoa na kuelekeza jitihada za kuhakikisha kila siku anawekeza ili ndoa kustawi.

jambo la msingi ni kuwekeza katika mawasiliano bora

Mawasilinao katika ndoa au mahusiano yoyote ni kama gundi inayounganisha ndoa.


Na ikitokea hiyo gundi ikaacha kufanya kazi basi mahusiano au ndoa huanza kukatika vipande vipande, na ndoa bila kuwasiliano lazima itakufa.

Katika jamii nyingi za kiafrika watu hawapo wazi sana kujieleza kile anahitaji kutoka kwa mwenzake.

Sema kile unataka bila kuzunguka.

Kama hujaridhika na style za sex za mpenzi wako sema ili ajue unataka kitu kipya, kama hujaridhika na chakula anachopika sema ili msaidiane na kuona inakuwaje, watoto, huduma kanisani maana wengine ni kanisani tu na mambo ya nyumba hana mpango, ndugu, kama hujaridhika na jinsi anavyotumia pesa sema ili ajue.

Kubaki kimya na kudhani atajua mwenyewe hata kama utahuzunika hatakuelewa eleza wazi ili kujenga ndoa yako.

hakuna njia nyingine zaidi ya ninyi wawili kuelewana na kukaa pamoja kupata jibu.

Kama unahitaji kitu Fulani kutoka kwa mwenzi wako sema nahitaji kitu Fulani, na kama kuna kitu Fulani anafanya wewe unaona kinakuletea shida mwambie kwa upole na moyo wa upendo na pia mwambie kwa nini unaona kinakuumiza kubaki kimya ni kama bomu ambalo linasubili muda na muda ukifika litalipuka.


Kama unahitaji muda wa kujibakia mwenyewe tu kufikiria mambo fulani fulani sema ili mwenzako ajue ila si kuwa mkali na kufukuza watu bila kusema kulikoni;

kuna wakati binadamu huhitaji awe yeye mwenyewe na Mungu wake, muhimu mawasiliano.


Huishi na malaika kwamba atajua kila kitu ambacho wewe unapenda au hupendi

Ndoa ni kujengana kila iitwapo leo

FANYA HAYA KUMFURAHISHA MWANAUME KITANDANI.

Mwanamke yeyote anayeweza kumfanya mwanaume kuwa mtu wa furaha anastahili pongezi kubwa sana kwa kazi nzuri anayofanya hasa kujitoa ili kuhakikisha ndoa yake inakuwa na afya kila siku.
Wapo wanaume (siyo wote) hata kama mwanamke anajitahidi kwa nguvu zote na ujuzi wake wote kumfurahisha, bado mwanaume haelewi somo anaendelea na maisha yake kama anavyojua yeye, hana muda wa kusikiliza kitu chochote kutoka kwa kiumbe anaitwa mwanamke.


Ili chumbani kuwe na furaha ni muhimu furaha kuanzia nje ya nyumba kabisa then sebuleni na kumalizia chumbani.
Jambo la msingi katika mahusiano ya ndoa; kila mwana ndoa anatakiwa kufanya lile ambalo na yeye anapenda kufanyiwa.
Jitahidi sana kutenga muda kwa ajili ya mume wako kwani maisha ni mafupi sana kuishi kwa kubishana, hasira, gubu, donge, kusemana na kulaumiana hakuna maana zaidi ya kupoteza muda kwani katika vita ya mume na mke anayepata hasara wa kwanza ni ninyi wenyewe then watoto.
Muhimu ni kuishi kwa kupeana mambo mazuri sasa hivi kwani huwezi kujua kesho kitatokea nini,
Anza kwanza wewe mwenyewe mwanamke kuwa mtu wa furaha then mwambukize na yeye, hapo mtakuwa mmefungua mlango wa furaha ya nje na ndani ya sita kwa sita.
Furaha ya kwanza kwa mwanaume ni wewe mwanamke unavyoonekana.
Idara ya mwonekano, urembo, uzuri ambao unakufanya uwe mwanamke.
Mwanaume siku zote anapenda sana mwanamke ambaye anapendeza jitahidi kujiweka safi muda wote,
kwa nini uwe rough,
mchafu, hujipendi,
mzembe, hujipambi,
unakuwa kama huishi dunia ya leo.
Kujipamba na kupendeza ni asili ya mwanamke na wanaume huvutiwa na jinsi mwanamke unavyoonekana.
Ni vizuri kumuonesha mume wako jinsi unavyompenda, jinsi unavyomjali na jinsi unavyomuhitaji na kujitengeneza vizuri ni moja ya njia ya kuonesha hayo.
Usitegemeee mwanaume atapata furaha chumbani kama mwanamke mwenyewe ndo huna mpango na uzuri wa mwili wako.

Je mwanaume kwa chakula unaweza kumpa furaha?

Ni kweli tupu, Unaweza kumfanya mwanaume ajisikie raha sana na furaha kubwa hadi chumbani hasa kama unajua jinsi ya kumpa mlo wa uhakika (chakula anachokipenda) na kama Mungu amekubariki kupika vizuri basi hiyo ni silaha muhimu sana.
Jaribu angalau kwa weekend mtengenezee chakula maalumu ili na yeye awe moja ya wanaume wenye furaha hiyo hapa duniani.
Hivi umewahi kupanga mkakati wa kuhakikisha kuna siku mume wako anakuwa ni mtu pekee mwenye furaha duniani?
Kama bado sasa ni wakati wake!
Hata kama unajua wewe kupika chakula kitamu ni kilaza, bado unaweza kusoma vitabu au kujifunza then ukampikia mumeo.
Wapo wanawake wanajua kabisa mume wake anapenda chakula aina fulani na anajua kabisa akimpikia hicho chakula mume huwa anafurahia lakini who cares, miezi inapita mume hajapata hicho chakula anachokipenda na wakati huohuo mwanamke ana lalamika eti mume siku hizi hanipendi na chumbani mambo si moto, anza kwazna kuwasha moto jikoni then usubiri na yeye awashe moto wa chumbani; thubutu utavuna ulichopanda!
Kama unataka chumbani kuwe na furaha lazima na wewe afanye sehemu yako kwa ajili yake.
Wapo wanawake miezi na miezi, mwaka hadi mwaka kila siku chakula anapika house girl, najua wanaume tunafahamu kabisa kwamba wake zetu mna majukumu makubwa, ila kitendo cha kupikiwa na msichana wa kazi mwezi mzima, mwaka mzima na wewe upo huwa wanaume hawafurahii.
mwanaume hujisikia furaha sana siku akila chakula alichopika na mke wake.

Utampaje furaha huko chumbani?

Ukisha kuwa umemtengenezea mazingira ya furaha nje ya chumbani, basi lazima hata chumbani atakuwa na furaha tu kwani kazi muhimu umeifanya, kilichobaki ni kuangusha mbuyu kwa shoka moja tu.
Wakati unaingia chumbani tu achana kabisa na mawazo yoyote hasi kuhusu yeye, achana kabisa na mambo usiyoyapenda kuhusu yeye na badala yake jiweke huru na wazi kabisa zaidi jimwage au jiachie kabisa.
Usimfiche kitu chochote unataka kutoka kwake, yaani uwe wazi na jisikie huru fanya kile yeye huwa anapenda hapo hakuna mipaka hakuna kuogopa kufanya kitu, hapo ni uhuru wa ajabu. Mpende kwa maneno,
kwa matendo,
kwa kunusa,
kwa kuonja kwa kugusu na
kwa hisia zote.
Usijilaze kama gogo mbele ya mume wako na kumsubiri yeye afanye kila kitu, participate fanya kile kimekuleta kutoka kwa wazazi wako, kwani kwa wazazi wako ulikuwa huvai, ulikuwa huli, si umemfuata kwa sababu yeye ndiye peke yake anaweza kukupa huduma ambayo wazazi wako hawawezi kukupa, yeye peke yake anaweza kuuhudumia mwili wako na feelings zake, ndiyo maana inabidi uchangamke, ujishughulishe na kuhakikisha unapata kile unahitaji kutoka kwake na kwa kuwa wote mna furaha na mnafanya kile mnapenda basi hapo kutakuwa na furaha kuu.
Mwanamke lazima uwe mtundu!

IFANYE NDOA YAKO KUWA MPYA.

Kawaida mahusiano ni kama kujenga nyumba ambayo ujenzi wake hudumu na kudumu hata kama ipo siku utaamua kuishi kwenye hiyo nyumba bado utaendelea na kufanya repair kila siku na kila mara.

Hivyo basi, ili ndoa yako iwe tamu na kuteka nafsi ya yule unampenda basi hakikisha huu mwezi unafanyia kazi mambo Yafuatayo;

Mapumziko ya pamoja:
Inatakiwa kujadili na kupata muda wa kuwa peke yenu, hii inawezekana ikawa mara mbili au tatu kwa mwezi, hata kama mna watoto wengi kiasi gani lakini faraja inayotukuka katika mapenzi ni kuwa pamoja. Tafuteni siku maalum ambayo mtatulia, mtajadili mambo yenu kwa usiri na mtatenda chochote kinachostahili, hapa mtashangaa kuona mnatengeneza penzi ambalo kwa muda mrefu mlikuwa hamjalipata.
Watu wanaokaa pamoja wakajifungia sehemu kwa zaidi ya masaa matatu manne si rahisi kuwa na kisirani, kwa vile kwa kukaa hivi kila mtu anakuwa na muda mzuri wa kumrekebisha mwenzake.
Kutafuta raha katika mwili:
Unatakiwa uwe mwepesi wa kuzigusa sehemu zinazomsisimua mwenzako hii inapendeza ikawa ni siku zile zile mnazoziteua kukaa pamoja, hata kama siku hiyo hamkuwa na ahadi za kutenda mambo yoyote ya kuchosha lakini ukishapita katika sehemu mbili kati ya 29 zenye raha basi ujue umetengeneza mapenzi mapya.
Kuondoa woga:
Hili nimekuwa nikilipigia kelele siku nyingi kwamba mpenzi wako hustahili kumwogopa, japokuwa kuna mila kama hizo ambazo mumeo unaweza ukamuona kama baba, hii si mbaya lakini ubaba huu uwe na mipaka na inapofikia wakati raha inahitajika basi kila vurumai lazima zitumike.
Yapo mambo mengi sana ambayo unaweza kufanya ili kuhakikisha penzi na yule umpendaye linazidi kuwa na fukuto kubwa zaidi kama vile kupeana zawadi, kuhakikisha unaongea maneno yanayomtia moyo na kumsifia vitu anafanya nk.

