Saturday 31 January 2015

SABABU HIZI ZINAWEZA KUSABABISHA KUACHIKA KWENYE MAPENZI.

KUPENDA SANA AU KUMGANDA MTU;

Kwenye mahusiano
mmojawapo anapokuwa anaelekea kumpenda mwenzake sana na kumganda husababisha mmoja wapo kumchoka mwenzake. Wote mkiwa kwenye mahusiano pendaneni sawa ili kutopelekea kuchokana.
Kukata tamaa kwenye mahusiano: Unapoonyesha namna ya kukata tamaa kwenye mahusiano au hali ya kusikiliza ya watu ni rahisi kupelekea mahusiano kuvunjiaka. Wengi kwenye mahusiano wanakaa kufikiria kuwa hadi kwenye ndoa. Hivyo unapokuwa na hali ya kukata tamaa kutokana na mazingira ni dhahiri kupelekea kuona bora mahusiano yaishe.
Kuwa mkali kwenye mahusiano: Hii ikiwa inawahusu zaidi wavulana/Wanaume wenye tabia hii kuwa kutokujali hali y ampenzi wako na kuwa mkali kwenye mahusiano. Kuto thamini kila hali ya shida au udhaifu wa mpenzi wako. Pia kuna wasichana/Wanawake ambao huwa na hali hii.

UTOTO KWENYE MAPENZI. Hakuna masichana anayependa mvulana ambaye ana tabia za kitoto. Kama mvulana ukiwa na tabia za kitoto kama kuto kujiheshimu au kuwa mchafu kama mtoto inapelekea kupunguza mapenzi na hata kuachika.
Mavazi na Muonekano: Hakuna mtu ambaye ni mabaya, Ila unaweza kujiona ni mbaya kutokana na muonekano wako wa mavazi na unavyo ishi. Ni vyema kujiweka nadhifu kwenye mavazi ili kuto hatarisha penzi lako.
Uchafu wa Kucha na Vidole: Shughuli unazozifanya zinaweza zikawa ni zakuchafuka ila nivyema kuhakikisha baada ya hapo unaweka vidole vyako nadhifu na visafi. Kuwa makini kuzitunza kucha maana nimahususi kwenye kuamsha hisia za ngono. Hivyo unapokuwa mchafu wa kucha na vidole mpenzi wako anaweza kuku acha na kama ni wakike, mvulana kuogopa hata chakula chako.

KUONYESHA HISIA.
Kuwa na muonekano wa hisia za kumpenda mpenzi wako ni muhimu na unaposhindwa unahatarisha mahusiano yako hata kama unampenda.
Tamaa: Kwenye mahusiano jiepushe kuwa na tamaa ya vitu vingi. Kuwa na kiasi sio kila unachokiona au kukisikia basi uhitaji. Mpenzi wako atakuona unamchuna na kukuchoka mwishowe kukutupilia mbali.

MIZOZO YA MARA KWA MARA.
Unapokuwa na mzozo au kila mara kugomba na kumpiga mpenzi wako ni dhahiri hata kama unampenda atakuwa hana uhitaji kwako tena. Jiepusha kuwa na mzozo hata kama mwenzio amekosea mrekebishe taratibu.
Heshima kwenye mapenzi ni kitu muhimu, Haijalishi hali aliyonayo. Nidhamu ni jambo linaloweza kukufikishia malengo yenu.

ZIJUE DALILI ZA UJAUZITO.

Dalili za ujauzito hutofautiana kati ya mwanamke na mwanamke, ingawa kuchelewa au kukosa hedhi ni dalili moja muhimu sana
Ni muhimu kuzitambua na kuzifahamu dalili hizi kwa sababu zinaweza kusaidia kuelezea au kutofautisha matatizo mengine mbali ya ujauzito.
Hebu sasa tuangalie dalili na ishara za Ujauzito:
>Kutokwa damu kidogo ukeni wakati kiumbe kikipandikizwa kwenye mfuko wa uzazi, ingawa siyo wanawake wote hupatwa na dalili hii
>Kukosa hedhi, hii ni moja ya dalili kubwa za ujauzito
>Maumivu ya matiti na kuvimba matiti (huweza kutokea kati ya wiki ya 1 hadi ya 2)
>Uchovu, wanawake wengi hujihisi uchovu na hali ya kutopenda kufanya lolote.
>Kupoteza ladha au kuhisi ladha ya chuma mdomoni
>Kuongezeka kwa hisia ya harufu, kipindi cha ujauzito wanawake wengi huongezeka hisia ya harufu
>Kichefuchefu na kutapika
Maumivu ya kichwa
>Kizunguzungu
>Kukojoa mara kwa mara (hasa kati ya wiki 6-8)
>Kubadilika rangi kwa ngozi inayozunguka chuchu kuwa nyeusi
>Kutamani baadhi ya vyakula na kuchukia vingine
>Kupanuka kwa mfuko wa uzazi
>Tumbo kujaa au kuvimbiwa
>Kununa na kukasirika haraka
>Kiungulila au kupata choo kigumu
>Kolostramu kuanza kutoka kwenye matiti
>Kuongezeka uzito
>Kuweza kupapasa mtoto (palpation of the baby)
>Kulainika na kuvimba kwa shingo ya uzazi (Hegars sign) - kuanzia wiki ya 6
>Shingo ya uzazi kubadilika rangi kuwa ya samawati kutokana na msongamano wa damu katika mishipa ya vena. Ishara hii huitwa pia Chadwick's sign
>Dalili nyingine ni pamoja na
>Mstari wima mweusi hutokea tumboni kuanzia chini ya kitovu (linea nigra)
>Mama kuhisi mtoto akicheza (kuanzia wiki ya 20)
>Maumivu ya mgongo hasa mimba ikishakuwa kubwa.
>Kipimo cha mimba kuwa chanya (positive).
>Kusikia mapigo ya moyo ya mtoto

MAMBO MUHIMU YANAYOMSHAWISHI NA KUMPA RAHA MWANAMKE KUFANYA NGONO.

Leo tuzitazame dalili za mwanamke anapotaka ngono.

Kwanza kabisa nikujulishe kuwa kitaalam mwanaume huwa anawaza ngono kila baada ya sekunde sita huku akiwaza mahala pa kufanyia tendo hilo wakati mwanamke huwaza ngono kila baada ya sekunde tisa na akikubali kuvua nguo ni lazima awe na sababu za msingi.

‘’Mimi sijisikii kufanya mapenzi’’ hii ni moja kati ya kauli ambazo wanaume huambiwa na ukisikia hivyo ujue si peke yako unayeambiwa hivyo na hii ni kauli inayolalamikiwa sana na wanaume wengi ambapo baadhi yao wamediriki hata kuchepuka wakidhani wenzi wao wamewachoka.

Wanawake wanapagawa na huhitaji kufanya mapenzi kuliko wanaume wengi wanavyodhani na ukijua mazingira hayo hautamwacha mwanamke wako,naye hatatamani mwingine kwasababu wanawake wanajieleza wazi kuwa katika mazingira nitakayoyataja hapa chini yakifuatwa wanajisikia raha mno…

1.      Mfurahishe
Hali yeyote ya furaha kupita kiasi inamfanya mwanamke kuwa na nafasi nzuri zaidi ya kufanya mapenzi bila kizuizi chochote.

2.     Baada ya kuzozana
Kugombana ninakozungumzia hapa ni kule kwa pande mbili mnakwazana na baadaye kila upande ukatoa dukuduku zake hata kama kwa kufikishana kwa wakubwa kwa nia ya kupata muhafaka na baada ya hapo hakuna kitu kizuri cha kubadilisha upepo huo zaidi ya kukumbatiana, kubusiana kwa huba huku mkiziamsha hisia zenu.

Ukiona hata kama mwanamke wako analia au ameghafirika kwelikweli, mwache anyamaze au mnyamazishe huku ukimbembeleza hata kumfuta machozi kisha …….hapo tatizo linaisha na wakati huo wote kwa pamoja mtafurahia tendo hilo.

3.     Siku ya 14 (Heat Period)
Wataalam husema kuwa hiki ni kipindi cha joto kwa mwanamke, ni kipindi cha aina yake katika mahusiano ambapo mwanamke anakuwa na hisia nyingi wakati mayai yanapotungwa.

Hivyo zikiwa zimepita wiki tatu baada ya kumaliza Afya yake ya ‘’uchinjaji kisha damu kukauka’’ wakati huu ni muhafaka kufanya mapenzi na hata kama mwanaume ni mbishi kiasi gani au umechoka mwanamke atakuamsha na kukutega na mara nyingine atakueleza kuwa anataka.

4.     Mapenzi ya Mbali.
Mapenzi ya mbali yanaweza kuwafanya mkawa na maisha yasiyokuwa na migogoro ya mara kwa mara huku kila mmoja akiwa anamtamani mwenzake na kitu pekee kwa wakati huu wa utandawazi kinachoweza kuwaunganisha zaidi ni simu na internet.

Mkikutana siku hiyo kila mmoja anamtamani mwenzake na kama ni asubuhi mtaona siku haiendi haraka hasa kwa wale wenye familia na kama mtakuwa wawili katika chumba ama nyumba hiyo aaaaaaahhhhh hiyo niwape hongera kwasababu hamtakawia hata sebuleni.......

