Saturday 2 April 2016

KUPATA MCHUMBA SAHIHI.

"Apataye Mke Apata Kitu Chema; Naye Ajipatia Kibali Kwa Bwana"
(Mithali 18:22)

Moja ya mambo ya msingi ambayo kila kijana anahitaji ni Ndoa ya Kudumu ukiacha ongezeko la kufeli kwa ndoa nyingi.

Wakati huohuo moja ya uamuzi (wa maana sana katika maisha ya binadamu ni kuamua nani atakuwa mume wako au mke wako na huu uamuzi ndiyo utakufanya uweze kuishi maisha ya namna gani katika ndoa yako na pia kuathiri kabisa mfumo wa maisha yako kuwa raha au kuwa karaha

Watu wengi katika maisha wamekuwa wakilaumu upande mwingine iwe mke wake au mume wake kwamba ndiye sababu ya kuvunjika kwa uhusiano au ndoa yao.
Huu ni ujinga muhusika mara nyingi ni wewe kwani asilimia 99 ni jinsi ulivyompata huyo mtu ambaye amesababisha ndoa yako au uhusiano kuvunjika.

Mtu anayestahili kupewa lawama zote ni wewe.

Kama hujaolewa au ndio upo kwenye process za kuolewa au kuoa,Fahamu kwamba hakuna jambo muhimu maishani mwako kama huo uamuzi unaotaka kufanya, unaweza kukupa furaha ya maisha au uchungu wa maisha hapa duniani.

Unahitaji kutumia
akili zako zote,
maombi yako yote,
uwezo wako wote na
kila resource ulizonazo
kwani hapa makosa hayana nafasi kabisa

Wala usikubali kumuoa huyo binti au kuolewa na huyo kaka eti kwa sababu:

Watu wanasema Mbona hujaolewa au kuoa!
Au ndugu zako, au mchungaji, au wazazi wako au rafiki zako wamekwambia!
Au kwa sababu umeona muda unakwenda!

Amua mwenyewe na jichunguze kama upo tayari na kama mtu unayetaka kuwa naye anakupa uhakika unaoridhika nao wewe mwenyewe.

Kumbuka it is easy to reshape the mountain siyo mtu, kwa hiyo kama kuna tabia fulani ambayo unaiona kwa mtu unayetaka kuoana naye na hujaridhika nayo Please fikiri zaidi ya mara mbili.
Na kama unaweza give time au fikiri mara nyingi zaidi.

Mara nyingi wanaosema watawabadilisha matokeo yake wao ndo wamebadishwa

Hapa huhitaji kuwa blind kwa sababu ya fall in loves, bado unahitaji kuwa na akili timamu kumfahamu zaidi huyo unataka kuoana naye kabla love haijawafanya kuwa blind au otherwise muwe blind maisha yenu yote.

Kuna maswali matano (5) ya msingi sana kujiuliza kabla hujajikamatisha vizuri kwenye hii kamba ya ndoa.

ITAENDELEA..

No comments:

Post a Comment