Sunday 3 April 2016

WAKATI WA MIGOGORO.

Kukiwa na mgogoro kati ya mume na mke, kawaida mke hujitahidi kufanya bonding na mumewe kwa kuongea na kuhakikisha emotions zinakuwa wazi kwa kuwa hajui tofauti ya mwanaume huamini na mume wake naye atakuwa mwepesi kuongelea kama yeye na matokeo yake mwanamke huishia kuwa na hasira na frustrated.
Jambo la msingi ni kwamba mume anatakiwa kufahamu kwamba kunapotokea mgogoro au kupishana lugha ni jambo la maana sana kumsikiliza mke au kuhakikisha mnaongea na unampa mke muda na wakati wa kutosha kuongea yote aliyonayo (kutoa emotions zake hata kama atalia machozi ila hakikisha analia akiwa mwilini mwako) na kwa njia hiyo anajiona unamjali kuliko kumwambia tusiongee sasa au tutaongea baadae au kukwepa au ku-ignore maana hapo ataumia zaidi na kuona humjali, hapendwi na upo harsh.
Pia mke naye asikasirike pale anapoona mume anakwepa kuongelea tatizo au mgogoro uliopo kwani wanaume ndivyo walivyo (tofauti zilizopo kwani wanaume huamini kwa kuacha kuongelea ndiyo njia nzuri ya kumaliza mgogoro) hivyo wewe mke mpe muda na akitulia mnaweza kuongea zaidi.

No comments:

Post a Comment