Saturday 9 April 2016

USHAWAHI KUSIKIA HII MWANANDOA?

Binadamu akifikia miaka 9 – 14 mwili huanza kubadilika. Hiki ni kipindi ambacho msichana au mvulana hubadilika kutoka utoto na kuwa mtu mzima na hiki kitendo huitwa balehe na moja ya dalili ni kuota kwa nywele kwenye makwapa, sehemu za siri nk.

Leo tuzungumzie nywele za sehemu za siri yaani mavuzi.
Hizi nywele kawaida huwa na rangi tofauti na nywele za sehemu zingine kama kichwani, zingine huwa na rangi nzito zaidi, zingine huwa ngumu zaidi, zingine hunyoka, zingine hujisokota (curl)

Linapokuja suala kunyoa hizi nywele ni preference ya mtu, pia jambo la kushangaza ni kwamba wanawake ndio huzungumziwa zaidi kuliko wanaume ni kama vile wanaume hawana hizi nywele.
Imefika wanaume hujiuliza wenyewe je, mwenzangu unapenda mke kuwa na forest au kuwa na jangwa la sahara?
Kila mwanaume au mwanamke ana jibu lake.

Baadhi ya wanawake hujisikia more attractive wakiwa wamenyoa wakati wengine hujisikia raha wakiwa na thick forest.

Hata hivyo kama lilivyo suala la matiti au makalio wapo wanaume hufurahia na kujisikia excited zaidi kwa mwenzi wake kuwa na msitu wa asili wa uhakika wakati huohuo wapo wanaume ambao kwa mwanamke kuwa na msitu mnene kwake huona ni mwanamke mchafu na asiyejitunza kama anshindwa kujinyoa sehemu muhimu kama hiyo basi yupo careless na hajipendi.

Kunyoa au kutokunyoa ni suala la hiari yako na mpenzi wako hakuna sababu ya Kujiona upo sahihi au hupo sahihi pia wapo ambao hunyoana na nyakati kama hizo kwao ni faragha na kujuana.

Kutokupata information zinazotakiwa wakati mwingine huweza kusababisha mtu kuchukua hatua ambazo zinaweza kushangaza hata mpenzi wake.

FAIDA ZA KUACHA KUNYOA

Hizi nywele huwa zinashika homoni za pheromones ambazo zikisambaa huweza kuvutia mtu wa jinsi tofauti

Huweza kuzuia msuguano wakati wa tendo la ndoa, Kumbuka viungo vya uzazi vipo delicate sana.
Husaidia kufanya maeneo ya sehemu za siri kuwa jotojoto (warm)
Huzuia na Kulinda sehemu za siri hasa vitu vidogo kama mavumbi Kuingia sehemu nyeti hasa wanawake kama zilivyo nywele za kawaida zinavyolinda kichwa.
Huonesha kukua kwa mtu (sexual maturity)

FAIDA ZA KUNYOA

Huboresha tendo la ndoa hasa kwa wale wanaopenda Kipara.
Huboresha usafi; hizi nywele hushika harufu na kuweza kupelekea kutoridhishana kimapenzi, au kama muhusika hajaoga vizuri anaweza kukufukuza kwa harufu.
Kujisikia vizuri, kujiamini na kujisikia safi.

KUNYOA AU KUTOKUNYOA KATIKA NDOA
Kuwa na maeneo ambayo yanatunzwa ni moja ya njia ambayo mke na mume huweza kujisikia vizuri kwa mwenzake.
Wengine hujisikia vizuri zaidi kwa kila mmoja kuwa kipara na kufanya degree of intimacy kuwa juu zaidi (ngozi kwa ngozi hunoga zaidi)
Wanandoa wengi hukubaliana kunyoa au kunyoana kuliko kuacha msitu, sababu kubwa zikiwa
Kunyoa huleta ukaribu (intimacy)
Kuwa kipara (mwanamke) ni zaidi ya kuwa uchi kwani unakuwa kama umeondoa kile kinaficha uke hivyo mume huweza kuona kwa macho na kwa kugusa uzuri na jinsi Mungu alivyokuumba.
Pia wanandoa ambao hunyoana kuanzia honeymoon huwafanya kuwa karibu zaidi kwa kujuana zaidi.
Kunyoa ni usafi.
Agano la kale ilikuwa ni ishara ya kujitakasa.
Kunyoa mwanamke huonesha amejitoa kwa mumewe.


JE, KUNA STYLE ZA KUNYOA?
Wengine wanaponyoa huweka style mbalimbali,
Wengine hupunguza na si kunyoa Kipara kabisa.
Wengine hunyoa pembetatu ili wakivaa bikini nywele zisionekane.
Wengine hutengeneza mstatili ambao huitwa “Chaplin Moustache” kwa raha zao mke na mume.
Wengine hupaka rangi nyekundu na kuchora umbo la moyo kama zawadi kwa mwenzi wake.

JE,WEWE UNAPENDA VIPI??

No comments:

Post a Comment