Sunday 24 January 2016

NI MUHIMU.

KWA WANAWAKE TU:
Nini cha kutarajia kutoka kwa mpenzi wako mkiwa na faragha chumbani kwenu?


1.Haijalishi ni handsome kiasi gani au msomi kiasi gani hadi anaitwa Dr. au Professor; haijalishi ni diplomat au businessman au mbunge au tajiri linapokuja suala la sex wanaume wengi (siyo wote) ni zero wa kufahamu nini kinaweza kumfanya mwanamke asisimke na kufurahia sex.

2.Usijidanganye kwamba anajua mapenzi hata kama huko nyuma aliwahi kuwa na mpenzi.
Ukiwauliza wanaume wengi kisimi (clitoris) ni kitu gani katika mwili wa mwanamke, wanakuuliza kwa mshangao “Unasema kitu gani?”

3.Usijidanganye kwamba anajua ramani ya kupita katika kukufikisha kwenye raha ya mapenzi (kileleni) kama unavyohitaji bila wewe kumwambia; Ukweli ni kwamba unahitaji kumwambia si mara moja tu bali mara kwa mara vile unapenda akufanyie ili ufurahie sex na yeye kama vile;
“Mpenzi huwa najisikia raha sana unapofanya hivi au vile”
“Nilipenda sana na kiujisikia raha sana jana ulipoanza kwa kufanya hivi ila leo ningtependa uanze hivi”
“Huwa najisikia raha unavyochezea ………………….. namna hivi”
Baada ya hapo relax na mwache aendee kukupa raha!

KWA WANAUME TU:
Nini mpenzi wako (mke wako) anahitaji kutoka kwako mkiwa faragha!

1.Usifikirie sex ni bingo, sex ni sehemu ya mahusiano na ni kitu ambacho ni ziada baada ya kuimarisha na kutimiza mambo mengine katika mahusiano hata kama ni madogo madogo lakini kwa mke wako ni mambo muhimu kama vile kumsaidia kazi, kumwambia “nakupenda” kupiga naye story mbalimbali za maisha kwa upendo, kupeana zawadi nk.


2.Jitahidi kutimiza mahitaji ya mpenzi wako kwanza ndo yaje yako kila eneo la maisha yenu ya mahusiano.

3.Fahamu kwamba mpenzi wako anahitaji mazingira ya kimapenzi romantic, kujisikia unamjali (caring), unamwamini (trust) , kiasi cha kujisikia salama (safe/protected) na si kukimbilia sex.
Baada ya hapo hayo mengine utazidishiwa na atajituma kukupa kile unahitaji.

No comments:

Post a Comment