Friday 4 December 2015

KWENU WANAUME.

Kuishi na mwanamke kunahitaji mwanaume kuwa makini na jinsi unavyoishi naye pamoja na unavyoongea naye na mawasiliano yote kwa ujumla.
Mawasiliano ni ufunguo kwa mwanamke kumfurahia mume wake.
Ukiongea na mke wako kama mwanamke mrembo naye atajiona ni mrembo ukiongea na mke wako kama vile ni jimama lililopitwa na wakati ni kweli anajiona amezeeka na kupitwa na wakati.

Jambo la kwanza msifie kwa jinsi anavyoonekana yaani nguo alizovaa, nywele, viatu na hata perfume, anyway vitu hivi anavaa kwa ajili yake na wewe pia.
Kwa kumpa compliment basi atakuwa na confidence na kwamba umevutiwa na atajisikia vizuri. Suala la nguo ni kitu muhimu sana kwa mwanamke ndiyo maana hata wenyewe kwa wenyewe huweza kupeana sifa,
je wewe mwenye mali naamini si zaidi?

Unavyozidi kumsifia mwanamke kwa mwonekano wake, jinsi anavyofanya vizuri kitandani, jinsi alivyo, tabia njema na kila kitu anafanya naye atajitoa zaidi kuhakikisha anakupa huduma za uhakika.
Jambo la msingi hapa unaanda akili yake kwa ajili ya kuwa mwili mmoja baadae.

Jambo la pili ni muhimu sana kumuuliza jinsi alivyoshinda hasa ukikutana naye jioni baada ya kazi.
Hata hivyo unatakiwa kuwa makini sana na jibu la swali kwani kama alikuwa na siku mbaya anaweza kukumwagia kopo zima la worms. Pia unatakiwa kuwa na tactics za kuhakikisha unabadilisha mambo mabaya anayokwambia na kuwa mazuri au kubadilisha somo.
Kumbuka lengo lako ni kutaka kutengeneza mazingira ya yeye kuwa na mood nzuri kwa ajili ya kuwa mwili mmoja.

Jambo la tatu hakikisha anajifahamu jinsi unavyojisikia kuhusu yeye na pia ni jinsi gani unajisikia vizuri kufanya mapenzi, tendo la ndoa au kuwa mwili mmoja na yeye.
Kama umezoea kuwa na utaratibu unaojirudiarudia unatakiwa kubadilisha. Ikiwezekana kuanzia sasa kila touch mwilini mwake kuanzia mwanzo hadi mwisho hakikisha unamwambia unavyojiskia raha. Hakikisha amejifunza na anafahamu unavyojisikia unapombusu, mkumbatia, mpenda, mshika, mnusa, muonja nk zaidi mhakikishie jinsi unavyojisikia akikupa mahaba.

Jambo la nne hakikisha unamsifia mbele za watu au mbele za rafiki zako na zaidi sana ukiwa chumbani hakikisha unamuandaa hadi yeye analilia wewe kumuingia ili kuwa mwili mmoja hiyo ina maana kwamba utakuwa umemuandaa vya kutosha, tumia mwendo wa kobe na si cheater.

Jambo la tano, hujawahi ambiwa na mke wako kwamba “ hujawahi nipeleka hata Bagamoyo tu: hii ina maana kwamba anataka siku moja upange muwe na outing ya uhakika wewe na yeye tu, maana yake anataka romance. Hivyo fanya kweli maisha ni sasa!

Hii ilikuwa kwa ajili ya wanaume tu, nashangaa wewe ni mwanamke na umesoma hadi mwisho, ok haina shida muonyeshe ujumbe huu Mumeo.

No comments:

Post a Comment