Thursday 3 December 2015

NISIKILIZE KWA MAKINI..!

Kuna aina mbili za wanaume, wa kwanza ni wenye HESHIMA na wa pili ni wale WASIO NA HESHIMA.

Usikubali kuolewa na mwanaume kabla hujafahamu tofauti hizi mbili, mwanamke unayemuona kwenye kioo chako cha kujitazama atakushukuru sana.

Mwanaume mwenye heshima atakulinda, atalinda moyo wako na hisia zako, atasimama imara kulinda kiroho chako na mwili wako, kumchagua mwanaume mwenye heshima ni kuchagua maisha bora katika ndoa.
Wewe mwanamke si gari; Ukikutana na mwanaume anayetaka kukujaribu kama gari, palepale mwelekeze kwa wanaouza magari, mwambie kwa heri na usigeuke nyuma.

Ndiyo umekutana na mwanaume handsome, anaonekana ni mwema, mpole na anaonekana ana akili na shule imekubali na katika kuongea naye anakwambia ana mtoto na hana mpango wa kumtunza wala kumuona mama yake huyo mtoto;
Haraka iwezekanavyo mpeleke kwa mama wa huyo mtoto, USIANGALIE NYUMA anza mbele kwa kasi ya ajabu.
Usifanye kosa lilelile ambalo mama wa mtoto alifanya.
Kwani kuna tofauti gani kati ya mama wa huyo mtoto na wewe, kwa taarifa yako wote ninyi ni wanawake!

Jipende mwenyewe kwanza!
Kama huwezi kujipenda mwenyewe na kufurahia maisha mwenyewe, nakwambia upo off the market; usifanye kosa, kama hujipendi mwenyewe hakuna MWANAUME ANAWEZA KUKUPENDA ...

Usiwahukumu wanaume wote kwa sababu ya kosa la mwanaume mmoja; labda kama unataka wanaume wote wakuhukumu wewe kwa kosa la wanawake wengine wasio na adabu.


Je, unajikuta unawavutia wanaume ambao tabia zao ni mbovu?
Basi jichunguze aina ya perfume unatumia kwani wanaume walio na tabia mbovu huvutiwa na aina ya perfume mwanamke anatumia, serious!


Usijidanganye!
Urembo wako, umbo lako, uwezo wako kitandani, ustadi wa kupika chakula, uwezo wa kutetea wanawake wengine hata haiba yako inayovutia haitaweza kumfanya mwanaume abadilike; Never!

Kama mchumba wako anakuahidi kitu na hatimizi, weka rekodi, ukiona hii tabia inajirudiarudia, inawezekana anacheza na feelings zako, pia ni warning signs kwamba huna thamani yoyote kwake na inawezekana hakupendi na hakujali kabisa, Think twice.

Sawa, umekutana na mwanaume si mume wako anakutaka kimapenzi, huna haja kushangaa, huyo hakuheshimu !

Unajiuliza;
“Kwa nini hanipigii simu, kwa nini hana muda na mimi, kwa nini haoneshi kama ananipenda?”
Jibu ni kwamba ni kweli hana mpango na wewe, na kama hutamwacha aende zake na wewe kuendelea na maisha yako basi unachofanya ni kuzuia mtu wa kweli kuja katika maisha yako na kupata penzi la kweli.


Kuna baadhi ya wanaume hupenda kupiga wake zao haijalishi wamesoma au hawajasoma, wanapesa au hawana pesa, kwani kumpiga mke huwapa sense ya kujisikia kwamba wana power/control, na ukijipeleka mwenyewe kwa wanaume kama hawa wanaweza kukufanya wewe ni punching bag.
Ni muhimu sana ukiwafahamu tangu mapema ili uwaepuke.

IKIWAKA MULIKA

No comments:

Post a Comment