Friday 7 August 2015

LUGHA MUHIMU KWENYE NDOA.

Ndoa ni kama Kambai nayounganisha (kuwafunga) wawili kuwa mmoja. Kamba ya ndoa imetengenezwa kwa kuunganisha nyuzinyuzi za upendo wa ahadi nne yaani mawasiliano, kujitoa, kumwelewa mwenzako na kumsamehe.

Wakati mwenzi wako anajisikia kuridhishwa kimapenzi hujiona salama kihisia na hujiona ulimwengu unampa vyote na atajitoa zaidi kuhakikisha anajitoa katika kiwango cha juu kwao kuimarisha upendo na mahusiano.

Na anapojisikia kutoridhishwa kabisa kimapenzi, hujisikia ni kama vile anatumika au unamtumia tu kufanikisha hitaji lako la mapenzi bila kupendwa na kwake ulimwengu unageuka kuwa mahali hatari kwake na husababisha hata vitu vingine ulivyompa kama nyumba, gari, fedha nk kuwa havina maana katika uhalisia wa maisha.

Mapenzi yana lugha kama zilivyo lugha za mawasiliano, utamu wa lugha ni pale unapoifahamu kuisikia na kuiongea, pia utamu wa mapenzi katika ndoa ni pale unapofahamu lugha ya mapenzi kusikia na kuongea.

Raha ya Kiswahili ni pale unapoongea Kiswahili na mswahili mwenzako, na kuongea vile vimaneno vitamu vinavyofanya ufurahi na kucheka na kujiona kweli Kiswahili kitamu. Je inakuwaje unapoongea Kiswahili na mtu anayeongea kihindi?

Kuna watalamu na washauri ya mambo ya ndoa na mapenzi wameandika sababu nyingi sana zinazoelezea lugha halisi za mapenzi, wengine wanasema zipo 5, wengine 10, wengine 50, wengine 100 Mimi naona zipo sita ila moja (ile ya sita) ni muhimu kwa wote na ni msingi halisi wa ndoa na ni asili yake na kuizembea hiyo naamini inaharibu mtiririko wa lugha zote za hisia za mapenzi. Kuzijua hizi lugha sita na kufahamu ni zipi (ipi) mke wako au mume wako yupo basi ndoa inakuwa tamu kwelikweli, utamu halisi usio na hila, na utakiri kwamba kweli ndoa ni tamu.

Lugha za msingi za kuelewana katika ndoa kwa hisia za mapenzi ni kama ifuatavyo:-
1. Kuwa na muda na mwenzi wako
2. Kupeana zawadi
3. Kusaidia kazi/huduma
4. kumpa maneno ya kumsifia, kushukuru na kumtia moyo kwa kile anafanya
5. Mguso wa kimwili (wale wa mabusu na ma-hug kazi kwenu)
6. Mungu. Muhimu kuliko zote

Leo tutaongelea namba Moja

1. KUWA NA MUDA NA MWENZI WAKO.
Msingi wa kuwa na muda na mwenzi wako ni upamoja pamoja na kuwa kimawazo, kimwili na kiakili.

Kuwa na muda na mwenzi wako hatumaanishi kukaa pamoja kwenye sofa au makochi kuangalia TV; au movie hapo mnaipa time au muda wa pamoja TV au movie mnayoitazama siyo mwenzi wako.
Kuwa na muda na mwenzi wako ni kukaa pamoja na kumpa attention yote, anaongea na wewe unamsikiliza tena ninyi wawili tu, kutembea pamoja yaani mmeamua kwenda kutembea kwa ajili ya kwenda kutembea wewe na yeye tu si kwa sababu mnaenda kanisani au mnaenda kazini, kupeana muda wa pamoja ni kama vile kwenda kula pamoja (outing) ninyi wawili na mkifika hapo kwenye hoteli mnaongea kwa kuangaliana ninyi romantically.

Ukienda kwenye hoteli au sehemu yoyote watu wanaenda unaweza kula chakula au huduma zingine (outing) utajua tu wapenzi walio kwenye ndoa na wale ambao bado wachumba au dating couples, Guess what? Wachumba utakuta wanaongea kwa kuangaliana tena kwa karibu na vikolombwezo kibao na wanatamani wabaki hapo, tuje walio kwenye ndoa wanakula na kunywa kila mtu anaangalia kwake, wanaangalia kuta na watu na unajua wameenda kula na si kuwa na muda pamoja, halafu wana haraka sana, kidogo tu waaondoka kama vile wamelazimishwa kwenda outing.
Tuwe romantic jamani, tutaendelea kujadili zaidi huko mbele safari ya somo letu.

Ni kweli kila mtu anahitaji muda na mwenzi wake, lakini maajabu ni kwamba si kila mwanandoa ukimpa muda au kuwa naye kwake ndo anajisikia na kujiona unampenda kwani kwake kuwa na muda naye hakumgusi kama ukiwa unamletea zawadi, au unapo mpa maneno ya kumsifu kwa kitu amefanya, au kumshukuru na kumpa affirmation kwa kila anachofanya.

Kitu cha msingi ni wewe kuchunguza je mpenzi wangu anajisikiaje kwa kila mambo 5 ni lipi linamgusa sana na kujiona kwake ndo la msingi kuliko yote. Kama ni Kumpa muda ndo anajisia unampenda basi fanya makeke your baby ajipe raha.

Mbona tunapo date tunakuwa na muda pamoja huko tumepanga kukutana? Kwa nini baada ya kuoana watupeani time hata kama tunalala pamoja issue hapa ni kumpa muda ambayo katika masaa 24 hata kama ni dakika 20 tu mpe mpenzi wako na kama lugha yake ya mapenzi ni kuwa na muda na wewe basi utampatia sana na kama hufanyi ndo yale yale unampa zawadi ya gharama lakini bado anasema humpendi na love tank inazidi kuwa empty Hebu jaribu kufanya kweli uone kama mwenzi wako hajakwambia baba Fulani au mama Fulani siku hizi unanipenda sana, yaani umebadilika, acha kusema upo busy, gharama ya kusuruhisha ndoa unayoenda ICU ni mbaya sana kuliko huo ubusy.

Fanya yafuatayo katika suala zima la kumpa mwenzi wako muda wa pamoja hasa kama kwake kumpa muda ndo anajisikia unampenda
(a) Mwangalie usoni wakati anaongea atajua unamsikiliza
(b) Usimsikilize huku unafanya kazi nyingine, kama huwezi muombe akupe muda kidogo then utamsikiliza anachosema kuliko kuendelea kufanya kile unafanya huku unamsikiliza, utamuumiza sana
(c) Onyesha hisia kwa kile anakwambia, kama unahisia amekatishwa tamaa mwambia ukweli kwamba nahisi unajisikia umeumizwa au kukata tamaa, basi nitafanya hivi na hivi, changia kupata solution
(d) Hakikisha unajua anaongelea nini na anajisikiaje (body language)
(e) Usimkatishe anapoongea, sikiliza maana wengi huwa tunadhani tunajua hata alichokuwa anataka kusema hata kabla hajasema, eti nilikuwa najua utasema hicho tu

No comments:

Post a Comment