Saturday 21 November 2015

MKIHUDUMIANA VIZURI,UGOMVI UTAPUNGUA

Wakati mwingine mwanaume hujikuta amekuwa mkali, majibu ovyo na mkato, violent na mwenye hasira kumbe tatizo ni kutotoshelezwa kimapenzi na mke wake, acha wale wanaume ambao ukali kwao ni nature.
Pia wapo wanawake ambao huwa violent maofisini hasa kama ni boss (siyo wote lakini) hata kitu kidogo tu kwake inakuwa issue.

Moja ya matokeo ya kuwa na tendo la ndoa linaloridhisha, mke na mume kuridhishana na kila mmoja kuridhika na mwenzake ni kupunguza misuguano katika ndoa.
Mwanaume ambaye anapata huduma inayomridhisha kimapenzi huwa ni mwanaume aliyetulia
Hii haina maana kwamba matatizo makubwa yatatoweka yenyewe au kwa kuwa na tendo la ndoa linaloridhisha basi ada ya shule watoto itapatikana haraka au itasaidia budget kuwa shwari.

Wapo wanaume wengi hawafahamu kwamba baadhi ya matatizo yanayokuwa nayo nyumbani na kazini yanaweza kuwa traced kwa kutokana na utoshelevu wa tendo la ndoa wanavyopeana mke wake pia mke mwenye hekima na busara huweza kutambua namna mume wake ana-behave nyakati tofauti na anajua dawa yake ni ipi.

Katika ulimwengu wa ndoa wakati mwingine matatizo madogo madogo huweza kupungua size kutokana na hali nzuri ya utendaji kitandani.
Hii ina maana kuna mizozo mingi ingekuwa haisikiki katika ndoa kama kila mmoja angejua kwamba kumridhisha mpenzi kimahaba inaweza kuwa dawa tosha.

Kuridhishwa kwa tendo la ndoa pia husaidia nervous system ya mwananmke kuwa relaxed.
Wapo wanawake kutokana na kukosa huduma au kuhudumiwa vizuri na waume zao hadi kuridhika kimapenzi wamekuwa wakali, wenye vurugu, visilani na hata maofisini kama ni boss kuwaka moto kwa kila mfanyakazi pasipo sababu ya msingi acha wale wanawake ambao ni wakali by nature.

Mfumo wa fahamu wa mwanamke umeunganishwa moja kwa moja na viungo vya uzazi na kila mwanamke kutoka kila aina ya maisha duniani ameumbwa kuwa na uzoefu wa kupokea furaha ya Ku-relax kupitia kitanda cha ndoa (sex).
Hivyo basi mwanaume anayejua raha ya mwanamke kuwa relaxed anakuwa mjanja kuhakikisha kitanda kinakuwa na moto wa kutosha.

No comments:

Post a Comment