Thursday 24 November 2016

USAFI NI MUHIMU.


Jambo moja ambalo kila siku hulalamikiwa na wanawake kuhusu waume zao ni suala la mwanaume kuwa mchafu, kuingia kitandani huku ananuka kama soksi chafu na wakati huohuo unataka kuwa karibu na mke wako kimapenzi kila sehemu ya mwili wako.
Sidhani kama hilo ni jambo la kistaarabu!

Kuna siku kilirushwa kipindi redioni kinachowaomba wanawake kuuliza maswali au kutoa malalamiko kuhusu usafi na tendo la ndoa kuhusu waume zao, tofauti na nchi zinazoendelea ambazo wanawake huogopa kuongea kwa uhuru (in public) kuhusu waume zao, kwa kuwa ilikuwa katika nchi zilizoendelea wanawake waliongea kwa mfululizo na kutoa malalamiko yafuatayo:
Kwanza kuna wanaume hata huwa Hawajali usafi, wapo ambao hata kuoga ni kazi, kupiga mswaki kazi, au kujiandaa kiusafi wakati wa kwenda kitandani na matokeo yake mke hujikuta badala ya kusisimka anakasirishwa.
Saa nne usiku, unaingia kitandani na unataka sex, midevu yako haijanyolewa vizuri na matokeo yake inamchoma mke utadhani kidevu kina sandpaper, hujaoga na jasho la ofisini kupitia kwapa zako linanuka kama compost pile.
Kucha ndefu na chafu kwa ndani utadhani ni kucha za monkey.
Katika utafiti uliofanywa baada ya kuwauliza wanafunzi (chuo) 332 kile ambacho huwavutia zaidi kwa wanaume, iligundulika kwamba namna mwanaume ananukia huvutia zaidi kuliko namna anavyoonekana kwa mwanamke.
“Hii ina maana kwamba ni mwanaume hata kama umepiga pamba za uhakika huku unanukia kama panya aliyeoza huna maana”.
Hivyo ni muhimu sana kwa mwanaume kujifunza kutumia kipande cha sabuni, ni vizuri kuoga kabla ya kujirusha kitandani hata kama ulikuwa na busy day.
Pia Kumbuka kujinusa mwenyewe na kuamini kila kitu kipo shwari si gauge nzuri.
Pia Kumbuka mwanamke ana uwezo mkubwa kunusa kuliko mwanaume.
Usafi na sex ni vitu vinavyoendana huwezi kuvitenganisha.

No comments:

Post a Comment