Monday 14 December 2015

SIKIA HII..!

Wanaume wengi huwa hawaoni umuhimu wa kuwabembeleza wake zao kwa kuwakumbatia, pakata , busu, shikashika nk) baada ya sex.

Kibaolojia mwanaume akimaliza sex anarudi kwenye hatua yake ya kawaida (pre- aroused state) na mwanamke akimaliza sex (baada ya kufika kileleni) huwa anarudi katika yali ya kuwa nusu yaani semi- aroused state) yaani kwake bado moto upo na anaweza kupika tena chakula.

Hii ina maana kwamba mwanaume akimaliza tendo la ndoa anakuwa ameishiwa nguvu au anaenda ICU kwa matibabu ya karibu, hajiwezi wengine ndo huishia kukoroma kiasi kwamba hata vibaka hawawezi kuingia hiyo nyumba, wakati huohuo wanawake wao wakimaliza bado huhitaji kuendelea na tendo la ndoa zaidi na zaidi na kwao cuddling ni kuwapa connection na wakati mwingine y na sex tena na tena.

Hivyo ili mwanamke asiamini kwamba mwanaume huna feelings kama jiwe, inakupasa wewe mwanaume baada ya kumaliza sex fanya hitimisho kwa kuendelea kumkumbatia, busu na kumpa maneno matamu ya sifa na kimapenzi, kumbuka ni mkeo hivyo mpe kila anastahili na utaona mabadiliko.

Pia wanawake wengi wanashangaa kwa nini mwanaume anaweza kutenganisha sex na love.
Wakati wa sex wanawake huzalisha kiwango kikubwa sana cha homoni ya oxytocin ambayo husaidia kuwasisimua katika emotions zao na wanakuwa connected na mume wake wakati wa sex na hii husababisha mwanamke kujihusanisha sex na emotions (love).
Wanaume hawazalishi na kama yupo anayezalisha hiyo homoni basi ni kiwango kidogo sana kiasi kwamba kwake sex na love ni vitu viwili tofauti.
Ndiyo maana ni rahisi kwa mwanaume kufanya mapenzi na mwanamke ambaye hampendi na kwa mwanamke ni ngumu kwani mwanamke upendo kwanza ndipo huwa tayari kwa sex.

Mume ambaye hamjali mke, hampendi, hampi sifa kwa yale mke anafanya na kumkosesha upendo atajikuta kila siku anaomba sex na mke akijitetea kichwa kinauma.

No comments:

Post a Comment