Thursday 10 November 2016

TALAKA UHUMIZA


Talaka huumiza kuliko kifo, hata hivyo kwa baadhi ya wanawake walioolewa sasa wanaona talaka ni uhuru na maisha.
Hujiona wao young and beautiful, hakuna mtu wa kumwambia fanya hili au kile, no demands, hakuna kulaumiwa, kuonywa, kusemwa, kuamrishwa, hakuna kumpikia dinner wala lunch, hakuna utumwa, na akiangalia nje ya ndoa anaona mwanga ni mzuri unaopendeza, anajiuliza kwa nini kuteseka wakati huko nje kuna wanaume wengi tu wananihitaji.
Anafikiria namna anaweza kurudi kwenye maisha ya ujana upya, ulimwengu mpya kwani hakuna kuzozana tena, hakuna kulalamikiana tena, hakuna kuulizana umetumiaje fedha.
Mwanamke anafanya kweli, anaachana na mume wake na kila mtu kuanza kivyake.
Kwa mara ya kwanza anaona mambo ni mazuri, baada ya kusuguana na mume kwa muda mrefu sasa anajiona amepata ahueni, uhuru kwa kwenda mbele.

Sasa nikueleze ukweli wenyewe!

Kawaida wanawake wengi (siyo wote) wanaoachana na waume zao umri wao mara nyingi ni kuanzia miaka 28 – 40.
Maana yake huko nje wanakoamini kuna wanaume wa kuwaoa wapo wanaume wa aina mbili tu, kwanza ni wale ambao nao wameachana na wake zao na pili ni wale ambao ni single (hawajawahi kuoa).
Mara nyingi hawa wanawake huwaogopa sana wanaume wa kwanza hapo juu kwa kuwa ndo walewale ambao wameachana nao, hivyo Hujiuliza swali “kwa nini ameachana na mke wake?”
Hii ni dalili kwamba anaweza kuwa ni big trouble!
Hii ina maana sasa amepunguza idadi ya wanaume ambao anaweza kuoana nao tena kwani tumebakiwa na wanaume ambao hawajawahi kuoa yaani wapo single.
Hapa anamtafuta mwanaume ambaye ana sauti nzuri, mtaalamu wa kuongea, romantic, tender, passionate, mwelewa, mwenye fedha za kutosha, mwenye taaluma nzuri kama vile lecturer, Diplomat au millionaire, mwanaume ambaye hata
Watoto wake watajiona wana baba wa uhakika, ambaye si mlalamikaji, anayeweza kuwafanya kusafiri kila Mahali wanapotaka duniani na mwanaume ambaye atavutiwa na yeye tu na si vinginevyo.
Tuseme wewe mwanamke uliyeamua kutimka kwa mume wako sasa una miaka 38, je unadhani ni rahisi kumpata mwanaume wa aina hii ambaye amekuzidi umri au mnakaribia au sawa.
Ni mwanaume gani mwenye sifa kama hizo anaweza kukubali kuoana na mwanamke aliyeachana na mume wake?
Kama amekuzidi umri na wewe una miaka 38 inakuwaje hadi sasa awe hajaoa, utasema alikuwa anasoma PhD, yaani na PhD yake aje akuoe wewe uliyeachika na mume wako?
Si rahisi kama unavyofikiria!
Ukweli ni kwamba mwanaume wa aina hii anapatikana kwenye TV na Movies!
Anapatikana kwenye mawazo, anapatikana fantasy land na si kwenye maisha halisi!
Nafasi ya kumpa mwanaume wa aina hii ni moja kati ya milioni moja.
“Don’t permit the possibility of divorce to enter your thinking, even in a moment of great conflict and discouragement, divorce is not a solution”
Unaweza kujikuta wewe mwanamke ndiye unawawinda wanaume, kwa taarifa yako mwanaume hayupo wired kuwa kuwindwa badala yake yeye hufurahia kuwinda.
Utajikuta ni lonely na unazeeka haraka kuliko ulivyotegemea.
Wanawake walioolewa ambao walikuwa rafiki zako wataanza kujisikia uncomfortable na wewe, wanakuona ni mwanamke loose na dangerous kwa waume zao na wanaanza kukukwepa na kuweka ulinzi mkali kwa waume zao, na wanaume ovyo nao wanaanza kukushangaa mboni hutaki kulala nao, wanakuona wewe ni cheap target!
Kutafuta talaka ni kupoteza uraia wako, hadhi yako na uhuru wako.
Utajikuta unakaa nyumbani mwenyewe peke yako usiku hadi usiku, hofu itaanza kukuingia, kujiamini kunaanza kupotea, unaanza kujiona huvutii tena na watu wanakudharau.
Talaka ni kubadilisha matatizo ya zamani na kujipa matatizo mapya.
“Guard your relationship against erosion as if you were defending your very lives”
Kumbuka ukishirikiana na mume wako mnaweza kurudi tena kwenye raha ya maisha kama vile mwanzo mlipoanza ndoa yenu.

No comments:

Post a Comment