Saturday 11 June 2016

INAWAHUSU SANA WANAUME.


Kama mwanamke atajiona yupo appreciated nje ya chumbani basi akifika chumbani atakuwa mwenye furaha (excited), hivyo haina maana kusubiri umpe maneno matamu akiwa kitandani badala yake mpe maneno matamu kuanzia jikoni au sebuleni.

“Never tell a woman she is beautiful when lights are off”

Mwanamke ana hamu kubwa ya ukaribu wa kimapenzi (intimacy) kutoka kwa mume wake, kujisikia yupo karibu na connected.


Kwa mwanaume sex hutokea kule downstairs chini ya mkanda ulivaa, kwa mwanamke sex ni upstairs, kwenye kichwa chake (brain).

Ndiyo maana kwao foreplay ndiyo mfumo wa maisha ya mapenzi.

Na ndiyo maana hawafiki kileleni mara zote.


Wanawake hutumia muda mwingi kuwaza ni kitu gani wanaume wanahitaji katika mahusiano na tatizo kubwa ni kwamba wanaume wachache sana huwaza kuhusu nini wanawake wanahitaji katika mahusiano, basi unahitaji kuwa mmoja ya wanaume ambao si kuwaza tu bali wanafanya kile wanawake wanahitaji.


Mwanamke anapoongea usimkatishe kwani ndiyo njia pekee ya yeye kuwa karibu na wewe.

Kumbuka anapokwambia matatizo yake wakati mwingine hana maana umpe majibu namna ya kutatua (fix the problem) bali anahitaji wewe umsikilize tu na wewe kumsikiliza maana yake unamjali.


Kwa mwanaume fedha ni status hata, hivyo kwa mwanamke fedha ni security, hivyo usiseme fedha zangu, bali sema fedha zetu.

No comments:

Post a Comment