NDOA INA MFANO HUU.

Kujenga ndoa kuna fanana sana na kujenga jengo lolote kama nyumba tunazoishi.

Kwanza unaanza kwa kuwa na michoro mizuri na hatimaye unajenga jengo lenyewe.
Ndoa ni mahusiano ya juu sana kwa binadamu ni maamuzi ya ku-share moyo, akili, mwili; vyote kwa pamoja.

Katika kujenga jengo lolote suala la vifaa haliwezi kukwepeka kwani ndivyo husaidia jengo kusimama na ndoa ni hivyo hivyo kuna tools ambazo lazima utumie katika kujenga ndoa imara.

Kabla ya kununua hizo tools za kutumia kujenga ndoa kumbuka kwamba wewe na mwenzi wako wote mpo timu moja na lengo si kushindana kwani hatuhitaji mshindi bali tunahitaji kufanya kazi kama timu.
Ndoa si nani anashinda bali ni wanandoa wote kuelekeza nguvu kusukuma au kuvuta kama kuelekea upande mmoja.
Katika ndoa si lazima ushinde kila mgogoro unapojitokeza na wewe kuwa sahihi kuliko mwenzio bali ni kusaidiana na kumtanguliza mwenzako.

Kifaa cha kwanza ni KUWASILIANA.
Ni muhimu kuwa na mwasiliana ya pamoja kila siku. Tunapozungumzia mawasiliano tunaenda katika nyanja zote zinazomuhusu mtu pamoja na kuhusisha milango yote mitano ya fahamu yaanu kuguswa, kunuswa, kusikia, kuonana na kuonja.
Hapa ni mawasiliano ya kihisia, kiakili, kimwili na kiroho

Kihisia : jitahidi kutiana moja kati yenu na pia fahamu kwamba katika kuwasiliana ni asilimia 7 tu ni maneno asilimia 93 ni jinsi ya tone ya sauti yako na body language. Jinsi unavyoonekana wakati mwenzako anaongea na sauti yako unavyojibu huwasilisha hisia zako kwa mwenzi wako hivyo uwe makini kuhakikisha humuumizi. Watu wanapanda gari wote kwenda kazini na hawaongei hadi wanafika na hata wakiongea majibu ni mkato tu, kihisia hapo kuna jambo.

Kiakili: je, kuna gazeti umesoma na kuna kitu kimekufurahisha nawe wataka mwenzi wako ajue?
Mweleze basi. Je, una story yoyote unataka kumsimulia mkeo au mumeo msimulie basi.

Kimwili: mpe miguso mingi tu ambayo si ile ya chumbani wakati unataka ile kitu. Mkumbatie, mbusu, mshike mkono, unampompa mguso (touch) maana yake unamjali na touch ni hitaji la msingi la binadamu. Kama mnaweza oga pamoja .

Kiroho: kuna wanandoa wengi husahau kushirikiana katika mambo ya kiroho hata kama wapo imani moja. Unahitaji kumuombea mwenzi wako, na pia unahitaji kuomba pamoja kama wanandoa hii husaidia kuinua mahusiano yenu. Imba pamoja nyimbo za kumsifu Mungu. Soma Neno kwa pamoja na kila mmmoja kushiriki kutafakari.

Kifaa cha pili ni KUBARIKI
Mbariki mwenzi wako kila iitwapo leo.
Anza leo kutoa maneno ya baraka kwa mume wako au mke wako hata kama hukuzaliwa familia ambayo imekuridhisha kumbariki mwenzako.
Mpe sifa anazostahili kwa mambo mazuri anafanya, inawezekana anafanya kazi kwa juhudi, anapika vizuri, anakutunza vizuri, anakupenda, anakurishisha kitandani, mwambia “asante, nakupenda, pole sana, ubarikiwe, unapendeza nk.
Hata kama wewe ni mgumu mno kutoa neno la baraka basi anza leo kwa neno lolote dogo unaloona mwenzi wako amekufanyia.

Kifaa cha tatu ni KUSHIRIKIANA.
Shirikiana mambo mengi katika maisha kwa kadri mnavyoweza.
Kuwa pamoja katika muda, mawazo, kucheza, kutazama TV program pamoja, kikombe cha kahawa au chai pamoja, kusafisha nyumba pamoja, kuendesha baiskeli pamoja., kula chakula sehemu pamoja, kufanya vitu mmoja anapenda pamoja nk.
Mnapotumia muda pamoja husaidia kuwaunganisha zaidi na kuwa kitu kimoja.

Kifaa cha nne ni KUITIKA bila kulaumu kwanza
Usibishe, itikia kwa kukubali kwanza. Jinsi unavyoitikia kuna elezea zaidi kuliko vitendo wakati mwingine.
Je, kama mume wako au mke wako amechelewa kurudi nyumbani, na hajapiga simu, huwa una respond vipi. Kitu cha msingi si kurukia na kuanza kulaumu bali kwanza kumsikiliza na kujua sababu ni ipi kuliko kulalamika na kuanzisha moto au zogo la nguvu.
Je, ni umri upi unafaa kwa mwanamke na mwanaume kutofautiana wakati wa kuoana?

Ni kawaida kuona akina dada wengi wakiolewa na wanaume wenye umri mkubwa kuliko wao na pia kwa upande mwingine, tumekuwa tukishuhudia vijana wa kiume wakioa wanawake wenye umri mkubwa kuliko wao hadi kuwa gumzo kwa jamii ambazo hazijazoea kuona hayo.
Kwani masuala ya kuoana mara nyingi yamejikita ktk mila na desturi ambazo sasa zinapata challenge kubwa mno.

Katika hali ya ukweli, Umri ni namba tu na hauna nafasi katika kukusaidia kuwa na ndoa imara.
Wapo wanandoa wenye umri sawa na ndoa hadi zimekalia mabechi ya ICU ya ndoa, pia kuna wengine umri upo sawa na wanaaendelea kujienjoy utadhani wapo paradiso.

Ndoa inategemea kukomaa kwa akili kwa wahusika na upendo wa kweli uliopo kati yao, awe amekuzidi au umemzidi au mpo sawa misingi ya ndoa haijajijenga katika tofauti ya umri bali true love and satisfaction emotionally.

Wanasema love is blind ni kweli mapenzi hayaangalii umri bali mioyo miwili iliyopendana na kuwa mmoja.
Hata hivyo wataalamu wanapendekeza kwamba umri mzuri kuoana unapatikana kwa formula ifuatayo:

Umri wa kuoana = ½ ya Umri wako + 7 (Minimum)
Umri wa kuoana = 2 x Umri wako - 7 (Maximum)

Pia jinsi mtu anavyozidi kuongezeka umri zaidi ya miaka 50 kama unaoana naye na wewe upo chini ya miaka 25 fahamu kabisa kwamba suala la sex na kuzaa watoto uwe makini na umejiweka sawa na mmeongea mkamalizana kabla ya kuingia kwenye ndoa na mtu mwenye umri huo.


YAEPUKENI MAKOSA HAYA KTK NDOA.

1. Kutokuheshimiana
Si vizuri kumtamkia maneno mabaya mwenzi wako mbele za watu.
Mke au mume anahitaji kuheshimiwa, kupewa asante kuwa appreciated na zaidi kumsifia mbele za watu na sivinginevyo.
Kuongea mambo mazuri kwa mke au mume wako mbele za watu ni muhimu sana.
Wapo wanaume hutukana wake zao mbele za watu na wapo wanawake hujibu mbovu waume zao hata mbele za watu au wageni. Kama kuna kitu amekuudhi kwa nini usisubiri mkaongee chumbani mkiwa wawili?

2. Kutosikiliza mmoja akiongea
Hii inajumuisha kuwa na mawazo ya mbali wakati mume au mke anaongea, yeye anaongea wewe unaendelea kuangalia TV, Unaendelea kusoma gazeti, unaendelea kusoma kitabu, Unaisikiliza laptop kuliko mume wako au mke wako.
Pia hii inajumuisha kuwa mbali kimwili (body language) wakati mwenzako anaongea, wapo wanandoa ambao hata mwenzake hajamaliza kuongea tayari anadakiwa kwamba najua ulichokuwa unataka kusema, pia wapo ambao hata ukiuliza swali yupo kimywa, mbaya zaidi ni pale unapoona na kuhisi mwenzako ana tatizo lakini ukimuuliza anabaki kimya au anakwambia hakuna tatizo, Inaumiza sana hasa kwa wenzetu wanawake ambao asilimia kubwa ya wanaishi kwa hisia, na kuumiza hisia zao ni kitendo kibaya sana, ni vitu vidogo lakini ni muhimu kuliko unavyodhani.

3. Kukosa mahaba (sexual intimacy)
Ukiacha mke wako au mume wako anahangaika na kutoridhishwa kimapenzi maana yake unachimba shimo ambalo ukijifukia utatokea jehanam, na kama unaona umepoteza interest na sex fanya kila njia kupata ushauri na msaada ili urudi kwenye mstari.
Matatizo mengi ya ndoa zinazokufa huanza kwa ugonjwa wa kutoridhishwa kimahaba na mume au mke.
Kumbuka ndoto za watu wengi kuoana ni kupata mtu atakayemtosheleza kimapenzi.

4. Kujiona sahihi mara zote
Hii inajumuisha wewe kuwa ndo msemaji na muelimishaji wa mke wako au mume wako, yaani wewe ndo unajua kila kitu, upo sahihi siku zote, au bila neno lako la mwisho basi information haijakamilika.
Siku zingine kubali kwamba umekosea au huna jibu, hakuna mtu anaweza kufurahia kuwa na mtu ambaye siku zote yeye ndo yupo sahihi labda kama unaishi na mtu mwenye mtindio wa akili.

5. Kutokufanya kile unasema
Siku zote Imani bila matendo imekufa na Imani ni matendo, “Actions do speak louder than words”. Ukisema utafanya kitu Fulani, fanya.
Wanawake ni viumbe ambao hutunza sana ahadi tunazowapa, hivyo usiahidi kitu ambacho huwezi kufanya, kwani mwenzio anaandika kwenye ubongo wake siku akija kukutolea mahesabu ya ahadi hewa umefanya utaipata fresh, pia na wanaume (si wote) kwa ahadi hewa hatujambo, tujifunze kufanya kila tunachosema.
Tusitoe ahadi tamu kumbe hewa, unaumiza sana.

6. Utani unaoumiza
Kama mwenzio anakwambia utani wako unamuumiza achana nao, kuna utani mzuri lakini kuna wakati mnaweza kufikishana pabaya na lazima uwe makini kusoma saikolojia za mwenzi wako, kuna wengine anaweza kukutania wewe usikwazike, na utani huohuo ukimrudishia yeye anakwazika so be very careful usimuumize mwenzako.

