Thursday 10 March 2016

UNAWAJIBIKA KWENYE NDOA YAKO?

Kuwajibika na kujitoa ni moja ya mahitaji muhimu sana ya mafanikio yoyote dunia leo.
Pia hakuna sehemu muhimu kwa kuwajibika na kujitoa kama kwenye ndoa na mambo ya familia.

Watu wanaoamua kuoana huwa wanawajibika na kuhakikisha wanajitoa kwa ajili ya uamuzi na uchaguzi wamefanya kwanza kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake ili kuhakikisha ndoa inaendelea.

Kila anayeingia kwenye ndoa huwa anakuwa amebeba limfuko la matatizo binafsi na kutokukomaa katika maisha ya ndoa (immaturity), hana uzoefu na kinachofuata ni kupata uzoefu mpya.
Hivyo partners wote wanawajibika kukutana na matatizo na kuyashughulikia hayo matatizo bila kulaumiana au kumlaumu mwenzake kwa matatizo just focus to the solutions kuliko ku-focus kwenye matatizo na kuanza kulalamikiana, ingawa hapa kuna wengine huwa kichwa ngumu anajiona yeye yupo sahihi siku zote na anaweza ku-ignore kila kile mwenzake anapendekeza ili ndoa irudi kwenye amani na usalama.


Kila mwanandoa anahusika na kuwajibika kwa ajili ya furaha yake, hisia zake na kila reactions, hakuna mtu atakufanya uwe happy ila ni wewe kwanza, kwani ukishinda umekasirika siku nzima au mwezi mzima au hata mwaka unapata faida gani?

Furaha ni matokeo ya kukomaa kwa mtu na kufahamu kwamba yeye mwenyewe ni chanzo cha furaha na simwingine.
Wewe ukiwa na furaha na wengine watakuwa na furaha.
Watu wenye furaha hutengeneza ndoa zenye furaha na watu wasio na furaha hutengeneza ndoa zisizo na furaha.

No comments:

Post a Comment