Tuesday 14 July 2015

HUU NDIO UKWELI KUHUSU WANAUME..

Wanaume ni viumbe wa ajabu sana, atakupa raha zote na ahadi kedekede, muhimu ni kutambua je, ni tamaa au ni upendo wa kweli?

Ni vizuri wanawake wote wakajua kwamba:
Kufanya mapenzi kabla ya kuoana na mwanaume haiwezi kukusaidia yeye ku – fall in love au wewe kuwa mtu special kwake au kukuhakikisha mahusiano yanayoyumba yasimame vizuri au hata kusaidia mwanaume aji-commit kwako.

Mwanaume akiwa serious na mwanamke anayemtaka kumuoa ataweza kuvumilia sex kwa muda wowote mliokubaliana hadi ndoa.

Mwanaume anapokujia kuna mambo mawili kutoka kwake jambo la kwanza inaweza kuwa ni tamaa zake na jambo la pili ni upendo wa kweli.
Pia usichanganye hayo mambo mawili.

Kama mwanaume anakutaka kwa ajili ya tamaa zake, kitu cha maana anachokitaka kwako ni kutimiza malengo yake ya kukuchezea kwa ajili ya raha zake (sex).
hata kama atakuahidi mambo makubwa bado anakuwa lengo ni kukuchezea tu.

Kama mwanaume anakutaka kwa ajili ya upendo wa kweli, atakuwa tayari kuvumilia kukusubiri kwa sababu upendo wake ni zaidi ya sex, kwake maisha kwanza na yupo tayari kuvumilia.

Pia mwanamke kuwa bikira au mtakatifu (untouched) ni vitu ambavyo wanaume wanapenda sana, sababu ya msingi ni kwamba mwanaume akimpata mwanamke ambaye hajawahi kuwa na mwanaume mwingine hujisikia vizuri sana, anamwona ni mwanamke special na pia anampa feelings zaidi.
Hii ni kumaanisha kwamba jinsi mwanamke anavyokuwa na wanaume wengi kabla ya kuolewa hupunguza nafasi ya wanaume kujisikia vizuri kumuoa.

Njia nzuri ya kujua mwanaume anakupenda kwa upendo wa kweli uwezo wake wa kuwa serious na wewe ni jinsi anavyovumilia kuhakikisha mnaepuka sex kabla ya ndoa.

No comments:

Post a Comment