7. Kutokuwa mwaminifu
Kudanganya na kuwa na siri zako binafsi katika mahusiano huweza kujenga wawili kuwa mbali na kutokuaminiana.

8. Kuwa mtu unayeudhi kila wakati
Inaweza kuwa ni mzembe, mchafu, mtu wa kuchelewa kila mahali, mtu wa kusahihisha kila kitu mwenzio anafanya, mtu wa kulalamika tu kila wakati kila kitu, kuwa kimya tu mwenzio akitaka muongee masuala ya ndoa au familia. Unajua unaushi lakini unaendelea kuudhi.

9. Kuwa mchoyo
Yaani unatumia pesa nyingi sana kwa mambo yako na mume wako au mke wako akitumia pesa kidogo tu kelele na zogo hadi nyumba inakuwa moto.
Hadi nyumba yako haipo friendly maana hata kuburudika kwa soda tu kwako ni issue wakati ukiwa mwenyewe unajichana ile mbaya na kuku kwa chips na kitimoto na watu ambao ni nje na familia yako, hiyo ni aibu!

10. Ukali kama pilipili kichaa
Kila mwanandoa anahitaji kuwa mstaarabu linapokuja suala la kutatua mgogoro wowote, wapo ambao tatizo likitokea mke au mume na watoto wanatamani kuhama nyumba maana hapakaliki, Ni kweli kwa kelele zako na mihasira yako unaweza kuwin huo mgogoro lakini mbele ya safari bado utajikuta ni wewe ndo umeharibu zaidi.
Sidhani kama kuna mtu anapenda kukaripiwa kama mbwa ndani ya ndoa

WANAUME TU.

Kama wewe ni mwanaume ni dhahiri unajua umuhimu wa kufanikisha utundu wakati wa tendo la ndoa.
Utundu katika sex ni kitu ambacho hupelekea kuwa na siku zenye kumbukumbu tamu na siku zenye kumbukumbu ovyo kabisa.
Pia utundu wako ndio unaokupa njia ya kufanya mke wako afurahie sex au kuona kitu cha kawaida na kuwa mbali nacho kabisa.

Kama mwanaume techniques zifuatazo hutakiwi kuzikwepa kabisa siku zote ukitaka sex iwe kitu kitamu na mpenzi wako.

JIFUNZE KUCHELEWA KUFIKA KILELENI
Kuwahi kukojoa mapema (ejaculation) ni muuaji mkubwa wa faragha na huhitaji kufanyia kazi kurekebisha hii tabia. Kama unawahi kufika kileleni kabla ya mpenzi wako au kufika pale ambapo mpenzi wako anahitaji basi Unahitaji kupata solution ya kudumu. Inawezekana kupata jibu hata kwa wiki au mwezi na ukawa unafika pale panatakiwa.
Hakuna kitu huumiza wanawake kama kitendo cha wewe kumaliza dakika mbili na kumwacha akiwa bado ana hamu na zaidi sana akiugulia kumuacha solemba kwa kumuonjesha utamu ambao hakumalizia.

FAHAMU SEHEMU AMBAZO MWANAMKE ANASISIMKA
Kila mwanamke ana sehemu ambazo husisimka zaidi na kupelekea kunyegeka na kuwa na hamu na kutana tendo la ndoa, mwanaume Unahitaji kujua ni sehemu ipi mke wako husisimka zaidi ukizingatia kwamba kila mwanamke ana sehemu yake. Mwanamke mwingine akiguswa viganja vya mikono tu chini analowa kabisa, na mwingine ukigusa matiti mtakosana maana unamuumiza. Mwanaume mtundu katika mapenzi hujua mke wake anasisimka na kuwa hoi akichezewa wapi.
Ukishafahamu ni sehemu ipi na inafanywa vipi ili asisimke basi huna budi kutumia muda wako wa foreplay kumpa bibie tamutamu yake hadi aridhike kwamba ana mwanaume anayemjali na si kurukia tu kule chini Afrika ya kusini na kuanza kuchimba dhahabu bila hata kujua mgodi wenyewe upoje.

UBUNIFU
Wanawake wengi katika ndoa na mahusiano hulalamika sana hasa kutokana na kukosa msisimko wa mapenzi wakati wa faragha. Wanalalamika kwa kuwa wanaume kila siku hutoa kitu kilekile, anakubusu, anakugusa kidogo na akiona chini kumelowa tayari anachomeka kama anapigilia misumari na ikiingia tu anapigilia akiona tayari huyo amemaliza na kuondoka zake.
Wanawake wanapenda surprise na kusisimuliwa katika njia mpya, mwanamke anahitaji kitu kipya baada ya muda, anahitaji sex position mpya, anahitaji busu jipya, anahitaji kunyonywa kupya na anahitaji kusikia neno kipya kwenye masikio yake.
Ni juu yako wewe mwanaume kujifunza mbinu mpya na kuwa mbunifu kitandani, wanaume ndivyo tulivyo tunahitaji kuwa wabunifu, fanya kitu kipya ambacho kitamfanya mwanamke ajisikia ana mwanaume ambaye ni MWANAUME

MUHIMU KATIKA NDOA.

Ni jambo lisilopingika kwamba ndoa zina raha yake na utamu wake hasa kila mmoja akimtanguliza mwenzake na kufuata misingi sahihi ya kuimarisha upendo, furaha na amani katika ndoa.
Ni mafanikio ya ajabu sana kwa jamii za leo kuona watu wanasherehekea kufikisha miaka 5, 10, 15, 20, 45 na hata zaidi 50.

Unapoongea na watu ambao ndoa zao zimeweza kuvuka milima na mabonde hadi miaka 35 ni lazima usikilize kwa makini kwani kuna maneno ya hekima na busara.

Wao wanasema siri kubwa ya ndoa yao kudumu kwa muda mrefu ni kama ifuatavyo:

Msikasirike wote kwa wakati mmoja.

Kama unataka kulaumu basi fanya kwa upendo wa hali ya juu sana.

Usikumbushie makosa ya nyuma.

Ni vizuri wakati mwingine kuachana na ulimwengu wote lakini si kuachana ninyi wawili.

Usiende kulala huku mmoja akiwa na donge moyoni.

Hakikisha umempa mwenzako sifa kwa kazi moja aliyofanya angalau kwa siku mara moja.

Kama umefanya makosa, kubali na omba msamaha.

Ili kugombana wanahitajika watu wawili tu, hivyo chunga sana.

Wakati umekosea kubali na wakati upo sahihi kaa kimya.

JE,MUMEO ANACHEAT?

Wanawake wengi (siyo wote) wana hisi kwamba waume zao wanamahusiano ya mapenzi na wanawake wa nje ya ndoa zao lakini wanashindwa kufahamu namana gani au ni dalili zipi zinaweza kupelekea kupata ukweli na kuujua na hatimaye kumkamata au kuwabamba.

Wapo wanaume ambao hutumia ujanja wa hali ya juu sana ili asiweze kugundulika kwamba anafanya cheating hata hivyo zipo dalili za kawaida ambazo wanaume wengi ambao wana cheat unaweza kuwajua.
Kitu cha msingi si kwamba ukiona dalili moja basi unafikia uamuzi kwamba ana cheat, unaweza kuharibu mambo au kuishia kudundwa bure.
Hizi ni dalili za kukusaidia wewe kuweza kuchukua hatua zaidi kuchunguza hasa kutokana na wewe mwenye kuhisi kitu kisicho cha kawaida.

Zifuatazo ni dalili zinazoweza kupelekea kupata data kugundua kwamba hapa mwanaume ana cheat au anaanza ku-cheat.

MABADILIKO YA GHAFLA YA MWONEKANO WAKE
Mwanaume ambaye ana cheat au anayeanza cheating atajitahidi kuonekana smart na attractive, anaanza kuwa na aina mpya ya mwonekano wake hasa kutokana na yule nayetaka kuwa naye, kumpendezesha hawala yake, anaweza kuwa alikuwa si tabia yake kunyoa ndefu na sasa ghafla kila siku kipara kwenye kidevu bila maelezo,
Pia angalia tofauti na mazoea yake je, anapofika nyumbani anakimbilia kuoga au hataki usimguse akiogopa utamnusa na kupata harufu ya manukato ya hawala yake?
Ukihisi chunguza!

JINSI ANAVYOSHIRIKIANA NA WEWE
Jinsi mwanaume anavyo ku-treat unaweza kujua kuna kitu zaidi ya jinsi anavyo react.
Yeye kujihusisha na mwanamke mwingine lazima kutaleta mabadiliko na jinsi anavyoku-treat wewe.
Anaweza kuwa anakuchukia bila sababu au anaweza kuwa mpole kuliko kawaida hadi ukashangaa nini kimemtokea. Hata kama alikuwa hakupi zawadi unaweza kuona unapewa zawadi bila kutegemea.
Kumbuka sababu moja haitoshelezi kujua kwamba anafanya cheating, lazima uchunguze na upate ukweli.

MAONGEZI
Ikiwa kuna mambo anakataa kuyaongelea au anachagua au anakuwa na majibu mafupi kuliko zamani basi inabidi uwe makini, hasa story zinazohusu watu kuwa na nyumba ndogo, watu kutoka nje ya ndoa, watu kufumaniwa nk.
Pia ukiona anataja majina ya watu ambao huwafahamu vizuri hasa wanawake, anataja sehemu ambazo ni ngeni na si kawaida yake kuongelea unatakiwa kuwa makini inawezekana ni dalili kwamba ameanza kuvutwa shati.
Kumbuka si kweli kwamba kila mwanamke ambaye anamtaja basi unachukulia ni hawala yake.
Chunguza!

KAZINI
Mara nyingi wanaume wengi hujitetea kwamba walikuwa kazini au wanaenda kazini hata siku za weekend ili kupata muda wa kutoka nyumbani, siku nyingine mwambie tunaenda wote, ukiona anatapatapa ujue hiyo safari si ya kazini bali ya Sinza Madukani.
Pia wanaume wasiowaaminifu hutumia cover ya kazini kwa cheating zao na kama huwa anafanya kazi za shift wewe ndo unatakiwa kuwa makini zaidi kwani kuna shift za usiku na kama akipatia kwamba ameenda kazini usiku kumbe kaenda kwa hawala basi huko ni sherehe.
Kitu cha msingi chunguza mabadiliko ya ghafla ya ratiba yake ya kazini na kuwa tofauti na kawaida yake, pia ni vizuri kujua bosi wake au rafiki zake wa kazini ili kama amekwambia ameenda kazini unaweza kuongea na bosi wake kuhakikisha ila uwe na hekima na busara. Unaweza kukuta kazini hayupo wiki!

