Sunday 3 April 2016

KUOMBA MSAMAHA.

Wanawake wengi akisema samahani ni njia mojawapo ya kujiunganisha (connect) na Mume au mtu mwingine kama kuna mgogoro au tatizo au kitu chochote anaona hakipo sawa, anaweza kusema samahani hata upande mwingine unavyijisikia vibaya.

Kwa mwanaume kusema samahani ina maana anakubali kwamba amekosa na anatakiwa kuomba msamaha.
Mwanaume anaamini kwamba kwa kusema hivyo inamuweka chini zaidi na hujiona si mwanaume wa uhakika na kwake haikubaliki haikubaliki kabisa.
Kama mume wako huwa anatoa samahani waziwazi basi umebarikiwa kwani mwingine badala ya kusema samahani yupo tayari akanunue zawadi kubwa ujue anaomba msamaha, hata hivyo kama wewe ni mwanaume kumbuka kwamba ni muhimu sana kutamka neno samahani nimekosa kwa mkeo bila kuzunguka wala kuzungusha sentensi.

Na kukitokea conflict yoyote wanawake hujisikia wana wajibu wa kuhakikisha wanafanya kitu kuondoa hiyo conflict ndiyo maana wanawake wengi wapo tayari kwenda hata kwa mtu mwingine anayemwamini kuomba ushauri.
Wakati wanaume hukwepa na anaweza kutumia muda mwingine kufanya vitu na rafiki zake na kukwepa familia ambayo huko mke wake anamsuguano naye.
Kama ni mwanaume ni vizuri kufikiri na kujiuliza upya kipi muhimu?
Familia au rafiki zako?
Familia ilikuwepo hata kabla ya kanisa na familia ni mahali ambapo kanisa huanzia hivyo ni muhimu sana kuhakikisha unamaliza conflict yoyote na kurudi nyumbani kuwa na familia.
Ukipoteza familia umepoteza vyote!

No comments:

Post a Comment