Saturday 21 November 2015

Nilipata swali hili nami nikaamua kulijibu na kwa wengine wafahamu.

SWALI;
Je, Ni kweli kwamba kisimi, kinembe ni kiungo pekee ambacho mume ni lazima aguse (chezea) ili mke asisimke na kuwa tayari kuwa mwili mmoja?

JIBU;

Si kweli.
Mwanamke si Channel za radio kwa maana kwamba ukibonyeza kitufe pale station inapatikana basi utapata frequency na kuanza kufaidi matangazo yake (muziki au habari).
Mwanamke ni kiumbe cha tofauti ambacho hutawalaliwa na hisia (emotions, mood na feelings).
Pia wanawake wote hutofautiana na hata huyo mmoja huweza kuwa tofauti kila siku hii ina maana kwamba kama jana alisisimka sana ulipomchezea kisimi si kanuni kwamba na leo atasisimka kwani inaweza kuwa katika mzunguko wake basi matiti ndiyo yanasisimka zaidi au G-Spot ndo anasisimka zaidi nk.
Ni jukumu la wewe mwanaume kuwa sensitive na smart kujua hitaji lake au ni kiungo gani kwa huo anasisimka zaidi.

Kuchezea kisimi chake si kanuni au sheria au utaratibu ambao umewekwa na kwamba usipofanya basi hakuna kusisimka, ingawa ni kweli mwanamke huweza kufika kileleni kwa kuchezewa kisimi zaidi wakati mwingine kuliko kutwanga na kupepeta kwenye kinu.
Mwanamke anahitaji maandalizi kwanza, anahitaji busu, caring, anahitaji mwanaume mwororo, gentle, loving, anayebembeleza, mwanaume mwenye mikono slow na mwenye mwendo wa kobe kuzunguka (kumtembelea) kiwanja kizima cha mwili wake kabla ya kufika huko kwenye kisimi.

Ni muhimu kwenda sehemu zingine za mwili kwanza kama matiti (chuchu) na sehemu zingine kuanzia zile ambazo zinasisimka kidogo hadi zile ambazo ukimgusa mwili wake unapata joto kiasi cha yeye kutoa ukelele ambao utajua kweli tumeanza kupanda mlima na kileleni tutafika.
Wanawake wengi (siyo wote) hulalamikia kitendo cha mwanaume kuwa na full speed kwenda kwenye kisimi bila kupita maeneo mengine kiasi ambacho huwa ni kuumia au kuumizana kwani kisimi huwa hakijawa tayari kupokea msisimko.

Kumbuka hili eneo lina zaidi ya nerves 8,000 hivyo ni muhimu kuguswa wakati ambao eneo lipo tayari na evidence kwamba kupo tayari ni eneo zima la south pole kuwa wet.
Kupeleka vidole vyako vikavu na bado kukavu huweza kuumiza badala ya kutoa raha.

No comments:

Post a Comment