RATIBA
Binadamu ni mtu wa tabia, kila mtu ana ratiba ambayo baada ya muda huwa kama tabia yake. Chunguza mabadiliko ya tabia yake na ratiba zake kama zimebadilika ghafla.
Kama amebadilisha ratiba zake ghafla chunguza nini kimesababisha, kama alikuwa hana mazoea ya kusafiri kikazi na sasa kila siku anasafiri, chunguza.
Inaweza kuwa kweli anaenda kufanya kazi lakini wakati mwingine mmm anasafiri naye. Pia kama alikuwa hana time na nyumbani sasa mmemleta house girl na anapenda kubaki nyumbani wewe ukiondoka.
Chunguza! anaweza kuwa ameanza kukafuatilia hako katoto maana watoto wa siku hizi nao kazi kwelikweli!

MATUMIZI YA PESA
Kuwa na Affairs ni gharama.
Kama ana hawala lazima atatakiwa kumburudisha kwa vyakula, vinywaji, mapochopocho, kitimoto, chips kuku , hela za saloon, usafiri tena anataka tax, zawadi na kama amepata limbukeni basi kifedha ataumia hata kama ni makini namna gani lazima kutatokea matatizo ya kifedha katika familia kwani matumizi yataongezeka.
Na wanaume kwa kujidai wao ni Bill gates lazima uchumi utayumba tu.
Hivyo uwe makini na ku-track mabadiliko ya fedha au bajeti hasa ukiona pesa hakuna na pia hakuna mnachofanya.
Chunguza!

KUSAFIRI
Wanaume wengi wasiowaaminifu huambatanisha safari zao za kikazi na mambo ya cheating, wengine husafiri kikazi na mahawala hadi nje za nchi na unaambiwa mwanamke si lazima kwenda airport au hataki kuzindikizwa.
Chunguza kwa nini?
Unahitaji kuwa makini na hizo safari zake wakati mwingine anaweza kwambia ameenda kwenye semina Morogoro kumbe yupo Kimara, Au ameenda Arusha kumbe yupo Bagamoyo.
Ni vizuri mwanamke kujua kazini kwa mumeo pamoja na wafanyakazi wenzake ili akisema amesafiri basi waweza kuwasiliana na wenzake ili ujue kweli amesafiri au ndo amesafiri kwenda kwa hawala.
Tumia hekima na busara usikurupuke!

KUTOKUPATIKANA
Kwa mwanaume kuwa na wanawake wawili na kuwaridhisha na kila mmoja akaridhika anahitaji muda mwingi, kwa kuwa tuna masaa 24 tu kwa siku kama ana mtu lazima kupatikana kwake kutapungua maana anatakiwa kwenda kazini, kwenda kwa hawala na pia familia, hapo lazima hata kama atakuwa mjanja kutakuwa na mabadiliko ya yeye kupatikana nyumbani kama kawaida yake.
Ukiona ameanza kurudi nyumbani zaidi ya saa nne usiku bila sababu ya msingi anza kuchunguza hata kama anasema alikuwa na rafiki zake kwa ajili ya mambo ya business, familia ni zaidi ya business, hivyo mwanaume anayejali huwa ana balance muda wa familia na business.

SIMU
Hapa patamu kweli, wengine wamewekeana mipaka kwenye ndoa kila mmoja hakuna kugusa simu ya mwenzake, kwa nini? kuna siri gani?
Cheating nyingi zinahitaji mawasiliano na mawasiliano mengi ni kwa njia ya simu tena za mobile. Wapo wanaume hujiamini sana hadi kuruhusu kupigiwa simu hata nyumbani, hivyo uwe makini na simu za wanawake anazopigiwa na pia mwangalie usoni na jinsi anavyo react anapopigiwa simu za aina hiyo au kama akipigiwa simu anaenda mbali kuongelea wakati mpo wawili tu wewe na yeye.
Au hata kabla ya kuongea anakata na kusema atampigia.
Pia wapo wanawake (mahawala) wao ni- beep tu ili mwanaume ampige hivyo basi uwe makini na hao beeers kwa simu ya mumeo.
Pia chunguza kama simu yake ya mkononi anaibania sana yaani hata akienda kuoga anaenda nayo, lazima itakuwa ina mabomu mazito inayo.
Chunguza si mara moja ila kwa hekima na busara.

GARI
Kama mna gari wakati mwingine wengine husahau vitu bila kutegemea, hivyo uwe makini na kuangalia kwenye gari kuna kitu gani kimewekwa kwani kuna wanaume wasiowaaminifu hawathubutu kabisa kuacha au kuweka vitu vya mahawala wao nyumbani bali kwenye magari kwani wanajua wanawake hawawezi kuchunguza na kuanza kukagua, unaweka kukuta vitu vya ajabu ikawa go ahead kwa ajili ya kufanya u FBI.

TENDO LA NDOA
Uwe makini na mabadiliko ya kufanya mapenzi, wengi baada ya kuchoshwa na hawala akifika nyumbani amechoka au anaanza kukulaumu kwamba upo baridi au humpi mapenzi ya kweli ingawa unajitahidi kutoa utaalamu wako wote.
Pia anaweza kukosa hamu ya mapenzi na wewe, hivyo uwe makini kuchunguza kama kweli hakuna mtu wa tatu anayeingilia hapo.
Kuna wengine akifika kileleni anaweza kutamka jina la hawala yake hivyo uwe makini na maneno yake huko chumbani.

CHAKULA
Inabidi uwe makini na mabadiliko ya tabia yake ya kula chakula, mahawala wengi huweza kubadilisha tabia ya ulaji wa mumeo, anaweza kuanza ghafla kupenda chakula aina nyingine pia anaweza kuanza kupenda chakula cha hotel fulani ghafla.
Pia inaweza kutokea akawa kila ukimuandalia chakula hali kama kawaida yake, inawezekana kampitia sehemu na huyo mwanamke wakala so ameshiba, kwani wanaume wengi wa kiafrika tumelelewa mazingira ya kwenda kula chakula alichopika mke sasa inakuwaje leo hataki au kila mara ameshiba wakati huohuo amechelewa kurudi si ndo njaa ingeuma zaidi.
Chunguza!

HARUFU
Kila mtu ana harufu yake ya mwili ya asili. Inabidi uwe makini na harufu inayotofauti na kawaida yake.
Mnuse anaporudi kazini hasa anapokupa hug na pia kwenye gari lake. Unaweza kugundua harufu ambayo itakupa hints za kuanza kumchunguza zaidi

KAMA UMESAFIRI
Si kawaida kwa mwanaume asiyemwaminifu kumleta kimada wake nyumbani kwenu wakati hupo, lakini wapo ambao hudiriki kumleta kimada ndani ya chumba chenu na ni kawaida sana mwanamke mgeni akiingia kujisahau na kusahau vitu alivyokuja navyo kama chupi, leso, vito nk so siku ukirudi uwe makini kuangalia vitu ndani ya chumba chako, bafuni na sehemu zingine na ukikuta kitu kigeni tena hutumiwa na wanawake basi anza kuchunguza.

ZAWADI
Uwe makini sana na sikukuu zilizopo kwa mwaka kama vile Christmass au Valentine’s Day unaweza kukuta kadi au zawadi zimefichwa kwenye gari au ndani ya nyumba na pia risiti za manunuzi ya hizo zawadi unaweza kuzibamba mahali popote.
Chunguza upate ukweli.

MATUMIZI YA INTERNET
Ingawa hii si kawaida kwa nchi zetu za Afrika, kwa nchi zilizoendelea ambako kila familia nyumbani kuna internet, inabidi uwe makini na muda anaotumia kuchat au mawasiliano ya email zake zipo wazi au ni siri, anaweza kuanza kwa internet hadi akaja kukutana na huyo mwanamke kimwili.

USHAHIDI
Kama mtu anafanya cheating kuna wakati huwa inatokea bingo data zinakuja zenyewe by nature. Baada ya kuzoea anaweza kujisahau na kuacha kitu muhimu na kikakutwa, angalia wallet yake, nguo zake za ndani, kwenye mifuko ya suruali, drawer, shelves, kwenye begi lake, hata kule ofisini kwake nk.
Unaweza kupata ushahidi wa uhakika.

TABIA YAKE MBELE YA WANAWAKE WENGINE
Utafiti unaonesha kwamba mwanaume anaweza kufanya cheating mara nyingi na mwanamke ambaye anafahamiana naye iwe kazini, jirani, rafiki wa familia, house girl, watu anaofanya nao business, au watu aliosoma nao nk.
Kama wewe ni mtafiti unaweza kufahamu au kung’amua kitu hasa akiwa na mwanamke ambaye anatembea (sex) naye, kwani wanawake wenyewe akitembea na mwanaume mara nyingi humuona mwenye mume si lolote na pia kuna aina fulani ya aibu huwepo wakiwa pamoja na wewe.
Kama ni house girl unaweza kuona kaanza kiburi na kukuringia ambako ni tofauti kabisa na kawaida yake, maana anajua mzee tunakula wote.
Ipo silaha ambayo wapo wanawake wanaipenda sana kuitumia wakiwa kwenye ndoa.

