Wednesday 5 August 2015

KUKUMBATIANA...

KUKUMBATIANA NI NINI?

Neno kukumbatia (hug) linatokana na neno hugga lenye maana kufariji.
Kukumbatiana kuna faida kubwa kuliko mtu anavyofikiria.
Utafiti unaonesha kwamba kukumbatiana husaidia watu kisaikolojia na kimwili pia.
Pia utafiti umeonesha kwamba kwenye mwili wa Binadamu (nervous system) kuna kemikali inayoitwa endorphins ambayo inapatikana kwenye damu iliyomo katika mfumo wa fahamu na husaidia kupunguza maumivu na hutuwezesha kujisikia salama, ahueni, kutiwa moyo, raha na utamu (euphoric).
Utafiti unaonesha kwamba watu wanapokumbatiana hizi kemikali huongezeka mwilini na hivyo kukumbatiana ni dawa tosha kabisa ya kumaliza maumivu mwilini kisaikolojia na kimwili (painkillers).

Pia Utafiti umeonesha kwamba kukumbatiana huongeza kinga ya mwili imethibitika kwamba kwenye ubongo kuna sehemu inayohusika kuitikia wakati watu wanakumbatiana.

Mfano:
Mtoto asipokumbatiwa (touch) kwa muda unaotakiwa sehemu ya ubongo hupoteza seli za misuli (atrophies) na kinga ya mwili hupungua.

Tunapokumbatiwa tangu watoto tunajenga uwezo wa kuwa na
Upendo,
Kupenda na
Kupendwa,
watoto ambao wamekulia mazingira ya kutokumbatiwa huwa wagumu sana kuwapenda wenzao.
Utafiti wa jamii katika tamaduni mbalimbali unaonesha kwamba jamii ambazo watu hawakumbatiani ni violent na wauaji.


JE BARA GANI MAARUFU KWA WATU KUKUMBATIANA?
Mwanasaikolojia Bwana Sidney Jourard alisafiri mabara yote na kugundua kwamba bara la Ulaya ndiyo linaongoza kwa watu wengi wanaopenda kukumbatiana likifuatiwa na Amerika na mengine yakifuatia


Wanaume na wanawake wote wanapenda kukumbatiana kwa maana kwamba wote wanahitaji kulisikia joto la upendo wa kukumbatiwa.
Wakati wanawake wengi walipoulizwa kwa nini wanapenda kukumbatiwa wengi walikiri kwamba sababu kuuu ni Kujisikia wanapendwa, kwa upande wa wanaume wengi wanakiri kwamba hupenda kukumbatiana na wanawake kwa sababu hupenda kusikia Mguso wa matiti
(hapa hatuzungumzii mama au dada au ndugu)

SABABU ZINAZOFANYA WANAUME WAWE WANAPENDA KUKUMBATIWA NA WAPENZI WAO WANAWAKE
Raha ya mguso wa matiti
Wanaume hujisikia salama
Husaidia kushuka chini wakiwa na hasira
Hujisikia ana rafiki wa kweli
Hujisikia kupendwa
Naweza kumnusa mpenzi wangu na kupata harufu nzuri aliyonayo
Kufurahia kuamshwa kimapenzi
Hujisikia ni mali yake
Ni nafasi na kutoa na kupokea upendo
Kusikia joto la upendo

SABABU ZINAZOFANYA WANAWAKE WAWE WANAPENDA KUKUMBATIWA NA WAPENZI WAO WA KIUME
Inawafanya kujisikia kupendwa
Hujisikia wameunganishwa na kuwa karibu zaidi
Najisikia salama
Ni dawa kisaikolojia
Najisikia joto la upendo
Najisikia kulindwa
Hufarijika na kujiona mwanaume anamjali
Hujisikia vizuri miili kugusana na kujisikia mtu muhimu.





No comments:

Post a Comment