5.     Wivu
Ninachozungumzia hapa si ule wivu wa kijinga bali nazungumzia wivu wa mwanamke anayejitambua na kujiamini kuwa anamtii, kumnyenyekea na kumshauri kwa hekima mwanaume wake lakini anapata wivu anapoona mwanaume huyo yupo na mwanamke mwingine hata kama si katika mahusiano. Si unajua kila mtu ana moyo wa nyama? Hasa ukipenda, weeeeeee acha tu!

Mwanamke anapoona mwanaume wake ananyemelewa na mwanamke mwingine na kumshawishi kimapenzi huona wivu sana na wanawake wanaojitambua badala ya kufoka huamua kuwaonyeshea wanaume wao kitandani kwa kuwapa mapenzi motomoto huku wakionyesha stahili na kuonyesha kujiamini kuwa ni wazuri kila upande yaani sura, maumbile na hata kitandani kuliko wale wanaomnyemelea.

Hapa siruhusu wanaume kuwa vicheche ama kuambatana na wanawake wengine bila sababu eti tu unataka mwanamke wako akuonee wivu hapana hii ni mbinu ya kuotea maana kumrusha roho mtoto wa mwanaume mwenzako si vema.

6.     Mwanamke kujinyima
Kadri mwanamke anavyozidi kukaa muda mrefu bila kufanya usodoma na ugomora, ndivyo anazidi kupata ashki ‘’Nyege’’ na mwanaume unapompata mwanamke aliyekaa muda mrefu hakika utafaidi na yeye pia atakuweka kwenye historia maana atajisikia raha sana baada ya tendo hilo.

Na mwanamke wa namna hii haitoshi kuwa mmefanya tendo la ndoa siku moja huyu atahitaji walau siku mbili vinginevyo ukimwacha atachepuka ingawa ni wachache wanaoamua kufa kisabuni na kuamua kutumia maji ya moto kujikanda.

7.     Mawazo
Mwanamke ambaye amekuwa na mawazo kwa muda mrefu akihitaji faraja na akakosa hatimaye Mungu na malaika wake wakamwangazia nuru na kujikuta mikononi mwa mwanaume anayeweza kumpa mapenzi yatakayomfariji hakika mwanamke hufurahia tendo hilo ambalo anahisi linakata kiu yake na kushusha pumzi.

8.     Mbunifu wa Mazingira
Wanaume wengi wanawanyima uhuru wa mazingira wanawake zao huku wakihoji ‘’ameyapata wapi haya’’ nakushindwa kujua kuwa huo ni moja ya mtego wa kutaka mapenzi.

Mwanamke anaweza kukutaka mfanye mapenzi jikoni, bafuni, sebuleni kwenye kiti au popote pale na kama amekupagawisha vizuri katika penzi la jikoni kuna siku mnaweza kujikuta mkiacha chakula kikiungulia huku nyie mkiwa mnatoa jasho la Afya na hapo mwanamke atafurahi kwasababu mtego wake wa kwale haujanasa chui.

9.     Muziki na Kinywaji
Kucheza muziki na wengine wale ambao wanapata kidogo kinywaji ni moja ya mambo ambayo yanasisimua mwili na kuamsha hisia za mahaba kwa mwanamke.

Hapa kwa mwanaume unaweza kumchukua mwanamke wako na kwenda naye kwenye kumbi za muziki.

Wakati mnacheza jaribu kugusana ama kupapasana taratibu hapo mwanamke yeyote mradi akikubali kupapaswa, mambo yanakuwa si mambo.

Thursday 29 January 2015

NJIA MUHIMU ZA KUSAFISHA UKE.

Awali nilikuwa nikidhani kuwa kila mwanamke anapaswa na anafahamu jinsi ya kujisafisha ndani ya uke mara tu baada ya kuondolewa bikira (kuanza mahusiano ya kimapenzi na hatimae ngono), lakini nimekuja kugundua ukweli kwamba wanawake wengi hawajui uke unasafishwa vipi?
Baadhi huofia kuwashwa na sabuni na wengine hudhani utokwaji wa utoko ni kawaida hivyo hawana budi kuacha kama ilivyo na badala yake hutumia “pads” ndogo au “wipes” zenye manukato ili kuzuia harufu/shombo ya uke na vilevile kuzuia uchafukwaji wa “vyupi” vyao.
Huitaji kuficha(Bali punguza) harufu ya asilia ya uke kwa kutumia bidhaa zenye mahukato hasa ukiwa na mpenzi wako kwani hiyo harufu ndio uanamke wenyewe na ikikutana na ile ya kiume ndio raha ya kufanya mapenzi na ikiwa mpenzi wako ni “aliyejaaliwa” atakuwa akiipenda harufu hiyo na hubaki akilini mwake hali inayoweza kumfanya akupende zaidi au kutoweza kufanya ngono na mtu mwingine bali wewe.

Hujawahi kusikia wanaume wanashindwa kutoka (date) wanawake wengine baada ya wapenzi wao kufariki dunia? Au mwanaume kushindwa kuendelea na maisha yake ya kimapenzi bila wewe na matokeo yake hata mkiachana lazima atarudi tu kwako….sababu moja wapo ni hiyo.
Kujiswafi ili kupunguza ukali wa shombo/harufu ya uanamke:
Utoko hujikusanya ikiwa mwili umetulia (usiku) hivyo hakikisha unajisafisha kila asubuhi kabla hujaanza kuoga.
Kwa wale tunaoishi Bongo wengi tunatumia maji ambayo usalama wake ni wa utata, sasa ili kuepuka maambukizo hakikisha maji ya kujisafishia sehemu zako za siri yamechemshwa vizuri. Unaweza kutenganisha maji ya kuoga na ya kusafishia uke ukitaka.
*Kabla hujaguza uke wako hakikisha umesafisha mikono yako vizuri kwa sabuni (ukiweza tumia sabuni yenye dawa) na wakati huo huo pitisha sabuni juu ya uke wako ili kuondoa vijidudu kama vilikuwepo, safisha mahali hapo(juu ya uke kwa maji na hakikisha hakuna sabuni).
*Kisha kwa kutumia kidole chako cha kati, ingiza taratibu pale ambapo uume unaingia, kwa kuanzia huitaji kwenda mbali sana. Zunguusa kidole hicho taratibu huku ukijimwagia maji kwa kutumia mkono wa pili, kisha kitoe (kitatoka na weupe mzito) safisha kidole na maji yako.
*Rudia tena na sasa kiingize ndani zaidi na ukizunguushe tena (huku ukijimwagia maji) na kukitoa utaona “utoko” mwingi zaidi kidoleni, rudia hatua hizo mpaka uhakikishe kidole kinatoka bila weupe(utoko) na utahisi hali ya usafi, hakuna utelezi.
UTOKO huwa na madhara kama
1.Kukufanya uwe unatoa harufu/shombo kali ukeni haswa wakati wa kungonoka.

2.Utoko ukibaki ukeni haswa ule wa usiku huwa una tanua kuta za misuli ya uke kwa hiyo utajikuta uke wako unakuwa karai/beseni
Ni muhimu kujiswafi
Unapojimwagia maji ukeni huku kidole kiko ndani maji huingia pia ukeni na ndio maana mwishoni kabisa utahisi umesafishika vema kabisa na utoko huo hautotoka tena siku nzima na uke wako hautokuwa na shombo kali kama ambavyo siku zote ambazo ulikuwa hujisafishi.
Kwa wale wanaotumia bath unafanya kama nilivyoeleza ila tofauti ni kuwa maji yataingia vizuri zaidi ikiwa unapata “bath” hivyo hakikisha “bath” sio ya kuchangia, maji ni salama(safi), usiweke sabuni (bath cream) au bidhaa yoyote yenye kemikali kwenye “bath” yako ili kuepuka matatizo ya kiafya na maambukizo mengine.

Tuesday 27 January 2015

JINSI YA KUMPATA MSICHANA ANAEONEKANA MGUMU.

MWANAMUME yeyote anapotaka kumtongoza mwanamke hulazimika kwanza kumwonesha – japo kwa matendo – kuwa anampenda, au kwamba amevutiwa naye, hata kama ni kimwili tu. Hatua hii ndiyo yenye changamoto kubwa zaidi kwa mwanamume, maana ndipo wakati anapokuwa anajaribu kufikisha ujumbe kwa mlengwa huku yeye mwenyewe akijihakikishia kuwa haharibu mambo.
 
Mwanamume anapokuwa anajaribu kufikisha ujumbe wa “nakupenda” kwa mwanamke, mapigo ya moyo yanaweza kumwenda mbio, hususan kama mwanamke mwenyewe anaonekana kuwa “maji marefu”. Hata hivyo, ni kazi ambayo kila mwanamume hulazimika kuifanya.

Kazi hii ya kufikisha ujumbe kwa mara ya kwanza huhitaji umakini. Bahati njema, shughuli yenyewe ina sayansi yake, ambayo ina misingi katika mahusiano ya kijamii. Ukifahamu sayansi hii inaweza kuwa rahisi zaidi kwako kufikisha ujumbe kwa mtarajiwa wako – na kufanikiwa.

1. KUKUTANISHA MACHO NI MUHIMU
Kawaida, mambo yote huanzia – na pengine kuishia – katika kukutanisha macho. Mwanamke atakapobaini kuwa hujajaribu kumwangalia japo kwa sekunde mbili mfululizo, ataondoa mawazo na hisia zake kwako hata kabla hujasema neno lolote.