Kwa nini baadhi ya wanawake hupenda kutumia silaha ya kuwanyima unyumba (sex) waume zao kama njia ya kuwaadhibu pindi akifanya makosa au akitaka amnunulie kitu na mume akawa hanunui au hatimizi ahadi?
Ndoa inapaswa kuwa ni taasisi ambayo watu wanapaswa kupendana, kushirikiana, kufanya mambo kwa pamoja na pia kufurahia maisha pamoja ambayo wamekubaliana kuishi.
Kitu kinachoshangaza ni kwamba likitokea tatizo basi kitu cha kwanza kuharibika ni chumbani. (No sex today)
Hivi kwa nini msinyimane chakula tu, mnanyimana unyumba.
Njia sahihi likitokea tatizo ni kuzungumza na kupata ufumbuzi"

Ni dhahiri kabisa ndoa nyingi (si zote) likitokea tatizo, basi silaha ya kwanza mwanamke kuitumia ni kunyimana sex kitandani, na kama ndo wale wenye hasira, ujue wiki au mwezi mtalala mzungu wa nne mpaka unyoke.
Nidhahiri pia kwamba tendo la ndoa ni kitu muhimu sana katika ndoa, linapokuja suala la wanandoa kuamua kuadhibiana kwa kunyimana basi wawili hawa huwa katika wakati mugumu na hasa kwa yule anayeadhibiwa.
Wengi wanapenda kutumia hii silaha kwa sababu ni kweli tendo la ndoa lina control maisha si jamii tu bali hata uchumi, na ndiyo maana watu wanaoana kwa sababu wanataka sex, ingawa wengi wanaweza kupinga hilo.
Pia wapo wanawake wenye wanaume wababe ambao hata ukiamua kumuadhibu kwa kumnyima sex bado utatoa tu, kitu ambacho unafanya unajitoa katika kushirikiana naye na anakuwa kama vile anafanya kile kitendo peke yake na wakati mwingine unaweza kuongea kwa kutaka amalize haraka ili uendelea na msimamo wako kwamba umemuadhubu.
Unamwambie mumeo
Fanya haraka mimi nilale zangu"
au
"Bado hujamaliza?",
Naamini mwanaume mwenye busara hawezi kulazimisha sana sana atatafuta solution ya kudumu na kama mwanaume ni mwaminifu basi mwanamke umepatia na kama si mwaminifu umejimaliza maana usijesikia kesho amepata nyumba ndogo ambayo inaweza kufanya maajabu.
Napinga kabisa nyumba ndogo kwa nguvu zote, ila naomba wanawake kutumia njia zingine kama unataka kumuadhibu mume wako ila si kumyima tendo la ndoa.
Pia wapo wanawake ambao kama anataka kitu na mwanaume hajampa au hajamnunulia basi anatumia silaha yake ya kukunyima sex hadi ununue au ampe.

"Kwa mwanaume mwaminifu ni kweli unamuumiza sana, ila kwa mwanaume ambaye si mwaminifu fahamu unajimaliza mwenyewe"

HASIRA KATIKA NDOA.

Linapokuja suala la hasira hakuna cha mweupe wala mweusi, hakuna cha mfupi wala mrefu, hakuna cha mnene wala mwembamba;
wote tunapata hasira na tunatofautiana katika kuithibiti hasira.Hasira ni hisia asili ambazo humtokea mtu yeyote.
Na hasira ni mwitikio wa mtu kutokana na hisia za usalama wake, furaha yake au amani yake na kila mmoja wetu amewahi kuwa na hasira na inawezekana hata sasa hivi unaposoma hapa bado una hasira ambazo zimekujaa kutokana na kuudhiwa bosi wako, mume wako, mke wako, mchumba wako, kiongozi wako, rais wako, watoto wako, wanafunzi wako au kitu chochote.

Watu tunatofautiana sana linapokuja suala la kiwango cha hasira na jinsi ya kuiyeyusha hiyo hasira.
Wapo watu akipata hasira hata kuongea hawezi kabisa na wengine wanakuwa wepesi hata kuzipiga, wengine akiwa na hasira anazira kabisa kufanya kitu chochote.
Migomo mingi mashuleni na makazini wengi huongozwa na hasira ndiyo maana wakati mwingine hufanya vitu vya ajabu.
Na wale waliopo kwenye ndoa naamini wanajua mengi sana kuhusiano na neno HASIRA kwani kupata hasira katika ndoa ni jambo ambalo halikwepeki kwani mnakutana watu wa malezi tofauti na aina tofauti ili kuwekana sawa lazima kuna vitu mmoja hatapenda na wakati mwingine kupata hasira.
Wengine akishakuwa na hasira kama ni kwenye ndoa basi ujue umeumia na ni kasheshe kwelikweli, maana kulala ni mzungu wa nne, chakula utajijua mwenyewe, inakuwa vita ambayo huna jinsi.
Wapo ambao pia akiwa na hasira ni kilio utadhani kuna msiba.
Kuna wengine ni mashujaa wa kukaa na hasira zaidi ya wiki, wengine zaidi ya mwezi na wengine zaidi ya mwaka pia wapo wengine hasira zao huishi kwa muda kidogo sana na hasira zikiisha anaweza kukuomba msamaha mara moja.
Na wengine akipata hasira atakununia tu hata kukusalimia hana mpango.

Hasira zinajenga au kubomoa na hili linatokana na mwitikio wako ukipata hasira.
Tatizo si kuwa na hasira bali ni jinsi gani una react ukiwa na hasira.
Watu wanaojifunza mambo ya hasira wamepata data zinazoonesha kwamba watu waliopo kwenye ndoa ndiyo wenye hasira mara kwa mara kuliko taasisi yoyote duniani.

Uthabiti wa ndoa unategemea sana ni jinsi gani wanandoa wana deal vipi wakiwa na hasira kwani ndoa nyingi zimekuwa hell kwa sababu ya wao kushindwa kuthibiti hasira zao.

IMANI POTOFU KUHUSU HASIRA
Kama kwa nje unaonekana huna hasira basi huna tatizo na hasira.
Ukijifanya huna hasira basi hasira huondoka yenyewe.
Kuwa mwema muda wote ni njia ya kuonesha kwamba hasira haiwezi kukuumiza
Ndoa yako itapata shida kama utaonesha kwamba umekasirika.

Wataalamu wa mambo ya hasira wanakiri kwamba hasira ni kitu kizuri kwenye mahusiano ya ndoa na ni kitu ambacho kipo katika ndoa zote na kwamba hasira huimarisha ndoa na huimarisha pale tu mnapotatua tatizo la hasira kwa njia ya kuelewana.
Kila mwanandoa ana haki ya kumruhusu mwenzake kuonesha hasira yake, kujieleza kwamba umekasirika na kueleza nini kimesababisha kupata hasira.
Kitu cha msingi ni wewe mwenye hasira kueleza kwa upendo, hekima na busara kwa mwenzako kwa nini umekasirika na nini kimesababisha upate hasira.
Unapopata hasira ni vizuri kuelezea hasira zako kwa maneno ya upole na kwa sauti ileile kama vile unapoongelea mambo mengine ukiwa na mpenzi wako.
Pia ni vizuri kwa mwanandoa kumsoma mwenzako mwitikio wake akiwa na hasira unatakiwa kufanya nini. Wapo ambao akiwa na hasira kaa mbali kwani baada ya muda hasira zake kuishi ndipo mnaweza kukaa na kujadili.

Kujua mwenzako amekasirika na kumruhusu kuelezea hasira zake tena kwa upole na moyo wa upendo ni vizuri kwani utakuwa mwanzo wa kujua tatizo lilikuwa ni nini hadi kupelekea yeye kukasirika na kujua tatizo ni kitu kizuri kwani utafanya juhudi kutorudia tena.

JINSI YA KUONDOA HASIRA
Kwanza ni kukubali kwamba una hasira yaani mwenzako ajue una hasira, ingawa ni rahisi sana kujua mke au mume wako sasa ana hasira.
Kwa kuwa una hasira usikubali kumaliza hasira zako kwa kuanza kumlaumu mwenzako.
Elezea kwa utulivu na upole kabisa kwa nini una hasira na kitu gani kimesababisaha upate hasira.
Jitahidi kuchukua hatua, fanya kitu ili kuondoa tatizo lililosababisha uwe na hasira.

WANAWAKE WANGEPENDA WANAUME WAYAJUE HAYA.

MAANDALIZI HUANZA TANGU NGUO ZIMEVALIWA.
Mwanaume unahitaji kuanza kumuandaa mwanamke tangu mapema (kisaokolojia) tangu asubuhi mnaamka, mchana kwa kuwasiliana, jioni kwa kuwa pamoja, then chumbani ni mahali ambapo mnamalizia mission ya siku nzima tena kwa kila mmoja kumvua mwenzake nguo (siyo lazima ila yasiwe mazoea).
Kuna raha mtu kubaki na nguo za ndani tu, na pia kuna raha kuwa naked, kila kitu kina raha yake.

KUFANYA VILEVILE NA KUACHANA NA SEHEMU ZINGINE ZA MWILI WAKE
Uwe makini kuangukia kwenye utaratibu wa ratiba ya kila siku kitu kilekile wimbo uleule, mziki ule ule na mwimbaji yuleyule.
Una mbusu, unachezea matiti kisha penetration, huna time hadi chumbani?

Ukifanya hivi kwa kuzoea basi mwanamke atajisikia bored.
Unahitaji kuwa mbunifu na mtundu kujua sehemu zingine ambazo anaweza kusisimka na ukampa utamu mpya wa tofauti.

Na kuna wengine hata kukiss hakuna kila siku yeye ni kurukia tu.

KUWA BUBU
Hata kama wewe ni bubu naturally linapokuja suala la mahaba unahitaji kuongea lugha unayoijua wewe ambayo itaonesha unampa appreciation kwa juhudi ambayo mke wako anafanya wakati wa tendo la ndoa.
Kama anakuuliza au anakuomba uwe unaongea ni vizuri sana ukawa unaongea wakati wa mahaba kwani kuna raha yake na utamu wake.
Kumbuka kwamba mwanamke kuathirika sana na maneno ambayo mwanaume anaongea ndiyo maana linapokuja suala la kudanganywa wanawake wengi (si wote) ni rahisi sana, hivyo basi mwanaume anayeongea wakati wa mahaba ana raha yake kwa mwanamke.
Ila uwe na kiasi usiwe unaongea tu kama radio.
Pia kuna wanawake huwa wanapenda kusikia dirty words na wengine hawapendi kabisa so uwe makini na mke wako kama anapenda mpe na kama hapendi achana kabisa.

KUCHEZA RAFU
Uwe mstaarabu kwani tendo la ndoa si vita.
Hakuna mwanamke anapenda matiti yake yachezewe ovyo kwa kunyumbuliwa huko na huko kama vile unataka kuyanyofoa, pia chuchu zisibonyezwe kama vile unafungua radio ya Mkulima hasa huko Iringa mchana radio huwa hazishiki sio ubonyeze tu hadi radio ikome, fanya taraatibu, pia hata kama anakuruhusu upeleke mkono wako hapo chini basi fanya kila kitu kwa uangalifu ili usimuumize.
Kama unafanya vizuri utajua na kama anahitaji mgandamizo zaidi atakwambia hata kama ni aina ya mwanamke anayependa rough sex atakwambia tu, kwani mambo ya sex ni ya ajabu sana na yana vituko vya kila aina.
Hujasikia watu wanatukana matusi mazito wakifika kileleni?
Pia wapo ambao hufanya kama vile wapo kwenye mbio za Olympic na kujaza kama vile kuna mashindano ya hydraulic mashines.
Fanya kwa taratibu na wote mtapata utamu zaidi.

