Monday 4 April 2016

TOFAUTI HIZI CHUMBANI..

Tofauti ya kiumbo kati ya mke na mume ni asilimia ndogo sana ya tofauti kati ya mwanamke na mwanaume kwa ujumla.
Bila kufahamu tofauti zilizopo tunaweza kujikuta katika shida na matatizo au confusion ya uhakika chumbani.
Ukiacha tofauti zingine zote zilizopo kati ya mke na mume linapokuja suala la sex mwanaume sex ni hitaji la kimwili kwanza (physical) na baadae emotions wakati mwanamke ni hitaji la emotions kwanza then kimwili.
Hii ina maana kwa mwanamke sex ni upendo kwanza, kujisikia vizuri kwanza, kupata caring kwanza kwa mwanamume ni kuwasha tu na bus linaondoka.

Linapokuja suala la kile anakiona mwanaume anavutiwa kwa nguvu ya ajabu (hasa anapomuona mwanamke, wakati huohuo mwanamke naye anauwezo na nguvu ya ajabu ya hamu ya upendo, ukaribu, mapenzi na kusikilizwa na mwanaume.

Mwanaume huwaza ni mara ngapi anahitaji sex wakati mwanamke anawaza ni namna gani sex itakuwa.

No comments:

Post a Comment