Macho ndizo zana muhimu zaidi mtu anapokuwa anataka kufikisha ujumbe kwa mwenzake kuwa anampenda, au amevutiwa naye. Hii ni kwa sababu macho ndiyo vipitisho na visambazaji muhimu vya ishara baina ya mtu na mtu, hata kama si katika masuala yanayohusiana na mapenzi.

Kukutanisha macho na mtu wa jinsia nyingine unayevutiwa naye au anayevutiwa nawe ni jambo lenye nguvu za ajabu katika kuanzisha uhusiano. Kwa sababu hiyo, hata unapofanikiwa kumtazama moja kwa moja machoni mwenzako hutarajiwi kutumia zaidi ya sekunde mbili, kutokana na nguvu iliyomo katika mawasiliano haya.

Katika hili, wanaume mahiri hufahamu ni wakati gani wa kumwangalia mwanamke na ni wakati gani wa kutomwangalia. Mara nyingi, ni vizuri zaidi kumwangalia zaidi mwanamke wakati anapozungumza, huku ukikwepesha macho kidogo pale unapozungumza wewe.

2. UNATAKIWA UWIANO, UKWELI KATIKA MAZUNGUMZO
Ni jambo lisilopingika kwamba wanaume na wanawake wanatofautiana katika maana ya dhana ya mawasiliano. Hata hivyo, bado inawezekana kuendesha mazungumzo shirikishi na yenye kuburudisha ukiwa na mwanamke, bila kuonekana wa bandia.

Watu wa jinsia zote mbili wanaweza kutuhumiwa kwa kupindisha ukweli na kujaribu kuficha tabia na mienendo yao wanapozungumza na wapenzi watarajiwa. Naam, katika mazungumzo ya kwanza baina ya wapenzi au wachumba watarajiwa uwongo – ukiwemo ule usiotarajiwa – huwa mwingi.

Katika mazungumzo ya kwanza ni kawaida kwa mwanamume kubadilisha matendo yake na mtindo wake wa kuzungumza kwa maslahi ya kumpata mwanamke, jambo ambalo huifanya hulka yake ya wakati huo kuwa ya bandia. Lakini pia wasichana/wanawake husema “Nakupenda” bila kumaanisha, pengine kwa ajili ya kumfurahisha mwanamume, au kusikia mwanamume atasemaje.

Jambo la muhimu katika mazungumzo ya awali baina ya mwanamume na mwanamke ni kuepuka michezo ya kudanganyana na kukwepana, badala yake, yafanye mazungumzo kuwa rahisi na halisi. Hapo ndipo mwanamume hujitofautisha na wanaume wengine na kupendwa kwa sababu hiyo.

3. USIPUUZE NGUVU YA LUGHA YA MATENDO
Wakati mtu anapokuwa akijaribu kuwasilisha ujumbe wa “Nakupenda” kwa mwenzake, lugha ya matendo yake huzungumza kwa sauti kubwa zaidi kuliko maneno yake. Hili limeweza kuthibitishwa kwa nyakati mbalimbali kutokana na tafiti mbalimbali.

Katika muktadha wa kujaribu kufikisha ujumbe wa “Nakupenda” kwa mlengwa, lugha ya matendo ndiyo yenye nafasi kubwa zaidi. Kwa hakika, asilimia kubwa ya ujumbe unaowasilishwa kwa mlengwa huwasilishwa kwa njia ya matendo ya mwili na si maneno. Ni asilimia ndogo tu ya ujumbe inayowasilishwa kwa maneno – na wakati mwingine maneno huweza kuleta matatizo maana katika kuzungumza kuna kujikwaa kwingi, kwani ulimi hauna mfupa.

Ili uweze kufanikiwa katika kueleza nia yako kwa mwanamke, lazima ujue jinsi ya kutumia lugha ya matendo yako. Na pengine hutatumia nguvu, maana watu husema penzi kikohozi – kama unalo litaonekana tu machoni pa mlengwa.

Ukitafakari kwa makini utabaini kuwa huhitaji kusema sana ndipo uweze kupendwa, kwani maneno huchangia asilimia kidogo tu. La muhimu ni kuhakikisha kuwa mlengwa wako anakusoma na kukuelewa vizuri kwa kuangalia matendo ya mwili wako.

4. ACHA ASILI ICHUKUE MKONDO WAKE
Katika nadharia mbalimbali za kijamii na kidini ni jambo la kawaida kusikia kuwa binadamu wote ni sawa. Hata hivyo, katika muktadha wa kimapenzi, kila mtu mmoja mmoja anafahamu kabisa kuwa si kila mwanamume/mwanamke ni sawa na mwenzake.

Methali yenye asili ya kimagharibi husema “Uzuri wa mtu uko katika macho ya yule anayemtazama.” Hii ina maana pia kwamba, kila mtu anavyo vigezo vyake vya uzuri kwa kuzingatia maumbile yake. Pia jamii zinavyo vigezo vya uzuri, lakini hutangulia kwanza vigezo binafsi.

Unapokuwa umekaa na mwanamke ambaye anakuvutia kwa mwonekano wake, sauti yake na kadhalika, si rahisi sana kujizuia kuonesha kuwa anakuvutia. Hii ni kwa sababu si wewe, bali ni nafsi yako inayokusukuma. Na yeye mwenyewe atakusoma kwa kuangalia lugha ya matendo yako na kukwelewa, utakaobaki ni uamuzi wake tu.

Katika jamii kuna vigezo kuhusiana na kiuno, miguu, maziwa, makalio na kadhalika. Wengi wa wanajamii huvizingatia na kuongeza vyao. Huu ni ukweli wa kibiolojia ambao hauwezi kupingika. Mwanamke mwenye vigezo vinavyokubalika zaidi katika jamii yake atawavutia wanaume wengi zaidi. Hapa mwanamume hahitaji kutumia nguvu nyingi – asili ya maumbile itamsaidia humtambulisha mwanamke kuwa amempenda.

5. TUMIA CHANGAMOTO YA WALAKINI
Mara nyingi changamoto kubwa katika suala zima la mtu kubainisha nia yake kwa mwanamke hutokana na ukweli kwamba katika mchakato mzima huwa kuna wasiwasi na walakini. Kwa hakika, jambo hili ni la “pengine” au “labda” kutokana na kutoweza kufahamu kirahisi mwenzako anawaza nini.

Unapoonesha nia yako ya kumpenda mwanamke, ni kama unaamsha hisia zake kwako na ni kama vile unamuuliza: “Ungependa kuwa nami?” Kwa njia hii ni kama utakuwa unafungua mlango wa kupata jibu la “ndiyo” au “hapana” kwani huyo unayemwonesha kuwa unampenda na yeye ana matakwa yake na mapendeleo yake.

Kimsingi hakuna kanuni wala sheria rasmi unazopaswa kuzingatia wakati wote. La muhimu ni wewe mwenyewe kujiachia na kuingia katika maji usiyofahamu kina wala mwisho wake, bali wewe nenda na mkondo wake huku ukitarajia kuwa lolote linaweza kutokea. Hiyo ndiyo sehemu ya raha yake.

6. DHIBITI HISIA, MIHEMKO
Tofauti na mwanamke, mwanamume anayejaribu kuonesha nia yake hatakiwi kujiweka katika mkao wa mwanamitindo. Wanawake ndio hufahamika zaidi kwa mikao yao “ya kula” wanapokuwa katika mawindo (japo wengi hubisha), lakini si mwanamume. Wanawake ndio hutarajiwa kujieleza zaidi kwa njia ya matendo na mikao, lakini wanaume hutarajiwa kudhibiti hisia na mihemko yao .

Tofauti katika lugha ya matendo baina ya watu wa jinsia mbili hutokana na maumbile ya kujenetiki pamoja na utamaduni wa jamii husika. Yote yakizingatiwa, matakwa ya mwanamke ndiyo hupewa kipaumbele zaidi. Kwa ufupi, matendo ya kutongoza ya mwanamke huwa wazi zaidi, lakini mwanamume hulazimika kuficha hisia na mihemko yake.

IFAHAMU SAYANSI HII
Wajibu wa kufikisha ujumbe kwa mtu wa jinsia tofauti ni wa kila mmoja – mwanamume na mwanamke. Hata hivyo, wanaume ndio wenye jukumu kubwa zaidi la kuanzisha, kwa kuzingatia utamaduni wa jamii nyingi. Unaweza ukaona ugumu, lakini ipo sayansi itakayokusaidia. Kama una wasiwasi na uwezo wako, ni vizuri kuyazingatia yote yaliyobainishwa hapa.

Monday 26 January 2015

SIRI MUHIMU UNAZOTAKIWA KUZIJUA KUHUSU WANAWAKE.

UKWELI ambao haukwepeki kuhusu uhusiano na mapenzi ni uwepo wa furaha, amani na maelewano. Hivi ni vitu muhimu sana. Msingi wa yote ni pendo la dhati. Ikiwa wapendanao wana upendo wa kweli toka mioyoni mwao ni rahisi kutunza vitu hivyo.
Hakuna asiyependa kuwa na uhusiano wenye furaha na amani. Uhusiano wenye masikilizano huzaa matunda mema – kama ni marafiki tu, basi ujue ndoa inanukia lakini kama tayari ni wanandoa, maana yake mafanikio ndani ya nyumba yatakuwa rahisi kupatikana. katika yote hayo, inategemewa zaidi na namna wahusika wanavyoendesha uhusiano wao; kwa maana kwamba, yote yanahitaji ushirikiano wa wote. Hapo ndipo mwanzo wa matatizo. Wenzi wawili huwa na tofauti za hulka.