KUMALIZA MAPEMA
Kama ni mwanaume ambaye unamaliza mapema ni muhimu kuchukua tahadhari na kujifunza jinsi ya kuchelewa kumaliza mapema kwani mara nyingi mwanaume akimaliza mapema mwanamke hukatizwa utamu na anakuwa hana jinsi.
Ni vizuri kutumia utundu wako kumfikisha kileleni yeye kwanza kabla yako.

KUCHELEWA KUMALIZA
Wapo wanaume ambao hubaki wamedinda masaa na wakati huohuo mke amesharidhikaka, kitu ambacho hupelekea mchezo mzima kuwa gwaride na mwanamke humalizwa energy na kuanza kutokuwa na hamu ya tendo kila akikumbuka urefu wa gwaride alilopewa.
Ni vizuri kuwa makini kusoma saikolojia na mwendo wa tendo lenyewe ili kujua gia unayotakiwa kuweka ili kufika pamoja katika kituo cha basi kinachotakiwa.

KUTOKUSHUKURU
Mwanamke anahitaji kupewa credits kwa kazi aliyofanya, unahitaji kumshukuru, sema asante kwa hudumu yake na ili uwe mwanzo wa huduma nyingine bora zaidi.
Hujasikia tendo la ndoa ni dawa, na kama ni dawa maana yake amekupa tiba ndiyo maana hata ukiwa kazini unachangamka kwa sababu unapata kitu kizuri kwa mke wako, hivyo anastahili kupewa asante.
Shukuru kwa kila jambo!

FAHAMU HAYA.

Kila Mwanamke ana ndoto za kufanikiwa maisha, kuwa na familia, kuwa na mume atakayempenda n.k

Ni hakika wanawake ni tofauti na wanaume, inawezekana hilo umelijua, kuna mambo ambayo wanaume hufanya kitandani na kumfanya mwanamke ajione ni mwenye furaha duniani na pia kuna wakati kuna mambo yanafanywa na wanaume kitandani na hupelekea mwanamke kujuta na kuumizwa hisia zake.
Mambo yafuatayo ni muhimu sana kuzingatiwa na mwanaume akiwa chumbani kwani wanawake wengi wanakiri kwamba mambo madogo kama haya wakati mwingine huwafanya kujisikia vibaya hasa linapokuja suala la mahaba.

USAFI
Kuwa msafi ni msingi wa wa mambo yote kitandani, ni vizuri kuoga kabla ya kulala hata kama kuna matatizo ya maji lazima uweke bajeti yako vizuri kuhakikisha unaoga kabla ya kurukia kitandani.
Usafi ni pamoja na sehemu zote za mwili wako, mikono safi na kucha zilizopunguzwa vizuri, pia kunyoa ndevu vizuri, kuna wakati kidevu kikigusa mwili wa mwanamke humkwaruza na kumuumiza, labda uwe na mke anayependa kidevu kama cha Osama.
Pia wapo wanaume ambao huvuta sigara na bila kuwa makini huingia chumbani na harufu ya sigara huku midomo inanuka, hapo unaharibu kila kitu.


KUWEPO
Ni vizuri kuwepo kwenye tendo lenyewe na mhusika mwenyewe kiroho, kimwili na kiakili, kama upo kwenye tendo la ndoa mwanamke hujisikia vizuri kwa kuwa utashirikiana na mwanamke kwa kila hatua na atajiona ni sehemu ya utendaji.
Tamka jina lake, tamka maneno mazuri na kuonekana upo na yeye isiwe kama vile wewe upo na mashine fulani ya kukupa raha.
Pia wapo ambao anaanza then anaacha, mwanamke ni tofauti na mwanaume hivyo basi kama utaacha ujue lazima ukaanze square one from scratch.
Pia wapo wanaume wanajua kabisa mwanamke ni umbo dogo na yeye mwanaume ni umbo kubwa, sasa ukimlalia na kuendelea na shughuli bila kujua hapo chini anaendeleaje si anaweza akashindwa hata kupumua, wewe kuwepo ni pamoja na kujua na kumsoma anauonaje muziki wenyewe.

WANAWAKE NA SEX..

Wanawake ni kama mwezi na wanaume ni kama jua.
Wanawake ni mfano wa mwezi (moon) katika mwitikio na uzoefu wa tendo la ndoa.
Wakati mwingine bila kujali ana mwenzi anayejua mapenzi (mwanaume) kiasi gani, anaandaliwa (foreplay) na kuwa hot kiasi gani au kuwa wet south pole kiasi gani, bado anaweza asifike kileleni wakati wa tendo la ndoa.
Si kwamba tu hawezi kufika kileleni, bali ahitaji kufika kileleni.

Katika siku 28 za mzunguko wa siku za mwanamke, kuna siku akiwa
AMEIVA NA KUWA TAYARI
basi hupenda na kutaka afike kileleni.

Na siku zingine katika mzunguko hupenda tu kufanya tendo la ndoa kwa ajili ya kuwa close na mume wake na wala hajali kufika kileleni au kutofika.
Wakati mwingine anakuwa katika mzunguko ambao ni full moon, wakati mwingine ni half moon na wakati mwingine ni new moon katika stages zote hizo utendaji huwa tofauti ingawa anaweza kuwa na hamu ya sex na mumewe ingawa si lazima kufika kileleni na anajisikia raha na furaha kuwa hivyo.

Kwa upande mwingine, wanaume mwitikio wao kwenye sex ni mfano wa jua kwa maana kwamba kila asubuhi huchomoza na smile la nguvu.
Hakuna nusu jua wala robo jua wala jua jipya kila siku ni jua lilelile na akisisimuliwa tu kimapenzi kileleni atafika tu.
Mwanaume akisisimuliwa, mwili wake automatically utamani kufika kileleni na hawezi Kukosa hata kimoja.
Na hapa ndipo mwanaume huwa kwenye giza nene kutojua kwa nini mamsapu wake wala hajali kufika kileleni, na anaweza kufika mbali kwa kudhani kwamba kuna mushkeli.

Tatizo kubwa ni kwamba wanaume hupima uwezo na mafanikio ya tendo la ndoa kwa mwanamke kufika kileleni.
Kumlazimisha mwanamke kufika kileleni kila kukiwa na tendo la ndoa huweza kusababisha mwanamke kujisikia haridhiki kwani inabidi wakati mwingine adanganye (fake orgasm) amefika kumbe wala na yeye alitaka sex just to feel close.

Tendo la ndoa tamu ni lile ambalo huacha hisia na kumbukumbu bila kusahaulika na wakati mwingine hufanywa kwa hiari bila kulazimisha mwanamke kufika kileleni, pia kuruhusu kila partner kupata kile anataka kwa mume kufika kileleni na mwanamke kama hana au ana mood kuweza kufika kileleni na zaidi apate physical affection.

HAWA NDIO WANAUME.

Je, Mwanamke huwa unatoa ushauri kwa mumeo baada ya kuombwa na yeye au unatoa tu kwa sababu unampenda?

Je, utajibiwa au mzee anaamua kula jiwe na kuumiza hisia zako?

Ilitokea siku moja John na Mkewe walikuwa wanaendesha gari lao kuelekea kwenye sherehe za harusi posta mpya jijini DSM.
Mzee John ndiye alikuwa anaendesha gari.
Wakati wanadhani wamefika eneo la sherehe ilidhihirika kwamba ni dhahiri walikuwa wamepotea njia.
Mara moja Mkewe akamshauri mumewe waombe msaada kwa watu wawaelekeze jengo sahihi na sehemu sahihi ya sherehe, maajabu mumewe alibakia kimya bila kuongea wala kujibu chochote.
Mzee John aliendelea kuendesha huku anatafuta jengo hadi alifanikiwa kufika na kupata jengo sahihi la sherehe.

Kihisia mkewe aliumia sana hasa kwa kitendo cha mumewe kubaki kimya na kuonesha kutomsikiliza na kumjali pale alipokuwa anamshauri watafute msaada kuulizia njia na jengo sahihi.

Kwa upande wa mke wake kitendo cha kutoa ushauri kwa mumewe ni kuonesha anampenda ndiyo maana alimshauri watafute msaada kwa watu wengine.
Na Mzee John kwa upande wake alikuwa amekwazika sana na kitendo cha mkewe kumshauri kwani mzee alihisi kama vile mke wake hamuamini na hatamfikisha kwenye sherehe. Kwake haukuwa ushauri bali Dharau na kuelezea kwamba mwanaume hawezi.

Tofauti kubwa iliyopo kati ya wanawake na wanaume ni kwamba wanaume huwa hawapendi kupewa ushauri au kushauri mtu hadi wao wenyewe waombe.
Pia wanaume wana asili ya kujitatulia Matatizo yao wenyewe isipokuwa aombe mwenyewe msaada.
Mkewe hakujua kwamba kitendo cha mumewe kupotea njia hakikumaanisha apewe ushauri bali atiwe moyo na support kwamba atapata njia na kuonesha kumpenda zaidi.

Ukweli ni kwamba mwanamke katika ndoa au mahusiano anapoamua kutoa ushauri ambao hajaombwa (unsolicited) au kujaribu kusaidia kiushauri mwanaume bila kuombwa huwa hajui ni kiasi gani huwa inachukiza sana mwanaume na matokeo yake unaweza kuona mwanaume anakujibu kwa mkato au mwanaume anakula jiwe na kukuacha umeumia hisia zako.

Unapomshauri mwanaume kwa jambo dogo kama kuendesha gari na kupotea njia mwanaume hujiona kama vile umemdharau kwa jambo dogo sana je jambo kubwa utamuamini?

Tangu kale wanaume ni mafundi, ni wataalamu, ni mashujaa, ni experts, ni watatuzi wa Matatizo sasa unapompa ushauri bila kuombwa ni kama unamfanya yeye hana lolote.

Naamini jambo la msingi ni wewe mwanamke kusoma saikolojia za mume wako na jinsi ambavyo huwa anaitikia ushauri wako, kwani kuna wakati unatakiwa kumtia moyo na kuonesha upendo kuliko kushauri au kulalamika tu kwamba hajaweza kufanya hiki na kile.

Pia kumbuka mwanaume kujiamini kwingi hutokana na mafanikio anayopata kutokana na ufanisi, uwezo na taaluma yake na kitendo cha kumshusha humuumiza sana.
Pia wanaume huwa hawapendi kuongelea kuhusu Matatizo yao hadi yeye mwenyewe akueleze na pia hupenda kutatua Matatizo kivyao kwani huamini kwamba likitokea tatizo lazima yeye ndiye atoe solution.

