Monday 10 August 2015

NI KUENDELEA KUJIFUNZA TU.

Tendo la ndoa au kufanya mapenzi (sex) kwa watu wawili wanaopendana (Ndoa) ni moja ya vitu vya asili duniani vinavyowapa wahusika raha ya ajabu ambayo bado lugha za kawaida tunazotumia binadamu hazitoshelezi kuelezea.
Ingawa ni kweli mwanamke na mwanaume wapo tofauti linapokuja suala la sex bado kujifunza na kuwa equipped kwa ajili ya sex ni muhimu.
Miili yetu ni complex machines ambazo zinahitaji kutumia Owners Manual kusoma mara kwa mara ili kuelewa na kuwa wazuri kuitumia.
Wakati wanaume hujisikia vizuri baada ya sex wanawake mara nyingi hupenda kujisikia vizuri ili wajishughulishe na sex.
Pia mwanaume akiwa amesisimka kimwili ndipo hujisikia kusisimka kisaikolojia mwanamke akisisimka kisaikolojia ndipo hujisikia kusisimka kimwili.
Sex yenye utamu wa kweli hutokana na kujiachia katika fahamu zetu na kutojiachia fahamu huweza kufanya blocking ambayo huweza kuiba hamu ya kufanya mapenzi.
Ni kweli kwamba ubongo wako ni most important sex organ na kwa ubongo tunaweza kuhusanisha mwili, nafsi na roho kuumba raha ya mapenzi ambayo haiwezi kusaulika katika maisha yote tunayoishi.
Hakuna binadamu anazaliwa anajua kila kitu, hivyo basi kujifunza ndiyo silaha ya kwanza kabisa ya kufahamu mwili wako na wa Yule umpendae una react vipi linapokuja suala la kufanya mapenzi.
Wala huhitaji kununua libido meter ili kuhakikisha kitanda chenu kinakuwa na moto mambo ya msingi ni kwamba:
Hakikisha kufanya mapenzi ni moja ya priority kati yako na mume/mke
Jifahamu mwenyewe kama vile unapenda kitu gani na wapi katika mwili wako
Mfahamu vizuri partner wako
Fahamu aina mbali mbali za style za kufanya mapenzi (sex position) hiyo hiyo kila siku inakuwa mazoea, muwe wabunifu.
Hakikisha mnapata suluhisho kwa matatizo kabla ya kwenda chumbani ( wakati mwingine jifunze kukubaliana kutokubaliana.
Hakuna kitu muhimu kama romance.
Afterplay ni muhimu kama foreplay- huwezi kumaliza mazungumzo bila kutoa hitimisho.
Hakikisha unaimarisha mawasiliano.
Pia kubali mabadiliko au kutafuta kitu kipya.

No comments:

Post a Comment