Friday 20 November 2015

MKE HUPENDA MUME WA AINA HII

Mambo yanayomnyima raha mke kutoka kwa mume:

Mwanaume ambaye hana ufahamu wa kimapenzi.
Hajui ni nini na wapi kipi kinapatikana na kinafanywa vipi.
Kwa mfano hajui kisimi nini, kipo wapi na kina manufaa gani na hana mpango wa kujua au kujifunza lolote kuhusu mapenzi.

Mume ambaye hana hamu ya kujifunza jinsi ya kumridhisha mke zaidi.
Kutokuwa na hamu ya kutaka kujua skills na mambo mapya inaweza kuwa ni turn off kwa mke kwani kila mwanamke ni tofauti na katika mapenzi (kuwa mwili mmoja) huwezi kukoma kujifunza haijalishi unajua kiasi gani bado kuna vitu vingi sana vya kujifunza .

Mume ambaye ni mbinafsi kujipa raha yeye mwenyewe.
Kama unahitaji kujua maana ya tendo la ndoa linalowaridhisha wote basi jifunze kumtanguliza mwenzako na kumridhisha kwanza yeye.

Mwanaume asiyeuliza hata swali wakiwa kitandani.

Mke huhitaji mume ambaye ni initiator anayejua kuutumia uwanja (mwili wa mke wake) na kuuliza anajisikiaje kila sehemu anayogusa au kukanyaga.

*
Mambo ambayo huwa yanampa raha mke kutoka kwa mume wake:

Mume ambaye amejaa ufahamu kuhusu mwili wa mkewe.
Kwa mfano mume anaejua kisimi kipo wapi, kipoje, kina sifa gani, kina respond vipi, kinafanywa vipi kitoe raha na anajua ni namna gani mke atakuwa amepata raha anayohitaji kupitia hapo nk hapo ni kila kiungo ambacho mke anaweza kusisimka na kupata raha ya mwili kutoka kwa mume wake na kuridhika.

Mume ambaye focus kubwa ni kumpa raha mke na si kutimiza wajibu.
Hana haraka na kufanya na kumaliza na kutimiza wajibu bali ana mikono slow kiasi cha kufamfanya mke ajione ni mke anayeridhishwa na mume kuliko mwanamke yeyote duniani.
Ni mume ambaye mke akikumbuka jinsi wanavyofanya huko faragha basi kama mume amesafiri anaanza kutamani mume arudi haraka maana hakuna muda mzuri kwake duniani kama kuwa na mume faragha na kufaidiana.

Mume anayemfanya mke kujiona ni beautiful chumbani na nje ya chumbani.
Anampa sifa na kumfanya mke akione ni kweli ni mzuri na anapendeza chumbani na nje ya chumbani.

Mwanaume anayejali kuridhika au kutoridhika kwa mke katika sex.
Mwanamke yeyote hupenda kujua au kuona mume wake anakuwa completely involved kuhakikisha anampa raha ya kimahaba na mume anakuwa na mtazamo au anajitahidi kuongeza ujuzi ili kuhakikisha mke anapata raha zaidi kila wakiwa pamoja chumbani.
Siyo mwanaume ambaye hawezi hata kujua hali ya zoezi zima la tendo la ndoa lipoje zuri, kawaida au wanaelekea kwenye cliff.
Anapenda mwanaume anayetaka kujua ni kitu gani kinampa raha live, siyo kuwa selfish na baada ya kumaliza mke anaendea kuugua na kujiona ametumiwa tu.

Mume anayemfanya mke kujiona yeye ni namba moja kwake kwa kila kitu.
Mke hapendi tu kujiona yeye ni factor kwa mume bali anapenda kuona ni very important factor kwa maisha ya mume wake.
Mke lazima ajisikie salama na huru katika kile anatenda katika ndoa na mume wake.
Mume anahitaji kuwa creative jinsi ya kufanya mke vipi ajisikie.
Ni kweli sex ni kitu kizuri sana na huweza kumpa raha mume na mke hata hivyo Mungu amempa mume uwezo wa kufanya kazi apate pesa hata aweze kumnunulia mke vitu vidogo vidogo kama massage oil ili wakiwa wawili wapeane raha katika miili yao.

MWISHO.
Mume atimize wajibu wake wa ndoa kwa mkewe, naye vivyo hivyo mke kwa mumewe.
Mwanamke hana mamlaka juu ya mwili wake bali mumewe, wala mume hana mamlaka juu ya mwili wake bali mkewe.
Msinyimane, isipokuwa mmekubaliana kufanya hivyo kwa muda fulani ili mweze kujitoa kwa maombi, kisha mrudiane tena ili Shetani asije akapata nafasi ya kuwajaribu kwa sababu ya kutokuwa na kiasi.

No comments:

Post a Comment