Friday 4 December 2015

USIFANYE HAYA KWENYE NDOA YAKO.

1. Kumzoea mwenzi wako kiasi kwamba huoni yupo special
2. Kukosa interest kwa kile mwenzi wako anajihusisha kufanya
3. Kuwa mlevi.
4. Kutoshughulikia ndugu wanapoingilia ndoa.
5. Kukosa muda kuwa na mwenzi wako hasa baada ya watoto kuzaliwa.

6. Kujisikia huna kitu common na mwenzako
7. Kukosa kula chakula pamoja angalau mara 3 kwa wiki.
8. Kukosa kulala pamoja
9. Kutojua matokeo ya kuvaa nguo nzuri, usafi, kupendeza kwa mwonekano.
10. Kutosafiri pamoja hasa safari za ghafla na dhalula kwa lengo la kuwa wawili tu.

11. Kuishi pamoja kwa sababu ya watoto tu, na si upendo wa kweli.
12. Kushindwa Kukukubaliana kutokubaliana.
13. Kushindwa kujitunza mwenyewe kimwili, kiroho na kijamii.
14. Kushindwa kuchunga afya yako.
15. Kutumia muda mwingi na jamii badala ya mwenzi wako na familia yako.

16. Kushindwa kuwa na muda wa kuburudika pamoja.
17. Kutokuwa na interest zinazofanana.
18. Kutokubaliana katika pesa.
19. Kutotumia angalau saa moja kwa wiki wewe tu na mwenzi wako kuongea pamoja.
20. Kushindwa kujadili vitu unavyopenda au kutopenda likija suala la mapenzi.

21. Kushindwa kushikana mikono au kukumbatiana huku kila mmoja akiongea na mwenzake au kupeana ndoto za maisha.
22. Kuwa mwema zaidi kwa walio nje ya familia wakati suala hilo hilo unashindwa kufanya ndani ya familia au kwa mwenzi wako.
23. Kukosa kubusu asubuhi unapoondoka kwenda kazini au Unaporudi kutoka kazini.
24. Kukosa kufarijiana.
25. Kushindwa kuuteka moyo wa mwenzi wako.

26. Kufikiri na kuamini kwamba mwenzi wako kila siku yeye tu ndiye anakosea
27. Kukosa tendo la ndoa kwa siku 21 wakati mnaishi pamoja na kulala nyumba moja na hakuna tatizo la kimatibabu.
28. Kuwa na hisia kwamba mwenzi wako ni adui yako na humpendi.
29. Kukosa muda wa kucheka pamoja na mwenzi wako.
30. Kushindwa kwenda kanisani pamoja
31. Kutokujali kuongelea moja ya hayo hapo juu kuonesha kwamba unataka mabadiliko.

No comments:

Post a Comment