Wednesday 24 June 2015

NAKUPENDA..

Hivi unafahamu ni kitu gani kinaweza kumfanya mume wako au mke wako kuwa na mood kwa ajili ya sex?

Watu wanaofahamu hii sanaa wanasema kuna mambo 4 muhimu ambayo yanaweza kumfanya mke au mume kuwa na mood;


1:- Ni kile anaona; kwa maana kwamba anasisimka na kupata mood kutokana na kile anaona kwa macho yake kwako,

2:- Ni kusisimka na kupata mood kutokana na namna anaguswa (touch).

3:- Anasisimka na kupata mood kutokana na kile anasikia na

4:- mwisho huweza kupata mood kwa kuhusanishwa; kwa maana kwamba anasisimka kutokana na uangalifu anaopewa kihisia na wewe namna ulivyo caring and loving.
Kila mmoja wetu husisimka na kupata mood kwa ajili ya sex kwa hayo mambo manne hata hivyo kila mmoja hupendelea moja zaidi kuliko mengine.
Je, kati ya hayo mambo manne ni lipi humsisimua sana mke wako au mume wako?


Ukweli ni kwamba linapokuja suala la sex suala zima la kupeana mood ni namna kila mmoja anavyojiweka kwa mwenzake (presentation)

MFANO:
Ikiwa mwanamke atafahamu namna ubongo wa mwanaume unavyofanya kazi linapokuja suala la sex, basi ni rahisi sana kwake kumtega na kumweka kwenye mood ya sex hata kama hakutegemea.
Ni kawaida mume akiona chuchu za mke wake hata kama ni ndani ya nguo nyepesi aliyovaa, mume huweza kuanza kusisimka, wapo ambao hufika mbali kwa kuweza kuyeyuka mzimamzima hadi chini ya sakafu huku Mr.uume akifanya vitu ambavyo hajatumwa.
Mke akimjaribu kwa kufunua na kufunika hizo chuchu zake mbele ya macho 2 ya mume wake anaweza kuona mumewe anaanza kulegeza kwani magoti huanza kukosa kuvu na kuwa weak.
Fikiria wewe ni mke na ni saa nne na nusu usiku; mume wako yupo chumbani na wewe upo bafuni unaoga, ile mume kusikia sauti ya maji unapooga kwake ni foreplay tayari.
Si unataka awe na mood, unaamua kutoka bafuni huku umejifunga kipande cha khanga huku headlights (chuchu) zako zinaonekana ndani ya khanga na baada ya kuingia chumbani unamsogelea, mwangalia usoni, inama kumwelekezaj yeye kuhakikisha anaona au kugusa matiti na headlights zako na kumwambia “Nakupenda” kisha Mwangalie anavyohema!

No comments:

Post a Comment