Wednesday 5 August 2015

SIRI..!!

Kati ya wanawake na wanaume nani mabingwa wa kutunza
siri hatari wakati wa kuanza mahusiano?

Wanawake wengi ni innocent sana!

Wapo watu ambao wanapoanza mahusiano (urafiki wa kuelekea mke au mume) huficha siri zao za kwa kuogopa kwamba wakiziweka juu ya meza na kuwaambia wale wanaanza nao uhusiano mpya wanaweza kuwakataa na uhusiano kufa.

Ukweli ni kwamba siri zako kabla ya mahusiano mapya ni vizuri kumwambia mpenzi wako kwani ipo siku siri zako zitagundulika na kama zikigundulika basi hapo ujue utakuwa umepoteza trust na ukipoteza trust ni kama barafu linalowekwa kwenye jua likiyeyuka huwezi kulirudisha kwenye hali yake ya kawaida.

Kuna msemo wa kingereza ambao husema
‘If you do not deal with your past, your past will deal with you”

Ni vizuri kujiuliza mwenyewe hivi ni kweli mpenzi huyo uliyenaye anakuona wewe kama ulivyo mtu halisi au kuna siri fulani ambazo umezificha?
Je, kweli ni wewe mwenyewe uliye halisi ?

Wengi huficha kwamba huko nyuma walikuwa na watoto, wengine huficha huko nyuma walishawahi kuwa na mahusiano na kwa sababu ya tabia yake mahusiano hayakudumu.
Wengine huficha hata ukweli kuhusu familia zao
Wengine huficha hata kiwango cha elimu zao, kazi zao, dini zao nk

Haina haja kuficha siri ambazo unajua ni siri kubwa kwani ipo siku mambo yatawekwa sebuleni then hiyo kasheshe hapata tosha maana kuna swali utauzwa
"Kama umeweza kuficha siri kubwa kama hii kwa miaka yote hii je, nitakuamini kweli?"

No comments:

Post a Comment