Tuesday 17 March 2015

KWANINI WAPENZI HUGOMBANA?

Mara kwa mara nimeshuhudia viugomvi vya wapenzi au wanandoa....
" Tunapendana sana lakini tunaviugomvi vya mara kwa mara. Sijui ni kwa nini hii hali, tunajaribu kuondokana nayo lakini tunashindwa"

Katika makala hii ninajaribu kuonyesha baadhi ya sababu zinzaofanya wapenzi au wanandoa wengi kugombana mara kwa mara ingawa viugomvi hivi havimaanishi kwamba hawapendani na sio kwamba kugombana huku mara kwa mara wako tayari kuachana.

SABABU

1. PALE MPENZI MMOJA ANAPOSHINDWA KUFANYA YALE YALIYOTARAJIWA NA MWINGINE.

Kila mmoja wetu ana picha akilini mwake inayomwenyesha ni jinsi gani mpenzi au mwenza bora anatakiwa awe, picha hii yamkini imechoreka akilini mwetu tangia utotoni. Bila kudhamiria mara nyingi tunajikuta tunaanza kulinganisha kile tulichokuwa nacho akilini na kile kilicho dhahiri kinachotokea. Katika mapenzi kwa sasa. Mara nyingi wakati tunapojikuta tunagombana ni kutokana na utofauti wa vile mpenzi wako anavyofanya na vile ulivyomtarajia akilini mwako awe.

Uhalisi unatokea unapokuwa tofauti na tuliyotarajia, hisia zetu zina umizwa, chuki inaamka, maumivu yanaibuka na hivyo hasira na ugomvi huja. Hasira hapa hutumika kama njia ya kumlazimisha mpenzi au mwenza wako kukaribia au kujaribu kuwa kama yule mpenzi bora uliyekuwa unamuwaza akilini mwako. Ingawa mara nyingine pamoja na hasira hizi yawezekana tusione hata chembe moja ya badiliko. Wapenzi wengi husihi miaka mingi hususani kwenye ndoa nakuwa ndani ya chuki za aina hii na walioshindwa kukidhi haja za kila mmoja.

2. PALE UNAPOKUWA NA TOFAUTI KALI KATIKA MISIMAMO YENU

Misimamo hii ni zile imani au vitu tunavyoviamini na vinavyotusaidia kuendesha maisha yetu ya kila siku. Kila mmoja wetu anavimisimamo anavyosimamia kila siku maishani. Vitu ambavyo tunaviamini na tunavipa uzito tofauti vitu hivyo. Mfano, Kama msimamo au imani ya mmoja wenu ni kihifadhi fedha na mwingine ni kuzitumia lazima tofauti baina yenu itakuwa kubwa, kwa sababu wakati mmoja anajitutumua kutafuta fedha na kuziweka kwa maendeleo mwingine anajitahidi kuzitumbua kwa matumizi yasiyo na msingi, hapa lazima moto uwake baina ya wawili hawa.

Kama mmoja anapenda kujinyenyekeza na anaamini kuwa mume au mpenzi wa kiume anatakiwa kunyenyekewa, na wakati mwingine anaamini katika usawa wa jinsia, lazima hapa ugomvi usiishe. Ugomvi unakuwa lazima katika wapenzi wa aina hii maana kila mmoja anaamini kitu ambacho ni cha tofauti kabisa na mwingine, na kila mmoja anajaribu kuhimiza kila anachoamini kifanyike.

3. PALE TUNAPOTOFAUTIANA NAMNA TUNAVYOTAFSIRI MAHITAJI YETU YA KIHISIA

Wengi wetu kama sio wote hupenda vitu vitatu toka kwa wengine, Upendo, Kutambuliwa na Heshima. Ingawa tunajitahidi kutunza mahitaji yote matatu lakini moja lina yazidi mengine, hii ni hitaji la upendo au penzi toka kwa yule unayempenda. Tatizo linakuja kwamba penzi halishikiki kwa hiyo ni ngumu kulipa picha fulani, ndiyo maana ninapoouliza mwanaume yeyote, unajuaje kwamba mkeo anakupenda swali hili linakuwa gumu sana kujibu. Wengine hutokea haswa pale tupotofautiana kutafsiri jinsi ya kuelezea penzi. Wengine wanataka walione penzi kwa macho, waone wanavyopendwa, wengine wanataka wasikie jinsi wanavyopendwa na wengine wanataka wahisi vile unavyompenda, sasa kama wewe unaona kupenda kwa kweli lazima mtu aone penzi kwa macho, wakati yeye anaamini ni lazima asikie hilo penzi masikioni mwake basi mtatofautiana sana na hamtaisha kubishana.

Ndio maana wako wapenzi wnaoona wamependwa na kuthaminiwa pale tu wanapopewa vitu vya thamani au kufanyiwa suprize, wakati wengine hutaka wasikie maneno kama " nakupenda" I love u" "Umependeza" ndio wajue wanapendwa, hata kama hujapewa kitu chochote. Wapo ambao wanataka kuguswa, kukumbatiwa na wapenzi wao na katika hali hii watahakikisha kuwa wanapendwa, Jiulize sasa, wewe penzi unalitazamaje Nini kifanyike ili uone kama unapendwa.

3.PALE AMBAPO UJUMBE ULIOKUSUDIWA KUTUMWA SIVYO ANAVYOKOLEWA

Magomvi mengi tena makali hutokea baina ya wapenzi wengi pale ambapo mmoja anatuma ujumbe fulani au kusema kitu fulani na yule anayepokea msikilizaji anahisi kama anaeelewa na kuanza kutenda kumbe anatenda tofauti, pasipo kuuliza aeleweshwe anafanya kile alicho au anachokiwaza akilini mwake kuwa ndicho sahihi kwa jinsi alivyokitafsiri.

Mfano, mpenzi wa kiume anasema "njoo hapa" Mpenzi wakike mara anajibu " kwani nimefanya nini"? najibu hivi kutokana na kuhisi kuwa sauti hii iliyomwita ni yashari, kumbe sivyo awazavyo mpenzi wa kiume. Najua jinsi alivyouta yaweza maanisha anahasira na wewe lakini pia yaweza maanisha amekasirishwa na kitu au vitu vingine. Chakufanya hapa. jifunze kuhakikisha kile ulichosikia au unachohisi umekielewa kabla hajarukia katika kutafsiri isivyo sahihi.


No comments:

Post a Comment