Monday 29 June 2015

KUCHEPUKA..(PART 2)

Moral standard za ndoa sasa zimeshuka kiasi kwamba
si ajabu tena kuona bibi harusi na vazi la harusi huku ana mimba kubwa!

Karibu watu wote wanaokamatwa na suala la kutokuwa waaminifu katika ndoa zao hukubali kwamba ni kweli wamekosea na wengine husema ni shetani tu aliwaingia.
Tafiti zinaonesha kwamba katika jamii yoyote duniani asilimia 25 ya wanaume huchepuka nje ya ndoa zao na asilimia 10 ya wanawake hukiri kuchepuka kwenye ndoa zao hii haina maana wanandoa wenzao hujua suala ni kwamba huwa wanakiri kwamba wamewahi kutoka nje ya ndoa zao.

NINI HUSABABISHA WENGI KUCHEPUKA

Kutoridhika na ndoa zao idara zote na kuanza kutafuta mtu wa nje ili kuridhishwa.

Matatizo ya familia.
Wengine hujikuta amempenda mtu mwingine.

Kutengana kwa muda mrefu mume na mke inaweza kuwa masomo au kazi nk.

Kushuka kwa kiwango cha kiroho cha wanandoa.
Kuhitaji kuridhishwa zaidi kimapenzi; kuna watu wana libido la ajabu!
Kutafuta Kujiamini na kutambuliwa kwamba yeye ni nani katika jamii
Kuikata kweli ya Neno la Mungu.

Ukaidi na uhuni.
Hitaji la kupendwa baada ya kutelekezwa.
Kuzaliwa mtoto wa kwanza katika ndoa; Feelings za kumpa mume huhamia kwa mtoto na wanandoa hujikuta wapo emotionally distant.


NINI HUSABABISHA WENGI KUGOMA KUCHEPUKA.

Kujitoa kwa ndoa na kulinda ahadi na agano (covenant)
Kuaminiana kwa wanandoa.

Sababu ya dini yaani wokovu (uhusiano binafsi wa mwanandoa na Mungu).

Kuogopa matokeo ya kuchepuka kama vile magonjwa (UKIMWI) na crisis zingine.

Kujifahamu na kukomaa kiakili na Kujiamini.

Kupenda mke na watoto na kuwapa heshima iliyotukuka na kuishi kwa mfano kimatendo na kimaneno.

Uadilifu (moral standard)

No comments:

Post a Comment