Tuesday 26 April 2016

MAHITAJI MUHIMU KWA MUME.


Wanawake wengi leo wapo independent na inafika mahali wanajisahau kuwajali waume zao, ni muhimu sana kwa mwanamke kuwa na taaluma yake na pia ni muhimu sana kwa mke kukumbuka kwamba mume akifurahi nyumbani kunakuwa na furaha.
Mume akifurahi nyumbani kunakuwa na furaha, mke akifurahi maisha yanakuwa ya furaha na watoto wakifurahi nyumba inakuwa na furaha pia.
Kuna mahitaji matatu ya msingi ambayo mume akiyapata basi atafurahi na nyumbani patakuwa mahali pa furaha kwa mke na watoto.
Kumbuka mwanandoa akisema ndoa yake ina furaha na inaridhisha maana yake anatimiziwa mahitaji yake ya msingi katika ndoa au mahusiano na kama haridhiki na hana furaha maana yake hatimiziwi mahitaji yake muhimu.
Je, mahitaji ya msingi ya mwanaume kutoka kwamke wake ni yapi?
Kuna mahitaji 3 ya msingi ambayo mwanaume huhitaji kutoka kwa mke wake nayo ni
1. MWENZA.
Baada ya Adamu kuumbwa na Mungu alionekana ni mpweke hata baada ya kujichanganya na wanyama wengine; Mungu akaona haipendezi, akamuumba Hawa kwa ajili ya Adamu na akasema inapendeza.
Kwa nini mume anakuhitaji wewe mke kama mwenzi wake?
Ili uwe mtu wa kuwa naye, unayemfaa, mtu wa kucheza naye, kumbuka Adam alicheza sana na monkeys, samba, mbuni, Ng’ombe, kuku nk na vyote havikuweza kufanya ajisikia vizuri hadi Mungu alipomuumba mwanamke.

Ni muhimu sana Wake kufahamu kwamba waume zenu wanapenda kucheza na kwamba mume wako anapenda sana kucheza na wewe, kuwa na wewe, hivyo tafuta kitu chochote ambacho mume wako anakipenda, then fanya naye.
Kama humpi muda wa kuwa na wewe, kucheza na wewe basi atampata mwingine wa kuwa naye au kucheza naye, ndipo kilio huja.......

Pia jiulize kama mume wako hayupo kazini, au mahali unakofahamu yupo; je, atakuwa na nani? Wewe uliumbwa kwa ajili yake ili kuwa naye, kucheza naye na si kuwa vuvuzela!

2. TENDO LA NDOA
Sex ni neno zuri ambalo si chafu kama wengine wanavyoamini na kulitumia hata kama litatajwa kanisani; kwani Mungu aliumba sex kwa ajili ya mke na mume kufurahia uumbaji wake.
Hata hivyo linapokuja suala la sex wanaume wengi ni hitaji la pili katika mahusiano ya ndoa wakati wanawake ni hitaji namba 13 kwa kufuata umuhimu.
Mwanaume yeyote katika ndoa, hitaji la sex kwake ni msingi na bahati mbaya ni kwamba asipopata sex kwa mke wake dunia inaweza kumuuzia.
Hata hivyo nasisitiza kwamba sex nje ya ndoa huweza kumuongoza mtu kwenye kifo
Mungu aliumba hivyo:

3. HESHIMA (Respect)
Ukweli ni kwamba jambo la msingi kwa mume wako si kile unaongea kwake bali ni namna unavyongea kwake.
Inawezekana mume wako anao uwezo (potential) mkubwa sana kufanikisha maisha hata hivyo kutokana na ulivyo critical, blaming, kosa heshima na adabu kwa mumeo imekuwa ngumu sana yeye kupiga hatua.
Hitaji la kwanza la msingi kwa mwanaume yeyote ni heshima.
Kila maamuzi yanayofanyika katika ndoa yanahitaji kufanyika kwa ushirikiano wa mke na mume.
Kutoa sifa kwa mume wako ni njia ya maisha ya ndoa.
Behind every successful and great husband, there is an honouring and praising wife.
Kumbuka Baba akifurahi, nyumbani kunakuwa na upendo, furaha na amani na pia nyumbani kunakuwa mahali salama kwa kukimbilia.
Waefeso 5:21 – 24, 33

No comments:

Post a Comment