Kwa wanawake, wengi hupenda sana kufuatilia na kuhakikisha uhusiano unakuwa imara. Likitokea tatizo, mwanamke huwa mstari wa mbele kulishughulikia ili mambo yaishe. Wanawake wengi hawapendi kuwa wamewaudhi wenzi wao.
Ikitokea wakiona kuna tofauti ya kimawasiliano, mara moja husaka mbinu za kutatua na kubakisha uhusiano ukiwa kwenye hali nzuri. Hiyo ni tofauti na wanaume ambao mara nyingi wao ni watu wa harakaharaka.

Ni wepesi wa kusahau mambo au kuyachukulia kwa wepesi. Mfano, mwanamke wake akikasirishwa na jambo fulani, ni rahisi tu kuishia kusema: samahani. Wakati mwingine anaweza asiseme kabisa, akijua mambo yameshaisha. Wanawake ni tofauti. Wanafanya mambo yao kwa taratibu sana. Hasira zao zinachelewa kuisha, lakini ni rahisi zaidi kuzimaliza kwa kumwambia tu: nakupenda mpenzi, najua nimekosea, samahani mama.

Ni sentesi fupi sana lakini kwao ina maana na thamani kubwa sana. Mapenzi ni sawa na bustani, wakati mwingine inahitaji kumwagiliwa na kuwekewa mbolea. Kama ni kweli unampenda, tuliza akili na muda wako kuhakikisha furaha yake inaendelea kuwepo.

Inamaanisha kuwa, upendo wake kwako ukitamalaki muda wote – mafanikio ya kazi ya mikono yako yapo jirani tu. Mfanye mwanamke wako atabasamu. Pamoja na ubize wako, tenga nafasi kidogo kwa ajili yake.

MSAMAHA SI KUJISHUSHA!

Wanaume wengi wanaamini kumwambia mwanamke samahani ni kujishusha na kuwa chini yake, si hisia sahihi. Msamaha ni uungwana. Kama kweli unampenda kwa dhati, una shaka gani kumwambia akusamehe ili uhusiano uendelee kuwa wenye nguvu?

Hutapungua mahali popote kukubali kosa, ikiwa umekosea au kumrekebisha mwenzako badala ya kubaki bubu huku ukiwa umenuna na kusitisha baadhi ya huduma. Kama ilivyo kwako, tambua kuwa mwanamke naye ni binadamu, anaweza kufanya makosa lakini asijue!

Kumwambia kwa upole ni jambo zuri. Atakusikiliza, atakuelewa na atajirekebisha alipokosea. Kukaa nalo moyoni hakuna maana.

PUNGUZA UBABE.

Wapo baadhi ya marafiki wanaamini kuwa ubabe ni sehemu ya ukamilifu wa uanaume. Siyo kweli. Huna sababu ya kuwa mkali sana au mwenye amri muda wote. Mwanamke anahitaji kubembelezwa, upendo na kuonyeshwa namna anavyothaminiwa.

Wengine wana tabia ya kuwapiga wenzi wao, kitu kidogo tu, tayari kipigo. Vipi akikutana na mkarimu, asiyepiga na anayebembeleza? Akiachana na wewe utamlaumu nani? Ni kweli kuna wakati mwanamke anahitajika kukaripiwa akikosea, lakini si sawa kuwa mkali kupitiliza wakati wote.


Sunday 25 January 2015

ETI UKIMPA MPENZI WAKO KINYUME NA MAUMBILE NDIO ATAKUPENDA DAIMA?

Kuna siri moja ambayo nahisi ipo kwa wanawake wengi walio kwenye ndoa na hata wale walio kwenye uhusiano wa kawaida kwamba, wanafikia hatua ya kutoa aina hiyo ya penzi eti ili wapenzi wao wasiwasaliti. Jamani hii inaingia akilini kweli?

Unafikia hatua ya kuhatarisha maisha yako kisa unataka kukamilisha ile sentesi ya kwamba unampa mumeo kila anachokitaka? Huo ni ulimbukeni na kama wapo wanaoendelea kufanya hivyo, wanajitafutia matatizo yatakayowafanya waje kujuta baadaye.

Ni kweli washauri wa masuala ya mapenzi wanaeleza kuwa, ili uweze kumshika vilivyo mpenzi wako unatakiwa kuhakikisha unampatiliza katika kila anachokitaka lakini hawakuzungumzia ishu ya wewe kukubali mapenzi kinyume na maumbile. Hawakurusu hilo kwa kuwa wanajua madhara ya kufanya hivyo. Sasa iweje leo ukubali kufanya dhambi hiyo eti kwa kuwa mpenzi wako kataka na unampenda?
Katika ulimwengu wa sasa wapo wanaume wa ajabu sana. Hawa ni wale ambao si wastaarabu. Wao hawaangalii madhara yanayoweza kuwapata wenzao bali wanaangalia kujifurahisha wao tu. Mbaya zaidi baadhi ya wanawake nao wamekuwa mbumbumbu.
Eti kwa kuogopa kuachwa au kusalitiwa wanasema bora wafanye hivyo. Jamani, ifike wakati tufikirie kila tunalolifanya katika maisha yetu ya kila siku. Zipo mbinu nyingi za kumridhisha mpenzi wako na wala asifikirie kukuacha wala kukusaliti bila hata kumkubalia afanye hivyo.
Pia unatakiwa kufahamu kwamba, unaweza kumpa mpenzi/mume wako mapenzi hayo lakini bado akakusaliti tu. Sasa kwa nini ujidhalilishe?

Ni kamchezo ka’ nyumba ndogo

Ukijaribu kuchunguza utabaini kuwa wanaoongoza kwa mchezo huo mchafu ni wale wezi wa mapenzi ambao hufahamika kwa jina la nyumba ndogo.
Hawa eti wanatumia mbinu hiyo kuwashika waume za watu. Kimsingi hii ni aibu na wanaokubali kufanyiwa hivyo wanajidhalilisha na hawawezi kudumu na wanaume wao.

Usithubutu kabisa

Mapenzi kinyume na maumbile licha ya kwamba yamekatazwa hata na vitabu vitakatifu, madhara yake kiafya pia ni makubwa. Wapo wengi ambao sasa wanajuta kwa kufanya mchezo huo kutokana na kupata matatizo wakati wa kujifungua lakini pia wengi wao imekuwa ni rahisi kuambukizwa magonjwa mbalimbali ya zinaa ukiwemo Ukimwi.

Ni laana

Wanaofanya hivyo wamelaaniwa na wanaweza kushangaa uhusiano wao unakumbwa na matatizo kisha kusambaratika kwani Mungu hawezi kuubariki ule unaokwenda kinyume na maagizo yake.
Ni suala tu la kukaa na kujiuliza, wewe mwanamke unapata raha gani kufanya mapenzi kwa njia ambayo haijaruhusiwa? Wakati mwingine nashindwa hata kuwaelewa hawa wanaofikia hatua ya kujisifia kuwa eti wanawaachia waume zao ‘wajisevie’ wanachotaka kwa kuwa wanawapenda.
Hivi watakuwa na akili timamu? Kumpenda mtu ndiyo uwe tayari kuhatarisha maisha yako kiasi hicho? Tena kwa taarifa yako wale wanaowakubalia wapenzi wao mapenzi kunyume na maumbile wanaonekana wajinga na wanadharaulika. Hakuna mwanaume anayeweza kumheshimu mwanamke anayeweza kuuweka rehani mwili wake kwa njia hiyo.
Nimalizie makala haya kwa kusema kuwa, kanuni ya kwamba unatakiwa kuhakikisha unampatia mpenzi wako kile anachokipenda inabaki palepale lakini umkubalie katika yake yasiyo na madhara kwako. Yale ambayo unaona yatakuletea matatizo, mkatalie kwa kumpa sababu za msingi. Kama ni muelewa atakuelewa, asipokuelewa kuwa tayari akuache lakini usihatarishe maisha yako.

