Friday 20 November 2015

FAHAMU UTOFAUTI HUU WA MWANAUME NA MWANAMKE.

Hivi kwa nini wanaume huwa hawahangaikii upendo kama wanawake?

Jibu limelalia zaidi kutokana na walivyoumbwa wiring yao ipo tofauti.
Wanawake huanzia kwenye romance, mawasiliano mazuri na hatimaye sex wakati wanaume husafiri kwa opposite direction.

Ukichunguza kwa undani zaidi utagundua kwamba mwanaume anapokuwa na uhitaji mkubwa au hamu kubwa ya sex huwa anakuwa anataka kujiunghanisha emotionally na mwanamke, ndiyo maana kwa mwanaume sex ni mhimu sana wakati kwa mwanamke romance ni muhimu sana.

Kuwa na uelewa mdogo kuhusu hii tofauti hufika mahali wanawake waka –underestimate umuhimu wa sex kwa mwanaume na wakati mwingine wamewahukumu kwamba mwanaume anachotaka ni kitu kimoja tu nacho ni sex.

Hata hivyo mwanaume kusisimka kimapenzi na kuhitaji sex ni njia ya kujiunganisha na mwanamke kihisia na ili ajifahamu kihisia kwamba anakupenda.
Ni kupitia sex moyo wa mwanaume hufunguka na kumruhusu kupata hisia za upendo (love) kwa mke wake.

Ni kupitia sex mwanaume hupata feeling za kupenda ingawa kwa mwanamke sex huja baada ya kutoa na kupokea upendo (romance)

Wanawake huhitaji mawasiliano mazuri na kujisikia wanapendwa ili kufungua moyo kwa ajili ya sex wakati huohuo mwanaume huguswa na upendo wa mwanamke kupitia sex.
Kama mwanamke anavyohitaji mawasiliano mazuri na mwanaume (partner) ili ajisikia anapendwa, mwanaume huhitaji sex ili ajisikie anapendwa.

Sex drive ya mwanaume mara nyingi si rahisi kuweza kuifanya iwe turned off, yupo designed kuwaza kuhusu sex na kuhitaji sex muda mwingi na ni mara chache sana mwanaume hujikuta amechoka au yupo stressed kuhitaji sex.

Hii haina maana kwamba mwanaume huwa anaoa ili kupata sex tu na haina maana pia kwamba anaoa ili asipate sex, Bali sex ni moja ya sababu muhimu za yeye kuoa na jambo la msingi ni kwake kuwa na mwanamke special ambaye yeye kama mwanaume atakuwa anapata hitaji lake la sex maisha yake yote.

Wanaume wengi (siyo wote) likija suala la sex ni 24/7!

No comments:

Post a Comment