Sunday 24 January 2016

TATIZO SI SIZE,TATIZO NI UBUNIFU WAKO.

Kwa wanaojua Mchezo wa Soccer; Kitu cha Msingi si Size ya Kiatu, Bali ni Skills za Mchezaji Mwenyewe ndiyo Zinawezesha Mchezo uwe mtamu na Kisha Magoli ya Kutosha.
Maswali ambayo huwasumbua sana Wanandoa wengi na yamefika mezani kwa madaktari wa mambo ya afya na mahusiano ni kuhusu wanawake kutofika kileleni (orgasm) na wanaume kumaliza haraka tendo la ndoa (ejaculation) na pia, je kuna uhusiano wowote kati ya mwanamke kufika kileleni na size ya kiungo nyeti (penis) cha mwanaume?

Ukiangalia haraka unaweza kusema hayo mambo mawili yanafanana; kwani kama mwanaume anaweza kumaliza haraka (kukojoa au kufika kieleleni), ina maana ni dhahiri mwanamke atakosa kufika kilele kwani mwanaume anakuwa alishamaliza zamani,
Lakini ukweli ni kwamba kama mwanaume atamuandaa mwanamke vizuri basi hata kama huwa anawahi kumaliza haraka (dakika 2) itakuwa haina shida.

Pia watu bado wanajiuliza, ni size gani na urefu gani unafaa kwa kiungo nyeti cha mwanaume kuhakikisha mwanamke anafika kileleni?
Je ni udogo kiasi gani unafaa kumwezesha mwanamke kufika kileleni?

Wapo wanaume kutokana na walivyoumbwa kuwa na umbile dogo automatically hujasikia inferior au vibaya na kujiona kama vile hawana uwezo wa kuwapa wapenzi wao mapenzi halisi na kuwafikisha kule wanataka na matokeo yake wengi huwa hawapo wazi kujiachia kwa wake zao au wanaogopa hata wake zao kuona na kuwapa uhuru kukifurahia hicho kiungo nyeti na adimu wakati wa tendo la ndoa.

Kila mwanaume ana kiungo tofauti kama ilivyo kwa alama za vidole vilivyotofauti kwa kila binadamu.
Ukubwa au kimo cha kiungo si msingi wa ufanisi wa utendaji wa tendo la ndoa bali muhusika mwenyewe ndiyo msingi wa mafanikio katika tendo la ndoa.
Huhitaji kuwa mjinga kiasi hicho kudhani kwamba urefu au ufupi, unene au wembamba wa penis ndiyo unafanikisha mke wako wako au mpenzi wako kufikia kilele; badala yake unaweza kumsababishia maumivu na kumkosesha raha ya mapenzi.

Hata mwanaume mwenye penis ndogo anaweza kuwa mtaalamu wa kumfikisha mke wake katika furaha ya kweli katika tendo la ndoa.
Njia pekee ni kijifunza jinsi ya kufanya mapenzi vizuri, jinsi ya kuwa partner mzuri.

Huo ni mwili wako upende, jifunze kuutumia, jitahidi kuutumia kwa ubunifu na kwa kimahaba zaidi.
Mbusu na kumpa mgusu wa mwili mpenzi wako kwa muda mrefu hadi unahakikisha amenyegeka vizuri kwa kumchezea sehemu zote ambazo ukimgusa anapata raha inayomuwezesha kuwa hot kwa kuwa ni partner wako; mwili wake wote ni mali yako na ni wewe, hivyo safiri kila sehemu ya kiungo cha mapenzi kwa kadri unavyoweza kuliko kukimbilia kumwingilia wakati hata hajanyegeka.

Amini, usiamini kila mwanamke anapenda mwanaume au mume ambaye ana kipaji, talent, ana ubunifu, aliyemtaalamu anayeweza kumpa romance ya uhakika na si kuwa na penis kubwa tu bila ujuzi then baada ya dakika 2 upo pembeni unapiga usingizi wakati partner wako anaugulia kwa kuachwa kwenye mataaa.
Hapo ndipo utasikia mwanamke anasema hajisikii kama unampenda anaona kama vile unamtumia tu ili kutimiza matakwa yako ya mapenzi.

Kuwa na kiungo kidogo siyo kosa wala uhalifu bali umeumbwa hivyo na kuujua mwili wako na kujua majibu sahihi ya mahitaji ya kimahaba kwa mke wako hiyo ndiyo akili na unaonekana mwanaume Smart kwani wewe ndo unajua kupenda, unajua mapenzi.

Kuhusu mwanaume kumaliza haraka, pia si kosa wala uhalifu hata kukufanya ujione si lolote, badala yake elekeza jitihada katika kukabiliana na hilo tatizo na inawezekana kwa kupata ushauri wa daktari au kufanyiwa maombi.

Kitu cha msingi unatakiwa kujua kwamba kuna tofauti kubwa sana za kijinsia kati ya mwanaume na mwanamke.
Kwa asili mwanaume hupenda mara mwanamke akiwa uchi yeye mara moja aingize na kuendelea na mchezo wakati mwanamke yeye anahitaji maandalizi, jitahidi kuwa na muda wa kutosha wa foreplay kwa mke wako zaidi ya dakika 10-15 ili awe tayari kwa tendo la kuingiliwa na wewe.

Na kila mwanamke ana namna yake ya kufikishwa kwenye raha mwingine atapenda aina fulani ya mkao na mwingine atapenda aina nyingine ya mkao, mwingine atapenda achezewe kisimi na mwingine atapenda achezewe chuchu, na mwingine atapenda sehemu nyingine hivyo mwanaume anahitaji kuwa mvumilivu na sharp kumsoma mke na kujua ni kitu gani anahitaji na wapi anahitaji kuguswa zaidi ili afike huko kunako raha yenyewe.
Pia mawasiliano wakati wa faragha yenyewe ni muhimu; kwa maneno na vitendo wengine hawasemi bali wanakuelekeza kwa mkono.

No comments:

Post a Comment