Saturday 24 January 2015

SIMU ZINAVYOHARIBU MAHUSIANO

Mwanaume hata mwanamke ukiona simu yake ina password au anaichunga sana hata akiwa nyumbani, ujue hapo hakuna uaminifu.
Kama nilivyoizungumzia simu wiki jana kuwa makusudia ya mtu aliyeitengeneza kusudio lake kubwa lilikuwa kurahisisha mawasiliano si kingine. Lakini wanadamu wenye mioyo dhaifu tumeitumia kama kichaka cha kuficha maovu yetu.
Sasa hivi ndani ya nyumba simu imekuwa chanzo cha kuvunjika kwa amani, asiye muaminifu uilinda simu yake kama ikulu ya Barack Obama.
Sasa hivi ndani ya nyumba zetu inaonyesha jinsi gani zimepoteza uaminifu kila mmoja analinda simu yake kuliko hata wivu kwa mwenzake.
Imekuwa kila mmoja anamwinda mwenzake alale ili aipekue simu, kwa vile ni mzoefu hata ukibahatika kuipata utakuta uchafu wake amefuta ili kupoteza ushahidi.
Ukiona hivyo mnakuwa mnaishi kwa mazoea lakini fahamu hakuna upendo ndani ya nyumba yenu na kuvunja ile ahadi ya kuishi kwa upendo na uaminifu katika ndoa.
Unaweka password unamuonyesha nini mwenzako? kama mwanaume unamuonyesha kabisa mkeo kwamba una wengine zaidi yake hapo unamfundisha nini mkeo, akilipa kisasi umlaumu nani?
Nimekuwa nikisema kila siku kuhusu uaminifu ili tuangalie unachokifanya ni sahihi na ndiyo mapenzi?
Nilielezea mapenzi ni kupendana kuheshimiana kuoneana huruma kujaliana na uvumilivu.
Nilielezea mapenzi ni kupendana, kuheshimiana, kuoneana huruma, kujaliana na kuvumiliana. Ukiwa na mapenzi lazima utakuwa na vitu hivi kwa mwenzako, pia utakuwa muwazi kwake na mkweli ili kufanya muweze kuishi bila mmoja kuwa na mashaka na mwenzake.
Wapendanao siku zote hulinda heshima yao kwa kila mmoja kuilinda ya mwenzake, pia kuwa wawazi ili chochote kitakachokwenda kinyume, kiulizwe na kupatiwa majibu sahihi bila kujiumauma. Pia huwa hawana mipaka kuanzia katika miili yao na vitu vyote kwa vile huamini wao ni kitu kimoja, hivyo hawafichani kitu.
Watu kama hawa simu si chanzo cha matatizo, bali ni chombo cha mawasiliano, hakuna mtu wa kuificha simu yake wala kuweka password na kila mmoja ana uhuru wa kuishika au kuopokea ya mwenzake.
Nina imani somo langu limesomeka vizuri, sasa tunarudi kwenye mada ya leo kwa kuuliza swali, sifa nilizozieleza kuhusu mapenzi, je, wewe unazo au mwenzako anazo? Je, simu katika nyumba yenu inatumikaje? Ni chanzo cha migogoro au ni chombo cha mawasiliano ambacho kinaachwa popote bila masharti yoyote?
Tutumie simu kama chombo cha mawasiliano, hata kama si muaminifu katika uhusiano, si lazima mwenzako ajue jinsi gani unavyomdharau kupitia simu.
Simu isiwe chanzo cha migogoro na kuvunja nyumba zetu ambazo sasa hivi zimeingia mdudu ambaye ameonyesha jinsi gani tusivyo waaminifu, kitu ambacho kimeongeza ukosefu wa amani katika ndoa zetu.
Tuwe wawazi na wakweli kwa wenzetu, tuone aibu kuonyesha kwa vitendo sisi si waaminifu. Kama ulijua wazuri kuliko mwenzako wapo wengi, ulikaa naye kwa sababu gani?

KUACHANA SI UAMUZI WAHARAKA,INAHITAJI UMAKINI KUAMUA.

Upo uhusiano ambao umelengwa kudumu, hasa kwa wanandoa.  Kuna wengine hawana sura ya kudumu, wapo kwa muda kwa kuzingatia mazingira pamoja na kile kilichomo ndani ya nafsi zao.

Unaweza kujiuliza; Kwa nini ufike wakati utake kuvunja uhusiano wako na mwenzako? Iwe wa kirafiki au kimapenzi, Ipo wazi kwamba kuna sababu mbalimbali zinazoweza kuwafanya wahusika kuamua.

Yawezekana uhusiano wako na mpenzi au rafiki yako wa jinsia tofauti unakutia hasara, au unakuharibia biashara, au unakupunguzia heshima katika jamii, au pengine uaminifu wako kazini. 

Mathalan, mpenzi wako anafahamika kuwa ni kahaba. Inawezekana uhusiano wako na mwenzako unaidhuru nafsi yako. Mfano, mwenzio ana nguvu sana juu yako kiasi kwamba huwezi kusema “hapana” kwa lolote analokwambia. 

Pengine kutokana na hali hiyo umekuwa ukilazimika kufanya mambo ambayo huyapendi na ambayo hayaendani na maadili.

Lakini pia yawezekana umeanza kumchukia mwenzako.  Mazingira yamebadilika, kwa hiyo wewe na yeye hampatani tena. Unajitazama na kugundua kwamba ulivyo huendani naye. Ni matokeo ya kuchokana!

Uhusiano wowote unapoyumba, uwe wa kirafiki au kimapenzi, huwaweka wahusika katika wakati mgumu kiasi kwamba ni lazima mmoja achukue hatua ili aweze kuishi kwa amani na furaha ya kweli.

Hata hivyo, ikae akilini kwamba inauma mno kuachana na mtu unayempenda!
Kumaliza uhusiano wa kimapenzi au kirafiki si hatari, lakini la msingi ni kuhakikisha kuwa unamwacha mwenzako akiwa hajaathirika kisaikolojia kwa namna yoyote. 
Kwa sababu hiyo unapaswa kujifunza njia sahihi za kumaliza uhusiano wako na mwenzako inapobidi.

Kuna jamii inaweza kuthubutu kusema, unapochoshwa na mtu, mchukue uende naye mahali kisha umueleze kwa uwazi kuwa hutaki tena kujihusisha naye kwa sababu moja, mbili, tatu. 
Hata hivyo, hilo si jambo rahisi kwa wengi. Badala ya kukabiliana na mtu ana kwa ana na kumweleza kuwa humhitaji tena, zipo njia za kirafiki ambazo unaweza kuzitumia bila kusababisha matatizo yoyote ya kisaikolojia.



ANDAA SABABU ZAKO!
Unapotaka kumbwaga rafiki yako au mpenzi wako ambaye hujampa ahadi yoyote ya kuishi naye katika ndoa, anza mchakato kwa kuweka bayana sababu zinazokufanya utake kuachana naye. 
Hakikisha kuwa sababu unazoziweka ni zile ambazo mpenzi wako huyo hatapata namna ya kuzipinga.

Zitengeneze sababu hizo kwa kuzingatia mtazamo wako mwenyewe, na si wa kwake ili hatimaye kusiwe na mwanya kwamba atajirekebisha na mtaendelea kuwa pamoja.
Namna hii utakuwa unayaangalia zaidi maslahi yako mwenyewe na iwapo utalazimika kumweleza mwenzako ni kwa nini unataka kumaliza uhusiano wako na yeye, sababu zako hazitaonekana kama shambulio kwake wala tabia yake.

USITHUBUTU KUWASILIANA NAYE!
Utakapokuwa umeweka wazi sababu zako na kuziamini, weka mkakati kuwa hutaanzisha tena mawasiliano na mwenzako.

Jiwekee msimamo kuwa hutampigia simu, wala kumtumia  ujumbe wa simu, wala barua pepe na kadhalika, ila utajibu tu yeye atakapoanzisha.

HAYA YATAKUFANYA UDUMU NA MPENZI WAKO.

Kwanza kabisa, napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wote ambao mmekuwa mkiwasiliana nami kwa njia ya simu na kunipongeza, kunikosoa na kuuliza maswali kuhusu mambo mbalimbali yanayowakabili katika uhusiano. Kufanya kwenu hivyo kunanipa moyo kwamba, ujumbe unawafikia vilivyo.

Sasa twende moja kwa moja kwenye mada yenyewe. Nazungumzia juu ya mambo ya kuzingatia kama unahitaji kudumu katika uhusiano ulionao. Hapa naomba nizungumze na wanawake zaidi. Nasema hivyo kwa sababu wao ndiyo wanaokumbana zaidi na matatizo ya kuachwa na wapenzi wao kuliko wanaume.

Ni sahihi kusema, wanawake ndiyo huumizwa zaidi katika mapenzi kuliko wanaume. Hii ni kutokana na sababu kubwa mbili; kwa kawaida wao ndiyo hufuatwa na kutongozwa na wanaume, lakini lingine ni kwamba, mara nyingi wanaume ndiyo hutoa uamuzi wa kuacha au kuachana.

Kwa sababu hizo, hakuna ubishi kuwa wanawake ndiyo welengwa wakubwa wa mada hii. Rafiki zangu, kuna mambo kadha wa kadha ambayo yanaweza kusababisha uhusiano kuwa butu na baadaye kuishia njiani.

TAMBUA THAMANI YAKO
Ili uweze kuwa bora ni lazima uanzie kwako, ujitambue kama mwanamke na thamani yako kwa mwanaume wako.  Ukiijua thamani yako, lazima utakuwa makini na kila kitu. Rafiki yangu, ninaposema thamani ninamaanisha kwanza kujiamini na kujipa nafasi ya kwanza.

Uamini kwamba wewe ni mwanamke mrembo na unayevutia. Imani hiyo ikishaingia, tayari utakuwa unajali mambo mengi ya msingi, ikiwemo usafi wako binafsi. Waswahili wanasema, mwanamke ni pambo la nyumba. Pambo haina maana ya ua, inamaanisha ule usafi wa kila kitu.

Kwamba nyumba bila mwanamke haiwezi kukamilika, wewe kama mwanamke unatakiwa kufahamu wewe ni kila kitu ndani ya nyumba. Umakini wako na kujitambua ndiyo vitu vitakavyokuweka katika nafasi nzuri ya kudumu katika uhusiano wako na baadaye kuingia kwenye ndoa.

TAMBUA THAMANI YAKE
Ukiijua thamani ya mwanaume kutoka ndani ya moyo wako ni wazi kwamba hata vipengele vifuatavyo hapa chini havitakuwa vigumu kwako kutekelezeka. Inakupasa ujue thamani ya mwanaume wako ipasavyo.

