Saturday 27 June 2015

KWANINI WANAWAKE HUBADILIKA?

Wanaume wengi walio katika ndoa hulalamika kwamba hawapati sex kiasi cha kutosha kutoka kwa wake zao kama ilivyokuwa zamani au mwanzo wa ndoa zao.
Wanaume hawa hushangaa ni kitu gani kimetokea kwa wake zao ambao si suala la kupoteza hamu ya sex tu bali hujisahau na kuacha kuwa na mwonekano unaovutia kimapenzi.
Ni kweli wanawake wanafahamu sana namna ya kumvutia mwanaume wanayemhitaji na hii hujidhihirisha pia siku za uchumba au mwanzo za ndoa ambapo mwanamke hupendeza kimavazi na hata kunukia.
Enzi zao wakati wa uchumba au ndoa ilipokuwa mpya huweza mwanamke alivalia nguo zinazovutia na kuonekana ni mke na si mama, alichagua nguo za kuvaa chumbani (sexy) na za kuvaa sebuleni au kazini. Alijipamba kwa makeup za uhakika kuanzia kwenye kucha za miguu hadi nywele.
Alijipulizia delicious perfumes kama moja ya strategy kuhakikisha mume anavutiwa na anatulia ndani.
Ukirudi kwa namna alikuwa anaongea kwa sauti ya Urembo basi mwanaume alijiona kama ni ndoto za kumpata mwanamke anayemtaka zimetimia.
Hata hivyo baada ya miaka kadhaa na watoto kuzaliwa mke badala ya kuwa mke sasa amekuwa mama, na mama kwelikweli kwani kuoga kwenyewe kazi hadi muda wa kwenda kulala, mwili mzima ni maziwa ya mtoto ndo imekuwa perfume, kajichokea mwenyewe kama kuolewa ameolewa who cares!
Mume anashangaa hivi ndo huyu mwanamke wa wakati ule mboni sasa hata kuoga hadi nimkumbushe!
Sex ndo usiseme ni kuvutana kama manati!
Sex ilikuwa mara 3 au 4 kwa wiki sasa ni mara moja napo lazima mwanaume akomae maana bila kukumbushia mwezi unapita.
Mwanaume anajikuta thamani yake ni sawa na kipande cha furniture
Kila kitu sasa kimekuwa watoto kwanza na wewe mume ni mtu mzima subiri.
Hata hivyo tukumbuke kwamba:
Kuwa mwanamke katika ulimwengu huu wa kisasa ni kazi sana kwani mwanamke huyohuyo mwenye mtoto ndiye Anafanya kazi zote za nyumbani na ndiye anaenda ofisini na ndiye Anahakikisha mume ametimiziwa mahitaji yake yote. Mke akifika muda wa kwenda kulala anakuwa amechoka na hatazamiki.
Hivyo kukosa hamu ya sex huja bila yeye kuwa na uwezo wa kufanya chochote kwani majukumu na kuwajibika ndiko kumemfanya kujisikia hivyo.
Na wapo wanaume huchukulia wake zao “for granted” na huhitaji sex wakati siku nzima hajafanya jambo lolote kumsaidia mke na hata kuwasiliana naye acha kuonesha upendo.
Ukweli ni kwamba:
Ndoa ni kazi (hard work) ambapo mume na mke wote kwa pamoja hawatakiwi kuanza kulaumiana badala ya kushirikiana pamoja kwanza kusaidiana kazi za nyumbani na mume kumtengenezea mke wake mazingira mazuri ambayo atajisikia hajachoka.
Binadamu ni wepesi sana kulaumu mwingine pale mambo yakiwa yanaenda visivyo na wanandoa kwa hili ndo wenyewe.
Kuimarisha afya ya uhusiano wa kimapenzi kati ya mke na mume ni kazi inayoendelea maisha yao yote ya ndoa.
Kuonesha upendo kwa vitendo na mawasiliano mazuri ni mambo muhimu sana kwa ndoa imara.
Ndiyo kuna wanawake ambao baada ya kuolewa na kuzaa watoto hujisahau, hata hivyo wengi ni kutokana na wanaume wenyewe wanavyochukulia ndoa zao.
Kama ni mwanaume unahitaji mke awe na hamu ya sex basi unahitaji kumjengea mazingira ya kuhitaji sex na si kulaumu tu.

No comments:

Post a Comment