Friday 4 December 2015

HAMU YA SEX HUTOFAUTIANA.

Katika mahusiano mengi mmoja ya wanandoa huwa na hamu ya sex na kutaka sex mara nyingi zaidi kuliko mwenzake kwa sababu binadamu tunatofautiana levels za drive ya sex.

Kama wewe na mwenzi wako mna kiwango kinachofanana cha kuhitaji sex basi ninyi mmebarikiwa.

Ukweli ni kwamba suala la sex ni moja ya eneo ambalo ni tete sana katika ndoa, ndiyo maana kukataliwa sex na mwenzi wako huwa ni jambo linaloumiza sana (hasa wanaume) ingawa wapo wanawake wana drive kubwa ya sex kuliko mwanaume ambaye siku zote anaonekana anahitaji sex 24/7.

Hata hivyo kuna sababu za msingi za kibaolojia zinazopelekea mmoja wa wanandoa kuhitaji sex zaidi ya mwenzake.

*Nini husababisha hamu ya sex?
Hamu ya kutaka sex husababishwa na homoni ambayo kitaalamu huitwa testosterone.
Wote wanaume na wanawake wanayo hii homoni kwenye miili yao.
Wanaume wanayo nyingi zaidi kuliko wanawake kwa sababu wanawake wanayo homoni nyingine inayojulikana kama estrogen.

Msingi ni kwamba kiwango cha testosterone ulichonacho mwilini huweza kuelezea ni kiasi gani au hamu ya sex itakuwaje.
Ukiwa na kiwango kikubwa unakuwa na sex drive kubwa na ukiwa na kiwango kidogo unakuwa na sex drive ndogo.

Mbili ya tatu (theluthi mbili) ya wanaume wana kiwango kikubwa sana cha testosterone na hii husababisha wao kuwa na hitaji kubwa la sex.
Moja ya tatu ya wanaume wana kiwango kidogo cha testosterone na husababisha wao kuwa na low sex drive.

Kwa upande mwingine mbili ya tatu (theluthi mbili) ya wanawake wote wana kiwango kidogo cha testosterone na husababisha wao kuwa na kiwango cha kawaida cha drive ya sex na moja ya tatu (theluthi moja) tu ndiyo wenye kiwango kikubwa cha testosterone na hawa huwa na sex drive kubwa.

Hii ina maana kwamba mbili ya tatu ya wanaume wenye strong sex drive huishia kuishi (kuoana) na wanawake ambao wana sex drive kidogo na wapo wanawake hujikuta wapo ndani ya nyumba na wanaume (theluthi moja) ambayo sex drive ni ndogo sana.

*Je, ni homoni peke yake husababisha kutokuwa na hamu ya sex?

Siyo homoni peke yake ndiyo inayosababisha mwanaume au mwanamke kuwa na sex drive ndogo kuna vitu vingine vingi huweza kufanya sex drive kuwa ndogo kama vile kuchoka na kazi, kulea mtoto, migogoro katika ndoa, nk.

Pia ni jambo la msingi kutambua kwamba kwa mwanamke suala la maisha huchukuliwa kwa pamoja kwa maana kwamba yupo connected na kila eneo la maisha yake kama vile familia, kazi, sex nk.

Kama mwanamke amekuwa na siku mbaya kazini au amekuwa na wakati mgumu na watoto wake ni ngumu sana kujisikia ana hamu na sex.

Wanawake huhitaji muda wa kuondoa masumbufu au kusafisha mawazo yao kabla ya kujihusisha na sex na hii hufanywa na mwanaume ambaye kwake ni mtu wa karibu.
Mwanamke huhitaji kuwa connected na mume kabla hajawa tayari kujiingiza kwenye masuala ya kuwa mwili mmoja.

No comments:

Post a Comment