Friday 10 June 2016

NDOA NI KAZI..


Ndoa ni kazi.
Inayochukua muda, jitihada na commitment na wakati mwingine huhitaji professional counselling.
Kama umefika Mahali ambapo wewe na mume wako au mke wako hamuwezi hata kuwasiliana (kuongea) bila kuvurugana na umeanza kufikiria kuachana kama njia bora zaidi basi unahitaji msaada kwani kuachana bado si jibu la matatizo yote.
Katika ndoa mwanaume na mwanamke ni tofauti na kila mmoja ana mahitaji muhimu ambayo ni lazima mwenzake ayatimize na kutotimizwa hayo mahitaji husaidia kukwetua njia ya kila mmoja kutoridhika na mwenzake.
Kwa ufupi mahitaji muhimu ya mwanaume (yale anapenda mke wake amtimizie) ni kama ifuatavyo

1. HITAJI LA KURIDHISHWA KIMAPENZI (SEX).

2. HITAJI LA KUBURUDISHWA, RAHA, KUSTAREHE, KUPUMZIKA, NAFASI YA KUPUMUA, BURUDANI.

3. HITAJI LA KUWA NA MKE ANAYEVUTIA.

4. HITAJI LA KUWA NA AMANI NA UTULIVU.

5. HITAJI LA KUAMINIWA, KUHUSUDIWA NA KUHESHIMIWA.

Mahitaji ya mwanamke katika maisha ya ndoa (vile mwanamke anapenda mume amfanyie au kumtimizia) ni kama ifuatavyo:

1. HITAJI LA UPENDO, KUPENDWA, MAHABA NA HURUMA.

2. HITAJI LA MAONGEZI, MAZUNGUMZO, MISEMO, POROJO, KUSIMULIANA NA SOGA.

3. HITAJI LA UKWELI, UADILIFU, KUAMINIANA, UNYOFU, WIMA NA UWAZI.

4. HITAJI LA UHAKIKA WA KIFEDHA, AMANA KIFEDHA, UHAKIKISHO KIFEDHA, ULINZI KIFEDHA, USALAMA KIFEDHA, UTHABITI NA AMANI KIFEDHA.

5. HITAJI LA KUJITOA KWA AJILI YA FAMILIA.

Kwa ufafanuzi ni kwamba mwanamke hupenda mume akimaliza kazi jioni kwanza ajithidi kuwahi nyumbani ili ale chakula (supper/dinner) na mke na watoto, akae na mke na kuongea masuala ya familia kama watoto, matumizi ya fedha nk na hupendelea baba kutumia muda na watoto na mke na si kuangalia TV.
Mume naye hupenda anaporudi kazini mke ampe angalau dakika 15 apumue ndipo aanze kuuliza maswali na kuelezea siku ulivyokuwa na ikifika muda wa kulala mke aanzishe kwamba anahitaji tendo la ndoa.

No comments:

Post a Comment