Wednesday 10 December 2014

NDOA NA MSINGI WAKE MKUU.

  Ndoa yoyote ambayo mke au mume hafiki kilele cha Mlima Kilimanjaro..hiyo sio ndoa inayokwenda sawa na kuna madhara makubwa kwa pande zote,kwa maana ya mwingine kuweza kuamua kutoka.Ni vizuri walio kwenye ndoa  kujifunza namna ya kupeana raha iwapasayo wanandoa kuipata.Kama unafikiri mkeo unaye kwa sababu amekuja kutafuta kula au kununuliwa magari na nguo,hilo ni kosa.Tafakari namna ya kupeana raha kwa kila kona.
Kama ni kula,kila mtu anaweza kujitafutia kwa njia mbalimbali.Mwanamke yuko kwa mume kwa sababu anahitaji kupata vitu anbavyo wanawake huvipata kutoka kwa wanaume;Mume ndiyo kichwa,iongoze ndoa yako vizuri kwa hekima.
     Kwa asili,inatakiwa mke na mume kufanikisha zoezi hilo la kuwezeshana kufika kileleni na ni jambo  muhimu kama ilivyo kutoka jasho mwilini,maana sio tu mwili unaondoa uchafu ndani ya mwili,pia inasaidia kuupoza mwili kuwa sawasawa.
Najua wapo wanaoweza kusema aah mbona mimi nimekaa mwaka sitaki tena mwanaume au mwanamke na sijapata madhara...Inawezekana ni kweli,lakini wengi hupata madhara.Kadhalika kuna wengine wanafanya vitu vya hatari kama kutumia vitu mbalimbali kama mwanasesere (sex toys) na mashine maalumu zenye umbo kama la mwanaume au wengine kujichua au kusagana.
Ukidumu bila tendo la ndoa muda mrefu,baadhi ya madhara madogo madogo ni kama kuwa na hasira za mara kwa mara katika mambo madogo,hii hasa kwa wanawake ambao walishawahi kuwa na uhusiano unaokaribiana kuoana au waliwahi kuwa kwenye ndoa kisha wakatoka.
Kwa wanaume madhara yake ni kupendelea zaidi kuangalia picha za ngono.Kwa wote kwa maana ya wanawake na wanaume huwa na hali ya kusahausahau.
  Kwa wanawake wapo ambao hutokwa damu nyingi wakati wa hedhi.Kwa wote yaani wanaume na wanawake hupenda kurukia mambo ya watu wengine ( Tabia ya kufuatilia mambo yasiyokuhusu) na wakati mwingine huongea kwa sauti ya juu hasa kunapotokea migogoro.Wengine wana uwezo mkubwa wa kutukana au kutoa kauli yoyote  unapomuuzi.
Athari nyingine ni kuumwa na kichwa kwa wanaume na wanawake,kupoteza umakini katika kazi na kwa jumla sehemu za kazi wengi wa watu ambao wamesema hawataki tena kusikia mapenzi,siyo viongozi wazuri,wana kauli chafu,hata uamuzi wao mara nyingi siyo mzuri,Ingawa siyo wote.
Hali kadhalika siku ukikutana kimwili na mwenye virusi bila kinga utaambukizwa kirahisi mno.Aidha unaweza kuanzisha tabia nyingine kama ulevi,kukaa ofisini tu bila sababu.
Ni jambo la msingi sana kutafakari kwa umakini mkubwa hali ya uhusiano wako,kwani maisha bila kujipa muda wa kutafakari ni kosa kubwa.Kama ilivyo kawaida ya watu wa biashara ambao hufanya mahesabu ili kuangalia hali za biashara zao,muhimu sana kuangalia mbinu za kufanya ili kama kuna tatizo kwenye uhusiano wako kurekebisha kasoro hizo.
  Ndoa au uhusiano  ambao watu wake hawana muda wa kujitafakari ni vigumu sana kuwa nauhusiano mzuri.
Msingi wa kuwa na maisha bora ni pamoja na kuhakikisha ndani ya ndoa yako kunakuwa na amani thabiti.Unaweza kuwa na fedha kadri unavyoweza,lakini fedha hizo haziwezi kukupa furaha kama huna ndoa nzuri.

No comments:

Post a Comment