Hilo si tu kwa maneno, bali ni jambo ambalo linatakiwa kufanyika kwa ridhaa ya moyo wako. Ni rahisi zaidi jambo hili kufanyika ikiwa utakuwa na mapenzi ya dhati. Mpende kwa moyo wako wote na ujue kuwa maisha yako yanakamilishwa na uwepo wake.

Ndiyo! Yanakamilishwa na uwepo wake, maana una mategemeo ya kuingia katika ndoa naye. Hapo mtakuwa mwili mmoja na maisha ya kila mmoja yatamtegemea mwenzake.

MHESHIMU
Mwanaume anapenda sana kuheshimiwa na mpenzi wake. Mwanaume akigundua haheshimiwi au unafanya hivyo kwa kumridhisha tu na si kutoka moyoni, ni rahisi kukuacha.

Kama kichwa cha familia, lazima apewe nafasi ya kutoa uamuzi tangu mapema. Ikiwa utakuwa na majibu mabaya kwake, humheshimu ni wazi kwamba atakuacha mapema, maana utakuwa umepoteza sifa za kuwa mama wa familia.

Friday 23 January 2015

HIZI NDIO NJIA 5 ZA KUPUNGUZA TUMBO KIRAHISI.

WADADA au WAMAWAKE wengi wanatamani kuwa na matumbo madogo, lakini wengi hushindwa kufikia ndoto hiyo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za uzazi na kupenda chakula. Makala hii inaangalia njia rahisi ya kupunguza tumbo.

1. Uangalifu katika kula
Epuka chakula chenye wanga, mafuta mengi na sukari. Badala yake unaweza kula matunda na mboga za majani. Vile vile samaki wa baharini si wabaya kwani hawana mafuta mengi.

2. Namna ya kula
Usiache kula kwani jambo hilo litakunyima nguvu, unatakiwa kula milo mitatu mpaka minne lakini kwa kiasi kidogo. Unatakiwa kukaa zaidi ya saa tatu kabla ya kula mlo mwingine.

3. Mazoezi ya kawaida
Si lazima ufanye mazoezi makali kwa ajili ya kupunguza tumbo. Unaweza kufanya zoezi la kutembea badala ya kupanda basi, kama hufiki mbali sana. Kama unaweza kuogelea, unaweza kufanya hivyo mara kwa mara, hiyo pia itakusaidia.

4. Zoezi maalum
Kama unaweza kufanya zoezi la kulala chali na kukaa, 'abs exercise' unaweza kufanya kwa dakika chache kila siku. Hiyo itasaidia kukomaza misuli ya tumbo hivyo tumbo kutokulegea.

5. Kunywa maji
Maji yanasaidia mmeng'enyo wa chakula, hilo husaidia mtu kuwa na afya njema. Kwa kuwa mtu akiwa katika hatua za awali za kupunguza tumbo husikia njaa mara kwa mara, ni bora anywe maji badala ya kula.

MADHAIFU 5 YANAYODIDIMIZA MAHUSIANO.

1. Mchanganyiko mkubwa kuhusu maana yamahusiano, mapenzi na ndoa: Labdakipengele hiki tuanze kwa kueleza kuwa kunaweza kuwepo ndoa, lakini yasiwepomahusiano... wala mapenzi. Inaweza kuonekana kama inachanganya kidogo, lakini ndioukweli wenyewe. Ndoa ni namna tuu ambayowawili walio kwenye
mahusiano wanaamua kuwataarifu rasmi watu wengine kuwa waowapo rasmi katika mahusiano. Ndoa ni kiapo mbele ya watu wengine , na ni namnaya kutaka kumuhakikishia mwenza wako kuwa endapo kiapo hicho kitatokeakuvunjika, basi unakubali rasmi kuwajibika kwa mujibu wa taratibu zilizopo zandoa husika, ikiwemo kukubali kuitwa kwenye mabaraza ya usuluhishi, kugawanamali, n.k. Na kwa upande wa kiroho, inabeba maana zaidi kuwa unaweka kiapo kwaMungu wako kuwa utalinda mahusiano yako na huyo unayemchagua. Hivyobasi, ndoa haijengi mahusiano wala mapenzi.
Kiuhalisi inabidi kwanza yawepomahusiano na mapenzi kisha ndio kiapo kifanyike, kwani kinyume
cha hivyo nikuwa unakula kiapo 'feki'. Ndiomaana basi, ni muhimu kwa wapenzi kutambua kweli kama wanahitajiana, kuwakwenye mahusiano na kutafakari kwa uhuru kama kweli wanataka kuweka kiapo rasmicha kuwa pamoja. Kutumiandoa kama kinga ya kuhakikisha mahusiano yako yanadumu ni maamuzi magumu ambayopengine yanaweza yasilete faida hapo baadae.

2.Mahusiano na ndoa nyingi huyumbishwa naMatarajio yasiyo halisi Kablahata ya kuingia katika mahusiano na hatimaye ndoa wengi wetu huwa na matarajiobinafsi ya kimaisha. Matarajio haya yanajumuisha vile tunavyotaka sie wenyewekuwa hapo baadae, pamoja na matarajio ya vile tunavyotaka wenza wetu wawe. Hatahivyo katika hali
halisi tunajikuta sisi wenyewe hatuwezi kujibadilisha aukujiweka kwa usahihi vile tunavyotamani kuwa (kwa sababu kwa kila tunachojaribukufanya kuwa bora, tunajikuta bado tuna madhaifu mawili matatu). Pamoja naukweli huu, tunajikuta tupo na matarajio ya kuwafanya wenza wetu wawe watu waaina fulani. Kwakuwa kiasili binadamu ni kiumbe huru, tunajikuta wenza
wetu naowakiwa 'busy' kutimiza ndoto za vile wanavyotamani kuwa iwe kimavazi, aina yamarafiki,
utafutaji wa kazi , kujiendeleza kimasomo, aina ya mali za kununua,hata kufikiria tofauti aina ya maisha wanayotaka muishi. Matokeoyake ukinzani huu wa matarajio ni mkanganyiko wa mgongano wa mawazo kati yawawili nyie, na mwanzo wa vita ya chini kwa chini ya nguvu ya maamuzi katikamahusiano yenu.

3. Kuweza kumbadili tabia mwenza wako Mojawapoya jambo ambalo hufanywa na wengi walio katika mahusiano ni kuwa na 'tamaa' yakutaka kumbadili tabia fulani mwenza wake. Hata hivyo 'tamaa' hii ni sehemu yayale tunayoyaita matarajio yasiyo halisi, kwani tabia ya mtu hujengwa na mambomengi sana, ikijumuisha aina ya makuzi, aina ya mfumo wa imani mtu anaouamini,aina ya marafiki alio nao, uwezo wake wa kujiamini katika kubadili tabia kwaniwengine wameshakata tamaa kuwa hawawezi kukata tamaa, na zaidi sana, mabadilikoya tabia huhitaji mfumo endelevu na wenye kusoma vema asili ya tabia ili kuwezakuirekebisha. Hatahivyo wengi wetu kwenye mahusiano, hutegemea 'mapenzi'au vitisho tuu kama
vile'nitakuacha mie ', kama sababu yakumfanya mtu abadilike kitabia.Udhaifu wetu katika kutambua asili
ya tabia yamtu husika na mbinu za kisayansi za kubadili tabia hufanya zoezi lakubadilishana tabia kuwa gumu na pengine lisilowezakana.

4. Kuvumilia ndio kuonyesha upendo na ndiokudumisha mahusiano Hiini aina nyingine ya matarajio ambayo sio halisi kwani kiukweli kila mtu analojukumu la kufanya bidii kuwa mtu mwema, hivyo hauhitaji kubeba 'uzembe' wamwingine kwa kisingizio tuu cha kuwa unaonyesha upendo hususani pale ambapo nikwa
uzembe tuu au kutokujali kwake mwenza husika amefanya jambo fulani. Kwajinsi kasumba hii ilivyo enea sio ajabu kukuta mtu akifanya mambo mabaya kwamwenza wake kwa makusudi ili tuu eti apime kama kweli mwenza wake ni mvumilivu. Kumbukahapa hatumaanishi kuwa kusamehe ni kosa. Hapana, kusameheana ni muhimu, lakinisio kwamba ni muhimu tuu katika mapenzi. Kusameheana ni jambo la asili, natunapaswa
kusameheana kwa mambo mengi nje hata ya mahusiano.
Tunachosemani kuwa kuna kasumba ya baadhi yetukuona kuwa wanayo 'haki' ya msingi ya kukosea eti tuu kwakuwa tuu mwenza wakeanalazimika kusamehe ili kuonyesha kweli anao upendo wa dhati. Amini usiamini, kasumba hii ya kutarajia ainaya pekee ya kusamehewa na kuvumiliwa kwa kisingizio tuu cha kuwa upo kwenyemapenzi namwenza wako, hurudisha nyuma maendeleo ya mahusiano yenu kwanimwenzi wako nae ni binadamu na kumbuka anayo matarajio mengine ya maisha,isitoshe na yeye anahitaji upendo na
kujaliwa na wewe, hivyo kutarajia kwakokusamehewa na kuvumiliwa kuna mnyima haki mwenza wako. Hatimaye kutegema kwakokusamehewa kila wakati, kunamfanya mwenza wako atilie mashaka upendo wakokwake.