MAPENZI NI MATAMU LAKINI PIA NI MACHUNGU.

Ukweli Mapenzi ni Matamu na ni Machungu!

Je, umewahi kumpenda mtu kuliko maisha yako mwenyewe na ukampa kila anachohitaji lakini ukaishia kujuta kwa sababu amekusaliti na kukuumiza?
Sisi sote kwa kuwa tuna hisia tumeshapitia (au tunapitia) katika kuguswa na machungu ya aina hii.
Maisha ni kama fumbo huwezi kujua nani utakutana naye na itakuwaje, kuna watu tunakutana nao na kuachana nao baada ya siku moja, au wiki moja au mwezi mmoja au mwaka mmoja au miaka kadhaa, lakini wapo ambao tukikutana nao hugusa mioyo yetu na kujiona maisha bila wao hayana maana ndipo tunapotoa mioyo yetu na roho zetu kwao hata hivyo huishia majanga makubwa na ukichaa wa ajabu na kuumizwa kusikotamkika.
Kuna swali kubwa ambalo huulizwa na watu wengi kwamba inakuwaje watu wawili mwanaume na mwanamke ambao walikuwa wanapendana pia wakapata watoto, wakajenga maisha pamoja na kuishi pamoja lakini wakaishia katika zogo kubwa la aibu na kutukanana, kuumizana na kuaibishana hadi mahakamani kwa uadui mkubwa?
Hakuna mtu anayeingia kwenye Ndoa akitegemea ndoa kuishia njiani.
Pia hakuna mtu anayeweza kuutoa moyo wake na roho yake ili aishie mikononi mwa mtu atakayemuuumiza na kumtesa kihisia, kiakili au kimwili.
Hata hivyo hasira tunaziona, machungu tunayaona, kudanganyana tunakokuona na wakati mwingine kuuana tunakuona hutokea kwa sababu ya upendo.

Upendo ni kitu kinachofanya maisha kuwa na maana duniani.
Mapenzi ni kiini cha maana ya maisha ya dunia, upendo huweza kuhamisha milima, upendo huweza kudondosha kuta nene na ndefu kwa kuziyeyusha kama barafu.

Hata hivyo ukweli ni kwamba Love is never painless.
Hili halipingiki kwani kila unavyopenda zaidi yule mtu akikuacha basi kuumia kupo.
Wapo watu wamepitia katika kuumizwa na wapenzi wao wa mwanzo na wakipata mpenzi mpya hutoa masharti kwamba tupendane ila usije kuumiza moyo wangu.

Hicho ni kitu kisichowezekana kwani huwezi kupata upendo mkubwa ambao siku ukiachwa huwezi kuumia.
Unavyozidi kupendwa na kupenda mambo yakigeuka kuumia kupo hakukwepeki.

HUU NDIO UKWELI KUHUSU WANAUME..

Wanaume ni viumbe wa ajabu sana, atakupa raha zote na ahadi kedekede, muhimu ni kutambua je, ni tamaa au ni upendo wa kweli?

Ni vizuri wanawake wote wakajua kwamba:
Kufanya mapenzi kabla ya kuoana na mwanaume haiwezi kukusaidia yeye ku – fall in love au wewe kuwa mtu special kwake au kukuhakikisha mahusiano yanayoyumba yasimame vizuri au hata kusaidia mwanaume aji-commit kwako.

Mwanaume akiwa serious na mwanamke anayemtaka kumuoa ataweza kuvumilia sex kwa muda wowote mliokubaliana hadi ndoa.

Mwanaume anapokujia kuna mambo mawili kutoka kwake jambo la kwanza inaweza kuwa ni tamaa zake na jambo la pili ni upendo wa kweli.
Pia usichanganye hayo mambo mawili.

Kama mwanaume anakutaka kwa ajili ya tamaa zake, kitu cha maana anachokitaka kwako ni kutimiza malengo yake ya kukuchezea kwa ajili ya raha zake (sex).
hata kama atakuahidi mambo makubwa bado anakuwa lengo ni kukuchezea tu.

Kama mwanaume anakutaka kwa ajili ya upendo wa kweli, atakuwa tayari kuvumilia kukusubiri kwa sababu upendo wake ni zaidi ya sex, kwake maisha kwanza na yupo tayari kuvumilia.

Pia mwanamke kuwa bikira au mtakatifu (untouched) ni vitu ambavyo wanaume wanapenda sana, sababu ya msingi ni kwamba mwanaume akimpata mwanamke ambaye hajawahi kuwa na mwanaume mwingine hujisikia vizuri sana, anamwona ni mwanamke special na pia anampa feelings zaidi.
Hii ni kumaanisha kwamba jinsi mwanamke anavyokuwa na wanaume wengi kabla ya kuolewa hupunguza nafasi ya wanaume kujisikia vizuri kumuoa.

Njia nzuri ya kujua mwanaume anakupenda kwa upendo wa kweli uwezo wake wa kuwa serious na wewe ni jinsi anavyovumilia kuhakikisha mnaepuka sex kabla ya ndoa.

UKIWA "SINGLE" JIAMINI..

Ukijiamini una kuwa huru kimawazo na kutokuwa tegemezi kusubiri wengine wakupe furaha.
Ukiwa single unahitaji kujiamini kwani wewe mwenyewe ni chanzo cha furaha, upendo amani na maamuzi mbali mbali ya kila siku katika maisha yako.
Lakini linapokuja suala la sex wapo wanaothani kwamba kuwa na mtu ambaye una share naye mapenzi au sex unaweza kupata furaha ya kweli na na wewe kujiona mtu unayejua kutoa upendo kwa wengine.
Hii hupelekea kuwa tegemezi kimwili, hasa linapokuja suala la hisia zako na matokeo yake unakuwa target rahisi kwa partner asiye sahihi anayeweza kukuumiza moyo wako.

Kwa hiyo ufahamu na elimu ya kujiamini ni vitu muhimu sana vinavyoweza kukusaidia usiweze kupata maafa yanayoweza kukuangamiza na kuuumiza moyo wako kuuvunja vipande vipande hasa wakati huu ambapo unatafuta mwenzi wa maisha.

Kujiamini hujengwa kwa msingi wa mafanikio ya kitu kimoja kwanza.
Mafanikio huzaa mafanikio na kushindwa kuzaa kushindwa.
Tunapojifunza kitu kipya kama vile kuendesha gari mara ya kwanza huwa tunakuwa na hofu ya kushindwa na tukishaweza tunaendelea kujiamini na kuweza zaidi na zaidi..
Mafanikio madogo madogo ni ngazi za kupanda kupelekea mafanikio makubwa.
Kwa hiyo Kukosa kujiamini (self confidence) kunaweza kukufanya kuwa dhaifu katika hisia zako na maisha yako kwa ujumla.
Unahitaji kufahamu kwamba hata kama huna mwanaume au mwanamke bado maisha yanaweza kuwa ya furaha na yenye kukupa amani.

Kutojiamini kunaweza kukufanya upoteze nafasi nyingi katika maisha yako na pia Kukosa uwezo ulionao kujiendeleza na kufanya mambo makubwa katika maisha.

Tuesday 7 July 2015

NI RAHISI SANA KUIMARISHA NDOA YAKO.

ILI uwe na ndoa yenye furaha ni lazima utenge muda wa kutafakari namna ya kuiboresha na
kutafuta furaha ya ndoa hiyo. Ndugu zangu, kila kitu kinatengenezwa.

Waswahili wanasema, ukiona vyaelea, ujue vimeundwa. Huwezi kuacha mambo yakajiendesha hovyo ukategemea kuwa na ndoa bora. Uhusiano imara unakutegemea wewe.
Kila mmoja ana wajibu wa kuangalia furaha ya mwenzake. Yapo mambo mengi muhimu ambayo kama
wanandoa wakiyafanya huboresha uhusiano wao, lakini hapa nitakutajia yale muhimu zaidi.

ISHI KIRAFIKI.

Kuna baadhi ya wanandoa wakishaingia kwenye muunganiko huo, ule urafiki uliokuwa zamani wakati wa uchumba, hilo ni tatizo. Ukitaka kuwa na ndoa yenye furaha lazima umfanye mwenzi wako kama rafiki yako.Baadhi ya wanaume wana tatizo la ubabe na kujiona kuwa wao ni wanaume hivyo hawapaswi kuguswa kwa lolote.

Ndoa inageuka jeshini. Hilo ni tatizo.
Mshirikishe mwenzako kwenye mambo yako. Kuwa na kauli njema muda wote. Sikiliza shida za
mwenzako na namna ya kuzitatua.

Sikiliza pia hisia zake.Usipoishi naye kirafiki, maana yake ataogopa hata kukueleza mambo fulani ya msingi ambayo labda havutiki nayo. Ukimsogeza kama rafiki atakueleza mambo ambayo hayamfurahishi.
Mkiishi kama marafiki ni rahisi kusameheana. Ndoa nzuri ni ile yenye kusameheana ndani yake.
Kukaa na mambo moyoni husababisha mikwaruzano ya kudumu.
Kama marafiki, mtapata muda wa kushughulikia kero zenu haraka kabla hazijakua.

MIPANGO YA KIFEDHA.

Kama kuna jambo linalosabisha migongano na kupunguza uaminifu ndani ya ndoa ni suala la
fedha. Kwa bahati mbaya sana wanaume wengi ni wasiri sana kuhusu mapato yao.
Huna sababu ya kumficha mke wako kuhusu kipato chako. Mshirikishe, ajue unapata kiasi gani kwa mwezi. Labda una biashara nyingine au vyanzo mbalimbali vya mapato nje ya ajira yako ya kudumu, zungumza na mwenzako.

Ziko faida nyingi, kwanza ataona unavyomwamini na kumthamini na kumfanya sehemu ya mafanikio
ya familia, lakini pia anaweza kukushauri mambo ya msingi ambayo yatasaidia kukuza kipato
chenu.

Kubwa zaidi ni kwamba, utamfundisha namna ya kuendesha biashara zako, hata siku ikitokea
umeugua atasaidia kuimarisha biashara.

MATATIZO YA FAMILIA
Kuangalia matatizo ya pande zote mbili za familia mlizotoka, inasaidia kuimarisha mapenzi.
Mwenzako akikuambia kuhusu tatizo labda la mtoto wa dada yake, usipuuze.
Hata kama hamna fedha, unaweza kumshauri jambo zuri ambalo litamuweka vizuri kihisia.

Wengine huwa na majibu mabaya: “Kwani nimekuoa wewe au ukoo mzima?” kauli hii siyo sahihi na
hubomoa nyumba.

