Thursday 28 January 2016

WANAUME HUKOSEA HAPA TU..

Wanaume mara nyingi hujulikana kwa kuwa wajuaji, hata kama kitu hajui basi akiwepo mwanamke huanza kuonesha anajua na ikiwezekana anaweza kuonesha kwamba yeye ni expert wa hicho kitu.

Lakini linapokuja suala la tendo la ndoa wakati mwingine mume hujikuta amekwama kwenye basic errors and omissions na kusababisha makosa makubwa kama si usumbufu kwa mke wake.

Wakati mwingine tatizo ni mazingira kwani wanaume wengi hulelewa katika mazingira ya kuhakikisha yeye anakuwa breadwinner wa familia yake na suala la mahusiano (ndoa, mapenzi) hujifunza mwenyewe.


Hebu tuangalie kwa ufupi baadhi ya makosa ambayo mara nyingi mwanaume hufanya akiwa na mke wake chumbani.


1.ANAJIFANYA ANAJUA KILE MKE WAKE ANAHITAJI CHUMBANI:

Mara nyingi mwanaume hufanya mapenzi na mke akifikiri kwamba kile anafanya basi mke atakipenda hii ni kutokana kile anajua yeye kuhusu mwanamke.

Ukweli ni kwamba kila mwanamke yupo tofauti.

Kumbuka hata mwanamke mmoja anatofautiana namna ya kusisimka kimapenzi hata kwa mwezi mmoja au miaka kadhaa katika mahusiano ya kimapenzi na mume.

Si mara zote katika mwezi au miaka yote katika ndoa basi mwanamke kila siku mkiwa chumbani ukigusa matiti yake anasisimka.


Hii ina maana kile kinachomfanya kusisimka zaidi mwanzo wa mwezi ni tofauti na katikati ya mwezi na mwisho wa mwezi hii ni kutokana na utendaji wa hormones.

Pia kile kilichokuwa kinamsisimua sana miaka 5 iliyopita kinaweza kuwa tofauti sana na mwaka huu.


2.ANAJIFANYA ANA KILA ANACHOHITAJI MKE.

Wapo wanawake ambao hataweza kufika kileleni maishani mwake, kwani ili kufika kileleni anahitaji kusuguliwa kisimi mizunguko 3,000 kwa dakika moja. Je, ni kiungo gani cha binadamu kinaweza kufanya hiyo kazi?

3.KUDHANI VILE MWANAUME UNAJISIKIA WAKATI WA TENDO LA NDOA NI SAWA NA MWANAMKE.

Anavyojisikia mwanaume na mwanamke ni tofauti kutokana na umbali wa uume kwenye uke.

Eneo linalozunguka uke huwa sensitive zaidi kuliko ndani kabisa.

Hivyo deep thrusting wakati mwingine huweza kusababisha mwanamke kusikia kizunguzungu kama si tumbo linapigwa ngumi.


4.UNADHANI UNAFAHAMU ELIMU YA MAUMBILE YA MWANAMKE.

Wanaume karibu wote wanafahamu kisimi au kinembe kipo wapo ingawa hawajui kina manufaa gani kwa mwanamke na yeye mwenye mwanaume kuhusiana na suala la tendo la ndoa.

Na bado wanaume wengi wanaamini kwamba mwanamke lazima afike kileleni kwa njia ya uke tu na si kisimi.

Kwa wanawake wengi kufika kileleni kwa njia ya kusuguliwa uke (intercourse bado ni kitendawili (utakesha).

Pia tatizo kubwa wanaume wengi hawafahamu ni namna gani kisimi kihudumiwe, namna anavyohudumiwa mwanamke mmoja inaweza kuwa si lolote kwa mwingine kwani kila mmoja ana aina yake.

Ukitaka kufahamu namna gani ahudumiwe kisimi chake, muuulize mke wako mwenyewe.


5.UNADHANI AKIWA WET MAANA YAKE AMESISIMKA.

Kuna wakati baadhi ya wanaume hujikuta kwenye mataa baada ya mke kushindwa kuwa wet.

Kuna imani potofu kwamba akiwa wet maana yake amesisimka hata hivyo wanawake hutofautiana kuna wengi huwa wet zaidi ya wengine na wengine kuwa wet si kawaida yao.

Pia kuwa wet hutofautiana kutokana na siku zake au mzunguko wake, pia stress na medication na wengine wana tatizo la hormones.

Jambo la msingi mfahamu vizuri mke wako, jambo la msingi anatakiwa kutayarishwa kabla hata hajaingia chumbani ili akiingia chumbani awe alishajiweka na kuwa tayari hapo itakuwa sahihi kwamba “wet means stimulated”


6.UNADHANI KUWA BUBU NDO KANUNI ZA MCHEZO.

Wanaume wengi hudhani kuwa kimya wakati wa tendo la ndoa ndiyo kanuni bora.

Ukweli ni kwamba unampa wakati mgumu sana mke wako kukisia kile unahitahitaji ili kuridhishwa kimapenzi.

No comments:

Post a Comment