5. Uaminifu = Upendo= Kudumu kwa mahusiano Pamojana ukweli kuwa mwenza wako anatarajia utakuwa muanifu kwake, elewa kuwa kuwamwaminifu pekee katika mahusiano yako sio tiketi ya kudumu kwa mahusiano yenukwakuwa watu wanaingia kwenye mahusiano sio tuu kwa kuwa wanataka kuwa na mtummoja muaminifu bali wana mahitaji mengine wanayohitaji. Zungumzana mwenza wako, fanya utafiti wako binafsi kuhusu mpenzi wako ujue mambomengine anayohitaji toka kwako. Pia msikilize anapokutaka urekebishe mambokadhaa au ufanye mambo fulani. Inapendeza pale unapomfanyia mtu
mamboyanayompendezesha kwa kuwa hivyo ndivyo anavyotaka, sio kwakuwa tuu weweunadhani kufanya hivyo kutampendezesha mhusika.

NAMNA YA KUJUA KAMA UMEMRIDHISHA MWENZI WAKO.

Leo nitawaelezea kidogo namna ya kujua kama umemkuna ipasavyo mwanamke wakati wa tendo la ndoa.

1.Kufinya shuka kwa nguvu au kitanda kwa nguvu wakati unampa mambo
ni ishara mojawapo ya
kuonyesha kwamba inamkuna vizuri.

2.Kukukumbatia kwa nguvu au kukufinya:
Hii pia ni moja kati ya ishara nyingi anazoonyesha
mwanamke pindi anapo
- vizuri.

3.Kutokwa na jasho ndani ya
sekunde chache:
Ukiona anatokwa na jasho ndani ya sekunde chache na katika hali isiyo ya kawaida basi jua kua utendaji wako ni mzuri na
unamridhisha.
Acha niishie hapo kwa leo, lakini sina maana kwamba kama mwanamke wako haonyeshi moja kati ya ishara hizo au zote
basi ndio inamaanisha
haumridhishi, hapana. Hizi ni baadhi tu, zipo nyingi tu.

HAYA NI MUHIMU KUFANYA MNAPOMALIZA TENDO LA NDOA.

Labda kwa wale wasiofahamu niwaambie tu kwamba dhana ya mapenzi ni dhana yenye wigo mpana sana na ndiyo maana hutasikia hata siku moja tumepumzika kuizungumzia.
 
Hata hivyo, tunachofanya siku zote ni kukumbushana kwa yale tunayoyafahamu na kushauriana kwa pale tunapohisi wengi hufanya makosa.
 
Baada ya kusema hayo sasa nigeukie mada yangu ya leo ambayo kwa kiasi kikubwa inawahusu wale walio kwenye ndoa na kikubwa nazungumzia yale ambayo wawili waliotokea kupendana kwa dhati wanatakiwa kuyafanya mara baada ya kumaliza kufanya tendo la ndoa.

Nalazimika kuandika makala haya baada ya kubaini kuwa wengi wamekuwa wakifanya makosa na kujikuta wakishamaliza kufanya tendo hilo takatifu, kila mmoja anageukie kwake kisha kuuchapa usingizi.
 
Sisemi kwamba ni lazima kuyafanya haya nitakayoyaeleza leo ila 
yakifanywa huwa na manufaa yake na mara nyingi yanaboresha uhusiano.
 
Kuoga pamoja

Mtakuwa ni watu wa ajabu kama mtamaliza kufanya tendo hilo kisha kila mmoja kulala na majasho yake. Wapowasiojali katika hili na kuona kuoga au kutooga ni uamuzi wa mtu. Elewa linapokuja suala la usafi inashauriwa mkimaliza lazima muoge.
 
Wapo wanawake ambao wakishamaliza hukimbilia kuwaandalia maji wenza wao, wakishaoga ndipo nawo huenda kuoga. Hivi unaona ugumu gani kwenda kuoga na mwenza wako? Unaijua raha ya kuoga na huyo wako wa maisha?
 
Wanaofanya hivyo wanajua raha yake na wewe ambaye hujawahi, anza leo. Mmemaliza mambo yenu, chukuaneni kimahaba, elekeeni bafuni kisha ogeshaneni kimahaba.
Baada ya hapo rudini chumbani, mkishajifuta maji pandeni kitandani mkiwa wapesi.
 
Kusifiana

Hakuna muda maalum uliotengwa kwa ajili ya wanandoa kusifiana. Hilo linaweza kufanyika wakati wowote lakini pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa ni lazima utakuwa na jambo zuri la kumuambia mwenza wako.
Msifie kwa utundu na ubunifu wake. Msifie pia kwa mapenzi matamu anayokupa na ikibidi mpe sifa ya uzuri wake kiasi cha kukufanya kila unapokuwa karibu yake ujisikie amani ya kupitiliza.
Wapo ambao hawana kabisa kasumba ya kuwasifia wala kuwashukuru wenza wao kwa mazuri wanayofanyiwa. Yaani wao wanachukulia kila kitu poa tu bila kujali kwamba kusifiana kunanogesha mambo.
 
Kuelekezana

Kwenye kale kamchezo, wapo ambao wanakosea, kuelekezana na kukosoana kwa wapenzi ni jambo la kawaida. Yawezekana mwenza wako alifanya kitu ambacho hakikukufurahisha wakati mkiendelea na burudani yenu, mnapomaliza mwambie lakini kwa lugha ya kimahaba na ya upole. Naamini kwa kufanya hivyo atakuelewa na kubadilika.
 
Zungumzieni maisha

Huu ni wakati muafaka wa kujadili changamoto na malengo katika maisha yenu. Hapa akili zinakuwa zimetulia na kila mmoja anakuwa na mawazo chanya kwa mwenza wake. Jadilini mambo yenu, wekeni mikakati ya kuliboresha penzi na maisha yenu kwa ujumla.
 
Hayo ni baadhi ya mambo ambayo mnashauriwa kuyafanya pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa.

Thursday 22 January 2015

KAAMA ANAKUPENDA KWELI,KWANINI MAPENZI YENU YAWE YA SIRI?

Bila shaka msomaji wangu utakuwa unaelewa vizuri nikizungumzia mapenzi ya siri. Inawezekana umewahi kuwa katika aina hii ya uhusiano, umewahi kusikia au kushuhudia watu wawili wanaopendana, wakiendesha uhusiano wao kwa siri kubwa.

,kwa nini kuna baadhi ya watu hupenda kuishi kwenye uhusiano wa siri?
Najua wapo wengi ambao wapo kwenye uhusiano wa siri na wanazo sababu zinazowafanya waishi kwenye aina hiyo ya uhusiano, lakini je, kama unampenda, na yeye anakupenda kwa dhati, kuna haja gani ya kuishi kwenye uhusiano wa siri?

MAPENZI YA SIRI YANAVYOKUWA
Katika aina hii ya mapenzi, kila kitu wanachokifanya wahusika, kinakuwa kimetawaliwa na usiri wa hali ya juu. Uko naye, siku zinazidi kuyoyoma lakini humfahamu rafiki yake hata mmoja na yeye hamfahamu rafiki yako au ndugu yako hata mmoja.

Hata watu wenu wa karibu wanaowazunguka, hakuna hata mmoja anayejua kwamba nyie ni wapenzi. Mazungumzo yenu mnayafanya kwa siri sana, kukutana kwenu pia kunakuwa ni kwa kuibia sana, tena kwenye maeneo ya vificho.

Hata kama mnafanya kazi ofisi moja, hamuoneshi dalili yoyote ya kuwa wapenzi, hakuna ukaribu kati yenu na kila kitu kinatawaliwa na usiri. Muda pekee mnaokuwa huru, ni pale mnapokuwa peke yenu, yaani wewe na yeye tu.
Hata kama mnataka kutoana ‘out’, mpo radhi msafiri kwa umbali mrefu kwenda sehemu ambayo hakuna anayewafahamu.

DALILI MBAYA
Yawezekana umejikuta tu katika mkumbo wa mapenzi ya siri! Yaani mwenzi wako ndiye anayekulazimisha muishi aina hiyo ya maisha lakini ndani ya moyo wako unaona kama unaidhulumu nafsi yako.

Unatamani kila mtu ajue kwamba ninyi ni wapenzi lakini mwenzi wako anakukataza kufanya hivyo. Pengine hata anakupa vitisho kwamba utakapotoa siri ya uhusiano wenu, huo ndiyo utakuwa mwisho wa mapenzi yenu.

Shtuka! Chunguza kwa kina kwa nini mwenzi wako anataka muishi maisha ya mapenzi ya siri wakati kila siku anakwambia kwamba anakupenda na yupo tayari kufanya chochote kwa ajili yako. Mara nyingi, uhusiano wa siri huwa ni dalili mbaya kwa wahusika! Kwamba lipo jambo ambalo analificha na ndiyo maana anataka muwe wapenzi kwa siri.

Zifuatazo ni baadhi ya sababu zinazofanya mtu apende kuwa na uhusiano wa siri na mwenzi wake.

1. AMEOA/ AMEOLEWA
Sababu kubwa ya kwanza inayowafanya wengi wapende kuwa na uhusiano wa siri na wenzi wao ni kwa sababu wanakuwa wapo kwenye ndoa halali lakini kwa sababu ya tamaa zao, wanaamua kuchepuka. Katika kuchepuka huko, hawawaambii wenzi wapya ukweli kwamba tayari wanao wake au waume zao halali.