Kujua na kuthamini matatizo ya mwenzako ni kati ya mambo muhimu sana yanayoleta furaha kwenye ndoa. Kuwa na kauli nzuri. Kweli, inawezekana huna fedha au mipango yenu imeingiliana, isiwe tatizo.

Mjulishe mwenzako kwa lugha laini na ikiwezekana mawazo yako yanaweza kumfanya akajua mahali
pa kuanzia. Kuchukulia tatizo la mwenzako kama lako, inaongeza amani, maana anajiona sehemu
kamilifu ya muunganiko wenu wa ndoa.

Wengi hawajui hili na hata kama wanajua, hawatoi umuhimu mkubwa kwa wenzi wao. Ndoa ni tunu
rafiki zangu. Tujitahidi kuheshimu na kuzilinda kwa nguvu zetu zote.

JINSI GANI U BUSY UNAVYOWEZA KUSABABISHA UPWEKE KWA MWENZI WAKO.

Kuna ndoa ambazo ukizifuatilia zinasikitisha sana. Ni ndoa ambazo furaha imetoweka, yaani kila mmoja yuko kwenye ndoa ili mradi tu yupo lakini hatimizi yale ambayo yanatakiwa kufanywa na mwanandoa.
Upweke ni jambo linaloumiza sana hasa kwa mtu aliye kwenye ndoa.
Mapenzi si pesa, mapenzi si kumvalisha na kumlisha mkeo kila anachokitaka. Mapenzi ni ukaribu wa wewe kwake. Unatakiwa kujua kwamba, mumeo/ mkeo atajisikia faraja sana ukiwa pembeni yake pale atakapokuhitaji.
Ni jambo linaloumiza sana kwa mke kukosa muda wa kuwa na mume wake eti kisa ‘ubize’. ‘Ubize’ huu mpaka lini? Sikatai kuchakarika ndiyo maisha lakini ndiyo iwe kila siku?
Hiyo furaha ya ndoa itapatikana vipi ikiwa wanandoa wenyewe hawapati muda wa kuwa pamoja? Hili ni tatizo na kwa kweli tusipoangalia tunaweza kuwanyong’onyesha wenza wetu bila kujua na mwisho kuwafanya waumie kimoyomoyo.
Lakini cha ajabu ni kwamba, kama ilivyo kwa wanaume, wapo wanawake pia ambao wanajifanya wako bize sana na maisha kuliko kuzijali ndoa zao.
Yaani wao wanakutana na waume zao kwenye tendo la ndoa kwa masharti na tena kwa ratiba. Mapenzi gani haya? Mumeo anataka haki yake unamwambia umechoka! 
Sasa kuna faida gani ya wewe kuolewa? Kama unahisi kazi ni bora kuliko kumjali mumeo, heri uwe muwazi kwake ili aoe mwanamke mwingine atakayejali hisia zake.
Kikubwa ninachotaka kusisitiza kwenye makala haya ni kwamba, kila aliye kwenye ndoa ahakikishe anatenga muda wa kutosha wa kuwa karibu na mwenza wake bila kujali ubize unaotokana na mishemishe za kimaisha.
Hii itaimarisha ndoa na hakika kila mmoja atafurahia uwepo wa mwenzake. Tukumbuke hakuna asiyetaka mwenza wake kujishughulisha kwani maisha bila kuwa bize hayawezi kuwa mazuri lakini sasa ubize huu ukizidi kiasi cha kumfanya mwenza wako akawa mpweke, inakuwa siyo poa.

Sunday 5 July 2015

MAMBO WANAYOPENDA KUFANYIWA WANAWAKE.

Mapenzi yanataka elimu,lakini si wote wanaojielimisha namna ya kuwafanya wapenzi wao wajione kuwa ni salama na hivyo kuyafanya mapenzi yao kudumu kwa muda mrefu.Wanaume wa siku hizi wamekuwa hawafahamu ni vitu gani ambavyo wanawake wanapenda kuvipata kutoka kwao,,kushindwa kuwa na elimu hii,wanaume wengi wamejikuta wakitumia ukali kuwatawala wake zao,jambo ambalo limekuwa likizidisha migogoro ya kimapenzi.

1: KUTATULIWA MATATIZO.
Wanawake wengi hutegemea kuwa wanapokuwa na wapenzi watasaidiwa katika matatizo ya kimaisha na migogoro ya kimawazo.Mfano ushauri juu ya maisha yao,kulindwa na hatari za kimaisha,kusaidiwa katika shida na kuongozwa pale wanapohisi kushindwa kufanya jambo.Kama mwanaume hatamfanyia mpenzi wake hili,atakuwa amekosa sifa za kuteka penzi la mwanamke.

2: KUBEMBELEZWA.
Wanawake wanapenda kubembelezwa pale wanapokuwa na huzuni,wengi wao hawapendi kukaripiwa,mara nyingi hupenda kuungwa mkono wanapokuwa na misuguano na wengine,Ili mwanaume amteke kimapenzi mwanamke ni lazima awe nyuma yake hata kama atakuwa na kosa.Wanawake wengi hupenda kuelimishwa zaidi kuliko kufokewa.

3: KUWA NAMBA MOJA.
Safari ya penzi la mwanamke haliishii kwenye kumpata na kummiliki,kisha kujisahau kwa kisingizio kuwa umemuoa au umemvisha pete ya uchumba,ni zaidi ya hapo.Jambo lingine ambalo wanawake wengi uhitaji ni kuwa namba moja au kupendwa.Wanapenda watangulizwe katika mapenzi na kusiwepo na mwingine wa kuchukuwa nafasi yao katika mazungumzo na mapenzi kwa ujumla.Wanawake hawapendi kuutwa majina mabaya kwa mfano mjinga,malaya au kuwalinganisha na wanawake wenzao wabaya.

4: KURIDHISHWA KWENYE TENDO.
Hata kama utakuwa na kiwango kikubwa cha mapenzi juu ya mpenzi wako kwa kiwango gani,Ukiwa dhaifu katika tendo la ndoa utayumbisha penzi lako.Ni wajibu wa mwanaume kuhakikisha kuwa anamtosheleza mpenzi wake katika tendo hilo.Utndu unahitajika ili kumkata kiu mpenzi wako.

RAHA YA KUWA NA MWENZA .

Watu hungia kwenye uhusiano ili kupata wa kushirikiana nao katika maisha,Kubwa watu husaka watakaowapa raha na si karaha.Kama unae mwenza halafu unampa shida,tambua kuwa haupo sawa na unapaswa kubadilika haraka.

Inashangaza kuna watu wapo katika uhusianolakini kila kukicha wanachokifanya ni kutiana hasira na mambo ĺmengine ya aina hiyo.Ukweli ni kwamba wanaofanya mambo hayo wanakosea.Maana ya kuwa na mpenzi ni kwamba awe mshirika wako mkubwa katika maisha,kwamba ukilia awe anauliza jamani unalia nini? Jamani nini kinakusumbua?.Siyo unakuwa na mtu unamringia.Hapo raha ya kuwa kwenye uhusiano inapungua.Maisha yanatuhitaji wakati mwingine kuwa kama watoto wadogo.Eeh ndugu yangu usione watu wanatembea mtaani,kuna wengine sehemu zingine wanapokuwa na wenzi wao wanakuwa kama watoto.Kuna ambao husema..tata kunywa uji..” na mtu analishwa hadi anashiba.Mpe raha mwenzi wako akufurahie.
Kuna watu kwa kweli kwa namna ambavyo wanaishi ni vile tu kwamba wao si Mungu,lakini wangekuwa na uwezo wangesema huyu mwanaume/mwanamke bora afe.Hata hivyo ni vizuri kwamba kunapokuwa na migogoro kuangalia namna ya kufanya ili kuondoa tatizo ambalo liko.
Katika maisha kukwazana ni suala la kawaida japo si vizuri.Cha msingi kunapokuwa na matatizo ni kukaa chini kuzungumza ili kuondoa tatizo lililoko,si vinginevyo.Mapenzi ni kama kilimo.Mtu anapokuwa na shamba mathalani la mahindi,majani yakiwa mengi watu si huwa wanapalilia ili mahindi yastawi? Na mapenzi hivyo hivyo,lazima yapaliliwe.Ni vizuri kuangalia namna ya kufanya ili kuhakikisha unaendelea kuwa na uhusiano imara na mtu ambaye uko naye.Matatizo ni sehemu ya maisha,kama ni kuachana,utaachana na wangapi ndugu yangu?
Hata kama labda mwenzi wako anaonekana kuwa na uhusiano na mwingine,katika maisha kilicho cha msingi ni kuangalia hasa sababu ya mtu kuwa wa ovyo ni nini? Kwa nini jana alikuwa mzuri,leo amekuwa mbaya?

Raha ya mapenzi au kupenda ni nini ikiwa kwenye uhusiano hakuna amani? Ni swali ambalo baadhi ya watu wamekuwa wakijiuliza.Uhusiano unapokuwa kwenye migogoro haina maana kwamba watu waachane,bali ni suala la kawaida,lililo la msingi kama watu wazima,kuyamaliza,mwendelee na maisha.

Raha ya mapenzi ni mapenzi.Hata kama mmekasirikiana,bado mnapaswa kuelewa kwamba hata babu zetu nao walikasirikiana,lakini walivumiliana.
Raha ya mapenzi ni kutoa na kupewa kitu roho inapenda pasipo kumuumiza mwenzio kwa namna yoyote.
Raha ya mapenzi ni kuvumiliana na kusameheana.kwa maana hiyo unapaswa kufahamu kuwa katika maisha ya mapenzi hua kuna migogoro,hivyo inapotokea unatakiwa kufahamu nini cha kufanya ili kuondoa kasoro hiyo.
Raha ya mapenzi ni kuwa na mtu ambaye moyo umeridhia kuwa naye,mnaheshimiana,kila mmoja anamjali mwingine na mnashirikiana kimawazo,kimali,kiushauri na maisha mengine kwa ujumla.Zaidi ni pale mnapokuwa wakweli,wawazi,wenye kusamehe na wenye malengo sahihi na yanayoeleweka na pande zote.
Raha ya mapenzi ni kumpenda anayekuoenda na vingine vitafuata.Hilo ni la msingi,unapaswa kumpenda mtu kutoka moyoni mwako,wala si kwa kushinikizwa kwa namna au sababu zozote.
Kwa mtazamo wangu raha ya mapenzi ni kumpata akupendaye kwa dhati na umpendaye kwa dhati katika shida na raha mkipeana mapenzi ya dhati.