Tuesday 23 June 2015

MAWASILIANO KATIKA TENDO LA NDOA.

1:-Uwe mkweli, muwazi, unayeongea moja kwa moja bila kuzunguka, usijifanye (pretending), uwe wewe halisi, kama hufahamu mke wako au mume wako anawaza nini, anahitaji kitu gani, au anajisikiaje (inawezekana hujui) muulize, usifanye kwa kudhania.

2:- Achana na imani potofu kwamba mwanaume anafahamu yote au anatakiwa awe anafahamu kila kitu kuhusu kufanya mapenzi.
Hakuna mwanaume anayefahamu mwanamke anavyojisikia, au ni kitu gani anahitaji ili kufika kileleni, kila mwanamke ni tofauti, ni muhimu sana kuwasiliana ninyi wawili.
Usiache kujadili ili kuondoa tatizo.
Kila mmoja lazima awasirishe kwa mwenzake namna au ni kitu gani kinamfanya ajisikie vizuri wakati wa sex.

3:- Sahau imani potofu kwamba mwanaume siku zote ndiye anatakiwa kuanza, au mwanaume anawajibika kuhakikisha sex inakuwa tamu, au Kumwachia mume afanye kila analoweza kukufanya wewe mwanamke ujisikie vizuri huku wewe umelala kama gogo huna habari unasikilizia tu.
Hayo ni mawazo potofu ambayo ni ya kizamani.

Asilimia 80 ya wanandoa wanaoridhishwa kimapenzi ni pale ambapo mke na mume wote hujihusisha na kusaidiana kupeana raha ya mapenzi.


4:- Jitahidi sana kuachana na mawazo negative kuhusu mke wako au mume wako, ni muhimu sana kuwa makini kumlaumu mwenzako kutokana na matatizo yako.

Hizi negative thinking ni vitu vinavyoficha udhaifu wa mhusika mwenyewe.


5:- Hakuna kitu kinachoweza kuharibu mapenzi kama tabia ya kulaumiana.

6:- Mara nyingi ni vizuri kuonesha namna ya kufanya kitu fulani kuliko kuelezea kwa maneno.
Kama mwanaumke anachukua mkono wa mwanaume na kuupeleka kadi kwenye kisimi na kumuonesha namna ya kufanya huleta mawasiliano mazuri kuliko kubwabwaja maneno.


7:- Usitegemee maisha ya mapenzi kuwa juu siku zote.
Namna wanandoa wanashiriki tendo la ndoa hutofautiana kila baada ya muda fulani. Hakuna kitu kinaitwa perfect, ingawa ni kweli una haki ya kufurahia maisha mazuri ya sex.
Ni muhimu kuongelea “new things” na msisahau kucheka pamoja pia.

No comments:

Post a Comment