Wanawadanganya kwamba wapo singo ili wawatumie kimapenzi na watakapomaliza haja zao ndiyo wawaeleze ukweli na kuvunja mapenzi yao. Upo ushahidi wa wanawake wengi ambao walitongozwa, wakakubali kuanzisha uhusiano wa siri na wanaume na kukaa nao kwa kipindi kirefu lakini baadaye wakaja kugundua kumbe wao ni ‘spea tairi’.

Vilevile wapo wanaume ambao wameingizwa mkenge kwa kuingia kwenye uhusiano wa siri na wanawake, wakiwahudumia na kuwatimizia kila kitu lakini kumbe nyuma ya pazia ni wake za watu.

2. ANA MICHEPUKO MINGI
Sababu nyingine inayosababisha wengi wapende kuishi na wenzi wao kwa usiri, ni tabia ya umalaya au uhuni anayokuwa nayo mtu. Kwamba katika sehemu hiyohiyo moja, wewe unadhani uko peke yako lakini kumbe kuna wenzako kadhaa unapanga nao foleni. Kwa kuwa kila mmoja anatunza siri, inakuwa vigumu kujuana.

Thursday 15 January 2015

MFANYE MWENZI WAKO ASAHAU MAUMIVU YA MWAKA JANA.


KWANZA kabisa namshukuru Mungu kuweza kunifikisha salama mwaka 2015 nikiwa na afya njema. Nina imani hata wewe mdau wangu upo salama.

Natumia nafasi hii kuwaombea wote walioingia mwaka huu wakiwa wagonjwa na ambao walitaka kufika lakini Mungu aliwapenda zaidi wakaishia mwaka jana.
Leo napenda kuzungumza na wadau wangu wa kona hii Mwaka umekwisha umejifunza nini? Je, kupitia kona hii matatizo yameondoka , yamepungua au yameongezeka?
Kwa vile tunauanza mwaka, basi napenda  tufanye utafiti kuhusiana na mwenendo mzima wa maisha yetu ya kimapenzi. Huu ndiyo muda muafaka wa kujichambua mwenyewe ulibeba vipi uhusiano ndani ya penzi lako.

Katika muda wote kulikuwa na migongano, je, chanzo chake nini? Kama ni wewe ni muda wako wa kujirekebisha ili usiwe chanzo cha matatizo ya kila siku.
Ni makosa mtu kurudia kosa moja kila mara, mwanadamu anayejitambua hujifunza kupitia lile linalokemewa sana na mwenzake, japokuwa unapenda kulifanya.

Sifa kubwa ya mwanadamu ni kufikiri kabla ya kutenda, siku zote mapenzi ni kusikilizana, kufarijiana na kubembelezana. Bila shaka mwaka uliopita kuna mambo yalitokea hadi kufikia hatua ya kutishia kuvunja ndoa au uhusiano wenu.
Mwaka umeisha, umekaa na kujiuliza tatizo nini? Umejichunguza na kujua labda wewe ndiye chanzo?
Mmeukaribisha mwaka, mmekaa kama wanandoa au wapenzi kumaliza tofauti zenu ili kuuanza mwaka nanyi mkiwa wapya.
Kama hamjakaa kujadili mwenendo mzima wa uhusiano wenu kwa mwaka mzima hamjachelewa. Hebu kupitia makala haya kaeni chini na kuchambua matatizo yote yaliyowakwaza sana.
Tafuteni sehemu tulivu ili kupata nafasi ya kuzungumza kwa kujiamini. Sehemu hii haitakiwi mmoja kujiona yupo juu ya mwenzake au ubishi kwa kile ambacho kimemgusa.

Mazungumzo yenu yawe ya kirafiki, kosoaneni kwa sauti za kawaida, ondoeni jazba kwani muda huo haina nafasi. Uwe mwepesi kukubali kosa na kuomba msamaha. Kwa vile nia yenu ni kujenga, hakikisheni yote yaliowakwaza mwaka uliopita hamyapi tena nafasi.
Jiepusheni kuwa chanzo cha maumivu ya wenzenu, umeamua huyo awe wako wa kufa na kuzikana kwa nini muumizane? Sawa, mwanadamu ana upungufu, basi makosa yako yasiwe mazoea kwa vile tu upo juu ya mwenzako. 

Mapenzi hayaangalii cheo, fedha wala uzuri wa sura na umbile, bali kujitoa kwa ajili ya mwenzako.
Jutia makosa uliyofanya mwaka jana na kutokuwa tayari kuyarudia, hii itakufanya mwaka huu uwe makini sana na kumfanya mpenzi wako asahau maumivu ya mwaka jana. Muahidi mpenzi wako kuwa mwaka huu utakuwa sehemu ya furaha yake ya kila siku, kama utakwenda tofauti basi utakuwa msaliti.
Kiapo hiki si cha mtu mmoja bali kiwe cha wote. Kama kweli unayoyasema yanatoka moyoni na kuwa tayari kutorudia yaliyomkwaza mwenzako mwaka jana, basi mwaka huu utakuwa wa furaha na amani. Nakutakieni mwaka mpya wenye mapenzi ya dhati, kila mmoja awe sehemu ya furaha ya mwenzake.


Posted via Blogaway

WALIO NJE WANALAZIMISHA NDOA,WALIO NDANI WANADAI TALAKA.

Ndoa  inafahamika kuwa ni heshima kwa kila mmoja, namaanisha kwa anayeoa na anayeolewa. Mwanaume akioa, anaheshimika na anajiona ameingia kwenye majukumu ambayo yanamlazimu atie akili ili aweze kukabiliana nayo. Kwa wanawake ndiyo usiseme. Yaani idadi kubwa ya wanawake wanalilia ndoa hasa kwa wanaume ambao wamewapenda na kuwaamini kwamba wakiwa nao ndani maisha yao yatakuwa ni ya furaha zaidi. Kwa kifupi ndoa ni tamu ila kama utaijulia na ni chungu kama utakuwa umeingia kwenye maisha hayo na mtu ambaye awali alikuwa akijifanya anakupenda sana lakini baadaye akaamua kutoa makucha yake. Wapo wanaume ambao leo hii wanalia, wanajuta ni kwa nini waliamua kuwaoa wanawake ambao wamewaoa. Wanajuta kwa kuwa wanakutana na mambo ya ajabu ambayo hawakuyatarajia. Si hivyo tu, wapo wanawake ambao walifurahi walipovishwa pete za uchumba na hatimaye kuvaa mashela lakini leo hii wanaomba talaka kutoka kwa waume zao kutokana na mazingira tofauti wanayokumbana nayo. Kwa kifupi baadhi ya walio kwenye ndoa wanalia, unaweza kuwaona wakipita mbele za watu wanachekacheka na kuonesha kuwa wanapendana lakini kumbe katika uhalisia, wamechokana na ndoa zao zimeshikiliwa na nyuzi. Unaweza kujiuliza ni kwa sababu gani? Inakuwaje watu waliotokea kupendana sana wanaishi kwa muda mfupi tu kisha wanaanza kujutia maamuzi yao ya kuingia kwenye ndoa?   Hakuna sababu nyingine zaidi ya kwamba aidha walikurupuka kufanya maamuzi hayo au kulikuwa na mazingira ya mmoja kujifanyisha na kumfanya mwenzake aone amempata mtu sahihi kumbe hamna kitu. Ukijaribu kuchunguza sana, utabaini kuwa wengi wako kwenye ndoa za Kichina. Ndoa ambazo hakuna mapenzi ya dhati baina yao na kusalitiana imekuwa ndiyo mtindo wa kisasa. Katika mazingira haya furaha haiwezi kupatikana na ni lazima majuto yatokee. Ni kwamba, ndoa kweli ni heshima na kama umetokea kuwa kwenye uhusiano na mtu ambaye unaona ana kila kigezo cha kuwa mwenza wako, una kila sababu ya kufanya kila uwezalo kukaribisha ndoa. Oa au olewa ili furaha yako iweze kukamilika. Lakini sasa angalizo ni kwamba, si kila anayeonesha kukupenda sasa anafaa kuwa mumeo au mkeo. Elewa kwamba kuna wanawake wengine ambao wao kupenda kwao hawamaanishi ni ili waolewe, wanapenda tu na kufurahia kampani lakini ukiwatajia ndoa, usije ukashangaa wakakataa kuolewa. Hawa wa sampuli hii ukiwalizimisha utakiona cha mtemakuni. Namaanisha kwamba, wapo wanawake ambao lile neno ndoa tu kwao limewakalia kushoto lakini wanajua kupenda na kuwaridhisha wanaume. Ni sawa na kulazimisha kumuoa changudoa ambaye ni mtaalamu wa kudatisha, mtaalamu wa kubembeleza na mtaalamu wa kumpa furaha mwanaume yeyote kwa kuwa ameona pesa. Ukimuoa mwanamke wa aina hiyo ukidhani utapata mambo kama hayohayo,umeumia. Hilo lipo pia kwa wanaume, kuna wale ambao wanaweza kuonesha upendo wa hali ya juu lakini hawako tayari kuingia kwenye ndoa. Ukilazimisha kuolewa na mwanaume huyo, umeula wa chuya kwani huwezi kuyapa mapenzi aliyokuwa akikupa kabla ya ndoa. Kwa maana hiyo nihitimishe kwa kusema kuwa, lazimisha ndoa lakini kwa mtu ambaye una uhakika anahitaji kuingia kwenye ndoa na umemsoma vizuri na kubaini hawezi kuja kukuletea maumivu siku za baadae.