Sunday 13 December 2015

JENGA MAHUSIANO MAZURI NA MTOTO WAKO.

Mahusiano yako na mtoto wako atakapokuwa mtu mzima huelezea ubora wa mahusiano uliyokuwa nayo wakati yeye angali mtoto mdogo.

Aina mbalimbali za wazazi ambao watoto huwa nao.

Kundi A
Wakali, wasumbufu, wasio na utaratibu, wasio samehe, wakorofu, wanaoweka donge moyoni, wanaopenda sifa, wasioaminika, wasio na subira, wanaowaka wakikasirika, wanakasirika haraka na wanaoshindwa kuwa na kiasi nk.

Kundi B
Wakarimu, wanaojali, wapole, wanaosamehe, wanaoheshimika, ukifanya makosa wanasamehe na kusahau, wanyenyekevu, wakweli, wenye subira, wanahasira lakini wanazihimili, wana kiasi, wacheshi, wanaofurahisha nk.
Je, ungekuwa mtoto ungechagua mzazi wa kundi gani?

Ni yupi kama una matatizo shule ungemwambia?

Ni yupi anaporudi nyumbani ungemkimbilia na kujisikia upo mahali salama?

Ni yupi ukifanya makosa unaweza kukiri wazi kabisa kwamba umefanya makosa?

Kumbuka mtoto hawezi kubaki mtoto miaka yote hivyo wakati akiwa mtoto hakikisha unampa kile anastahili kwa wakati wake.
Kwa mfano usipocheza na mtoto leo usidhani miaka 10 ijayo unaweza cheza mchezo uleule ulitaka kucheza naye miaka 10 iliyopita.

Je, ili kujenga uhusiano na mtoto wako ni mambo gani ya msingi kufanya?

CHEZA PAMOJA NYUMBANI:
Cheza mchezo wowote kama vile kadi, colouring, puzzle nk.
Unatakiwa kubuni mchezo ambao unaweza kucheza na mtoto/watoto wako.

CHEZA NJE YA NYUMBANI:
Unaweza kutembea au kukimbia kwa ajili ya maendelea ya afya ya mtoto. Unaweza kwenda naye kwenye Pak, kutafuta maua au wadudu au kurusha mawe kwenye mto nk.
Kumbuka issue si kwenda naye tu bali na wewe uhusike kucheza nay eye.

PENDA VITU AMBAVYO MTOTO WAKO ANAVIPENDA.
Ni muhimu sana uwe una admire vile vitu mtoto wako anapenda au kuonesha interest na wewe husika na endelea kumsaidia yeye kuwa mbunifu zaidi kwa vitu anavipenda kufanya.
Kama anapenda kutengeneza magari msaidie na kumtia moyo kwani anaweza kuwa designer wa magari baaadae, au kama anapenda kufuga wadudu anaweza kuwa ni conservation officer (wildlife) baadae.

MSAIDIE HOMEWORK NA PROJECT ZA SHULE:
Utakuwa unamtia moyo sana mwanao kwa kuwa kile muhimu kwake na kwako ni muhimu.
Unapofanya hivyo unamsaidia mtoto kuwa organized, pia unaweza kumwingizia ethics zako kuhusu maisha ya shule kama vile juhudi na kutokata tama.

TAFUTA MUDA WA KUJIBU MASWALI YAKE:
Ni muhimu sana kujibu maswali ya mtoto aina zote hata kama atakuuliza swali ambalo ni la mambo ya kikubwa kwani ni mtoto anataka jibu na si kumkemea, kwani hata akiwa na swali mahali popote atajua mzazi wangu ni mtu muhimu nitamuuliza hivyo utamlinda pia.

MTOTO AKIKASIRIKA RESPOND VIZURI:
Hakuna kitu muhimu kama kuwa makini na mtoto akikasirika na jinsi wewe unavyo respond kwani ukiwa na hekima na busara utakuwa unamtengeneza vizuri mtoto wako jinsi yak u-behave akiwa amekasirika hata katika maisha yake baadae akiwa mkubwa kwenye ndoa yake.

MWAMBIE NAKUPENDA:
Hivi ni lini umemwambia mtoto wako nakupenda? Hakuna kitu kizuri kama mtoto kuambiwa anapendwa na wazazi wake na pia ni vizuri mtoto afahamu baba na mama wanapendana.

SHUGHULIKIA TABIA MBAYA MAPEMA
Mtoto wako akionesha tabia mbaya mshughulikie kwa upendo.
Pia kusema HAPANA maana yake bado unampenda, si busara kumwambia ndiyo mtoto hata kitu ambacho unaona hakina faida kwake eti atalia.

UKIKOSEA OMBA MSAMAHA
Wakati mwingine wazazi hukasirika na kuwaadhibu watoto wakati mwingine wakiwa hawana makosa.
Hivyo kama ni kweli umekosea, omba msamaha.

UWE NAO KWENYE SHUGHULI ZAKO:
Ni muhimu sana kuhakikisha unakuwa na mtoto kwenye shughuli zako kama ni ofisini siku zingine nenda naye ili na yeye akakae kwenye kitu chako na kujiona ni boss fulani.
Pia inampa picha nini mzazi anafanya na itampa picha ya maisha na future yake.
Kama ni dereva nenda naye kwenye gari siku moja.
Kama ni forester nenda naye kwenye forest nay eye ajifunze kupanda miti.
Kupika je? Kufua nguo je? Kulima Je?

WAFUNDISHE KUHUSU MUNGU:
Ni muhimu sana watoto wanavyoongezeka na imani yao ya kumjua Mungu iongezeke, imani ya wazazi ina impact kubwa sana kwa mtoto kuliko mahali popote.
Linapokuja suala ma Mungu mtotot huambulia 80% kwa wazazi, asilimia 15 Sunday school (kanisa) na 5% mtaani.
Hivyo mzazi una impact kubwa sana kuhusu Mungu kwa mtoto wako.

TUMIA MUDA PAMOJA KAMA FAMILIA
Kila mtoto ana picha ya wazazi (baba na mama) na kwamba anajisikia raha pale anapokuwa pamoja na wazazi wote.
Pia kama mzazi jifunze kumfurahia mtoto, jitahidi mtoto ajisikia raha kuwa na wewe na si kukukimbia.

MBARIKIWE

No comments:

Post a Comment