Wednesday 18 November 2015

MAHUSIANO.

Eti mahusiano mazuri hayana sexual problems?

Wanandoa wote kuna wakati hupitia matatizo kuhusiana na sex na hii haina maana kwamba uhusiano wako na mume au mke basi umeota mabawa.
Hata hivyo kama tatizo linabaki kwa kula jiwe kati yako na mwenzako ni kweli linaweza ku ruin ndoa yenu na mahusiano.
Signal yoyote ya kuwepo tatizo katika mahusiano linapokuja suala la sex si alama ya kuwa ninyi ni failure ni sehemu katika mahusiano.
Inawezekana sexual needs za mume wako au mke wako zimebadilika, hasa katika dunia ya leo ambayo watu wanakimbizana na maisha bila mafanikio.
Umenunua gari ukimbize maisha lakini wapi, umejenga nyumba ukimbize maisha lakini wapi, umeoa mke mzuri kukimbiza maisha lakini wapi na wewe unayesoma hapa umeolewa na mwanaume mzuri lakini maisha wapi bado ni kukimbizana tu, mimi simo!
Hata hivyo kubadilika kwa hamu, kuridhika nk vinahitaji muda ili muweze kufanya adjustment na kurudi kwenye mstari na kuendelea na maisha kwa raha zenu.

Eti mwanamke lazima afike kileleni kwa intercourse peke yake (uume kuingia kwenye uke)

Wanawake wengi hawawezi kufika kileleni kwa hicho kitendo peke yake hata kama unatumia ukuni mkubwa kiasi gani au jogoo anawika kwa muda mrefu kiasi gani kwa sababu uume hauwezi kutoa stimulation ya kutosha hadi kufika kileleni isipokuwa kisimi.
Pia kutumia milalo ya aina tofauti hasa ile inayoweza kusisimua kisimi au G- spot huweza kusaidia kwa wengine.
Pia kumbuka foreplay ni muhimu kuliko sex yenyewe na hilo ni muhimu kuhakikisha kila mmoja anafika kileleni kwa raha zake hata hivyo muhimu zaidi ni mood hasa kwa mwanamke.
Ni busara ya hali ya juu kwa mwanaume kuacha kufanya sex kama mwanamke unahisi hana mood.

Eti mke wangu au mume wangu atajua mwenyewe tu jinsi ya kunipa raha hata nisipomwambia wakati wa mahaba.

Mkeo au mumeo si mind reader hana scanner yoyote ya kujua unajisikia raha wapi na aongeze efforts kwenye hilo eneo huku wewe umelala kama gogo.
Kukosa mawasiliano wakati wa sex ni moja ya factor kubwa inayochangia kuwa na tendo la ndoa lisiloridhisha kwa kila mmoja.
Kila mmoja anajua sex ni kitu gani kila mtu hili eneo ni genius hata hivyo kila mtu ana sexual needs tofauti na mwingine.
Ni lazima umwambia partner wako nini unahitaji, acha aibu tena mwambia kwa details na kuwa huru hata kama yeye huwa bubu au huchanganyikiwa kabisa ukishamwambia twende south pole.

No comments:

Post a Comment