Saturday 27 June 2015

AINA ZA CHEATING.

Kama wanandoa wapo katika kufanya matengenezo ya damage iliyofanywa na mwanandoa mmoja kuchepuka basi ni muhimu kufahamu kitu ambacho wanashughulika nacho kwani bila kufahamu ni sawa na kumpa mgonjwa wa Malaria dawa za kutuliza maumivu ya meno.
Watu wanaotoka nje ya ndoa wamegawanyika katika makundi makubwa matatu ambayo ni:
1. KUCHEPUKA KWA USIKU MMOJA.

2. KUCHEPUKA KWA KUNASWA NA KUFUNGAMANA.

3. KUCHEPUKA KWA URAIBU.

UFAFANUZI ZAIDI:

1. KUCHEPUKA KWA USIKU MMOJA.

Hutokea katika jamii ambayo masuala ya sex yameilemea, kukosa uadilifu, kukosa nidhamu na kuheshimiana.
Katika modern world ambapo watu wanasafiri (business trips) sana basi cheating za usiku mmoja kwa wanandoa zimekuwa nyingi kuliko watu wanavyofikiria hasa baada ya wanawake kuingia kwa wingi katika ajira zinazowafanya wasafiri mara kwa mara.
Hii hutokea kwa kufanya sex kwa usiku mmoja (au mara moja) bila hata kuwa na uhusiano na baada ya sex wahusika hawajuani tena.
Wakishamaliza haja zao kinachofuata ni kumpiga chini huyo mhusika kama vile hawajuani.
Hutokea ghafla kutokana na kushindwa kuhimili tamaa za kimwili au kuwaka kwa tamaa.
Ni rahisi mhusika kurudi kwenye mstari kama vile Daudi alipokuwa confronted na Nabii Nathani aliutubu dhambi yake (2 Samuel 12)
Wanaume au wanawake wa hili kundi akibanwa na kukomaliwa anaacha na kugeuka.
Hii haina maana kwamba cheating kama hii haina damage kwani isiposhughulikiwa vizuri huweza kuzaa affair nyingine.
Kama umefanya affair kama hii na umeficha fahamu kwamba hilo ni bomu ambalo muda wowote linaweza kufumka na kuleta madhala katika ndoa iwe kukosekana kwa ukaribu na partner wako au kujiingiza zaidi kwa mwingine nje ya ndoa.

2. KUCHEPUKA KWA KUNASWA NA KUFUNGAMANA:

Hapa cheating huanza kwa mahusiano na urafiki na hatimaye kuwa na uhusiano wa kimapenzi wa kudumu kwa muda mrefu na kuvunja hii bond huhitaji kazi ya ziada.
Hutokea polepole na baadae baada ya urafiki kukomaa kutokana na mazingira ya kufanya kazi pamoja au kuhusiana katika shughuli mbalimbali na kujenga urafiki na mahusiano.
Wanakuwa wame-fall in love kama mahusiano ya ndoa yanavyoanza.
Wanapokuwa pamoja hujikuta wanatimiza lile hitaji ambalo mmoja au wote wanakosa kwenye ndoa zao.
Hapa ndipo tunakutana na neno “nyumba ndogo”.
Huwa kazi sana kuvunja mahusiano kama hayo kwani watu hawa huwa na uhusiano unaohusisha mioyo na hisia zao.
Pia ili kuvunja uhusiano wao lazima mwanandoa ajue “hitaji” ambalo lilikuwa linakosekana nyumbani au katika ndoa hadi mwenzake akanasa kwa huyo mwanamke au mwanaume.

3. KUCHEPUKA KWA URAIBU:

Hutokea kwa kusukumwa hisia zake kwa kuwa hana uwezo wa kuhimili emotions ni kama mvuta sigara au mlevi wa pombe.
Haya ni mahusiano tofauti kabisa na kundi la kwanza na la pili hapo juu.
Kwa kuwa ana hisia zinazomsukuma anaweza kuathiri hata maisha yake kwani huwa Huyu huwa na msululu wa partners kila port meli yake inatua au mji.
ladha kutoroka kazi na kujiingiza katika sex haramu kama vile ukahaba, ubakaji, pornography na anaweza kukamatwa na polisi mara kwa mara kutokana na addiction aliyonayo kuhusiana na ngono.
Pia anakuwa na risk kubwa kupata magonjwa ya zinaa (bila kusahau UKIMWI) kutokana na tabia zake, wakati mwingine huuawa kutokana na kuwa violent.
Wakati mwingine anakuwa mwizi, mwongo ili kukamilisha kiu yake.
Pia huendana na tabia chafu na za ajabu zinazohusiana na masuala ya sex kama kubaka, sex kinyume na maumbile, kupigana nk.
Ili kuvunja tabia kama hii huhitaji ushauri kutoka kwa mtaalamu wa masuala ya addictions ambaye anaweza kutumia approach tofauti na aina zingine.

No comments:

Post a Comment